Monday, January 7, 2013

WAKALA WA LAMPARD ASEMA LAZIMA AONDOKE KWANI VIONGOZI WAMEMCHOKA LAKINI MASHABIKI BADO WANAMTAKA.

 


Imethibitika kuwa Frank Lampard ataihama Chelsea mwishoni mwa msimu huu, kwa mujibu wa wakala wake Steve Kutner.
Akikaririwa na magazeti ya nchini Uingereza akisema,
"watendaji wa Chelsea walimwambia Frank kule Japan wakati wa michuano ya kombe la dunia la vilabu na hata mara baada ya ushindi dhidi ya Everton mwezi uliopita kuwa hakuna chochote kitakacho pelekea klabu kumpa ofa nyingine Lampard baada ya msimu huu"
"hakuna kitakacho badilika kwa vyovyote vile. Frank anapashwa kukubaliana na hayo inabidi ajikusanye kumalizia msimu kwa mafanikio katika klabu ambayo aliipenda sana."
Lampard alipata nguvu mpya kutokana na kushangiliwa na mashabiki wa Chelsea katika mchezo wa mzunguko wa tatu wa michuano ya FA dhidi ya Southampton jumamosi pale alipofunga goli ambalo kimsingi lilimfanya kuwa sawa na mchezaji wa zamani klabu hiyo Kerry Dixon mwenye rekodi ya juu ya ufungaji magoli, lakini inaonekana sherehe ya ushangiliaji baada ya kufunga goli akiwa katika jezi yake maarufu namba 8 mgongoni inaelekea ukingoni.
Mashabiki wa Chelsea wamekuwa wakitaka Lampard apewe mkataba mwingine lakini hali inavyo onekana ni kuwa hakuna nafasi nyingine ya kuendelea kusalia Stamford Bridge.
Mwenyewe Lampard amekaririwa akisema
"pengine sikuwa na mvuto wa kutosha lakini mashabiki wamekuwa na mimi katika kipindi chote ambacho tumekuwa pamoja hapa"
Rodgers amtetea Suarez baada ya mpira wa mkono.
 Brendan Rodgers: 'Nadhani haikuwa makusudi ya mwamuzi'
Brendan Rodgers amesema goli la ushindi la Luis Suarez ambalo lilitokana na mpira uliotengenezwa kwa mkono kabla ya kufunga kwa mguu wa kulia halipaswi kuendelea kuzungumziwa aambapo pia amemsifia mshambuliaji huyo baada ya mchezo huo kati ya Liverpool na Mansfield.
Luis Suarez aliutuliza mpira kwa mkono kabla ya kufunga goli, ambalo lilikubaliwa na mwamuzi na kutoa matokeo ya ushindi wa kwa Liverpool.
Liverpool inajipanga na mchezo wa mzunguko wa nne wa michuano hiyo ya FA dhidi ya Oldham Athletic baada ya kupata goli la fuluku na kupelekea ushindi wa mabao 2-1 katika dimba la One Call Stadium.
Daniel Sturridge alifunga goli lake la kwanza katika timu yake mpya ya Liverpool dakika ya saba kabla ya Suarez kuandika bao la pili baada ya kuingizwa uwanjani kipindi cha pili.
 Kelele za kuzomea zilisikika uwanja mzima baada ya goli hilo kuruhusiwa, ambapo licha ya jitihada za wenyeji kuweka mpira kati na kuanza kwa lengo la kusawazisha jitihada zao hazikuza matunda ili kupata mchezo wa marudiano kule Anfield.
Akikaririwa Rodgers amesema,
"nimeona hakuna shaka yoyote kuwa ulikuwa ni mpira wa mkono, nadhani walichokiona waamuzi ni kuwa haikuwa makusudi, na ni wazi kabisa haikuwa makusudi.
"nilimuuliza mwamuzi wa akiba baada ya mchezo kama ulikuwa ni mpira wa mkono kwa kuwa sikuona moja kwa moja alinijibu ni kweli. Kwa hiyo ni wazi ilikuwa bahati mbaya kwa Mansfield na bahati kwetu kupata goli."

MASHALI KUTETEA UBINGWA WA AFRIKA MASHARIKI.


Mabondia nane wanatarajiwa kupambana katika mapambano ya utangulizi katika mpambano wa kutetea Ubingwa wa afrikia mashariki na kati kati ya Mtanzania Thomas Mashali na Bernad Mackoliech wa Kenya katika ukumbi wa Friends Corner Manzese Januari 12 siku ya Mapinduzi.Akizingumza na Waandishi wa habari mratibu wa pambano hilo Aisha Mbegu aliwataja mabondia hao kuwa ni Amadu Mwalimu atakayepambana na Cosmas Chibuga Bakari Dunda na Godfrey Pancho, Shadrack Juma na Nasoro Juma wakati Abdul Awilo atapambana na Six Juma.“ Tumueamua kuwa na mapambano machache ya utangulizi ili kutoa fursa kwa watu kuangalia mapema pambano amabalo linasubiriwa kwa hamu na mashabiki wengi kutokana na tambo za Mashali kuahidi ushindi kwa K.O, aslisema Aisha.Aisha alisema mapamnabo ya utangul;izi yatakuwa ya raundi nne na mpaka sasa maandalizi yako vizuri na Mashali amesharejea Jijini Dar es salaam na anaendelea na mazoezi kwa ajili ya pambano hilo litakalofanyika siku ya Mapinduzi.Kwa upande wake rais wa TPBO Yaasin Abdalah alisema maandalizi yamekamilika na Tiketi kwa Ajili ya bondia mackoliech na kocha wake imeshatumwa na kupokelewa kinachosubiriwa ni wao kuwasili nchini kwa ajili ya pambano.Bondia Thomas Mashali anatetea ubingwa huo alioupata Oktoba 14 baada ya kumpiga bondia Medi Sebyala wa Uganda kwa pointi katika Ukumbi wa Friends Corner Manzese.

UNITED BADO YAMFUKUZIA ZAHA KIMYAKIMYA.


KLABU ya Manchester United bado inajiamini kwamba itamsajili kinda wa klabu ya Crystal Palace Wilfried Zaha pamoja na Tottenham Hotspurs kutangaza dau la kumyakuwa nyota huyo. Tottenham tayari wameshaanza mazungumzo na Palace kwa ajili ya uhamisho wa kinda huyo ambaye ana thamani inayofikia paundi milioni 20. Hata hivyo meneja wa Palace Ian Holloway ameonyesha wasiwasi kuwa kiwango cha Zaha hivi sasa kinaathiriwa na tetesi za usajili ambapo vilabu vikubwa vimekuwa vikipigana vikumbo kutaka saini yake. Meneja wa Tottenham Andre Villas-Boas ameonyesha kuwa tayari kumsajili kinda huyo na kisha kumruhusu kuendelea kucheza kwa mkopo kama klabu hiyo inavyotaka. Kwasasa meneja wa United Sir Alex Ferguson anatafuta nafasi ya kuzungumza ana kwa ana na Zaha ili aweze kumshawishi kutua katika klabu hiyo akiamini kuwa atamsaidia kinda huyo mwenye miaka 20 ili aweze kuwa tishio hapo baadae

YADAIWA FERGIE ANASAKA KIPA MPYA!!

>>WALENGWA NI BEGOVIC & REINA!
FERGUSON_KUBADILI_KIPA_KILA_MECHIGAZETI la Uingereza, The Mirror, limeripoti kuwa Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson anafikiria kumpiga shoka David De Gea na kusaka Kipa mpya katika kipindi hiki cha Dirisha la Uhamisho la Mwezi Januari.BEGOVIC_n_REINA
Gazeti hilo limedai Sir Alex Ferguson amezidi kuvunjwa moyo na uchezaji wa Kipa De Gea ambae anashindwa kudhibiti eneo la Penati Boksi na mara nyingi huonekana mwenye mchecheto katika eneo hilo, hasa kwa mipira ya juu ya frikiki na kona, ambayo wapinzani wamechukulia hilo kama ni udhaifu wa Manchester United.
The Mirror limedai kuwa Ferguson amemwomba Mkurugenzi Mtendaji, David Gill, pamoja na Wamiliki wa Klabu, Familia ya Glazers, kutoa Fedha ili kumnunua Kipa ambae ataruhusiwa kuichezea Man United kwenye Mashindano ya UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu huu.
Tangu atue Man United kutokea Atletico Madrid Mwaka 2011, De Gea amekuwa hana namba ya kudumu na mara nyingi amekuwa akibadilishana na Kipa mwingine, Anders Lindegaard, kutoka Denmark.
Ripoti za Gazeti hilo zimedai walengwa wa Sir Alex Ferguson ni Makipa wa Stoke City, Asmir Begovic, na yule wa Liverpool, Pepe Reina, kwani wote wataruhusiwa kuichezea Man United kwenye Mashindano ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Hata hivyo, kumng’oa Begovic kutoka Stoke City itakuwa kazi kubwa kwani yeye ndie moja ya nguzo kubwa Klabuni hapo lakini duru hizo za habari zimekiri kumpata Reina ni rahisi kidogo maana inaonekana sasa Liverpool inatafuta mwelekeo mwingine kuhusu Kipa.

DIRISHA la UHAMISHO JANUARI: NANI KENDA WAPI HADI SASA!

DEMBA_BA-ATUA_CHELSEADIRISHA la UHAMISHO la Mwezi Januari lipo wazi na litabaki wazi hadi Januari 31 Saa 8 Usiku, Bongo Taimu, na ifuatayo ni Listi ya Klabu kwa Klabu za Ligi Kuu England kuhusu Wachezaji waliochukuliwa na wale waliohama.
**FAHAMU: LISTI HII ITAKUWA IKIREKEBISHWA MARA KWA MARA KADRI UHAMISHO UNAVYOFANYIKA
ARSENAL
WALIOINGIA: Hamna
WALIOONDOKA:
4 Jan: Marouane Chamakh (West Ham United)- MKOPO 
6 Jan: Johan Djourou (Hannover 96) MKOPO
ASTON VILLA
WALIOINGIA: Hamna
WALIOONDOKA: Hamna
CHELSEA
WALIOINGIA: 
4 Jan: Demba Ba (Newcastle) ADA HAIKUTAJWA
WALIOONDOKA: 
2 Jan: Daniel Sturridge (Liverpool) ADA HAIKUTAJWA
EVERTON
WALIOINGIA: Hamna
WALIOONDOKA: Hamna
FULHAM
WALIOINGIA: Hamna
WALIOONDOKA: Hamna
LIVERPOOL
WALIOINGIA:
2 Jan: Daniel Sturridge (Chelsea) ADA HAIKUTAJWA
WALIOONDOKA:
4 Jan: Joe Cole (West Ham United) BURE
MANCHESTER CITY
WALIOINGIA: Hamna
WALIOONDOKA: Hamna
MANCHESTER UNITED
WALIOINGIA Hamna
WALIOONDOKA:
3 Jan: Bebe (Rio Ave) MKOPO
2 Jan: Angelo Henriquez (Manchester United) MKOPO
2 Jan: Joshua King (Blackburn Rovers) ADA HAIKUTAJWA
NEWCASTLE UNITED
WALIOINGIA:
4 Jan: Mathieu Debuchy (Lille) ADA HAIKUTAJWA
WALIOONDOKA: Hamna
Norwich City
WALIOINGIA: Hamna
WALIOONDOKA: Hamna
QUEENS PARK RANGERS
WALIOINGIA:
4 Jan: Tal Ben Haim (Hana Klabu) BURE
WALIOONDOKA: Hamna
READING
WALIOINGIA:
1 Jan: Daniel Carrico (Sporting Lisbon) ADA HAIKUTAJWA
WALIOONDOKA: Hamna
SOUTHAMPTON
WALIOINGIA: Hamna
WALIOONDOKA: Hamna
STOKE CITY
WALIOINGIA: Hamna
WALIOONDOKA: Hamna
SUNDERLAND
WALIOINGIA: Hamna
WALIOONDOKA:
1 Jan: Ji Dong-won (Augsburg) MKOPO
SWANSEA CITY
WALIOINGIA: Hamna
WALIOONDOKA: Hamna
TOTTENHAM HOTSPUR
WALIOINGIA: 
3 Jan: Ezekiel Fryers (Standard Liege) ADA HAIKUTAJWA
WALIOONDOKA:
1 Jan: Carlo Cudicini (LA Galaxy) ADA HAIKUTAJWA
WEST BROMWICH ALBION
WALIOINGIA: Hamna
WALIOONDOKA: Hamna
WEST HAM UNITED
WALIOINGIA:
4 Jan: Marouane Chamakh (Arsenal) MKOPO 
4 Jan: Joe Cole (Liverpool) BURE 
3 Jan: Sean Maguire (Waterford United) ADA HAIKUTAJWA
WALIOONDOKA:
WIGAN ATHLETIC
WALIOINGIA:
1 Jan: Roger Espanoza (Sporting Kansas City) BURE 
2 Jan: Angelo Henriquez (Manchester United) MKOPO
WALIOONDOKA: Hamna

MIEMBENI YAITUPA NJE COASTAL UNION KOMBE LA MAPINDUZI


Kikosi cha Miembeni
TIMU ya Coastal Union ya Tanga imetolewa katika mashindano ya Kombe la Mapinduzi, baada ya sare ya bila kufungana na Miembani FC jioni hii kwenye Uwanja wa Mao Dze Tung, Zanzibar.
Matokeo hayo yanaifanya Miembeni isubiri hatima yake ya kuingia Nusu Fainali katika mchezo wa usiku wa leo kati ya Mtibwa Sugar na Azam FC Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Miembeni sasa ina pointi nne, baada ya kumaliza mechi zake tatu ikiwa katika nafasi ya pili, nyuma ya Azam inayoongoza Kundi A kwa pointi nne pia na wastani mzuri wa mabao.
Timu tatu sasa zina nafasi ya kuingia Nusu Fainali, Miembeni yenye pointi nne sawa na Azam na Mtibwa Sugar ambayo ikiwa na pointi moja hivi sasa, ikishinda usiku itatimiza pointi nne na mustakabali wake wa kusonga mbele utatazamwa kutokana na wastani wake wa mabao.  
Tayari kutoka Kundi A, mabingwa wa Kenya, Tusker FC wamefuzu kama vinara wa kundi hilo, wakati Simba SC, mabingwa wa Bara wamefuzu kama washindi wa pili.
Mshindi wa kwanza wa Kundi A atamenyana na mshindi wa pili wa Kundi B katika Nusu Fainali, wakati mshindi wa kwanza wa Kundi B atamenyana na mshindi wa pili wa Kundi A.

YAYA TOURE ALAZWA HOSPITALI


Football | Afcon

Yaya Toure hospitalised in Abu Dhabi


Reigning African Footballer of the Year Yaya Toure is currently receiving treatment for cough and fever at a clinic in Abu Dhabi where Ivory Coast are fine tuning for the upcoming Africa Cup of Nations.
The Ivorian delegation arrived in the United Arab Emirates capital on Saturday from Paris, where the group joined officials from Abidjan before their final trip.
Toure was exempted from their inaugural training session on Sunday, while the team’s medical staff said all hands were on deck to restore the player’s health but refused to say when he would probably be fit to return to training.
The Elephants opened workshop on Sunday afternoon at the Mohammed Bin Zayed Stadium under the direction of coach Sabri Lamouchi, who said he was confident of his outfit’s experience and improvisation but that the players’ physical form was worrisome.
Team captain Didier Drogba was excused from the session after he suffered a light headache, which Lamouchi said played down on when the group returned to their Rocco Forte Hotel at the end of the session.
Ivory Coast will play a friendly match against Egypt on January 14 before flying to South Africa two days later for the showpiece set for kick off on January 19.

TOURE APATIWA MATIBABU ABU DHABI.


57247935.jpgMCHEZAJI bora wa mwaka wa Afrika Yaya Toure anapatiwa matibabu ya homa na kifua katika kliniki moja jijini Abu Dhabi ambapo timu ya taifa ya Ivory Coast imeweka kambi kwa ajili ya michuano ya Mataifa ya Afrika. Wachezaji wa timu ya taifa ya nchi hiyo waliwasili katika mji mkuu huo wa Umoja wa Falme za Kiarabu-UAE Jumamosi wakitokea Ufaransa ambapo walijiunga na maofisa kutoka Abidjan kabla ya safari yao ya mwisho kuelekea nchini Afrika Kusini kwa ajili ya michuano hiyo. Toure hakuonekana katika mazoezi ya timu hiyo jana wakati timu ya madaktari wa timu hiyo wakijaribu kuhakikisha afya ya nyota huyo inatengemaa ingawa haijajulikana ni muda gani atarejea mazoezini na wenzake. Ivory Coast ilianza mazoezi rasmi kwa ajili ya kujiandaa na michuano hiyo katika Uwanja wa Mohammed Bin Zayed chini ya kocha Sabri Lamouchi ambaye ana matumaini makubwa ya kufanya vizuri kutokana na uzoefu wa wachezaji alionao. Kabla ya michuano hiyo Ivory Coast inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Misri Januari 14 kabla ya kusafiri kuelekea nchini Afrika Kusini siku mbili baadae.

MAPAMBANO BADO HAYAJAISHA - VILANOVA

.

MENEJA wa klabu ya Barcelona, Tito Vilanova amekiri kuwa mapambano yake dhidi ya ugonjwa wa kansa unaomsumbua bado hayajaisha na kwamba anaweza kupumzika tena kuinoa timu hiyo kwa ajili ya matibabu. Vilanova mwenye umri wa miaka 44 alifanyiwa upasuaji kwa mara ya pili kuondoa uvimbe wa kansa katika koo lake Desemba 20 mwaka jana. Kocha huyo alikosa mchezo wa ugenini dhidi ya Valladolid lakini alirejea jana wakati Barcelona ilipopata ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya Espanyol ambao umeifanya kung’ang’ania kileleni kwa tofauti ya alama 11 dhidi ya Atletico Madrid ambao wanashika nafasi ya pili. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Vilanova amesema vita anavyopambana na ugonjwa huo bado kwani kuna siku ambazo hataweza kuhudhuria mazoezini na shughuli nyingine lakini aliwaomba watu wa habari kujua kwamba ugonjwa huo ni wake na jambo binafsi hata kama yeye ni maarufu. Kocha huyo pia alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wote ambao wameonyesha kuwa pamoja naye katika kipindi chote toka alipogundulika kuwa na ugonjwa huo wakiwemo wachezaji, viongozi na mashabiki wa klabu hiyo.

MESSI, RONALDO, INIESTA NANI ATASHINDA BALLON D'OR LEO?


MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo, mshambuliaji nyota
Nani atatwaa tuzo ya FIFA Ballon d'Or leo?
Barcelona Lionel Messi na Andres Iniesta ni miongoni mwa majina ya wachezaji watatu ambao wanagombea tuzo ya mchezaji bora wa dunia kwa mwaka 2012 maarufu kama Ballon d’Or. Majina hayo matatu ya wachezaji hao yalichujwa kutoka majina 23 yaliyoteuliwa na kamati ya Shirikisho la Soka Duniani ambapo yalipigiwa kura na makocha na manahodha wa timu za taifa ambao ni wajumbe wa FIFA. Baada ya mchujo huo ndio yakachomoza majina ya nyota hao watatu ambao leo usiku katika sherehe zitakazofanyika jijini Zurich, Switzerland mmoja wapo atanyakuwa tuzo hiyo huku jina Messi likipewa kipaumbele ili kuibuka na kidedea. Kama Messi ambaye ni raia wa Argentina akiibuka kidedea atakuwa ameweka historia ya kuwa mchezaji wa kwanza kunyakuwa tuzo hiyo mara nne mfululizo. Nyota wengine waliowahi kunyakuwa tuzo hiyo mara nyingi ni pamoja na Ronaldo de Lima na Zinedine Zidane ambao wote kwa pamoja wamenyakuwa tuzo hiyo mara tatu kila mmoja lakini katika vipindi tofauti.

YANGA WAPIGA MECHI NYINGINE NA TIMU LA ULAYA KESHO


Yanga SC
Timu ya Young Africans Sports  Club kesho itashuka dimbani kucheza na timu ya Denizlispor FC ya ligi daraja la kwanza nchini Uturuki katika mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu utakaofanyika katika uwanja wa Selen Football -Kalimya Complex pembeni kidogo ya mji wa Antlaya.
Young Africans ambayo imeweka kambi ya mafunzo jijini Antalya itatumia mchezo huo kama fursa ya kujipima nguvu na timu hiyo la Denizlispor FC  ambayo imeshuka kutoka ligi kuu ya Uturuki mwaka jana na hivi sasa inapamabana kurudi tena katika Ligi Kuu ya Uturuki.
Kocha Mkuu wa Young Africans Ernest Brandts amesema kwao ni furaha kupata nafasi ya kucheza na timu kubwa kama ya Denizlispor FC ambayo ina wachezaji wa kiwango cha kimataifa hivyo anaamini utakua ni mchezo safi na kuwavutia.
Baada ya kuwa na wiki moja ya mazoezi na mechi moja ya kirafiki dhidi ya Armini Bielefeld ya ujerumani mwishoni mwa wiki itakua ni fursa nyingine nzuri ya kucheza mchezo wa kirafiki na timu nyingine, hii itanisadia kuona maendeleo ya kikosi changu kutokana na mazoezi ambayo tumekuwa tukiyafanya tangu tulipofika alisema 'Brandts'
Denizlispor FC ni miongoni mwa timu zaidi ya 200 kutoka shemu tofauti duniani ambazo zimeweka kambi katika mji wa Antlaya kwa ajili ya maandilizi ya mzunguko wa pili wa Ligi Daraja la kwanza nchini Uturuki.
Mchezaji wa zamani wa Leicester City ya Uingereza, Dundee United ya Scotland na Ivernes ya Uholanzi, mtanzania mzaliwa wa Uingereza Eric Odhiambo ni miongoni mwa washambuliaji wa kutegemewa wa timu ya Denizlispor FC.
Young Africans imeendelea na mazoezi katika viwanja wa Fame Residecne tayari kabisa kujiandaa na mchezo huo utakaochezwa kesho katika uwanja wa Selen Football - Kalimya complex pemebeni kidogo ya mji wa Antalya.
Kikosi cha wachezaji 27 waliopo mjini Antalya wote wako katika hali nzuri na hakuna maheruhi hata mmoja hali itakayompa kocha Brandts kuamua kumtumia mchezaji yoyote katika mchezo huo.
Athumani Idd 'Chuji' na Hamis Kiiza waliokuwa wakijisikia vibaya kabla ya mchezo wa juzi dhidi ya Amrnini Bielefeld wanaendelea vizrui kabisa kwani wanaendelea na mazoezi pamoja na wachezaji wengine waliopo na timu mjini Antalya.
Kuhusu hali ya hewa leo haijaonekana kuwa tatizo kwa wachezaji kwani wanaonekana kuimudu na mda mwingi kwa sasa kumekua na jua linalowaka kuanzia asubuhu wakati wa mazoezi mpaka mida ya jioni, kwa leo hali ya hewa ni nyuzi joto 17 - 21, hivyo hali ya hewa ni nzuri tu.

SAFARI YA SIMBA SC OMAN BADO SI UHAKIKA


Simba SC ya Mapinduzi Cup
JAPOKUWA imepanga kuondoka Jumatano kwenda Oman kwa ziara ya wiki mbili, lakini hadi unaposoma habari hii, Simba SC haijapokea tiketi za safari hiyo kutoka kwa wenyeji wao, klabu ya Fanja ya huko.
Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesema mchana huu kwamba, wanasubiri kutumiwa tiketi na wenyeji wao hao ndipo watangaze rasmi ziara hiyo ya Oman.
Kikosi cha Simba kwa sasa kipo visiwani hapa kikishiriki Kombe la Mapinduzi na tayari kimefuzu hatua ya Nusu Fainali.
Mapema leo, BIN ZUBEIRY ilimnukuu Kocha Mkuu wa Simba SC, Mfaransa Patrick Liewig akisema anataka kwenda Oman na kikosi kamili ili aweze kuwajua wachezaji wote na kuweza kuipanga vyema timu yake.
Kuhusu wachezaji wa timu ya taifa, ambayo Januari 11 itacheza mchezo wa kirafiki na Ethiopia, Liewig alisema suala hilo linashughulikiwa na viongozi wa klabu hiyo. “Najua viongozi walikuwa wana kikao na viongozi wa shirikisho (TFF).
Sijui wamekubaliana vipi, lakini naweza kuwavumilia wachezaji hao wajiunge na timu Oman baada ya mechi na Ethiopia,”alisema.
Simba jana ilifuzu Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi, licha ya kutoka sare ya 1-1 na Bandari ya hapa katika mchezo wa mwisho wa Kundi A, kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Hadi mapumziko, timu hizo zilikuwa zimekwishafungana bao 1-1, Bandari wakitangulia kupata bao kwa penalti, mfungaji Haitham Juma dakika ya sita kabla ya Kiggi Makassy kuisawazishia Simba SC dakika ya 16.
Refa aliwapa penalti Bandari baada ya Haruna Shamte kumchezea rafu Fauzi Ally katika eneo la hatari na Haitham akaenda kupiga penalti, ambayo ilipanguliwa na kipa Dhaira na mpira kumkuta tena mpigaji, aliyeukwamisha nyavuni.
Kiggi alifunga kwa mpira wa adhabu kutoka upande wa kulia wa Uwanja, umbali wa mita 20, baada ya Abdallah Seseme kuangushwa.    
Kipindi cha pili, Simba walianza kwa kuimarisha kwa kikosi chao wakiwaingiza kwa mpigo, Mwinyi Kazimoto, Haruna Chanongo na Jonas Mkude kuchukua nafasi za Mussa Mude, Salim Kinje na Ramadhani Singano ‘Messi’, wakati Bandari walimtoa kipa wao Hassan Hajji na kumuingiza Ahmad Suleiman.
Kwa matokeo hayo, Simba SC imeungana na Tusker ya Kenya kufuzu Nusu Fainali ya michuano hiyo. Tusker ni kinara wa kundi kwa pointi zake saba na Simba imeingia kama mshindi wa pili kwa pointi zake tano.
Wachezaji wa Simba SC walioitwa Stars ni kipa Juma Kaseja, mabeki Amir Maftah na Shomari Kapombe, viungo Amri Kiemba na Mwinyi Kazimoto na mshambuliaji Mrisho Ngasa.
Katika wachezaji wote hao walioitwa Stars, walio kwenye kikosi cha Simba kinachocheza Kombe la Mapinduzi ni Kapombe na Mwinyi Kazimoto pekee. Kaseja, Ngassa, Kiemba ni majeruhi, wakati Amir Maftah imeelezwa ana madai yake anayosubiri alipwe ndipo ajiunge na timu.  

STARS KAMBINI BILA WAKALI WA YANGA


Kim Poulsen
TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars itakayocheza mechi ya kujipima nguvu na Ethiopia Januari 11, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Addis Ababa, Ethiopia inatarajiwa kuingia kambini leo mjini Dar es Salaam kujiandaa na mechi hiyo.
Stars chini ya Kocha Mkuu Mdenmark, Kim Poulsen, itakuwa na timu ya mwisho kucheza na Ethiopia kabla ya Wahabeshi hao kwenda Afrika Kusini kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) zitakazoanza Januari 19 mwaka huu.
Ethiopia iko kundi C pamoja na mabingwa watetezi Zambia, Nigeria na Burkina Faso. Ethiopia itacheza mechi yake ya kwanza Januari 21 mwaka huu dhidi ya Zambia.
Katika mechi yake ya mwisho, Taifa Stars iliifunga Zambia bao 1-0 katika mchezo wa kirafiki uliofanyika Desemba 22 mwaka jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo ya kirafiki dhidi ya Ethiopia ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya mchujo dhidi ya Morocco kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia 2014. Mechi hiyo itachezwa Machi mwaka huu.
Wachezaji wanaotakiwa kambini ni Juma Kaseja kutoka Simba ambaye pia ndiye nahodha wa Stars, Aishi Manula na Mwadini Ally wote kutoka Azam. Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga) na Shomari Kapombe (Simba).
Viungo ni Salum Abubakar (Azam), Athuman Idd (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Khamis Mcha (Azam), Frank Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar).
Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba), Simon Msuva (Yanga), na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
Wakati benchi la Ufundi lina Kim, Sylvester Marsh (Kocha Msaidizi), Juma Pondamali (Kocha wa makipa), Leopold Tasso (Meneja), Dk. Mwanandi Mwankemwa (Daktari wa timu), Frank Mhonda (Mtaalamu wa tibamaungo) na Alfred Chimela (Mtunza vifaa).
Hata hivyo, kocha Poulsen atawakosa wachezaji wa Yanga, Kevin Yondani, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Athuman Idd ‘Chuji’, Frank Domayo na Simon Msuva ambao wapo na timu yao Uturuki.

AZAM, COASTAL NA MTIBWA ZAWANIA NUSU FAINALI MAPINDUZI LEO


Mabingwa watetezi Azam, watafuzu?

TIMU mbili zitakazokamilisha idadi ya timu za kucheza hatua ya Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi, zinatarajiwa kujulikana leo, wakati mechi mbili kali zitakapopigwa kwenye viwanja viwili tofauti visiwani hapa leo.
Coastal Union ya Tanga inayoshiriki michuano hii kwa mara ya kwanza, itaanza kumenyana na Miembeni kwenye Uwanja wa Mao Dze Tung saa 10:30 jioni, kabla ya mabingwa watetezi kupambana na mabingwa wa zamani wa michuano hii, Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Amaan, kuanzia saa 2:30 usiku wa leo.
Azam ndio inaongoza Kundi B kwa pointi zake nne, wakifuatiwa na Miembeni wenye pointi tatu, Coastal pointi mbili na Mtibwa yenye pointi moja inashika mkia.
Iwapo Mtibwa itaifunga Azam na Coastal itatoka sare, timu hiyo ya Manungu itaangaliwa mustakabali wake wa kufuzu Nusu Fainali kwa kulinganishwa wastani wake wa mabao na Miembeni.
Coastal wakishinda wanaweza kufuzu moja kwa moja hata kama Mtibwa ikiifunga Azam, kwani watafikisha pointi tano.
Kwa ujumla, hadi sasa timu yoyote kati ya zote nne za Kundi B inaweza kufuzu Nusu Fainali na hii inamaanisha hili ndilo lilikuwa Kundi la kifo. 

BEKI MREFU KULIKO WOTE AFRIKA MASHARIKI SHIKOKOTI ASEMA KOMBE LA MAPINDUZI NI LA TUSKER TU



NAHODHA wa Tusker, Joseph Shikokoti amesema kwamba haoni timu ya kuwazuia kutwaa Kombe la Mapinduzi, michuano inayoendelea visiwani hapa.
Akizungumza jana, Shikokoti aliyewahi kuchezea Yanga alisema kwamba anafahamu Simba na Azam ni wazuri na anajua mojawapo watakutana nayo fainali, lakini amesistiza hakuna kati yao inayoweza kuwazuia wasitwae Kombe.
“Hili Kombe letu, tumeona uwezo wa timu zote, hata Simba na Azam ni wazuri, lakini tutawafunga wote tukikutana nao, hawana uwezo wa kutuzuia,”alisema Shikokoti.
Tusker, mabingwa wa Kenya, jana jioni walikuwa timu ya kwanza kufuzu Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi, baada ya kuilaza Jamhuri ya Pemba bao 1-0, lililofungwa na mshambuliaji wake hatari, Jesse Were dakika ya 23 kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Ushindi huo, umewafanya wababe hao wa soka ya Kenya wamalize mechi zao za Kundi A wakiwa na pointi saba, wakifuatiwa na Simba SC iliyomaliza na pointi tano.
Jamhuri iliyomaliza na pointi tatu na Bandari ambayo imeambulia pointi moja, zimeaga mashindano haya. Simba na Tusker zinasubiri mechi za leo za mwisho za Kundi B ili kujua wapinzani wao katika Nusu Fainali.

SIMBA A YAJITOA KOMBE LA MAPINDUZI LICHA YA KUTINGA NUSU FAINALI


Kikosi cha Simba kilichotinga Nusu Fainali jana

PAMOJA na kufuzu hatua ya Nusu Fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi jana, Simba SC italazimika kuiachia timu yao ya pili, maarufu kama Simba B iendelee na michuano hiyo hata kama ikiingia fainali, ili kikosi cha kwanza kiende Oman keshokutwa.
Kocha Mkuu wa Simba SC, Mfaransa Patrick Liewig alisema  jana kwamba, anataka kwenda Oman na kikosi kamili ili aweze kuwajua wachezaji wote na kuweza kuipanga vyema timu yake.
Kuhusu wachezaji wa timu ya taifa, ambayo Januari 11 itacheza mchezo wa kirafiki na Ethiopia, Liewig alisema suala hilo linashughulikiwa na viongozi wa klabu hiyo. “Najua viongozi walikuwa wana kikao na viongozi wa shirikisho (TFF).
Sijui wamekubaliana vipi, lakini naweza kuwavumilia wachezaji hao wajiunge na timu Oman baada ya mechi na Ethiopia,”alisema.
Simba jana ilifuzu Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi, licha ya kutoka sare ya 1-1 na Bandari ya hapa katika mchezo wa mwisho wa Kundi A, kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Hadi mapumziko, timu hizo zilikuwa zimekwishafungana bao 1-1, Bandari wakitangulia kupata bao kwa penalti, mfungaji Haitham Juma dakika ya sita kabla ya Kiggi Makassy kuisawazishia Simba SC dakika ya 16.
Refa aliwapa penalti Bandari baada ya Haruna Shamte kumchezea rafu Fauzi Ally katika eneo la hatari na Haitham akaenda kupiga penalti, ambayo ilipanguliwa na kipa Dhaira na mpira kumkuta tena mpigaji, aliyeukwamisha nyavuni.
Kiggi alifunga kwa mpira wa adhabu kutoka upande wa kulia wa Uwanja, umbali wa mita 20, baada ya Abdallah Seseme kuangushwa.    
Kipindi cha pili, Simba walianza kwa kuimarisha kwa kikosi chao wakiwaingiza kwa mpigo, Mwinyi Kazimoto, Haruna Chanongo na Jonas Mkude kuchukua nafasi za Mussa Mude, Salim Kinje na Ramadhani Singano ‘Messi’, wakati Bandari walimtoa kipa wao Hassan Hajji na kumuingiza Ahmad Suleiman.
Kwa matokeo hayo, Simba SC imeungana na Tusker ya Kenya kufuzu Nusu Fainali ya michuano hiyo. Tusker ni kinara wa kundi kwa pointi zake saba na Simba imeingia kama mshindi wa pili kwa pointi zake tano.
Wachezaji wa Simba SC walioitwa Stars ni kipa Juma Kaseja, mabeki Amir Maftah na Shomari Kapombe, viungo Amri Kiemba na Mwinyi Kazimoto na mshambuliaji Mrisho Ngasa.
Katika wachezaji wote hao walioitwa Stars, walio kwenye kikosi cha Simba kinachocheza Kombe la Mapinduzi ni Kapombe na Mwinyi Kazimoto pekee. Kaseja, Ngassa, Kiemba ni majeruhi, wakati Amir Maftah imeelezwa ana madai yake anayosubiri alipwe ndipo ajiunge na timu.  

SIMBA FANS YAPASULIWA 7 - 3 NA YANGA FANS!!

>>RIPOTI NA Mpeli Jr Ngonywike [Yanga Team Manager]
YANGA_MTANDAONITimu ya Soka ya Mashabiki wa Yanga wa Mtandaoni, Yanga Facebook Fans, jana January 6, 2013 waliipasua timu ya Simba wa Mtandaoni, Simba Facebook Fans, Mabao 7 - 3 katika mchezo mkali wa Bonanza uliofanyika Viwanja vya Airwing, Ukonga Jijini Dar es Salaam.SIMBA_MTANDAONI
Katika mchezo huo, Yanga waliizidi Simba kila idara hali iliyopelekea mchezo kuwa Mabao 5 - 1 mpaka mapumziko.
Pia katika mchezo huo Simba walipata penati mbili na zote walikosa.
Walipata penati ya kwanza na mpigaji wao akakosa lakini YANGA_MTANDAONI2Refa akaamuru irudiwe na kukosa tena kitu kilichomfanya huyo Mchezaji apandishe hasira na kuamua kumtukana Refa ambae alimzawadia Kadi Nyekundu.
Hata hivyo, Refa huyo alishindwa kumzawadia Kadi Nyekundu Mohamed Mashango wa Simba ambaye alimchezea rafu ya "Boban kwa Yondan" Mchezaji wa Yanga.
Yanga iliwakilishwa na  1.Juma Yakuti, 2. Harrison Chadema 3. Korroso Samwel 4.Mucky's Zayumba, 5.Hassan Msafiri, 6.Stanley Kulola, 7.Khalid Likhanga, 8.Valerian Lihega 9.Ombeni,  10.Osama Yanga na 11.Castor William
Magoli yao yalifungwa na Kulola, Harrison Chadema, Likhanga na Valerian Egitho aliyeingia kipindi cha pili.
Majina ya Simba hayakuweza kupatikana mara moja baada ya kusambaratika na kukataa kutoa ushirikiano baada ya mechi. Walitambulika wawili tu ambao ni Dulla Jane na Mohamed Mashango.
Picha zilizoambatanishwa ni vikosi vya timu zote mbili na jezi walizovaa Yanga zikionyesha kabisa ni Yanga FB Fans

MTOTO WA PELE ATEMWA KIKOSI CHA GHANA MATAIFA YA AFRIKA



Football | Afcon

Ayew © Action Images

Ghana drops Andre Ayew


Ghana coach Kwesi Appiah has dropped midfielder Andre Ayew from his squad for this month’s Africa Cup of Nations.
The French-based star got a hamstring injury in training last week and failed to meet Saturday’s deadline for players to report for Ghana’s pre-tournament training camp in Abu Dhabi.
A statement on the Ghana FA website read: “I have decided to exclude midfielder Andre Ayew from the Ghana squad for the 2013 African Cup of Nations.
“Following Andre’s inability to join the Black Stars squad by Monday morning for Ghana’s team doctors to assess the extent of his injury and fitness for the tournament, I have decided to work only with the players currently in camp.
“All the players were given the deadline of Saturday to report to camp in Abu Dhabi unfortunately Andre did not turn up despite being released by his club and air tickets provided by the GFA for him to travel from France to beat the deadline.
“As he did not turn up by Saturday night, I ordered for him to be contacted over his absence but he said he could not depart from France because he was seeing his doctors.
“The uncertainty over Andre’s fitness started when the GFA received a letter from his club side Marseille that he had had a hamstring injury so could not meet the GFA deadline of Saturday 5th January 2013 for reporting to camp in Abu Dhabi, UAE.
“In response the GFA wished the player a speedy recovery and requested him to report to camp by the Saturday 5th January 2013 deadline and submit himself to the medical team of the Black Stars for examination and if possible for treatment.
“The club wrote back to the GFA confirming it had released the player to join the Black Stars at its camp in Abu Dhabi on Saturday 5th January 2013.
“Unfortunately, Andre failed to report to camp and indicated that owing to the treatment he was receiving from his doctor he would report to camp on Wednesday 9th January 2013.
“He was further advised to endeavor to report to the camp by latest Monday 7th January 2013 because Wednesday 9th January 2013 was the deadline for submission of the list of 23 players to Caf.
“As Andre plans to arrive on Tuesday it means he would be unable to join any of my six training sessions before CAF’s Wednesday deadline for the submission of the final squad.
“In line with my vision of taking only fit players for the Africa Cup of Nations, I have decided that to work only with the players currently in camp.
“I have personally explained the rationale behind the decision to Andre and I will continue to count on him in future matches if he is fit.”

LIGI ULAYA: RONALDO AIOKOA REAL, BARCA HATARI, JUVE HOI!!

>>MESSI AANZA HESABU 2013 KWA PENATI, KIPA CASILLAS AANZA BENCHI!!
>>EDINSON CAVANI APIGA HETITRIKI, MFUNGAJI BORA SERIE A!!
BARCA_v_REALLIGI VIGOGO za Ulaya, Serie A na La Liga, Wikiendi zilirudi tena kilingeni na jana Jumapili huko Spain, Nyota Cristiano Ronaldo aliipigia Mtu 10 Real Madrid Bao 2 na kuipa ushindi wa 4-3 dhidi ya Real Sociedad huku vinara Barcelona wakizidi kupaa kwa kuichabanga Espanyol 4-0 katika Dabi ya Jiji la Barcelona lakini huko Italy vinara Juventus walishituliwa kwa kupigwa nyumbani Bao 2-1 na Sampdoria.
Ronaldo ainusuru Real!!
Jana Real Madrid, wakiwa kwao Santiago Bernabeu, walianza Mechi dhidi ya Real Sociedad huku Kipa Nambari Wani wa Spain, Iker Casillas, akianza Benchi kwa Mechi mbili mfululizo lakini ilibidi aingizwe baada ya Dakika 5 tu kufuatia kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu Kipa Adan Garrido na kuzaa Penati iliyoipa Real Sociedad Bao lao la kusawazisha baada ya Karim Benzema kuipa Real Bao la kuongoza katika Dakika ya Pili.
Katika Mechi hiyo Real Madrid walishinda Bao 4-3 na Bao nyingine kufungwa na Sami Khedira na mbili za Cristiano Ronaldo.
Bao zote 3 za Real Socied zilifungwa na Xabi Prieto.
Real Sociedad nao walimaliza Mtu 10 kufuatia Kadi Nyekundu kwa Daniel Estrada aliepewa Kadi za Njano mbili.
Huko Nou Camp, Bao 4 ndani ya Nusu Saa ya kwanza za Xavi, Pedro, Bao 2, na Messi, kwa Penati, ziliwapa Barcelona ushindi wa Bao 4-0 dhidi ya Espanyol kwenye Mechi ambayo ni Dabi ya Jiji la Barcelona.
Ushindi huo umewafanya Barcelona wafikishe Pointi 52 wakiwa Pointi 11 mbele ya Timu ya Pili Atletico Madrid na Pointi 16 mbele ya Timu ya 3, Real Madrid ambao ndio Mabingwa watetezi.
Juve yabondwa, Cavani apiga Hetitriki kuizamisha AS Roma
Mabingwa na vinara wa Serie A Juventus walipatwa mshtuko baada ya kuchapwa 2-1 Uwanjani kwao na Sampdoria na kuuanza Mwaka 2013 vibaya.
Juventus ndio walitangulia kufunga kwa Penati ya Sebastian Giovinco katika Dakika ya 24 lakini Bao mbili za Straika kutoka Argentina Emanuel Icardi, Dakika ya 52 na 68, ziliwapa Sampdoria ushindi wa Bao 2-1.
Licha ya kufungwa Juventus bado wako kileleni wakiwa na Pointi 44 zikiwa ni Pointi 5 mbele ya Timu ya Pili Lazio ambao Jumamosi waliifunga Cagliari 2-1.
Napoli wamepanda nafasi mbili hadi nafasi ya 3 baada ya kuichapa AS Roma 4-1 huku Straika wao kutoka Uruguay, Edinson Cavani, akipiga Hetitriki iliyomfanya aongoze katika Listi ya Mfungaji Bora akiwa na Bao 16 akifuatiwa na Mchezaji wa AC Milan, Stephan El Shaarawy, mwenye Bao 14.
SERIE A
MATOKEO:
Jumamosi Januari 5
Catania 0 Torino 0
Lazio 2 Cagliari 0
Jumapili Januari 6
AC Milan 2 Siena 1
Chievo Verona 1 Atalanta 0
Juventus 1 Sampdoria 2
Parma 2 Palermo 1
Udinese 3 Inter Milan 0
Napoli 4 AS Roma 1
Genoa 2 Bologna 0
Fiorentina 0 Pescara 2
LA LIGA
RATIBA/MATOKEO:
Ijumaa Januari 4
Real Zaragoza 1 Real Betis 2
Jumamosi Januari 5
Sevilla FC 1 Osasuna 0
Levante 3 Athletic de Bilbao 1
Granada CF 1 Valencia 2
Deportivo La Coruna 1 Malaga CF 0
Jumapili Januari 6
FC Barcelona 4 RCD Espanyol 0
Celta de Vigo 3 Real Valladolid 1
Real Mallorca 1 Atletico de Madrid 1
Real Madrid CF 4 Real Sociedad 3
Jumatatu Januari 7
Rayo Vallecano v Getafe CF