Uongozi umethibitisha kwamba kambi itakuwa Antalya ambao ni mji ulioko kilomita 490 kutoka Instanbul yalipo makao makuu ya nchi hiyo yenye baridi kali muda mwingi. Umbali kutoka Dar es Salaam mpaka Instanbull kwa ndege ni kilomita 5,394.5 ambao ni mwendo wa saa saba kwa ndege. Lakini kocha wake Ernest Brandts alisema: "Lengo letu ni kutwaa ubingwa kwenye ligi kuu, tupo kileleni hivi sasa tutang'ang'ania hapo hapo." "Kila kitu katika soka ni nidhamu, iwe ndani ya uwanja au hata nje, mazoezi na hata kwenye mechi. Kama mchezaji hana nidhamu hawezi kuwa bora, ninachoshukuru wachezaji wangu wanafuata kile ambacho mimi ninataka. "Mimi ni mkali wakati mwingine ninapoona mchezaji anakwenda tofauti nampa adhabu." Yanga inaendelea kujifua kwenye Uwanja wa Kijitonyama jijini Dar es Salaam na kesho Jumatano itacheza na Tusker ya Kenya katika mchezo wa kirafiki utakaofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. |
Thursday, December 27, 2012
YANGA KUPAAA KESHO KUTWA JUMAPILI KWENDA UTURUKI
KADI NYEKUNDU GIBSON, COLE ZAFUTWA, FERGIE ANUSURIKA…REDKNAPP, MANCINI….!!!
![MANCINI_n_MICAH](http://www.sokainbongo.com/images/stories/MANCINI_n_MICAH.jpg)
Chama cha Soka England, FA,
kimethibitisha kuwa Sir Alex Ferguson, hatapewa adhabu yeyote kwa
kitendo chake cha kabla Kipindi cha Pili kuanza, cha kumvaa Refa Mike
Dean na kumlalamikia kisha kumkabili Refa wa Akiba Neil Swarbrick na pia
Refa Msaidizi Jake Collin, kwa vile Refa Dean hakuzungumza lolote
kuhusu tukio hilo katika Ripoti ya Mechi.
Hata hivyo, Mameneja wa Man City na QPR,
Roberto Mancini na Harry Redknapp, wako matatani kufuatia kauli zao
baada ya Mechi zao za kulalamika kuhusu Marefa na kudokeza uchezeshaji
usio wa haki kitendo ambacho ni kinyume cha Kanuni za FA.
Mancini, Meneja wa Man City, alilalamika
kuhusu Refa Kevin Friend baada kufungwa 1-0 na Sunderland kwenye Mechi
ya Ligi Kuu England iliyochezwa Desemba 26 kwa Refa huyo kutopiga
Filimbi ya Faulo aliyochezewa Mchezaj wake Pablo Zabaleta na badala yake
kuachia mpira uchezwe na kuzaa Goli la Adam Johnson, Winga wa zamani wa
Man City, lililowaua City 1-0.
Mancini alidai: “Pengine Refa alivimbiwa na Mlo wa Krismasi! Haiwezekani Waamuzi wawili wasione tukio hilo! [Akimaanisha Refa Na Msaidizi wake]”
Nae Harry Redknapp, Bosi wa QPR, yuko
matatani baada ya kuhamaki na maamuzi ya Refa Chris Foy ambayo alidai ni
‘Skandali!’ wakati walipofungwa 2-1 na West Brom na kutupwa mkiani mwa
Ligi Kuu England Siku ya Boxing Dei.
Refa Chris Foy alilikubali Goli la
kujifunga mwenyewe Kipa Robert Green ambae alionekana akibanwa waziwazi
na Mchezaji wa WBA, Marc-Antoine Fortune, na pia aliwayima Penati ya
wazi mwishoni baada ya Beki Liam Ridgewell kuunawa mpira.
Redknapp amewaka: "Ile ni Faulo ya wazi kwa Kipa wetu na ile ni Penati ya wazi! Hii ni kashfa!”
Msimamo wa FA kwa Mameneja ni kwamba
hawatakiwi kuwalaumu Marefa kuhusu maamuzi yao na wakifanya hivyo
wanaandikiwa Barua kutaka maelezo yao na kama hayaridhishi hufunguliwa
Mashitaka.
Wakati huo huo, FA imetangaza kuwa Rufaa
za Everton na West Ham kupinga Kadi Nyekundu kwa Wachezaji wao, Darron
Gibson wa Everton na Carlton Cole, zimekubaliwa na Adhabu za kufungiwa
Mechi 3 kila mmoja kwa Wachezaji hao zimefutwa.
Wachezaji hao wote wawili walitolewa
katika Mechi moja na Refa Mark Anthony Uwanjani Upton Park Wikiendi
iliyopita ambako Everton walishinda 2-1 baada ya kutoka nyuma kwa kwa
Bao la Carlton Cole na kutolewa kwa Mfungaji huyo kuliwapa mteremko
kusawazisha na kushinda huku Mchezaji wao Gibson akitolewa Dakika za
majeruhi.
Wachezaji hao wote wawili sasa wako huru kuziwakilisha Klabu zao Mechi za Ligi Wikiendi hii
MARWA NA KIRWA KUCHEZESHA KOMBE LA MATAIFA KULE AFRIKA KUSINI,HAWA KUTOKA KENYA LAKINI TANZANIA NA UGANDA HALI TETE HATA WA KUFUTIA MACHOZI HAKUNA
![Marwa](http://www.futaa.com//images/350x300/AdenMarwa.jpg)
Aden Marwa, ambaye ni mwalimu kutoka Nyanza kusini, amechaguliwa pamoja na refa mwingine Sylvester Kirwa, kutoka Eldoret.
Wawili hao wamechaguliwa kuamua mechi za michuano hiyo baada ya kushiriki katika kozi ya CAF ya marefa iliyofanyika huko Egypt mapema mwezi uliopita.
Marefa hao wa pekee kutoka ukanda huu wa Afrika mashariki wataenda South Africa siku ya jumanne tarehe 15, siku nne kabla ya michuano kuanza.
Marwa – ambaye alishiriki katika 2012 AFCON, zilizofanyika nchini Gabon na Equatorial Guinea – amesema kuchaguliwa kwao kwenda AFCON ni ishara nzuri kwa soka la Kenya.
Sylvester Kirwa
KOCHA MPYA SIMBA KUKISHUHUDIA KIKOSI CHAKE KIKIIVAA TUSKER FC JUMAMOSI
KOCHA mpya wa Simba Mfaransa Patrick Liewang anatarajia kukishuhudia kikosi ya timu hiyo jumamosi ya keshokutwa kitakapokwaana na mabingwa wa soka wa Kenya, Tusker Fc.
Mchezo huo wa kimataifa wa kirafiki unatarajiwa kupigwa kwenye dimba la Taifa jijini Dar es Salaam ambapo pia Simba itautumia kutambulisha nyota wake wapya iliyowasijili kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu ya Vodacom na michuano ya kimataifa.
Ofisa habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga amesema leo kwamba, kocha huyo ambaye alikuwa awasili nchini leo imeshindikana baada ya kukosa nafasi kwenye ndege, hali itakayomfanya asubiri mpka jumamosi.
Alisema kocha huyo ambaye anakuja kurithi mikoba ya Mserbia Milovan Cirkovic, atakishuhudia kikosi cha Simba kikicheza mechi hiyo kabla ya kuendelea na taratibu nyingine ikiwemo kusaini mkataba wa kazi na baadaye kuanza kutumikia kibarua chake kipya.
Naye mratibu wa mchezo huo, George Wakuganda alisema kwamba maandalizi ya mchezo huo yamekamilika ambapo viingilio ni sh 15,000, 10,000, 7,000 na 5,000.
Tusker Fc jana ilikwaana na Yanga na kuitandika bao 1-0 mchezo ulipigwa kwenye uwanja wa Taifa.
NYOTA 27 YANGA SC KUKWEA PIPA LA UTURUKI USIKU WA JUMAMOSI
KIKOSI
cha wachezaji 27 wa Yanga Sc kinatarajiwa kuondoka nchini usiku wa
jumamosi kuelekea nchini uturuki kwa ajili ya kuweka kambi maalum ya
kujiandaa na mashindano mbalimbali.
Mwenyekiti
wa kamati ya Mashindano na mjumbe wa kamati ya Utendaji ya Yanga,
Abdallah Binkleb ameiambia Sports Lady maandalizi ya safari hiyo
yamekamilika na kwamba wachezaji watakaokwenda huko pamoja na viongozi
watajulikana kesho.
Amesema
kwamba kambi hiyo itakisaidia sana kikosi katika maandalizi yake ya
mzunguko wa pili wa ligi kuu ya vodacom pamoja na michuano ya Kagame
itakayofanyika Kigali, Rwanda ambapo Yanga ni bingwa tetezi.
"Ndo
maana tumetaka kwenda Uturuki kwani huko kuna facilities nzuri kwa
ajili ya kambi...pia huko tunataraji kiucheza mechi kadhaa za
kirafiki,"amesema.
Yanga
inayonolewa na Ernie Brandts jana ilichapwa bao 1-0 na mabingwa wa soka
nchini Kenya, Tusker Fc katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Taifa
jijini Dar es Salaam.
MAPINDUZI CUP :AL AHLY YAJITOA ,RAGE TUNAWACHEZAJI 36 ,YANGA HATUTASHIRIKI LABDA KIKOSI CHA PILI
![](http://api.ning.com/files/e71hN0SaRlG6Z-MerpfmqYK7VD0OovPa1AGyWdW4vIUsELBEx-zN4rqdJhkVUEjPfTN8uy6jaHGdQra3Cl*HYAE0L0phs6XE/SIMBANAYANGA19.jpg?width=650)
Katika hari isiyotarajiwa klabu kubwa
nchini simba na yanga zinaonekana kuitolea nje michuano ya mapinduzi cup
inayotarajia kuanza mwezi january mwakani huku timu zote zikititoa
sababu binafsi Mabingwa tanzania simba ambao wanasafari ya kwenda muscat
Mwezi january wameshasema Kupitia Mwenyekiti wa klabu hiyo Ismail Aden
Rage kuwa timu yao ina wachezaji 36 hiii inamaana kuwa kuna uwezekano
mkubwa wapereka kikosi cha pili.
huko zanzibari kwani wanasafari ya kwenda oman kujiandaa na mzunguko wa pili ligi ya primia Tanzania Bara
Yanga kupitia katibu mkuu wake Mwalusako
imesema haita shiriki huku sababu kubwa ikiwa kama ya simba kwenda
uturuki kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi huku akisistiza kuwa labda
wapereke kikosi cha pili ![Tusker FC are the 2011 KPL Champions](http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2011/11/Tusker-FC-are-the-2011-KPL-Champions.jpg)
![Tusker FC are the 2011 KPL Champions](http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2011/11/Tusker-FC-are-the-2011-KPL-Champions.jpg)
mwenyekiti wa kamati inayosimamia
mashindano hayo said Khamis Abdallah amesema kuwa watatoa jibu kesho
kama timu hizo zitashiriki au hazitoshiriki huku Tusker ya kenya
ikisibithia kushiriki wakati Al ahly ya Masir imetangaza kujitoa
kutokana na sababu sizizo weza kuzuirika Timu pekee zilizo thibithisha
kushiri kutoka bara ni Azam na coast union ambapo michuno hiyo inataraji
kuanza tarehe pili january .
aidha michuano itachezwa unguja pekee tofauti na ilivyopangwa awali kuwa ingechezwa na pemba .
MAKUNDI:
KUNDI A:
Simba (Dar-es-Salaam),
Tusker (Kenya)
Bandari (Unguja)
Jamhuri (Pemba).
KUNDI B:
Azam FC (Dar-es-Salaam)
Mtibwa Sugar (Morogoro)
Coastal Union (Tanga)
Miembeni (Unguja).
FERGIE KULIKWAA RUNGU LA FA? MANCINI AKIRI MATATIZO!!
>>REDKNAPP AMLAUMU REFA KWA KURUDISHWA MKIANI!!
>>BENITEZ ASEMA 1-0 NI MUHIMU KAMA 8-0!!
![FERGIE_KAZINI](http://sokainbongo.com/images/stories/FERGIE_KAZINI.png)
Ferguson alikuwa amekasirishwa na Refa
Mike Dean kufuta Ofsaidi iliyotolewa ishara na Msaidizi wake Jake Collin
na kuamua ni Bao kwa vile Jonny Evans alijifunga mwenyewe.
Wakati Kipindi cha Pili kinataka kuanza,
Ferguson alimvaa Refa Mike Dean na kumlalamikia kisha akamvaa Refa wa
Akiba Neil Swarbrick na pia Refa Msaidizi Jake Collin.
Ikiwa tukio litatajwa kwenye Ripoti ya
Mechi ya Refa Mike Dean basi huenda Sir Alex Ferguson akaadhibiwa FA
lakini kwa vile Refa Dean hakumchukulia hatua yeyote Ferguson huenda
akakwepa adhabu.
Akielezea tukio hilo Ferguson alisema:
“Refa alimfanya Mshika Kibendera abadilishe uamuzi wake wa Ofsaidi.
Alisema ni Goli la kujifunga mwenyewe lakini ukilirudia Goli lile, yule
Mchezaji wa Newcastle alikuwa Ofsaidi na tena alimvuta mkono Evans! Sasa
hilo kama si kuingilia uchezaji ni nini? Ni uamuzi mbovu!”
ROBERTO MANCINI AKIRI MATATIZO MANCHESTER CITY!!
Roberto Mancini amekiri kuwa ana matatizo makubwa mara baada ya jana kuchapwa 1-0 na Sunderland.
Mancini amesema: “Tatizo kubwa Mastraika hawafungi nafasi wanazopata!”
Sasa ni mara ya 3 mfululizo kwa Man City
kufungwa Stadium of Light na Sunderland ambao jana Bao lao pekee
lilifungwa na Winga wa zamani wa Man City, Adam Johnson.
Msimu huu, Man City wamefunga Bao 34 katika Mechi 19 za Ligi Kuu England ikiwa ni Magoli 14 nyuma ya vinara Man United.
Lakini, ingawa Man City sasa wako Pointi
7 nyuma ya Man United, Roberto Mancini amesema wao bado wana nafasi ya
kutetea Taji lao.
Ametamka: “Man United wanafunga Bao
nyingi kupita sisi lakini pia wanafungwa Bao nyingi kupita sisi! Msimu
ni mrefu na ni juu yetu kubadilika!”
HARRY REDKNAPP CRITICISES REFEREE AFTER QPR'S LOSS TO WEST BROM
![harry-redknapp](http://georgeogier.files.wordpress.com/2012/04/harry-redknapp.jpg?w=300&h=225)
Bosi wa Queens Park Rangers Harry
Redknapp amekasirishwa na maamuzi ya Refa Chris Foy ambayo amedai ni
‘Skandali!’ wakati jana walipofungwa 2-1 na West Brom na kuwatupa mkiani
mwa Ligi Kuu England.
Refa Chris Foy alilikubali Goli la
kujifunga mwenyewe Kipa Robert Green ambae alionekana akibanwa waziwazi
na Mchezaji wa WBA, Marc-Antoine Fortune, na pia aliwayima Penati ya
wazi mwishoni baada ya Beki Liam Ridgewell kuunawa mpira.
Redknapp amewaka: "Ile ni Faulo ya wazi kwa Kipa wetu na ile ni Penati ya wazi! Hii ni kashfa!”
BENITEZ ASEMA 1-0 NI MUHIMU KAMA 8-0!!
![Chelsea’s new interim 1st team manager Rafa Benitez during his 1st training session](http://www.thetimes.co.uk/tto/multimedia/archive/00358/117143216_football_358621h.jpg)
Bosi wa Chelsea Rafael Benitez anaamini
ushindi wa Bao 1-0 dhidi ya Norwich hapo jana ni muhimu kama kile
kipondo cha 8-0 walichowashushia Aston Villa Siku 3 zilizopita.
Ingawa Wadau wengi wa Klabu hiyo
watahisi kimchezo ushindi wa 1-0 ni tofauti na ule wa 8-0, Benitez
ametetea matokeo hayo kwa kusema: “Ni muhimu kuiona Timu ikicheza kwa
bidii na kujilinda kisawasawa! Muhimu ni kuwa hatukufungwa Bao.”
Chelsea sasa wako nafasi ya 3 wakiwa Pointi 4 tu nyuma ya Man City na Mechi moja mkononi.
+++++++++++++++++++++++
MECHI ZIJAZO:
Jumamosi 29 Desemba 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Sunderland v Tottenham
[SAA 12 Jioni]
Aston Villa v Wigan
Fulham v Swansea
Man United v West Brom
Norwich v Man City
Reading v West Ham
Stoke v Southampton
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Arsenal v Newcastle
Jumapili 30 Desemba 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Chelsea
[SAA 1 Usiku]
QPR v Liverpool
Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Brom v Fulham
[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Southampton v Arsenal
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
BRUNO GOMES MBRAZIL ANAYEKUJA OLD TRAFFORD MWAKANI - AIPA UBINGWA TIMU YAKE - ACHUKUA KIATU CHA DHAHABU
Mchezaji aliyesajiliwa na Manchester United kutoka Brazil Bruno Gomes ameiongoza klabu yake ya Desportivo Brasil kutwaa ubingwa nchini hiyo wa vijana wenye miaka U17.
Gomes, 16, atajiunga na United kipindi kijacho kiangazi, alifunga hat trick katika fainali ya pili ya kugombea ubingwa huo dhidi Marília, na mwishowe Desportivo wakashinda 6-0.
Mshambuliaji huyo hatari, tayari amekuwa chaguo muhimu katika kikosi cha Brazil cha vijana chini ya umri wa miaka 17, amefunga mabao 27 katika mechi 32 na kubeba kiatu cha dhahabu.
United wana mahusiano rasmi na klabu ya Desportivo Brasil, ambao wachezaji wao wamefunga mabao 88 katika mechi 32 msimu huu.
Inaeleweka kwamba pamoja na Gomes, United wapo katika mazungumzo ya kumsajili winga wa Desportivo aitwaye Welder.
Desportivo pia walishinda ubingwa Milk Cup huko Northern Ireland mwaka huu.
Gomes, 16, atajiunga na United kipindi kijacho kiangazi, alifunga hat trick katika fainali ya pili ya kugombea ubingwa huo dhidi Marília, na mwishowe Desportivo wakashinda 6-0.
Mshambuliaji huyo hatari, tayari amekuwa chaguo muhimu katika kikosi cha Brazil cha vijana chini ya umri wa miaka 17, amefunga mabao 27 katika mechi 32 na kubeba kiatu cha dhahabu.
United wana mahusiano rasmi na klabu ya Desportivo Brasil, ambao wachezaji wao wamefunga mabao 88 katika mechi 32 msimu huu.
Inaeleweka kwamba pamoja na Gomes, United wapo katika mazungumzo ya kumsajili winga wa Desportivo aitwaye Welder.
Desportivo pia walishinda ubingwa Milk Cup huko Northern Ireland mwaka huu.
ASILIMIA 82 YA MASHABIKI WA MADRID WANATAKA MOURINHO ATIMULIWE KAZI REAL MADRID
Kufuatia kupigwa benchi kwa Casillas katika mechi dhidi ya Malagamtandao wa gazeti maarufu nchini Hispania MARCA.com uliuliza "Je inabidi Real Madrid imtimue Mourinho?" na majibu ya takribani wasomaji 100,000 yalikuja yakisema ndio kwa asilimia 82.4%.
Kwa mujibu wa MARCA, mapenzi baina ya washabiki wa Los Blancos na Mourinho yamekwisha kabisa. Madrid wamekuwa na mfululizo wa matokeo mabaya katika kipindi cha hivi karibuni na kusababisha maneno mengi juu ya mustakabli wa kocha Jose Mourinho ndani ya klabu hiyo.
Real Madrid wapo nyuma kwa 16 dhidi ya viongozi wa La Liga Barcelona, na tayari Mourinho ameshasema kwamba ubingwa wa La liga msimu huu hawawezi kushinda tena, na inasemekana kwamba ikiwa atashindwa kuiongoza klabu hiyo kushinda ubingwa wa 10 wa mabingwa wa ulaya basi Mreno huyo atatemeshwa kibarua chake mwishoni mwa msimu.
MENEJA WA LIVERPOOL BRENDAN RODGERS AKUBALIANA NA MATOKEO YA JANA DHIDI YA STOKE CITY
Meneja wa Liverpool
Brendan Rodgers amesisitiza kuwa hawakuwa na la kujivunia katika mchezo ambao
walipoteza kwa kuchapwa mabao 3-1 na Stoke City iliyocheza vema hapo jana kule
katika dimba la Britannia jioni ya jana.
Wekundu hao
walipata bao la mapema kupitia kwa nahodha Steven Gerrard kwa njia ya penati
baada ya Luis Suarez kuangushwa katika eneo la hatari na Ryan Shawcross.
Hata hivyo
Stoke wakafanikiwa kusawazisha na baadaye kuandika bao la pili la uongozi
kupitia kwa Jonathan Walters na kisha bao la kichwa la Kenwyne Jones.
Brendan Rodgers
amekiri kikosi chake kuvurunda katika mchezo huo lakini pia akionekana kuhuzunishwa
na aina ya magoli yaliyokuwa yakifungwa na kusema timu yake inapaswa kujifunza
namna ya kulinda kama inataka kupata alama katika michezo ya ugenini.
“ulikuwa ni
mwanzo mzuri kwetu kwa kupata goli la mapema kupitia njia ya penati, lakini tulishindwa
kujilinda nadhani magoli yote matatu na makosa ya ulinzi, kiukweli
hatukustahili chochote katika mchezo huu”
TIMU YA BLACKBURN ROVERS YAMTIMUA KOCHA WAKE HENNING BERG NA MAAFISA WATATU WA TIMU HIYO
Blackburn
Rovers imemfukuza kazi meneja wake Henning Berg na maafisa wengine watatu
katika safu ya makocha ikiwa ni hatua ambayo imefuatia klabu hiyo kutereza
katika vibaya katika msimamo wa ligi ndogo ya nchini England, Championship.
Meneja huyo
raia wa Norway, ambaye aliajiriwa mwezi October, katika jumla ya michezo 10
amefanikiwa kushinda mchezo mmoja tu katika kipindi chake cha utumishi wake wa
siku 57.
Berg, ambaye
alikuwa mchezaji wa Rovers mwaka 1995 wakati huo Rovers ilishinda taji la ligi
kuu ya England “Premier League” na
baadaye akishinda taji la “League Cup” akiwa nahodha wa kikosi mwaka 2002, alirejeshwa
katika klabu hiyo kama meneja mwezi Oktoba.
Baada ya Blackburn
kuanza kwa kusuasua chini ya meneja wake wa zamani Lyn Oslo na Lillestrom klabu
hiyo ikaamua kumpa Berg jukumu la kukinoa kikosi hicho katika kipindi hiki cha
mwisho wa mwaka.
Kichapo cha
bao 1-0 kutoka kwa Middlesbrough jana Boxing Day kilipelekea Rovers kujikuta
katika nafasi ya 17 ikifanikiwa kukusanya alama 7 ndani ya uwezo wake wa
kukusanya alama 30 kama wangeshinda michezo yote chini ya meneja Henning Berg.
Meneja msaidizi,
Eric Black, kocha wa namba moja Iain Brunskill kocha wa makipa Bobby Mimms nap
wamekumbwa na dhahma hiyo ya kufukuzwa kazi pamoja na Berg kutoka katika viunga
vya Ewood Park.
GARETH BALE AFURAHIA HAT TRICK YAKE YA KWANZA BPL
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg2I6uyqLKflOMQQCyoe0NtKIgWBEbI1Hi6MDl4yirOZArX__c36EnK_WUOEYtG_dtMPkr-TrbaGMdo4g-1Sj4-2k2jgdSBYIxwCR27YUOYL2cPE17n_nkOCctN91b4ZySWvvknF_nsLyOD/s400/GARETH+BALE.jpg)
Jermain
Defoe alifunga goli la kwanza kwa Spurs kunako dakika ya 58 kabla ya Bale
kufunga magoli mengine matatu yaliyowapa uhakika wa ushindi katika mchezo huo.
Vijana hao
wanaotoka London ya Kaskazini waliingia katika mchezo huo wakiwa na kumbukumbu
ya sare ya bila kufungana dhidi ya Stoke, ambapo walikuwa wakijua wazi kwamba
muhimu kwao ulikuwa ni ushindi ili kuendelea kuleta ushindani katika nafasi ya
juu katika msimamo wa ligi.
Akinukuliwa kupitia
ukurasa wa mtandao wa kijamii wa twitter wa klabu yake, Bale amesema,
"vizuri kufunga magoli na kupata ‘hat
trick’ yangu ya kwanza katika ‘Premier League’ lakini muhimu ni kupata alama 3".
"wachezaji
wote walifanya kazi nzuri, sasa tunajipanga kwa ajili ya mchezo na Sunderland"
Kwa upande
wake meneja Andre Villas-Boas amepongeza vijana wake walivyokuwa uwanjani tangu
kuanza kwa mchezo mpaka mwisho
NEW CASTLE KUKUMBANA NA RUNGU LA FIFA
Newcastle na
Millwall huenda wakakumbana na adhabu ya shirikisho la soka duniani FIFA kufuatia
vilabu hivyo kugomea kuwaachia wachezaji wa kimataifa wa Nigeria Shola Ameobi na Danny Shittu kwa ajili ya
kulitumikia taifa lao katika michuano ya fainali za mataifa ya Afrika nchini
Afrika Kusini mwezi Januari
Bosi wa Newcastle
Alan Pardew anasema mshambuliaji wake Shola Ameobi hatasafiri kuelekea Afrika
katika fainali hizo.
Ameobi na Shittu
wote wanatarajiwa kujitoa rasmi katika uteuzi wao katika timu ya taifa ya
Nigeria (Super Eagles), jambo ambalo limeonekana kulikasirisha shirikisho la
soka la nchi hiyo (NFF).
Meneja wa Newcastle
Alan Pardew amesema Ameobi hatatokezea katika michuano hiyo ambayo inatarajiwa
kuanza January 19, wakati ambapo mlinzi wa Millwall er Shittu naye anatarajiwa
kutolea nje uteuzi wake kama ilivyo kwa Ameobi.
Sheria za FIFA
zinasema mchezaji yoyote ambaye atashindwa kuripoti katika timu yake ya taifa
baada ya kutajwa na nchi yake kwa ajili ya majukumu ya kimataifa , basi
mchezaji huyo atakuwa si halali kutumika katika kipindi chote kilichopendekezwa
wakati wa jukumu hilo pamoja na kuongezewa siku tano zaidi kama itawezekana vinginevyo
kuwepo na makubaliano mengine kati ya klabu yake na nchi husika.
Mjumbe wa
bodi ya shirikisho la soka la Nigeria Chris Green amesema watahakikisha klabu
za wachezaji hao zinaadhibiwa kama watagomea kuwaachia wachezaji hao.
SIMBA SC YAPANGWA NA TUSKER FC YA KENYA MAPINDUZI CUP
![]() |
Simba SC |
MABINGWA wa soka
Tanzania Bara, Simba SC wamepangwa kundi moja, A na Tusker FC ya Kenya, Bandari
ya Unguja na Jamhuri ya Pemba katika michuano ya Kombe la Mapinduzi, inayotarajiwa
kuanza kutimua vumbi hivi karibuni visiwani Zanzibar.
Aidha, katika
Kundi B, washindi wa pili wa Ligi Kuu ya Bara, Azam FC ya Dar e Salaam pia,
imepangwa na Mtibwa Sugar ya Morogoro, Coastal Union ya Tanga na Miembeni ya Unguja.
Michuano ya Kombe
la Mapinduzi, ambayo ni maalum kwa ajili ya kuherehekea Mapinduzi matukufu ya
Zanzaibar, inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Januari 2, hadi kilele cha miaka 49
ya Mapinduzi ya Zanzibar, Januari 12, mwakani, huku ikishirikisha timu kutoka
ndani na nje ya Tanzania.
Kwa mujibu
wa ratiba ya michuano hiyo iliyotolewa na Kamati Maalum ya Kusimamaia michuano
hiyo, inaonesha kuwa katika mchezo wa kwanza utakaochezwa siku ya ufunguzi
itakuwa ni kati ya Bandari kutoka Unguja ambayo itacheza na Jamhuri kutoka
kisiwani Pemba ambao ni wawakilishi wa Zanzibar katika Kombe la Shirikisho
Barani Afrika, pamabano litakalochezwa katika uwanja wa Mao Tse Tung mjini
Unguja, huku usiku wa siku hiyo hiyo katika Uwanja wa Amaan kisiwani Unguja
pambano la ufunguzi rasmi katika mashindano hayo likiwakutanisha mabingwa wa
soka nchini Tanzania, Simba SC ambao watapambana na mabingwa wa soka nchini
Kenya, Tusker.
Kwa mujibu
wa ratiba hiyo jumla ya timu nane zitashiriki katika mashindano hayo ambayo
yamejipatia umaarufu mkubwa visiwani hapa, timu hizo zimegawanya katika makundi
mawili ambayo ni kama ifuatavyo:
Awali
michuano hiyo ilitarajiwa kuanza kisiwani Pemba tarehe 1 Januari, lakini
kutokana na kujitoa katika mashindano kwa klabu ya Al-Ahly ya Misri kutokana na
klie kilichoelezwa sababu za kiusalama, mechi zote sasa zitachezwa kisiwani
Unguja na ufunguzi ukipangwa kuanza tarehe 2 badala ya tarehe 1 januari.
Bingwa wa
michuano hiyo ataondoka na zawadi ya kombe na fedha taslim Tsh. Milioni kumi
(10,000,000), mshindi wa pili Milioni tano (5,000,000), pamoja na zawadi
nyengine ambazo zimegawanywa katika makundi tofauti ikiwemo zawadi ya mfungaji
bora, mchezaji bora, mwamuzi bora, kipa bora, mwandishi wa habari bora, timu
bora na zawadi nyeanginezo.
Kupitia
matandao wako makini wa http://bongostaz.blogspot.com/ tutakuwa ukiwaletea kila
kitakachoendelea katika mashindano hayo kuanzia mwanzo mpaka mwisho
RIDHIWANI KIKWETE MGENI RASMI MKUTANO MKUU TASWA
![]() |
Ridhiwani, mtu wa watu |
MAANDALIZI
ya Mkutano Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA)
yanaenda vizuri na wajumbe wanatarajiwa kufika Bagamoyo kesho (Desemba 28, 2012)
mchana kwenye hoteli ya Kiromo View Resort watakapolala na kufanyia mkutano.
Ijumaa hiyo
washiriki watatembelea maeneo mbalimbali ya kihistoria Bagamoyo na jioni
kutakuwa na mechi ya kirafiki kati ya timu ya soka ya TASWA FC na Bagamoyo
Veterani itakayofanyika Uwanja wa Mwanakalenge na usiku wajumbe watakuwa na
chakula cha pamoja na kubadilishana mawazo kuhusiana na masuala mbalimbali
yahusiyo michezo na taaluma ya habari.
Mkutano Mkuu
utafunguliwa Jumamosi Desemba 29, saa tatu asubuhi na mgeni rasmi atakuwa
Mwenyekiti wa Kamati ya Kusaidia timu za Taifa za Vijana, Ridhiwani
Kikwete.TASWA imechukua jukumu la kumualika kutokana na kuwa mdau mkubwa na
rafiki wa chama chetu.
Mkutano
utafungwa jioni ya siku hiyo na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah
Mwambene ambaye hiyo pia itakuwa nafasi nzuri kwake kuweza kuzungumza na wana
habari kuhusiana na masuala mbalimbali ya kitaaluma.
Katika
mkutano huo wanachama wa TASWA watapata fursa ya kupokea na kujadili Ripoti ya
Utendaji ya chama, Mapato na Matumizi, maendeleo ya chama na masuala mbalimbali
yanayohusu waandishi wa habari za michezo na maendeleo ya michezo kwa ujumla
Pia kutakuwa
na semina maalum itakayoendeshwa kwa washiriki wa mkutano huo, ili wawe na
uelewa kuhusiana na ajenda ya kuinua kipato kwa wanachama ambayo nayo
itajadiliwa kwenye mkutano huo.
Kamati ya
Utendaji ya TASWA imekubaliana iwasaidie wanachama wake waweze kujitegemea kwa
kuanzisha Chama cha Akiba na Mikopo (SACCO’S), lakini imeamua kwanza iwaite
wataalamu wa vyama vya ushirika watoe elimu juu ya jambo hilo na kukishakuwa na
uelewa wa kutosha suala hilo litakuwa kama ajenda kamili ya kuanzisha chama
hicho kwenye mkutano wetu.
(Mwandishi wa habari
hizi ni Katibu Mkuu wa TASWA)
BAADA YA JANA KLUISAIDIA TIMU YAKE YA MAN U ROONEY ANATARAJIA KUKAA NJE WIKI MBILI.
MSHAMBULIAJI wa
Manchester United, Wayne Rooney anatarajiwa kukaa nje ya uwanja wa
kipindi cha wiki mbili hadi nne baada ya kuumia mguu wakati wa mazoezi
ya timu hiyo kabla ya mchezo wa jana wa Ligi Kuu nchini Uingereza dhidi
ya Newcastle United. Rooney
hakuwemo katika kikosi kilichoanza katika mchezo ambao walishinda mabao
4-3 dhidi ya Newcastle katika Uwanja wa old Trafford na meneja wa klabu
hiyo Sir Alex Ferguson amesema kuwa mshambuliaji huyo atakosa michezo
yote kwa mwaka huu. Kocha
huyo aliiambia tovuti ya klabu hiyo kuwa nyota huyo aliumia dakika za
mwisho mazoezini wakati akijaribu kuruka juu ndipo alipojiumiza kifundo
cha mguu wake wa kulia. United
inakabiliwa na mchezo dhidi ya West Bromwich Albion Jumamosi kabla ya
kusafiri kufuata Wigan Athletic Januari Mosi ambapo wanajipanga
kujizatiti kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo.
BAADA YA JANA KUFUNGWA BAO 1-O MANCINI ALIA NA MWAMUZI ASEMA HAKUWA FITI - NA FAIR PLAY
FOMENKO KOCHA MPYA UKRAINE.
ODIMWINGIE AMALIZIA HASIRA ZAKE KWA IKPEBA
.
![]() |
Ikpeba |
AFCON 2013: ZAMBIA, ANGOLA ZAWA TIMU ZA KWANZA KUWASILI AFRIKA KUSINI.
BPL: STOKE WAICHARAZA LIVERPOOL, SPURS YAINYUKA VILLA!
![BPL_LOGO](http://www.sokainbongo.com/images/stories/BPL_LOGO.png)
+++++++++++++++++++++++
MATOKEO:
Jumatano 26 Desemba 2012
Everton 2 Wigan 1
Fulham 1 Southampton 1
Man United 4 Newcastle 3
Norwich 0 Chelsea 1
QPR 1 West Brom 2
Reading 0 Swansea 0
Sunderland 1 Man City 2
Aston Villa 4 Tottenham 0
Stoke 3 Liverpool 1
+++++++++++++++++++++++
STOKE 3 LIVERPOOL 1
Stoke City, wakiwa kwao Uwanja wa
Britannia, walizinduka toka kufungwa Bao la Penati la Sekunde 35
iliyofungwa na Nahodha Steven Gerrard kwa kushinda Bao 3-1.
=================
MAGOLI:
Stoke 3
-Walters Dakika ya 5 & 49
-Jones 12
Liverpool 1
-Gerrard Dakika ya 2 [Penati]
=================
Bao mbili za Jon Walters na la Kenwyne
Jones ndio yamewapa Stoke City ushindi wao wa kwanza katika Mechi 4 na
kuendeleza wimbi lao la kutofungwa katika Mechi 9 ikiwa na pamoja ya
kutofungwa Uwanjani kwao tangu Februari.
Kipigo cha Liverpool Uwanjani Britannia
kimeendeleza Rekodi yao ya kutoshinda hapo na pia kuwarudisha hadi
nafasi ya 10 wakiwa Pointi 8 nyuma ya Timu iliyokamata nafasi ya 4.
VIKOSI:
Stoke: Begovic, Cameron, Shawcross, Huth, Wilkinson, Kightly, Nzonzi, Whelan, Etherington, Walters, Jones
Akiba: Sorensen, Adam, Whitehead, Upson, Crouch, Shotton, Jerome.
Liverpool: Reina, Johnson, Skrtel, Agger, Jose Enrique, Gerrard, Lucas, Downing, Shelvey, Suso, Suarez
Akiba: Jones, Cole, Henderson, Coates, Carragher, Allen, Sterling.
Refa: Howard Webb
ASTON VILLA 0 TOTTENHAM 4
Bao 4 za Kipindi cha Pili, ikiwemo
Hetitriki ya Gareth Bale, imewapa ushindi Tottenham wa Bao 4-0 dhidi ya
Aston Villa waliokuwa kwao Villa Park na hiki kimekuwa kipigo chao cha
pili kizito baada ya kutandikwa 8-0 na Chelsea majuzi.
VIKOSI:
Aston Villa: Guzan, Lowton, Herd, Clark, Baker, Bennett, Westwood, El Ahmadi, Delph, Holman, Benteke
Akiba: Given, Ireland, Albrighton, Bowery, Bannan, Lichaj, Carruthers.
Tottenham: Lloris, Walker, Gallas, Vertonghen, Naughton, Lennon, Dembele, Sandro, Bale, Defoe, Adebayor
Akiba: Friedel, Parker, Dawson, Sigurdsson, Livermore, Townsend, Caulker.
Refa: Mark Clattenburg
+++++++++++++++++++++++
MECHI ZIJAZO:
Jumamosi 29 Desemba 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Sunderland v Tottenham
[SAA 12 Jioni]
Aston Villa v Wigan
Fulham v Swansea
Man United v West Brom
Norwich v Man City
Reading v West Ham
Stoke v Southampton
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Arsenal v Newcastle
Jumapili 30 Desemba 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Chelsea
[SAA 1 Usiku]
QPR v Liverpool
Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Brom v Fulham
[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Southampton v Arsenal
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
SIMBA: HUKU ‘GOGORO’ LANUKIA, KOCHA MPYA KUTUA LEO!!
![SIMBA-normal](http://www.sokainbongo.com/images/stories/SIMBA-normal.jpg)
Akizungumzia Mkutano huo ulioitishwa na
Kundi la Mohamed Wandi ambalo limeripotiwa kukusanya Saini za Wanachama
698 ili kufanya Mkutano wa Wanachama Jumapili hii kwenye Hoteli ya
Traventine Jijini Dar es Salaam, Rage amesema uchunguzi wa Watu hao 698
umebaini kuwa 490 kati yao si Wanachama hai kwa vile hawajalipa Ada zao
za Uanachama na wengine kati yao ni Marehemu.
Akithibitisha kupokea Barua ya kuitishwa
Mkutano huo wa Dharura wa Wanachama, Rage amesema Kikatiba mwenye
mamlaka ya kuitisha Mkutano wa Dharura wa Wanachama ni Mwenyekiti au
Wanachama hai 600.
Kutokana na hitilafu hizo za Kisheria, Rage amesema Uongozi wake hautautambua Mkutano huo.
Pia, Rage amedai Kundi la Viongozi wa zamani ndio wanaotaka kuitisha Mkutano huo kinyume cha Katiba yao.
Hata hivyo, Mohamed Wandi amekaririwa
akitamka kuwa Mkutano huo hauna nia mbaya ila tu ni kuchambua mwendo
mbovu wa Simba katika mzunguko wa Kwanza wa Ligi Kuu Vodacom ambao
walianza vizuri mno lakini wakamaliza vibaya na kutupwa nafasi ya 3 huku
juu yao wapo Azam FC na vinara ni Mahasimu wao wakubwa, Yanga.
Wakati huo huo, Ismail Aden Rage,
amethibitisha ujio wa Kocha wao mpya, Patrick Liewing, kutoka Ufaransa
ambae atatua Nchini leo.
Rage amesema Kocha huyo, ambae aliwahi
kufundisha Timu za Vijana za Klabu maarufu huko France, Paris Saint
Germain, atakuwa Kocha Mkuu na pia atapewa jukumu la kuendeleza vipaji
vya Vijana.
Rage amesema: “Simba ndio Timu pekee
Nchini yenye mfumo wa kuendeleza Vijana na zipo timu za Vijana chini ya
Miaka 14, 16 17 na 20! Ujio wa Liewing utatusaidia sana kwa sababu ana
uzoefu wa kukuza vipaji!”
Kocha huyo mpya kesho anatarajiwa kukutana na Wachezaji wote kwenye Kambi yao ya Mazoezi huko TCC Chang’ombe, Dar es Salaam.
Liewing, ambae anambadili Kocha kutoka
Serbia Milovan Cirkovic, aliwahi kuwa Kocha wa Asec Mimosa ya Ivory
Coast kati ya Mwaka 2004 na 2009 na kuisaidia kutwaa Makombe kadhaa
Nchini humo pamoja na kuifikisha Nusu Fainali ya CAF CHAMPIONZ LIGI
Mwaka 2009.
Mwaka 2006, Kocha Liewing pamoja na Kocha wa Al Ahly ya Misri waliteuliwa kuwa Makocha Bora Afrika.
CHEKA AWAPA RAHA MASHABIKI WA NGUMI JIJI LA ARUSHA
Majaji wa pambano hilo ambao walikuwa watatu walitoa maksi kama ifuatavyo: David Chikwanje alimpa Cheka pointi 112/114 za Chimwemwe, Boniface Wambura alimpa Cheka pointi 118/114 za Chimwemwe na James Ligongo alimpa Cheka pointi 120/115 za Chimwemwe
Cheka ambaye alipigwa konde la haja likasababishwa kuchanika katikati ya paji la uso raundi ya pili aliweza kuhimili kumaliza raundi zote huku akitibiwa kila saa.
Baada ya Mpambano kumalizika Cheka allisema anashukuru ameshinda ila mpambano ulikuwa mgumu sana kwake na alikiri hajakutana na bondia mkali kama Chimwemwe kwa karibuni.
"Nashukuru nimeshinda ila nimeshinda kwa bahati kwani bondia niliyekutana naye ni bondia mzuri kwani angeweza kushinda ila alikosa mbinu chache tu", alisema Cheka.
Naye bondia Chiotka Chimwemwe alikubali matokeo na kusema ni mara yake ya kwanza kupigana nje ya nchi yake hivyo amechukulia kama changamoto kwake.
Cheka ameweza kutwaa Ubingwa wa IBF Afrika baada ya kunyang'anywa kwa kushindwa kuutetea kwa muda na akaenda kucheza na Karama Nyilawila ubingwa wa UBO ambao pia alimpiga Nyilawila.
Naye Meya wa jijini la Arusha Gaudence Lyimo alimpongeza promota wa pambano hilo Andrew George na Rais wa TPBC Onesmo Ngowi kwa kuleta pambano hilo la kimataifa Arusha na kusema atashirikiana nao kuwahakikisha anainua mchezo wa ngumi Arusha.
"Nawapongeza walioleta pambano hili Arusha na wnawaahidi tutakuwa tukishirikiana bega kwa bega kuahakikisha tunainua mchezo wa ngumi Arusha", alisema Meya.
Francis Cheka akiongea na waandishi wa Habari baada ya pambano kumalizika |
Frincis Cheka akikwepa konde la Chimwemwe |
Jaji Boniface Wambura akitafakari kitu kabla mpambano kuanza |
Subscribe to:
Posts (Atom)