Wednesday, October 24, 2012

YANGA YAZIDI KUNG'ARA LIGI KUU, AZAM YABANWA NA RUVU CHAMAZI

Msuva kulia akishangilia na wenzake baada ya kufunga bao la kwanza. Kushoto ni Jerry Tegete na David Luhende


YANGA SC imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kuichapa Polisi Morogoro mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo, unaifanya Yanga itimize pointi 17, baada ya kucheza mechi tisa na kuendelea kusimama katika nafasi ya tatu, nyuma ya Azam FC yenye pointi 18, baada ya sare ya 1-1 na Ruvu Shooting Uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.   
Ruvu walipata bao lao kupitia kwa Seif Abdallah na Kipre Tcheche akaisawazishia Azam.
Uwanja wa Taifa, hadi mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa mabao 2-0 yaliyotiwa kimiani na washambuliaji Simon Msuva na Didier Kavumbangu.
Msuva alikuwa wa kwanza kuwainua vitini mashabiki wa Yanga dakika ya tano kabla ya dakika moja baadaye, Mrundi Kavumbangu naye kuwapa raha mashabiki wa timu hiyo.
Yanga ingekwenda kupumzika ikiwa inaongoza kwa mabao 3-0 kama mkwaju wa penalti wa Haruna Niyonzima usingegonga mwamba na kurudi uwanjani kabla ya mabeki wa Polisi kuondosha kwenye hatari.
Refa Alex Mahagi kutoka Mwanza alitoa penalti hiyo, baada ya Msuva kuangushwa na beki John Bosco kwenye eneo la hatari wakati anakwenda kufunga.    
Kipindi cha pili Yanga walirudi kwa kasi tena na kuendelea kulishambulia lango la Polisi, ingawa walipoteza nafasi nyingi na kutumia moja tu, dakika ya 58, mfungaji Hamisi Kiiza aliyeingia kuchukua nafasi ya Jerry Tegete.
Katika mechi nyingine za Ligi Kuu leo, Coastal Union iliifunga 1-0 African Lyon Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga, Mtibwa Sugar imelazimishwa sare ya 1-1 na Kagera Sugar Uwanja wa Manungu, Morogoro.
Matokeo ya leo yanaziweka karibu mno, Simba, Azam na Yanga pale juu, kiasi kwamba ushindani na uhondo wa ligi hiyo unaongezeka.
Katika mchezo wa leo, kikosi cha Yanga kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Shadrack Nsajigwa, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ (Nahodha), Mbuyu Twite, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Haruna Niyonzima/Nurdin Bakari, Jerry Tegete/Hamisi Kiiza, Didier Kavumbangu na David Luhende/Nizar Khalfan.
Polisi; Manji Kulwa/Kondo Salum, Nahodha Bakari, John Bosco, Noel Msakwa, Salmin Kissi, Hamisi Mamiwa, Bantu Admin/Paul John, Paschal Maige, Mokili Rambo (Nahodha), Malimi Busungu na Nicholas Kabipe/Keneth Masumbuko.
Katika mchezo wa awali wa utangulizi, Yanga B imeifunga TMK United ya Ligi Daraja la Pili, mabao 6-1 katika mchezo wa utangulizi kabla ya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kati ya Yanga na Polisi Morogoro.
Mabao ya Yanga yamefungwa na Georgeb Banda matatu katika dakika za 61, 70 na 72, Hussein Moshi dakika ya 12 na Rehani Rehani dakika ya 19 na 27, wakati la kufutia machozi la TMK United, lilifungwa na Abdi Hashimu dakika ya 62.

YANGA B 'WAITILIA UBANI' YANGA A TAIFA, WAPIGA MTU SITA

Yanga B imeifunga TMK United ya Ligi Daraja la Pili, mabao 6-1 katika mchezo wa utangulizi kabla ya mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kati ya Yanga na Polisi Morogoro. Mabao ya Yanga yamefungwa na Georgeb Banda matatu katika dakika za 61, 70 na 72, Hussein Moshi dakika ya 12 na Rehani Rehani dakika ya 19 na 27, wakati la kufutia machozi la TMK United, lilifungwa na Abdi Hashimu dakika ya 62. Tazama picha za mechi.
Abdulrahman Ally kulia akienda kuutoa mpira nyavuni baada ya George banda kushoto kufunga bao la sita

Kikosi cha Yanga B

George Banda kulia anawafunga tela mabeki wa TMK United 

Mchezaji wa yanga B akimtoka beki wa TMK

Kocha Mkuu wa Yanga B, Salvatory Edward kulia akiwa na Msaidizi wake Abubakar Salum

Wachezaji wa Yanga A, Mbuyu Twite, Haruna Niyonzjma, Ally Bart6hez na Nadir cannavaro wakishuhudia wadogo zao wanavyotoa adhabu

Okwi wa Yanga akivaa jezi kuingia dakika 10 za mwisho

BOBAN, NYOSSO WASIMAMISHWA SIMBA SC


Boban
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KLABU ya soka ya Simba inapenda kutoa taarifa zifuatazo kwenu siku ya leo.
1.    Kuhusu Boban na Nyoso
Wachezaji wawili wa Simba, Haruna Moshi Shaaban (Boban) na Juma Said Halfan (Nyoso), wamesimamishwa kuitumikia timu ya wakubwa (senior) kwa sababu na nyakati tofauti.
Moshi amesimamishwa kuichezea timu ya wakubwa kutokana na vitendo vya utovu wa nidhamu na kutokuwa na heshima kwa mwajiri (timu). Klabu imempa Haruna muda wa siku 21 kutoa maelezo kuhusu makosa yake na iwapo atashindwa kutoa maelezo ya kuridhisha, klabu inaweza kumchukulia hatua zaidi.
Katika kipindi hicho (siku 21 kuanzia jana), Boban atapokea nusu ya mshahara wake wa kila mwezi na hatapata marupurupu yoyote yanayohusiana na timu ya wakubwa.
Kwa upande wa Nyoso, uongozi umemwagiza afanye mazoezi na kikosi cha timu ya pili (Simba B) hadi hapo atakapoimarisha kiwango chake cha uchezaji.
Hatua hii imetokana na ripoti ya benchi la ufundi iliyoonyesha kwamba mchezaji huyo amekuwa akifanya makosa mengi ya kiuchezaji yanayoigharimu na ingawa amekuwa akipewa maelekezo na walimu, bado amekuwa akirudia makosa yaleyale.
Kutokana na hilo, Nyoso atafanya mazoezi na wachezaji wa kikosi cha pili hadi walimu watakaporidhika kwamba amejirekebisha na yuko tayari kutumikia kikosi cha wakubwa.
Katika muda wake wote huo akifanya mazoezi na timu B, Nyoso atakuwa akipata mshahara wake wa kila mwezi kama kawaida na pia atapata marupurupu wanayopata wachezaji wa Simba B.

Emmanuel Okwi
Klabu ya Simba inaeleza kusikitishwa kwake na taarifa za vyombo vya habari vyenye lengo la kuuza magazeti pasipo kujali athari za habari zenyewe.
Kwa mfano, habari ya kwenye gazeti la CHAMPIONI la leo ina kichwa cha habari KATIBU MKUU AMFUKUZA OKWI SIMBA. Hata hivyo, kilichoandikwa ndani ya habari yenyewe kinamnukuu aliyewahi kuwa Katibu Mkuu kwenye miaka ya nyuma.
Gazeti hilo linafahamu kabisa kwamba Simba ina Katibu Mkuu mmoja tu kwa sasa na anaitwa Evodius Mtawala. Simba haijawahi kuwa na makatibu wakuu wawili kwa wakati mmoja.
CHAMPIONI linafahamu ukweli huu lakini kwa sababu inazozijua lenyewe, imeamua kuandika habari hiyo na kuweka kichwa cha habari cha namna hiyo pasipo kujali athari zake kwa wanachama wa Simba, Katibu Mkuu aliyepo madarakani kwa sasa na weledi wa fani ya uandishi wa habari
Kilichoandikwa kwenye habari hiyo ya CHAMPIONI ni maoni binafsi ya mwanachama wa Simba na kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake kuhusiana na jambo lolote ali mradi halivunji sheria za nchi.
Simba SC inarudia wito wake wa kuvitaka vyombo kubaki kwenye misingi ya kitaaluma na kuacha kuandika habari zilizotiwa chumvi na kuleta mitafuruku isiyo na sababu yoyote.

Kikosi
Simba inaendelea vizuri na mazoezi visiwani Zanzibar kujiandaa na mechi dhidi ya Azam itakayopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi hii.
Hata hivyo, mchezaji Salim Kinje ameruhusiwa kuondoka kambini Zanzibar leo kutokana na kupata msiba wa baba yake mkubwa uliotokea Dar jana.
Uongozi, kwa namna ya kipekee kabisa, unatoa salamu za pole kwa familia ya Kinje kutokana na msiba huu.

Boniface Wambura
Kwa niaba yangu binafsi na klabu ya Simba, napenda kumpongeza Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Boniface Wambura, kwa kuteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuwa miongoni mwa wasimamizi wa shirikisho hilo katika michuano ya Wanawake itakayofanyika nchini Guinea ya Ikweta (Equatorial Guinea).
Wambura ndiye Mtanzania pekee aliyeteuliwa na CAF kutumika kwenye michuano hiyo na jambo hilo ni la faraja kwa tasnia ya habari nchini ambako Wambura ametokea.
Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga
Ofisa Habari
Simba SC

 

YANGA NA POLISI TAIFA, AZAM YAWANIA USUKANI CHAMAZI MBELE YA RUVU SHOOTING LEO

Yanga SC


LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea leo kwa mechi nne za raundi ya tisa huku Azam ikiusaka usukani wa ligi hiyo ikiwa mwenyeji wa Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Kipre Herman Tchetche, tegemeo la Azam
Mechi hiyo namba 60 ambayo kama Azam itashinda itafikisha pointi 20, hivyo kuwa kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom itakayochezwa Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam, viingilio vyake vitakuwa ni Sh. 3,000 kwa sh. 10,000.
Lakini macho na masikio ya wengi yatakuwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambao Yanga wataikaribisha Polisi Morogoro, wanaoshika mkia kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Katika mechi hiyo ambayo viingilio vitakuwa Sh. 5,000, Sh. 8,000, Sh. 15,000 na Sh. 20,000, refa Alex Mahagi kutoka Mwanza ndiye atakayepuliza filimbi kwenye mechi hiyo namba 62, akisaidiwa na Frank Komba na Michael Mkongwa, wote kutoka Iringa wakati mwamuzi msaidizi ni Oden Mbaga anayetambuliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) wa Dar es Salaam.
Katika mechi hiyo, Yanga itawakosa mabeki wake wa kati, Job Ibrahim, Kevin Yondan na mshambuliaji Said Bahanuzi ambao ni majeruhi.
Job, ambaye amekuwa beki wa akiba tangu mwanzoni mwa msimu, aliumia kifundo cha mguu mazoezini mwishoni mwa wiki na juzi hakufanya mazoezi kabisa, wakati Yondan na Bahanuzi wanaendelea na programu ya mazoezi mepesi, chini ya kocha Mholanzi, Ernie Brandts.
Kwa sababu hiyo, Mbuyu Twite ataendelea kucheza pamoja na Nadir Haroub ‘Cannavaro’ katika beki ya kati, wakati Jerry Tegete ataendelea kucheza na Didier Kavumbangu katika safu ya ushambuliaji.
‘Dogo’ Simon Msuva amemaliza adhabu ya kadi nyekundu aliyopewa Oktoba 3, mwaka huu katika mechi dhidi ya Simba na ilikuwa aanze kucheza tangu Jumamosi, ila kutokana na kiwango duni cha Hamisi Kiiza alichoonyesha kwenye mechi na Ruvu Shooting Jumamosi, leo kinda huyo anaweza kurudishwa uwanjani.
Kiiza aliichezea Yanga kwa mara ya kwanza siku hiyo akitokea benchi kipindi cha pili, tangu atolewe kipindi cha kwanza katika mechi dhidi ya Simba, Oktoba 3, mwaka huu. Kiiza alikuwa kwao, Uganda, alipokwenda kuichezea timu yake ya taifa, The Cranes katika mchezo wa marudiano wa kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani nchini Afrika Kusini.
Uganda ilitolewa na Zambia kwa mikwaju ya penalti baada ya sare ya jumla ya 1-1, Zambia wakianza kushinda nyumbani 1-0 na Uganda wakashinda kwao 1-0 pia mwishoni mwa wiki, hivyo mchezo kuhamia kwenye mikwaju ya penalti, ambako timu ya Kiiza ilitolewa.
Yanga imeweka kambi katika hoteli ya Uplands, Changanyikeni, Dar es Salaam huku ikiendelea kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa shule ya sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam.
Yondan aliyeumizwa na kiungo wa Simba, Haruna Moshi ‘Boban’ katika mechi baina ya wapinzani hao wa jadi, Oktoba 3, mwaka huu, wakati Bahanuzi ‘Spider Man’ alichanika nyama za paja la mguu wa kulia katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba Oktoba 8, mwaka huu.
Bahanuzi aliumia dakika ya 23, baada ya kugongana na beki Benjamin Effe wa Kagera Sugar na kushindwa kuendelea na mchezo, nafasi yake ikichukuliwa na Jerry Tegete katika mechi ambayo Yanga ililala 1-0, beo pekee la Themi Felix.
Bahanuzi ndiye tegemeo la mabao la Yanga kwa sasa, kwani tangu ajiunge na timu hiyo akitokea Mtibwa Sugar msimu huu, ameifungia mabao 12 katika mechi 13, ikiwemo ile dhidi ya Kagera aliyocheza kwa dakika 23 kabla ya kuumia na kutoka. 
Yanga kwa sasa inashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu kwa pointi zake 14, baada ya kucheza nane, kushinda nne, sare mbili na kufungwa mbili. Simba iliyocheza mechi tisa, inaongoza ligi hiyo kwa pointi zake 19, ikifuatiwa na Azam FC yenye pointi 17, iliyocheza mechi saba.
Kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga, wenyeji Coastal Union wataikaribisha African Lyon ya Dar es Salaam, wakati Mtibwa Sugar itaikaribisha Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Manungu ulioko kwenye mashamba ya miwa Turiani mkoani Morogoro.

LIGI DARAJA LA KWANZA BARA YAANZA KUTIMUA VUMBI LEO

Wachezaji wa Moro United wakimdhibiti mchezaji wa Simba (kushoto) katika mchezo wao wa kujipima nguvu kabla ya kuanza Ligi daraja la Kwanza wiki iliyopita. Moro inaanza na Villa Squad Mlandizi


LIG Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL) inatarajiwa kuanza kutimua vumbi leo kwenye viwanja mbalimbali nchini.
Kundi A kutakuwa na mechi tatu ambapo Burkina Faso itacheza na Mbeya City kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro wakati JKT Mlale itakuwa mwenyeji wa Small Kids kwenye Uwanja wa Majimaji, Songea.
Nayo Kurugenzi itaumana na Majimaji katika Uwanja wa Wambi ulioko Mufindi mkoani Iringa. Kundi hilo litamaliza raundi ya kwanza keshokutwa (Oktoba 25 mwaka huu) kwa mchezo kati ya Mkamba Rangers na Polisi Iringa utakaofanyika Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Mechi za kundi B kwa leo ni Ndanda dhidi ya Transit Camp katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara na Villa Squad itakipiga na Moro United kwenye Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi. Oktoba 25 mwaka huu ni Green Warriors v Tessema (Mabatini, Mlandizi) na Polisi Dar v Ashanti United (Uwanja wa Chamazi).
Kundi C leo ni Kanembwa FC v Polisi Dodoma (Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma), Mwadui v Morani (Kambarage, Shinyanga), Pamba vs Polisi Mara (Kirumba, Mwanza) na Rhino Rangers vs Polisi Tabora (Ali Hassan Mwinyi, Tabora).

AFCON 2013: Droo ya Makundi ya Fainali kufanyika Jumatano Oktoba 24 huko Durban!!



Chansa (left) seen here celebrating a goal with Zambian team mates at AFCON 2012 finals
>>UWEZEKANO ‘KUNDI la KIFO’ la Ivory Coast, Nigeria, Algeria au Morocco, na Congo DR!!
Droo ya kupanga Makundi manne ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2013, zitakazochezwa huko Afrika Kusini kuanzia Tarehe 19 Januari 2013 hadi 10 Februari 2013, itafanyika Jumatano Oktoba 24 huko Mjini Durban Afrika Kusini huku Timu 16 zilizo Fainali zimegawanywa katika Vyungu vinne ambapo kila Chungu kitatoa Timu moja kuunda Kundi moja la Timu 4 na Chungu Namba 1 kina Wenyeji Afrika Kusini, Mabingwa watetezi Zambia, Ghana na Ivory Coast.
++++++++++++++++++++++++++++++++
VYUNGU:
CHUNGU 1: South Africa, Zambia, Ghana, Ivory Coast
CHUNGU 2: Mali, Tunisia, Angola, Nigeria
CHUNGU 3: Algeria, Burkina Faso, Morocco, Niger
CHUNGU 4: Togo, Cape Verde, Congo DR, Ethiopia
FAHAMU: Kila Chungu kitatoa Timu moja ili kupata Makundi manne ya Timu 4 kila moja.
++++++++++++++++++++++++++++++++
Mgawanyo huu wa Vyungu umechukuliwa kwa kutathmini matokeo ya kila Nchi katika Mashindano matatu yaliyopita ya Kombe la Mataifa ya Afrika na si Ubora kwa mujibu wa Listi ya Ubora Duniani ya FIFA.
Lakini mgawanyo huu wa Vyungu unaweza kuleta ‘Kundi la Kifo’ la Nchi za Ivory Coast, Nigeria, Algeria au Morocco, na Congo DR.
Wakongwe Misri, waliowahi kuwa Mabingwa mara 7, na Cameroun, Mabingwa mara 4, hawamo kwenye Fainali hizi za AFCON 2013 baada ya kuzikosa kwa kutolewa kama vile walivyoikosa AFCON 2012.
Timu mpya pekee ni Cape Verde, waliowabwaga Cameroun, na zipo Timu 9, Zambia, Ivory Coast, Mali, Ghana, Tunisia, Burkina Faso, Morocco, Niger na Angola, ambazo zilicheza AFCON 2012 huko Gabon na Equatorial Guinea Januari Mwaka huu.
Mechi ya ufunguzi AFCON 2013 na Fainali zitachezwa Mjini Johannesburg na Mechi nyingine 29 zilizobaki zitapigwa katika Miji ya Durban, Nelspruit, Port Elizabeth na Rustenburg.

 

MABINGWA Chelsea CHALI, Man United yatoka nyuma 2-0 na kushinda!!


UEFA_CHAMPIONZ_LIGI_LOGO-BOMBAZ>>BARCA yapewa ushindi na ALBA Dakika za Majeruhi!
Mabingwa watetezi wa Ulaya, Chelsea, wamepigwa bao 2-1 ugenini na Shakhtar Donetsk na wenzao wa England, Manchester United, wakiwa kwao Old Trafford, walipindua uongozi wa Braga wa Bao 2-0 ndani ya Dakika 20 na kushinda 3-2 huku huko Nou Camp Celtic ilivunjwa moyo Dakika za majeruhi baada ya Jordi Alba kuifungia Barca bao la pili na kuwapa ushindi wa Bao 2-1.
MATOKEO:
Jumanne Oktoba 23
FC Nordsjælland 1 Juventus 1
FC Shakhtar Donetsk 2 Chelsea 1
FC BATE Borisov 0 Valencia 3
LOSC Lille 0 Bayern Munich 1
FC Spartak Moskva 2 SL Benfica 1
FC Barcelona 2 Celtic 1
Galatasaray 1 CFR 1907 Cluj 1
Manchester United 3 Braga 2
++++++++++++++++++++++++++++++
BARCELONA 2 CELTIC 1
Bao la Dakika za majeruhi la Jordi Alba limewapa ushindi Barcelona Uwanjani kwao Nou Camp baada ya Celtic ya Scotland kutangulia kwa bao moja ambalo alifunga Samaras na Iniesta kusawazisha kabla ya haftaimu.
VIKOSI:
Barcelona: Valdes, Adriano, Bartra, Mascherano, Jordi Alba, Xavi, Song, Iniesta, Sanchez, Messi, Pedro
Akiba: Pinto, Fabregas, Villa, Jonathan, Montoya, Sergi Roberto, Tello.
Celtic: Forster, Lustig, Wilson, Ambrose, Izaguirre, Samaras, Brown, Wanyama, Ledley, Mulgrew, Hooper
Akiba: Zaluska, Matthews, Miku, Commons, Rogne, Kayal, Forrest.
Refa: Gianluca Rocchi (Italy)
++++++++++++++++++++++++++++++
MAN UNITED 3 BRAGA 2
Javier Hernandez, ‘Chicharito’, alipiga bao mbili na Jonny Evans bao moja baada ya Man United kutoka nyuma kwa bao 2-0 za Braga ya Ureno zote zikifungwa na Alan ndani ya Dakika 20 na kupata ushindi wa bao 3-2 wakiwa kwao Old Trafford huo ukiwa ushindi wao wa 3 mfululizo kwenye Kundi lao.
VIKOSI:
Man United: De Gea, Da Silva, Carrick, Evans, Buttner, Kagawa, Fletcher, Cleverley, Rooney, Hernandez, van Persie
Akiba: Johnstone, Ferdinand, Anderson, Giggs, Nani, Young, Welbeck.
Braga: Beto, Leandro Salino, Nuno Andre, Paulo Vinicius, Elderson, Custodio, Hugo Viana, Ruben Amorim, Alan, Ruben Micael, Eder
Akiba: Quim, Mossoro, Helder Barbosa, da Solva, Baiano, Ze Luis, Anibal.
Refa: Milorad Mazic (Serbia)
++++++++++++++++++++++++++++++
SHAKHTAR DONETSK 2 CHELSEA 1
Mabingwa wa Ulaya, Chelsea, leo wamegalagazwa ugenini na Shakhtar Donetsk baada ya kupigwa bao 2-1.
Shakhtar walifunga bao zao kupitia Alex Teixeira, Dakika ya 3, na Fernandinho, Dakika ya 52, na Chelsea kupata bao lao pekee katika Dakika ya 88 mfungaji akiwa Oscar.
VIKOSI:
Shakhtar Donetsk: Pyatov, Srna, Kucher, Rakitskiy, Rat, Hubschman, Fernandinho, Alex Teixeira, Mkhitaryan, Willian, Luiz Adriano
Akiba: Kanibolotskiy, Stepanenko, Eduardo, Gai, Douglas Costa, Kryvtsov, Ilsinho.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Terry, Luiz, Cole, Oscar, Ramires, Mikel, Lampard, Mata, Torres
Akiba: Turnbull, Romeu, Hazard, Sturridge, Cahill, Azpilicueta, Bertrand.
Refa: Damir Skomina (Slovenia)
++++++++++++++++++++++++++++++
RATIBA:
[MECHI ZOTE Saa 3 Dakika 45 Usiku isipokuwa inapotajwa]
Jumatano Oktoba 24
FC Porto v FC Dynamo Kyiv
GNK Dinamo v Paris SaintvGermain FC
Arsenal FC v FC Schalke 04
Montpellier Hérault SC v Olympiacos FC
FC Zenit St. Petersburg v RSC Anderlecht [SAA 1 USIKU]
Málaga CF v AC Milan
AFC Ajax v Manchester City FC
Borussia Dortmund v Real Madrid CF
++++++++++++++++++++++++++