Thursday, June 27, 2013

BADO HATUKO FITI KWA KOMBE LA DUNIA - SCOLARI.


KOCHA wa timu ya taifa ya Brazil, Luis Felipe Scolari amekiri kuwa kikosi chake bado hakiwezi kuanza kuota kunyakuwa taji lao la sita la Kombe la Dunia mwaka ujao lakini wamebakisha mechi moja kunyakuwa taji lao la tatu la Kombe la Shirikisho baada ya kuiengua Uruguay katika hatua ya nusu fainali. Scolari amesema anafikiri kikosi hicho kimefikia mahali pazuri lakini bado kuna vitu vingi vya kufanyia marekebisho mpaka kikamilike kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia mwakani. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa wanahamishia nguvu zao katika mchezo wa fainali na baada ya hapo wataangalia mapungufu yalijitokeza ili kuhakikisha wanakuwa na kikosi imara kitakachoweza kulibakisha Kombe la Dunia nyumbani. Brazil kwasasa wanasubiri mshindi wa nusu fainali nyingine ya michuano hiyo itakayopigwa baadae leo kati ya mabingwa wa Ulaya na Dunia Hispania watakaochuana na Italia.

ROGER FEDERER. ASEMA BADO SIJAFULIA -


MCHEZAJI tenisi nyota wa Switzerland, Roger Federer amesisitiza kuwa bado ataendelea kucheza mchezo huo kwa miaka mingi ijayo pamoja na kutolewa mapema katika michuano ya Wimbledon jana. Nyota huyo ambaye anashika namba tatu katika orodha za ubora duniani amesema hana hofu yoyote pamoja na kutolewa na Sergiy Stakhovisky wa Ukraine katika mzunguko wa pili wa michuano hiyo. Katika mchezo huo Federer aliburuzwa kwa kufungwa 6-7 7-6 7-5 7-6 na Stakhovsky anayeshika namba 116 katika orodha za ubora duniani. Baadhi ya wadau wa mchezo huo wamekuwa wakihoji kiwango cha Federer mwenye umri wa miaka 31 na kudai kuwa amekwisha lakini mwenye amesisitiza kuwa bado yuko fiti na ataendelea kucheza kwa miaka kadhaa ijayo. Kwa upande wa wanawake mwanadada nyota anayeshika namba mbili kwa ubora kwa upande wanawake Maria Sharapova wa Urusi naye aliyaaga mashindano hayo baada ya kukubali kipigo cha 6-3 6-4 kutoka kwa Michelle Larcher de Brito wa Ureno anayeshika namba 131 katika orodha hizo.

HATIMAYE MSHAMBULIAJI HATARI WA ZAMANI WA MAN U TEVES ATUA JUVENTUS.


KLABU ya Juventus ya Italia jana ilimtangaza rasmi kumsajili mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Argentina, Carlos Tevez kutoka timu ya Manchester City kwa mkataba wa miaka mitatu. Taarifa zinadai kuwa klabu yenye maskani yake katika jiji la Turin wamelipa kiasi cha paundi milioni 10 kwa nyota huyo mwenye umri wamiaka 29. Lakini Tevez atatakiwa kumaliza adhabu yake ya kutumikia jamii kwa saa 250 ili kuondoka jijini London salama na kuepuka kuburuzwa tena mahakamani. Tevez alikatisha likizo yake huko Amerika Kusini na kupanda ndege kuelekea Italia jana lakini pia atatakiwa kumaliza adhabu yake aliyopewa na mahakama ya Macclefield April mwaka huu kwa kuendesha huku akiwa amefungiwa kufanya hivyo.

WEBBER AAMUA KUACHANA NA LANGALANGA MWISHONI MWA MSIMU.


DEREVA nyota wa langalanga wa timu ya Red Bull, Mark Webber ameamua kuachana na mashindano hayo ikifikapo mwishoni mwa msimu huu. Katika miaka 12 ambayo amekuwa akishiriki michuano ya langalanga Webber ambaye pia amewahi kuendesha katika timu za Minard, Jaguar na Williams ameshinda mashindano mbalimbali ya Grand Prix mara tisa na kumaliza katika nafasi ya tatu katika mashindano ya dunia mara tatu. Akihojiwa kuhusiana na uamuzi huo Webber amedai kuwa anadhani huo ni wakati muafaka kwake kuachana na mbio za langalanga na kuangalia mambo mengine. Msimu wake mzuri ulikuwa ni mwaka 2010 ambapo aliongoza karibu msimu wote kabla ya kuteleleza katika mashindano matatu ya mwisho na kushuhudia dereva mwenzake wa Red Bull Sebastian Vettel na Fernando Alonso wa Ferrari wakimpita. Dereva wa Lotus Kim Raikkonen ambaye ni bingwa wa michuano ya dunia mwaka 2007 ndio anapewa nafasi kubwa kuchukua nafasi ya Webber ambaye aliingia katika langalanga mwaka 2002.

YANGA SC KUCHEZA NA KCC YA UGANDA KATIKA ZIARA YA KOMBE KANDA YA ZIWA


MSHAMBULIAJI nyota Tanzania, Mrisho Ngassa aliyerejea Yanga SC majira haya ya joto akitokea kwa wapinzani wa jadi, Simba SC, zote za Dar es Salaam ataanza rasmi kuichezea timu hiyo Juni 6, mwaka huu mjini Mwanza.
Mabingwa hao wa Tanzania Bara na Afrika Mashariki na Kati, Yanga SC watacheza na KCC ya Uganda badala ya Rayon Sport ya Rwanda Julai 6 na 7, mwaka huu katika sehemu ya ziara yake ya kulitembeza Kombe lake la ubingwa wa Ligi Kuu mikoa ya kanda ya Ziwa, ambayo inadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).
TBL imekuwa ikiidhamini Yanga SC kupitia bia yake, Kilimanjaro Premeum Lager tangu mwaka 2008 sawa na wapinzani wao wa jadi, Simba SC na ndiyo wamedhamini ziara hiyo.
Akizungumza na Waadishi wa Habari leo asubuhi, makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam, Ofisa Habari wa Yanga SC, Baraka Kizuguto amesema kwamba timu itaondoka Julai 5 Dar es Salaam, siku mbili tu baada ya kuanza mazoezi Uwanja wa sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam kuelekea Mwanza tayari kwa mchezo wa kwanza dhidi ya wapinzani wao hao, Uwanja wa CCM Kirumba, Julai 6.
Kizuguto amesema Julai 7, timu hizo zitarudiana kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga na baada ya hapo, mabingwa hao mara tano wa Kombe la Kagame (Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati), Yanga SC wataelekea mjini Tabora, kucheza mechi nyingine na wenyeji, Rhino FC waliopanda Ligi Kuu msimu huu Julai 11, mwaka huu Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi.
Katika ziara hizo, Yanga watatembeza Kombe lao la ubingwa wa Ligi Kuu, walilolitwaa kwa mara ya 24 msimu huu kwenye mitaa mbalimbali kushangilia na mashabiki wao. 
Yanga SC imeshindwa kwenda Sudan kutetea Kombe lake la Kagame mwaka huu, kutokana hofu ya machafuko yanayoendelea nchini humo na hii inakuwa mara ya pili kihistoria klabu hiyo kugoma kwenda kutetea taji hilo, baada ya awali mwaka 2000 kukataa kwenda Rwanda, hadi walipwe fedha zao za zawadi kwa kutwaa taji la mwaka uliotangulia 1999 mjini Kampala, Uganda.
Yanga SC, imekuwa na mafanikio makubwa tangu ianze kudhaminiwa na TBL, ikitwaa jumla ya mataji sita katika kipindi hicho, yakiwemo mawili ya Kagame, 2011 na 2012 na manne ya Ligi Kuu Bara, 2008, 2009, 2011 na 2013.
Katika kipindi hicho, hadhi ya klabu ya Yanga imepanda kutoka klabu isiyo na gari hata moja, hadi sasa kuwa mabasi matatu ya viwango tofauti, dogo aina ya Hiece, kubwa aina ya Coaster na kubwa zaidi aina ya Yutong kwa ajili ya safari za nje ya Jiji, ambayo yote wamepewa na wadhamini wao hao wakuu.
Kwa ujumla udhamini wa TBL umeleta ahueni kubwa ndani ya Yanga katika suala la uendeshaji wa timu, kutoka kwenye kushindwa kulipa mishahara ya makocha na wachezaji, hadi sasa kuwa na uhakika wa kufanya yote hayo sambamba na kusajili wachezaji ‘babu kubwa’ barani, kama Haruna Niyonzima, raia wa Rwanda. Mkataba wa awali baina ya Yanga na TBL, ulisainiwa Agosti 18, mwaka 2008 katika hoteli ya Movenpick, mjini Dar es Salaam, ukiwa na thamani ya Sh bilioni 3 za Kitanzania na kwa miaka mitatu, ikiwa kila mwaka inapata Sh Bilioni 1, kwa ajili ya shughuli za uendeshaji wa timu 
Agosti 2, mwaka 2011, TBL ilisaini Mkataba wa udhamini na Yanga wa miaka minne sawa na kwa watani wao pia, Simba SC.
Katika mkataba huo mpya, uliotiwa saini kwenye hoteli ya Double Tree, Masaki, Dar es Salaam, TBL iliongeza dau la fedha za mishahara kwa wachezaji kutoka Sh. Milioni 16 hadi Milioni 25 kwa mwezi, ikaongeza basi moja kubwa, Yutong lenye uwezo wa kubeba abiria 54 na fedha kwa ajili ya kugharamia mikutano ya wanachama ya kila mwaka Sh. Milioni 20 kugharamia tamasha la mwaka la klabu na vifaa vya michezo vyenye thamani ya Sh. Milioni 35 kila msimu.
Yanga pia inapewa bonasi ya Sh. Milioni 25 ikitwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara au Milioni 15, ikishika nafasi ya pili katika Mkataba huo wenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 5 tangu Agosti 8, mwaka huu hadi Julai 31, mwaka 2016.

BARCELONA YAHAHA KUMZUIA THIAGO ALCANTARA ASIENDE MAN UNITED...LAKINI WAAAPIII!


IMEWEKWA JUNI 27, 2013 SAA 1:00 ASUBUHI
KLABU ya Barcelona itakuwa na mazungumzo mazito kwa mara ya mwisho na Thiago Alcantara kujaribu kumzuia kiungo huyo wa Hispania asitimkie Manchester United.
Mabingwa wa Ligi Kuu ya England wamekubaliana na mchezaji huyo kumlipa mshahara wa Pauni Milioni 5.5 kwa mwaka kupitia kwa baba yake Thiago, aliyewahi kutwaa Kombe la Dunia akiwa na kikosi cha Brazil, Mazinho, na wana uhakika wa kumalizia dili kwa kuilipa Pauni Milioni 17 klabu yake ya uhamisho.
Barca bado ina matumaini ya kumbakiza kiungo huyo mwenye umri wa miaka 22 kwa kumuahidi atakuwa kiongozi klabu hiyo kwa miaka ijayo, lakini anabakia kuwa asiyeshawishika baada ya kusotea namba kwenye kikosi cha kwanza.
In demand: Thiago Alcantara, with the U21 Euros trophy, has agreed terms with Manchester United
Anabaki, habaki: Thiago Alcantara, akiwa na taji la Ulaya la U21, tayari amekubaliana na Manchester United
Thiago amekwenda mapumzikoni, akimuacha baba yake na wawakilishi wake wazungumze na mabingwa hao wa Hispania, ambao wanatarajiwa kuiambia Barcelona kwamba wanataka kutoka Nou Camp kuhamia Old Trafford.
United imefanya jitihada kubwa kuhakikisha inampata mchezaji huyo, ikiamini Manchester City na Bayern Munich wanaweza kutoa ofa.
Inafahamika hawana mpango na mshambuliaji wa Napoli, Edinson Cavani lakini wanaendelea kufuatilia sakata la Mkataba wa Cristiano Ronaldo Real Madrid.
Nyota huyo wa zamani wa United, ameahidiwa Pauni Milioni 12 kwa mwaka ili abaki Bernabeu, lakini anataka Milioni 5 zaidi na hajafirahishwa na maneno ya karibuni ya Rais wa Real, Florentino Perez kwamba kila kitu kina kiwango chake.
Hero's return? United are looking into the possibility of re-signing Real Madrid star Cristiano Ronaldo
Shujaa anarudi? United inaangalia uwezekano wa kumrejesha Cristiano Ronaldo
New boss: David Moyes is looking to stamp his mark on United's etam in his first season in charge
Kocha mpya: David Moyes anataka kujenga kikosi imara kabla ya kuanza kazi rasmi United

NI KIPIMO TOSHA 2014 POULINHO AIPELEKA BRAZIL FAINALI KOMBE LA MABARA IKIIUA URUGUAY 2-1, FORLAN AKIKOSA PENALTI


Paulinho ameibeba Brazil leo

IMEWEKWA JUNI 27, 2013 SAA 6:37 USIKU
BAO la kichwa la Paulinho zikiwa zimesalia dakika nne kabla ya filimbi ya mwisho, limeipa Brazil ushindi wa 2-1 dhidi ya Uruguay usiku huu na kutinga Fainali ya Kombe la Mabara.
Diego Forlan alikosa penalti dakika ya 13, baada ya beki wa Chelsea, David Luiz kumuangusha Diego Lugano kwenye eneo la hatari.
Brazil ilipata bao la kuongoza dakika ya 40, wakati Neymar alipoitokea pasi ndefu ya Paulinho na kuingia ndani kisha kufumua shuti lililombabatiza beki wa Uruguay kabla ya kumkuta Fred, aliyefunga.
Iliwachukua Uruguay dakika tatu tangu kuanza kipindi cha pili kusawazisha bao hilo, baada ya mabeki wa Brazil kuzembea kuondosha mpira kwenye eneo la hatari wakati pasi hafifu ya Thiago Silva ilipomkuta Edinson Cavani aliyefunga.
Fainali ya michuano hiyo 'amsha amsha' kuelekea Fainali za Kombe la Dunia, itapigwa mjini Rio de Janeiro kwenye Uwanja wa Maracana Jumapili.
Brazil ilibadilisha kikosi kutoka kile kilichoifunga Italia katika mechi yao ya mwisho ya Kundi A, ikimuanzisha Paulinho badala ya Hernanes katika kiungo.
Uruguay ilimuacha nje Abel Hernandez, mshambuliaji kinda wa Palermo, ambaye alifunga mabao manne dhidi ya Tahiti katikati ya wiki, na kuwaanzisha kwa pamoja mbele ya mdomo wa goli Luis Suarez, Diego Forlan, na Edinson Cavani.
Huo ni ushindi wa nne mfululizo kwa Brazil katika michuano ya mwaka huu na wao tano kwa jumla chini ya kocha Luiz Felipe Scolari, kasi ambayo inaweza kuwainua kutoka nafasi ya 22 katika viwango vya FIFA, nafasi ya chini zaidi kwao kuwahi kushika daima.
Pia unaendeleza rekodi ya kutofungwa na wapinzani wao hao wa Amerika Kusini katika mechi nane sasa tangu Julai 2001.
Katika mchezo huo, kikosi cha Brazil kilikuwa; Julio Cesar, Dani Alves, Thiago Silva, Luiz, Marcelo, Oscar/Hernanes dk72, Gustavo, Paulinho, Fred, Hulk/Bernard dk64 na Neymar/Dante dk90.
Uruguay: Muslera, Lugano, Godin, Caceres, Maxi Pereira, Rodriguez, Arevalo Rios, Gonzalez/Gargano dk83, Forlan, Suarez na Cavani.
Joy: Brazil booked their place in the final of the Confederations Cup with a 2-1 win over Uruguay
Furaha: Brazil wametinfa Fainali kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Uruguay
Hero: Paulinho headed home the winning goal for the hosts in the 86th minute
Shujaa: Paulinho akifunga kwa kichwa bao la ushindi dakika ya 86
Hero: Paulinho headed home the winning goal for the hosts in the 86th minute
Opener: Fred fired Brazil into the lead four minutes before half-time
La kwanza: Fred akiifungia Brazil dakika nne ya kabla mapumziko
Delight: Fred celebrates his strike in front of the adoring fans in Belo Horizonte
Delight: Fred celebrates his strike in front of the adoring fans in Belo Horizonte
Fred na Neymar wakishangilia mbele ya mashabiki Belo Horizonte
Brazil 
The crowd cheers
Response: Edinson Cavani equalised for Uruguay early in the second half
La kusawazisha: Edinson Cavani aliisawazishia Uruguay mapema kipindi cha pili
Uruguay's Edinson Cavani
Slotted: Cavani found the bottom corner as he guided the ball past the despairing Juilo Cesar
Kudadadeeki: Cavani alivyofunga
Slotted: Cavani found the bottom corner as he guided the ball past the despairing Juilo Cesar
Incredible: This Brazil fanshowed his support for Hulk as his side reached the final
Jitu Kali: Shabiki la Brazil likimsapoto Hulk
Hulk
Colourful: Brazil fans enjoy the atmosphere at Belo Horizonte for the semi-final
Maua mazuri: Mashabiki wa Brazi
Fans of Brazil