Sunday, January 13, 2013

UKURASA WA DONDOOO ZA USAJILI NA HABARI ZA KIMATAIFA NI HAPA WENGER ANAAMINI FABREGAS ANAWEZA KURUDI EMIRATES

 Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema upo uwezekano mkubwa wa kiungo wake wa zamani Cesc Fabregas kurejea Emirates Stadium.
Fabregas mwenye umri wa miaka 25, aliichezea kwa miaka minane Arsenal kabla ya kurejea nyumbani Hispania katika klabu iliyomkuza tangu akiwa mtoto ya Barcelona kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni 30 mwaka 2011.
Wenger anaamini kuwa kiungo huyo wa kimataifa ya Hispania kwasasa ametulia Camp Nou, na timu yake ikiongoza ligi ya nchi hiyo Liga lakini bado anaamini anaweza kurejea kusaini tena Arsenal.
"Sidhani kama hararejea moja kwa moja iko siku moja " amekaririwa na gazeti la Guardian.
"ni mtu wa Arsenal. Anaipenda Arsenal na anaangalia kila mchezo wa Arsenal. Lakini bila shaka Barcelona kulikuwa ndiyo nyumbani alikokulia lazima ukubali hilo.
"Huenda asije mwakani au miaka miwili au mitatu kwasababu ana uhusiano mkubwa na Barcelona. Lakini baadaye linawezekana."
Wenger kwasasa amepata faraja kubwa kwa wachezaji wake vijana waingereza Kieran Gibbs, Carl Jenkinson, Jack Wilshere, Aaron Ramsey na Alex Oxlade-Chamberlain – kusaini mkataba mpya na klabu hiyo.

KOCHA WA ZAMANI W ATIMU YA TAIFA YA ENGLAND FABIO CAPELO ANATARAJIA KUWA MGENI WA KUHUDHURIA SHEREHE ZA MIAKA 150 CHA FA
 Meneja wa zamani wa timu ya taifa ya England Fabio Capello atakuwa ni miongoni mwa watu watakao hudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 150 ya chama cha soka cha England jumatano jijini London.
Sherehe hizo ambazo pia zitahudhuriwa na meneja wa sasa wa England na zitafanyika Connaught Rooms huko Holborn.
Kwasasa Capello ni meneja wa timu ya taifa ya Russia, na tayari ameuarifu uongozi wa FA ataudhuria katika sherehe hizo.
Capello aliondoka kuifundisha England kwa mizengwe mwezi February 2012 baada ya kutofautiana na maamuzi ya kumvua unahodha John Terry kwa mara ya pili na tangu wakati huo hakuwa na mawasiliano na FA.
Ikiwa ni sehemu ya sherehe za maadhimisho ya miaka 150 ya FA, pia kumeandaliwa michezo miwili ya kirafiki kati ya England na Brazil na mchezo mchezo mwingine kati ya Scotland dhidi ya jamhuri ya Ireland. Michezo mingine dhidi ya Ujerumani na Argentina inatarajiwa kuchezwa baadaye mwaka huu.
O'BRIEN ASAINI MKATABA KATIKA WAGONGA NYUNDO W ALONDON WEST HAM UNITED
 Mlinzi wa West Ham Joey O'Brien ameongeza mkataba mwingine na klabu hiyo ambao utamuweka klabuni hapo mpaka 2016.
O'Brien akiwa chini ya Sam Allardyce katika klabu ya Bolton alipelekwa Upton Park mwaka 2011 na bosi wa washika nyundo.
Klabu hiyo imetangaza hilo kupitia ukurasa wake wa Twitter kwa maneno yaliyosomeka “West Ham United inayofuraha kubwa kutangaza kuwa Joey O'Brien amesaini mkataba mpya utakamuweka klabu mpaka kiangazi 2016.”
O'Brien mwenye umri wa miaka 26, ameitumikia timu ya taifa ya jamhuri ya Ireland michezo mitano na ameitumikia klabu yake michezo 16 huu wa ligi kuu ya England ‘Premier League’ akifunga magoli mawili.
 

DZEKO MGUU NDANI MGUU NJE CITY KUICHEZEA MAN CITY.

MSHAMBULIAJI wa Manchester City, Edin Dzeko ameonyesha nia yake ya kurejea katika Ligi Kuu nchini Ujerumani maarufu kama Bundesliga baada ya kushindwa kupata namba katika kikosi cha kwanza cha Manchester City. Dzeko amefunga mabao sita msimu huu akitokea benchi na kuna taarifa kuwa mchezaji huyo hafurahishwi kuwepo katika klabu hiyo na hivyo yuko tayari kusikiliza ofa kutoka katika timu yoyote kwenye kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili. Nyota huyo amesema kila kitu kinawezekana hivyo anaweza kuondoka kuondoka kipindi hiki au katika majira ya kiangazi lakini kwasasa anajaribu kutofikiria hilo na kujaribu kutumia nafasi anayopewa na City. Mbali na mchezaji huyo pia kumekuwa na tetesi za kuondoka kwa mshambuliaji mwingine nyota wa klabu Sergio Aguero lakini taarifa hizo zilikanushwa na mchezaji mwenzake Pablo Zabaleta ambaye alidai kuwa nyota huyo anafurahia maisha katika klabu hiyo na hama mpango wa kuondoka.

AFCON KUMPELEKA MPUTU ULAYA.

KIUNGO wa kimataifa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC, Tresor Mputu amekuwa akihusishwa na tetesi za kuhamia katika vilabu vya Ulaya mara nyingi zaidi kuliko alivyofunga mabao kwa klabu yake na timu ya taifa. Mputu mwenye umri wa miaka 27 mpaka sasa amefanikiwa kufunga mabao zaidi ya 200 kwa timu yake ya taifa ya DRC na klabu ya TP Mazembe yenye maskani yake jiji la Lubumbashi lililo kusini mwa nchi hiyo. Zikiwa zimebakia siku chache kabla ya kuanza michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon itakayofanyika nchini Afrika Kusini vyombo vya habari vimeanza tena kumfuatilia mchezaji huyo na kudai kuwa michuano hiyo itakuwa nafasi ya nyingine kwa nyota huyo kuonekana kwa vilabu vya Ulaya.  Vyombo vimeanza kutabiri kuwa kiwango alichonacho Mputu katika kukokota mpira pamoja na umahiri wa kufunga na kutengeneza mabao kitawavutia maskauti kutoka barani Ulaya ambao watakuwepo wakifuatilia kwa karibu michuano hiyo.

MOURINHO UNDER MORE PRESSURE BAADA YA JANA KUTOA SARE NA KUTOA KABISA MATUMAINI YA UBINGWA .

MENEJA wa klabu ya Real Madrid, Jose Mourinho ameingia katika shinikizo zaidi jana wakati klabu hiyo ilipolazimishwa sare ya bila kufungana na klabu ya Osasuna ambayo inashika mkia matokeo ambayo yamewaacha nyuma kwa alama 15 mbele ya mahasimu wao Barcelona ambao wanaongoza La Liga. Katika mchezo Madrid ambao hawakutengeneza nafasi nyingi za kufunga walimkosa mshambuliaji wake nyota Cristiano Ronaldo ambaye alifunga mabao matano kati ya nane ambayo timu hiyo imeshinda katika michezo yake miwili iliyopita. Madrid sasa wanabakia katika nafasi ya tatu wakiwa na alama 37 ikiwa ni alama nne nyuma ya Atletico Madrid wanaoshika nafasi ya pili ambapo pia kuna uwezekano wa kutofautiana na Barcelona kwa alama 18 kama timu hiyo ikishinda mchezo wake wa leo dhidi ya Malaga. Pamoja na matokeo hayo lakini Mourinho alikataa kuwalaumu wachezaji kwa kuwasifia kucheza vizuri na kufanya kila waliloweza kujaribu kufunga pamoja na kwamba hawakutengeneza nafasi nyingi.

AYEW AREJEA KATIKA KIKOSI CHA MARSEILLE BAADA YA KUPONA.

WINGA machachari wa kimataifa wa Ghana na klabu ya Olympique Marseille ya Ufaransa, Andre Ayew ambaye aliondolewa katika kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo, ameitwa katika kikosi cha Marseille ambacho kinatarajia kucheza na Sochaux katika mchezo wa Ligi Kuu nchini Ufaransa. Taarifa iliyolewa na mtandao wa klabu hiyo imedai kuwa Ayew ambaye ameichezea Ghana mechi 44 amepona majeraha ya paja aliyopata wakati wa mazoezi na klabu yake siku 10 zilizopita. Ayew mwenye umri wa miaka 23 ambaye ni mtoto wa nguli wa zamani wa Ghana Abeid Pele, alitarajiwa kujiunga na kikosi cha timu ya taifa mwishoni mwa wiki iliyopita kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya majeraha yake lakini hakutokea kwa wakati kitendo ambacho kilipelekea kocha Kwesi Appiah kumuengua kwa ajili ya michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon. Kama ilivyo kwa Ayew, golikipa wa Togo Kossi Agassa naye pia anatarajia kuwepo katika kikosi cha Marseille Jumapili pamoja na kuenguliwa katika michuano ya Afcon kutokana na kupata majeraha ya mguu. Michuano ya Afcon inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Januri 19 na kumalizika Februari 10 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment