Habari za michezo

 

AZAM YATUMA SALAMU YANGA, YAIPA COASTAL KIPIGO CHA MWANA UKOME

Khamis Mcha 'Vialli' na Gaudence Mwaikimba wakishangilia leo Chamazi
KOCHA Muingereza Stewart Hall amerejea na ‘bonge la zali’, baada ya leo kuiongoza timu hiyo kuichapa Coastal Union ya Tanga mabao 4-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Stewart alitua jana usiku Dar es Salaam akitokea Kenya alipokuwa anaifundisha Sofapaka ya Ligi Kuu ya huko, baada ya kufukuzwa Azam Agosti mwaka huu na leo ameanza kazi, akirithi mikoba ya Mserbia, Boris Bunjak aliyefukuzwa Jumatatu.
Kwa ushindi huo, Azam imefikisha pointi 21, baada ya kucheza mechi 10 na sasa inarejea nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu, nyuma ya Simba na Yanga, zenye pointi 23 zote baada ya kucheza mechi 11, kila timu.
Katika mechi hiyo iliyochezeshwa na refa Simon Mbelwa, aliyesaidiwa na Abdallah Rashid wote wa Pwani na Michael Mkongwa wa Njombe, hadi mapumziko Azam tayari walikuwa wanaongoza kwa mabao 3-0.
Gaudence Mwaikimba aliifungia Azam bao la kwanza kwa kichwa dakika ya 23 kabla ya Kipre Tcheche kufunga la pili dakika ya 36, baada ya kuipasua ngome ya Coastal na Khamis Mcha ‘Vialli’ akafunga la tatu dakika ya 44.
Coatsal walianza vizuri mechi hiyo na kusukuma mashambulizi langoni mwa Azam, lakini baada ya dakika 20, wakapoteza mwelekeo na kuanza kuwaruhusu wapinzani wao kuvuna mabao. 
Kipindi cha pil, Azam walirudi na moto wao, lakini kidogo Coastal walibadlika nao na kufanya mchezo uwe mgumu kidogo.
Hata hivyo, walikuwa ni Azam tena waliotikisa nyavu za Coastal, baada ya kiungo Othman Tamim kujifunga dakika ya 73 katika harakati za kuokoa.
Baada ya bao hilo, Coastal walizinduka na kuanza kushambulia kupitia pembeni, jambo ambalo liliwasaidia kupata bao la kufutia machozi lililofungwa ma kiungo Jerry Santo.
Kwa ujumla katika mchezo wa leo, Coastal walizidiwa katika safu ya kiungo ambako leo Stewart alipanga viungo wengi waliotekeleza majukumu yao vyema.
Baada ya mchezo huo, kocha wa Coastal, Hemed Morocco alisema kwamba walizidiwa uwezo na wapinzani wao na kwa ujumla vijana wake walicheza chini ya kiwango leo, hata hivyo anakwenda kufanyia kazi makosa ili timu irejeshe makali yake.
Stewart alisema anafurahi kukaribishwa na ushindi huo mnono na kwamba hizo ni dalili njema. Aliwapongeza vijana wake kwa kucheza kwa kufuata maelekezo yake na akasema kwamba sasa anaelekeza nguvu zake katika mchezo ujao dhidi ya Yanga Jumapili, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.   
 
 
Azam FC; Mwadini Ally, Samir Hajji, Ibrahim Shikanda, Aggrey Morris, Said Mourad, Kipre Balou/Ibrahim Mwaipopo, Jabir Aziz, Salum Abubakar/Himid Mao, Gaudence Mwaikimba/Abdi Kassim, Kipre Tcheche na Khamis Mcha ‘Vialli’.
 
Coastal Union; Jackson Chove, Said Swedi, Juma Jabu, Mbwana Hamisi, Jamal Machelanga/Salim Gilla, Jerry Santo, Suleiman Kassim ‘Selembe’, Razack Khalfan/Hamisi Shango, Daniel Lyanga, Atupele Green/Lameck Dayton na Othman Tamim

LEO TFF: UAMUZI KUHUSU RUFANI ZA CHAGUZI ZA WANACHAMA!!

>>IFUATAYO NI TAARIFA KAMILI YA TFF:
TANZANIA FOOTBALL FEDERATION (TFF)
ELECTIONS COMMITTEE
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UAMUZI KUHUSU RUFANI DHIDI YA KAMATI ZA UCHAGUZI ZA VYAMA VYA MPIRA WA MIGUU MKOA WA MWANZA (MZFA), MKOA WA GEITA (GEREFA) NA KUHUSU MICHAKATO YA UCHAGUZI YA VYAMA WANACHAMA WA TFF NA WANACHAMA WAO
OKTOBA 31, 2012
Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuzingatia Katiba ya TFF Ibara ya 49(1), Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF Ibara ya 8(2), 10(6), 12(1) na 26(2) na (3) katika kikao chake kilichofanyika Oktoba 30, 2012 ilijadili rufani dhidi ya Kamati za Uchaguzi za MZFA na GEREFA na michakato ya uchaguzi ya vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Mwanza, Rukwa, Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake (TWFA), Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) na Chama cha Wanasoka Tanzania (SPUTANZA) na kutoa uamuzi kama ifuatavyo;
1.      Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA)
(a)    Rufani ya Ndg. Jackson Manji Songora: Kamati ilijadili rufani iliyowasilishwa na Ndg. Jackson Manji Songora dhidi ya Kamati ya Uchaguzi ya MZFA, iliyoomba Kamati ya Uchaguzi ya TFF kubatilisha uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya MZFA kumpitisha Ndg. Jumbe O. Magati kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa MZFA, kwamba Kamati ya Uchaguzi ya MZFA ilikosea:
(i)Kupokea Statement of Results ya Baraza la Mitihani Tanzania yenye jina la Fredrick J. Magati wakati jina la mgombea alilojaza kwenye fomu ya maombi ya uongozi ni Jumbe O. Magati.
(ii)Kumsaili Jumbe O. Magati kwa kuwa hakuwasilisha nakala halisi ya cheti cha elimu yake.
(iii)Kumpitisha Ndg. Jumbe O. Magati kugombea uongozi na kuwa Ndg. Jumbe O. Magati hana sifa zinazokidhi matakwa ya Katiba ya MZFA Ibara ya 29(2).
Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilipitia maelezo ya Mrufani na ilijiridhisha kuwa rufani iliyowasilishwa mbele yake na Ndg. Songora haikutanguliwa na pingamizi mbele ya Kamati ya Uchaguzi ya MZFA, hivyo ilikosa sifa ya kuwa rufani kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF. Hata hivyo, kwa mujibu wa Katiba ya TFF Ibara ya 49(1); Katiba ya MZFA Ibara ya 47 na Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF Ibara ya 26(2), Kamati ya Uchaguzi ya TFF, kwa kutumia mamlaka yake ya kikatiba na kanuni za uchaguzi, ilimuhoji Ndg. Magati kuhusu elimu yake na majina yaliyo kwenye Statement of Results na fomu yake ya maombi ya uongozi.
Baada ya kupitia vielelezo na maelezo yaliyowasilishwa mbele ya Kamati kuhusu majina ya Ndg. Jumbe O. Magati, Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilijiridhisha kuwa Jumbe O. Magati na Fredrick J. Magati ni mtu huyo huyo. Kamati ya Uchaguzi imetupa rufani ya Ndg. Patrick Manji Songora.
2.      Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Geita (GEREFA)
(a)    Rufani ya Ndg. Abdallah H. Hussein: Kamati ilijadili rufani iliyowasilishwa mbele yake na Ndg. Abdallah H. Hussein ikipinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya GEREFA kuliondoa jina lake kugombea nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF, kwa kigezo cha kutokuwa Mkazi wa Mkoa wa Geita. Kamati ilipitia vielelezo vilivyowasilishwa mbele yake na Mrufani na ilijiridhisha kuwa vielelezo hivyo vinakidhi kuthibitisha kuwa mwombaji uongozi ni Mkazi wa Mkoa wa Geita. Kamati inakubaliana na maombi ya mrufani na inamrejesha Ndg. Abdallah H. Hussein kugombea nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF.
(b)   Rufani ya Ndg. Aziz Mwamcholi: Kamati ilijadili rufani iliyowasilishwa mbele yake na Ndg. Aziz Mwamcholi ikipinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya GEREFA kuliondoa jina lake kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa GEREFA, kwa kigezo cha kushindwa kuwasilisha cheti cha elimu ya sekondari.  Kamati ilipitia maelezo ya Ndg. Mwamcholi na ya Kamati ya Uchaguzi ya GEREFA na ikajiridhisha kuwa Ndg. Mwamcholi hakukidhi matakwa ya Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF, hususan Ibara ya 10(5). Kamati imekubaliana na uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya GEREFA wa kutompitisha Ndg. Mwamcholi kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa GEREFA. Kamati ya Uchaguzi ya TFF imetupa rufani hiyo.
(c)    Rufani ya Ndg. Kaliro Samson: Ndg. Samson aliwasilisha rufani kupinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya GEREFA kuliondoa jina lake kugombea nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF kwa kigezo cha kutowasilisha cheti cha kuhitimu elimu ya kidato cha nne. Kamati ilipitia maelezo na vielelezo vya rufani ya Ndg. Samson nay a Mrufaniwa na kujiridhisha kuwa nakala ya cheti cha elimu ya kidato cha sita inakidhi matakwa ya Katiba ya GEREFA Ibara ya 29(2). Kamati inakubaliana na maombi ya mrufani na inamrejesha Ndg. Kaliro Samson kugombea nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF.
3.      Mchakato wa Uchaguzi Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA)
Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilijadili mchakato wa uchaguzi wa MZFA ikiwa ni pamoja na mchakato wa uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Ukerewe (UDFA), baada ya uchaguzi wa awali wa UDFA kuwa umefutwa na Kamati ya Uchaguzi ya MZFA kutokana na Kamati ya Uchaguzi ya UDFA kutozingatia Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
Baada ya maelezo ya kina ya Kamati ya Uchaguzi ya MZFA na vielelezo vilivyowasilishwa mbele ya Kamati kuhusu mwenendo wa uchaguzi wa UDFA, Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilibaini kuwa kuna ukiukwaji mkubwa wa Kanuni na taratibu za uchaguzi uliofanywa na Kamati ya Utendaji ya UDFA kwa kutozingatia kikamilifu maagizo ya Kamati ya Uchaguzi ya MZFA na hivyo kusababisha mkanganyiko katika mchakato wa Uchaguzi ambao kwa wakati mmoja ulikuwa na Kamati mbili za Uchaguzi kusimamia uchaguzi huo. Mikanganyiko inayojionyesha dhahiri na kusababisha nafasi zote sita zinazogombewa katika mchakato unaoendelea kuwa na mgombea mmoja mmoja tu katika kila nafasi, imeufanya mchakato wa uchaguzi wa UDFA kupoteza hadhi ya uchaguzi unaozingatia Kanuni za Uchaguzi na misingi ya demokrasia na uwazi kama ilivyoainishwa katika Kanuni za Uchaguzi za TFF. Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa mamlaka yake ya kikatiba Ibara ya 49(1) ya Katiba ya TFF na Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF, Ibara ya 10(6) na 26(2) na (3) imeamua:
(i)Kuzifuta Kamati zote za Uchaguzi za UDFA zilizoteuliwa na Kamati ya Utendaji ya   UDFA kabla ya baada ya mchakato wa uchaguzi wa sasa wa UDFA.
(ii) Kuufuta Uchaguzi wa UDFA uliokuwa ufanyike Novemba 5, 2012. Mchakato wa uchaguzi utaanza upya kwa tarehe zitakazopangwa na Kamati ya Uchaguzi ya MZFA baada ya kupata maelekezo ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF.
(iii) Kuiagiza Kamati ya Uchaguzi ya MZFA katika kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Ibara ya 6 ya Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF kutoiruhusu UDFA kushiriki Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa MZFA kwa kuwa UDFA imeshindwa kuzingatia matakwa ya Katiba kuhusu ukomo wa mamlaka ya Kamati ya Utendaji na kufanya uchaguzi kwa wakati muafaka unaozingatia Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
4.      Mchakato wa Uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake (TWFA)
Kwa kuzingatia changamoto za kuijenga TWFA ambayo bado ni change, Kamati ya Uchaguzi ya TFF imekubali ombi la TWFA la kusogeza mbele tarehe ya uchaguzi kwa wiki mbili. Uchaguzi wa TWFA ngazi ya Taifa sasa utafanyika Novemba 18, 2012.
5.      Mchakato wa Uchaguzi wa Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania (FRAT)
Uchaguzi wa viongozi wa FRAT utafanyika Novemba 17, 2012 kama ulivyopangwa.
6.      Mchakato wa Uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Rukwa (RUREFA)
TFF imesimamisha kuanza kwa mchakato wa uchaguzi wa RUREFA kutokana na wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya RUREFA kuendeleza malumbano kati yao kuhusu uhalali wa uteuzi wa Kamati mpya ya Uchaguzi ya RUREFA, uteuzi ambao ulifanywa na Kamati ya Utendaji ya RUREFA, Oktoba 18, 2012. Kwa kuwa hali hii imetokea tena baada ya Kamati ya Utendaji ya RUREFA kuwa imepewa fursa ya kikatiba kuteua Kamati ya Uchaguzi na ni mwendelezo wa mgawanyiko ndani ya Kamati ya Utendaji ya RUREFA unaoathiri mchakato wa uchaguzi wa chama hicho, Kamati ya Uchaguzi ya TFF inatafakari hatua muafaka za kikatiba na kikanuni zitakazoondoa ukwamishaji wa mchakato wa Uchaguzi wa RUREFA unaosababishwa na Kamati ya Utendaji ya RUREFA. Uamuzi kuhusu mustakabali wa Uchaguzi wa RUREFA utatolewa baada ya kikao cha Kamati ya Uchaguzi ya TFF kitakachofanyika Novemba 6, 2012. 
7.      Mchakato wa Chama cha Wanasoka Tanzania (SPUTANZA) na Chama cha Makocha (TAFCA)
Uamuzi kuhusu mustakabali wa uchaguzi wa SPUTANZA na TAFCA utatolewa baada ya vyama hivyo kuwasilisha taarifa za kina kuhusu michakato ya chaguzi za wanachama wao katika ngazi ya mikoa, katika kikao cha Kamati ya Uchaguzi ya TFF kitakachofanyika Novemba 6, 2012.
Moses Kaluwa
Mjumbe- Kamati ya Uchaguzi TFF

WACHEZAJI YANGA WAPO BAGAMOYO, BRANDTS ANAIFANYIA USHUSHUSHU AZAM CHAMAZI

Brandts akiwa Uwanja wa Chamazi mida hii


YANGA SC leo imeingia kambini katika hoteli ya Kiromo, Bagamoyo mkoani Pwani kujiandaa na mchezo wake wa Jumapili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Azam FC, Jumapili, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwa kawaida, Yanga huweka kambi Bagamoyo katikati ya Ligi, inapokuwa inajiandaa na mchezo dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Simba SC hivyo kwa kwenda huko kuweka kujiandaa na mchezo huo, maana yake wanaupa uzito sawa na pambano la watani.
Wakati vijana wa Yanga wakiwa Bagamoyo, Kocha Mkuu wa klabu hiyo, Mholanzi Ernie Brandts yupo kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, akiwafanyia ‘ushushushu’ wapinzani wake hao wanaomenyana na Coastal Union ya Tanga mida hii, kipindi cha kwanza wakiwa wanaongoza 3-0.    
Brandts jana aliiongoza Yanga SC kuendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuichapa Mgambo JKT ya Handeni, Tanga mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo, unaifanya Yanga sasa iwe na pointi sawa na mabingwa watetezi, Simba SC waliotoa sare ya 1-1 na Polisi mjini Morogoro leo, ingawa inazidiwa bao moja tu katika wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Hadi mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa mabao 2-0, yaliyotiwa kimiani na beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na mshambuliaji Didier Kavumbangu.
Cannavaro alifunga kwa kichwa akiunganisha krosi ya Oscar Joshua dakika ya pili kutoka wingi ya kulia, wakati Kavumbangu alimalizia pasi ya Hamisi Kiiza dakika ya 39.
Pamoja na kutoka uwanjani wamelowa kipindi cha kwanza, lakini Mgambo JKT walicheza soka ya kuvutia na mara mbili walikaribia kufunga kupitia kwa Juma Mwinyimvua.
Yanga walicheza vema dakika 45 za kipindi cha kwanza, tofauti sana na mechi za awali ambazo wamekuwa ‘wakichezewa’ sana na wapinzani.
Ilishuhudiwa katika kipindi hicho, Yanga wakimiliki zaidi mpira na kupeana pasi za uhakika, ingawa mashambulizi yao mengi walipitisha pembeni, hasa upande wa kulia.
Hamisi Kiiza, Msuva na Kavumbangu walicheza kwa uelewano mkubwa pale mbele na kulitia misukosuko haswa lango la Mgambo. 
Kipindi cha pili, Yanga walirudi na moto wao tena na kuendelea kuwachachafya Mgambo.
Hata hivyo, iliwachukua Yanga dakika 34 kupata bao la tatu, mfungaji akiwa ni Jerry Tegete aliyeingia dakika ya 68 kuchukua nafasi ya Kavumbangu.
Tegete alifunga bao hilo akiunganisha krosi maridadi ya beki wa kushoto, Oscar Joshua.
Pamoja na kufungwa, Mgambo waliendelea kusukuma mashambulizi langoni mwa Yanga, ingawa leo mabeki wa timu hiyo, inayofundishwa na Mholanzi, Ernie Brandts walicheza kwa uelewano mkubwa na kudhibiti hatari zote langoni mwao. 
Mgambo inayofundishwa na Mohamed Kampira, ilipata pigo dakika ya 85, baada ya beki wake wa kulia, Salum Mlima kutolewa kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kumchezea rafu mbaya Mbuyu Twite. 

YANGA WAFURIKA DRFA, SEIF MAGARI MWENYEKITI, ALLY MAYAY MAKAMU WAKE

seif magari akipokea fomu leo hii
MDAU maarufu wa soka nchini, Ahmed Seif Hemed ‘Magari’ amechukua fomu za kugombea Uenyekiti wa Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA) mchana wa leo katika ofisi za chama hicho, zilizopo makutano ya Mtaa wa Mafia na Bonde, kariakoo, Dar es Salaam.
Seif, ametimiza wajibu huo kufuatia ombi la wazee na wadau wa soka mkoani Dar es Salaam, kumtaka ajitokeze kuiokoa soka ya Jiji hilo, ambayo imebakiza umaarufu wa Simba na Yanga pekee.
Wadau wa soka Dar es Salaam tangu wiki iliyopita wamekuwa wakimbembeleza Seif kuchukua fomu za kugombea nafasi hiyo, wakiahidi kumuunga mkono mfanyabiashara huyo wa magari na fedha za kigeni kwa asilimia 100 ashinde nafasi hiyo.
Kwa kujitosa huko DRFA, Seif sasa atachuana na Salum Mkemi, Evans Aveva, Ayoub Nyenzi, Juma Jabir na Meba Ramadhan katika nafasi hiyo, ambao ndio pekee hadi sasa wamechukua fomu.
Wagombea wengine waliochukua fomu hadi leo Ally Mayay, nafasi ya Makamu Mwenyekiti, Said Tuliy, Msanifu Kondo, Hamisi Ambari, ambao wanawania nafasi ya Ukatibu Mkuu, Shaffi Dauda na Muhisn Balhabou, Ujumbe wa Mkutano Mkuu, Shaaban Mohamed, Andrew Tupa, Siza Abdallah Chenje, Sunday Mwanahewa na Lameck Nyambaya Ujumbe wa kamati ya Utendaji na Philemon Ntahilaja, Mwakilishi wa Klabu.
Akizungumza baada ya kuchukua fomu, Seif aliyesindikizwa na swahiba wake, Abdallah Bin Kleb, alisema kwamba ameamua kuitikia wito huo wa wazee na wadau wa soka Dar es Salaam kwa sababu ana nguvu, uwezo, upeo na dira ya kuendeleza soka ya Dar es Salaam.
“Naamini, kabisa nikifanikiwa kuwa Mwenyekiti mpya wa DRFA, nitaleta mabadiliko makubwa na maendeleo makubwa ya soka katika Jiji la Dar es Salaam,”alisema Seif.
Seif amekuwa kwenye Kamati za Yanga tangu wakati wa uongozi wa Francis Mponjoli Kifukwe miaka saba iliyopita na pia amewahi kuwa mmiliki mshiriki wa klabu ya Moro United iliyokuwa Ligi Kuu.
Seif ameendelea kuwa ndani ya Kamati za Yanga katika zama za viongozi waliomfuatia Kifukwe katika klabu hiyo, Imani Madega, Lloyd Nchunga na sasa Yussuf Manji.
Kuna uwezekano mkubwa mpinzani mkuu wa Seif, akawa Mwenyekiti wa zamani wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Evans Aveva ambaye naye pia ana uzoefu wa kutosha katika uongozi wa soka.
Aveva, aliyekuwa Meneja wa Hoteli ya Embassy na sasa mfanyabiashara mwenye maduka kibao ya simu, amekuwa kwenye Kamati mbalimbali za uongozi Simba tangu enzi za Yussuf Hazali, Mwenyekiti wa klabu hiyo na ameendelea pia hata katika zama za viongozi waliofuatia akina Juma Salum (sasa marehemu) na Hassan Daalal.
Aveva pia amewahi kuwa mmoja wa viongozi wa iliyokuwa Tanzania Stars, timu iliyokuwa ikiundwa na wachezaji wakongwe nchini, ambayo mwaka 1998 na 1999 ilicheza Kombe la Washindi Afrika.
Uchaguzi wa DRFA utafanyika Desemba 8, mwaka huu na fomu za kugombea nafasi mbalimbali zilianza kutolewa tangu Oktoba 29, wakati Novemba 4 hadi 8, Kamati ya Uchaguzi, chini ya Mwenyekiti wake, Juma Simba itapitia fomu za walioomba uongozi.
Novemba 9 hadi 13 utakuwa muda wa pingamizi kwa wagombea, ambazo zitajadiliwa Novemba 14 hadi 16, wakati Novemba 17 hadi 19 watatoa fursa ya kukata rufaa, ambazo zitasikilziwa Novemba 20 hadi 24 na baada ya hapo, Novemba 25 yatatangazwa majina ya wagombea waliopitishwa.
Uchaguzi wa DRFA utafanyika siku chache tu kabla ya uchaguzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), mwishoni mwa Desemba, mwaka huu.   

Seif Magari kulia akiwa na Abdallah Ahmad Bin Kleb na Ally Mayay

Seif akiipitia fomu yake

Ally Mayay kulia akipokea fomu yake

Ayoub Nyenzi akipokea fomu yake

Philemon Ntahilaja akipokea fomu





 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 


BRANDTS: WACHEZAJI YANGA SASA WANANIKOSHA

Brandts

KOCHA Mhoalanzi wa Yanga, Ernie Brandts amesema kwamba taratibu wachezaji wa klabu hiyo wanaanza kushika mafundisho yake na anaamini kama wataendelea hivyo, hadi kufika Januari timu hiyo itakuwa inacheza anavyotaka.
Akizungumza  jana mara baada ya mechi  , Brandts alisema kwamba wana Yanga bado wanahitaji kuwa na subira ili kumpa fursa ya kuijenga timu vyema.
“Si kazi ya wiki moja au mwezi mmoja, unahitajika muda ili kocha aweze kutengeneza timu ya ushindi na kucheza soka nzuri. Nahitaji muda kuwajua zaidi wachezaji na kujua namna ya kuwabadilisha, unaweza kuona taratibu timu inaanza kucheza soka ya kuvutia,”alisema.
Brandts aliiongoza Yanga SC kuendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuichapa Mgambo JKT ya Handeni, Tanga mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo, unaifanya Yanga sasa iwe na pointi sawa na mabingwa watetezi, Simba SC waliotoa sare ya 1-1 na Polisi mjini Morogoro leo, ingawa inazidiwa bao moja tu katika wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Hadi mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa mabao 2-0, yaliyotiwa kimiani na beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na mshambuliaji Didier Kavumbangu.
Cannavaro alifunga kwa kichwa akiunganisha krosi ya Oscar Joshua dakika ya pili kutoka wingi ya kulia, wakati Kavumbangu alimalizia pasi ya Hamisi Kiiza dakika ya 39.
Pamoja na kutoka uwanjani wamelowa kipindi cha kwanza, lakini Mgambo JKT walicheza soka ya kuvutia na mara mbili walikaribia kufunga kupitia kwa Juma Mwinyimvua.
Yanga walicheza vema dakika 45 za kipindi cha kwanza, tofauti sana na mechi za awali ambazo wamekuwa ‘wakichezewa’ sana na wapinzani.
Ilishuhudiwa katika kipindi hicho, Yanga wakimiliki zaidi mpira na kupeana pasi za uhakika, ingawa mashambulizi yao mengi walipitisha pembeni, hasa upande wa kulia.
Hamisi Kiiza, Msuva na Kavumbangu walicheza kwa uelewano mkubwa pale mbele na kulitia misukosuko haswa lango la Mgambo. 
Kipindi cha pili, Yanga walirudi na moto wao tena na kuendelea kuwachachafya Mgambo.
Hata hivyo, iliwachukua Yanga dakika 34 kupata bao la tatu, mfungaji akiwa ni Jerry Tegete aliyeingia dakika ya 68 kuchukua nafasi ya Kavumbangu.
Tegete alifunga bao hilo akiunganisha krosi maridadi ya beki wa kushoto, Oscar Joshua.
Pamoja na kufungwa, Mgambo waliendelea kusukuma mashambulizi langoni mwa Yanga, ingawa leo mabeki wa timu hiyo, inayofundishwa na Mholanzi, Ernie Brandts walicheza kwa uelewano mkubwa na kudhibiti hatari zote langoni mwao. 
Mgambo inayofundishwa na Mohamed Kampira, ilipata pigo dakika ya 85, baada ya beki wake wa kulia, Salum Mlima kutolewa kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kumchezea rafu mbaya Mbuyu Twite.
Baada ya mchezo huo, Brandts alisema dakika 10 za mwanzo timu yake ilikuwa inashindwa kumalizia vizuri mashambulizi yake, lakini baadaye ikatulia na hatimaye kupata ushindi huo, ambao ameufurahia kwani unamuweka katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Kwa upande wake, Kampira wa Mgambo alisema kufungwa ni sehemu ya mchezo, akawasifu Yanga kwa kutumia nafasi walizopata, huku akijutia nafasi walizopoteza wachezaji wake leo.
Kikosi cha Yanga leo kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Nsajigwa Shadrack/Kevin Yondan dk 46, Oscar Joshua, Mbuyu Twite, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Frank Domayo/Nurdin Bakari dk 76, Didier Kavumbangu/Jerry Tegete dk68, Hamisi Kiiza na Haruna Niyonzima.
Mgambo JKT; Godson Mmasa, Salum Mlima, Yassin Awadh, Salum Kipanga/Godfrey Komba dk80, Bakari Mtama, Ramadhani Malima, Chande Magoja, Mussa Ngunda, Issa Kandulu/Nassor Gumbo dk 60, Fully Maganga na Juma Mwinyimvua/Omar Matwiko dk76.
Katika mchezo wa utangulizi, timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Yanga, imeifunga Mgambo JKT ya vijana pia 1-0, bao hilo pekee la Clever Charles dakika ya 65.
Katika mechi nyingine, Simba ilitoka sare ya 1-1 Polisi kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, wenyeji wakitangulia kupata bao dakika ya 35 kupitia kwa Mokili Rambo kabla ya Amri Kiemba kusawazisha dakika ya 57. 

STEWART AWASILI KUICHINJA COASTAL UNION CHAMAZI LEO


LEO NI LEO kwenye Uwanja wa Chamazi, maarufu kama Azam Complex, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, ambako timu mbili zinazopigana vikumbo katika nafasi ya tatu, wenyeji Azam FC watamenyana na Coastal Union ya Tanga katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Hiyo ni moja kati ya mechi tamu za Ligi Kuu, zisizozihusisha Simba na Yanga, kwani ukiondoa wababe hao wa soka Tanzania, kama kuna timu nyingine inayoweza kufikiriwa japo kushika nafasi ya pili kwenye ligi hiyo, ni kati ya hizo, Azam na Coastal.
Azam imekuwa katika nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu kwa muda mrefu, kabla ya kushushwa hadi nafasi ya nne ndani ya siku mbili mwishoni mwa wiki na Coastal ndio ya tatu sasa, nyuma ya Yanga na Simba, zinazolinganana kwa pointi.
Coastal inayofundishwa na kocha mtaalamu, lakini ‘simpo tu’, Ahmed Morocco itamenyana na Azam leo ambayo itaongozwa na Kali Ongala, anayekaimu Ukocha Mkuu, kufuatia kufukuzwa kwa Mserbia, Boris Bunjak Jumatatu.
Baada ya kufukuzwa kwa Bunjak, Azam imekwishamrejesha kocha wake wa zamani, Muingereza Stewart Hall ambaye alitua jana usiku na leo atakuwapo Chamazi.
Bunjak ameondoka Azam baada ya kuiongoza timu katika mechi 16, akifungwa nne tu, zote dhidi ya Simba ikiwemo ya juzi ya Ligi Kuu, waliyofungwa 3-1 na kutoa sare tatu.
Bunjak mwenye leseni ya Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA), alitua Azam, Agosti 7, mwaka huu akitokea FC Damac ya Saudia Arabia aliyoanza kuifundisha mwaka jana na kabla ya hapo alifundisha klabu kibao za kwao, zikiwemo FK Sloga Kraljevo, FK Javor Ivanjica, Crvena Zvezda Gnjilane, FK Radnicki Nis, FC Uralan Elista, FK Mladi Radnik, FK Crvena Zvezda Beograd, Al-Shaab, FK Hajduk Kula na Al-Nasr.
Awali, Bunjak aliyezaliwa Novemba 17, mwaka 1954 ( miaka 57), alicheza soka katika klabu za FK Sloga (Kraljevo), FK Vozdovac (Beograd), FK Radnicki (Kragujevac), FK Olimpia (Ljubljana), FK Sumadija (Arandjelovac), FK Sloga (Kraljevo), FK Borac (Cacak) na FK Sloga (Kraljevo).
Stewart alifukuzwa kwa kosa la kukaidi maagizo ya Bodi ya Ukurugenzi ya klabu hiyo, kumpanga Mrisho Khalfan Ngassa katika mechi ya fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame dhidi ya Yanga.
Mserbia huyo anakuwa kocha wa tano kufukuzwa Azam, ndani ya miaka minne tangu ianze kucheza Ligi Kuu, 2008 baada ya Stewart, Mbrazil Neider dos Santos, Sylvester Marsh na Itamar Amorin, Mbrazil mwingine.
Lakini Stewart angalau aliacha kumbukumbu ya taji na Medali Azam, baada ya kuiwezesha kutwaa Kombe la Mapinduzi Januari, kushika nafasi ya pili katika Ligi Kuu Aprili, kabla ya kushika nafasi ya pili Kombe la Urafiki na Kagame mwezi uliopita, mambo ambayo bila shaka yamemfanya afikiriwe tena.
Stewart ana sifa ya kutokuwa mbinafsi na mwenye kuwaamini watu wa chini yake, kwa mfano namna ambavyo alikuwa akimpromoti Kali Ongala. Alimkuta Kali kama mchezaji, lakini kwa sababu ya umri kumtupa mkono, akashauriana naye awe Kocha Msaidizi na mshambuliaji huyo wa zamani wa Yanga, akakubali.
Chini ya Stewart, Kali alikuwa akiachiwa timu aiongoze ili kumjengea kujiamini zaidi na mwezi uliopita aliachiwa timu kwenye Kombe la Urafiki, akaifikisha fainali, ambako ilifungwa na Simba kwa penalti kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90. 
Yote kwa tote, Chamazi leo kinachotarajiwa ni soka safi, ile ya burudani, isiyokuwa na presha kutokana na timu hizo kutokuwa na mashabiki wenye ugonjwa wa moyo kama wale wa Simba na Yanga.
Wakati huo huo: Stewart Hall alitua jana usiku mjini Dar es Salaam na kusema anataka Azam ishinde kila mechi kuanzia sasa baada ya kurejea kazini.
Hall amerejea katika klabu yake ya zamani ya Azam baada klabu aliyokuwa akiifundisha Sofapaka ya Kenya inayomilikiwa na tajiri kukiri kwamba haiwezi kupambana na kampuni kubwa ya Azam ambayo imeahidi kumpa mshahara mara mbili ya waliokuwa wakimlipa Wakenya hao.
Mashabiki waliokuwa uwanjani hapo wakipuliza mavuvuzela na kupiga ngoma, waliimba nyimbo mbalimbali ukiwamo uliosema "Hall amerejea, homa na presha za Simba na Yanga ziko juu."
Baada ya kutua kocha huyo, alivishwa mataji ya maua na viongozi wa Azam waliokuwapo kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere kwa ajili ya kumpokea



RATIBA TUSKER CHALLENGE YASOGEZWA MBELE.

Rogers Mulindwa, Cecafa Media Officer.
RATIBA ya michuano ya Kombe la Tusker kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati-CECAFA ambayo ilikuwa ipangwe Novemba 8 mwaka huu jijini Kampala imesogezwa mbele kwa siku nne zaidi. 

 Michuano hiyo ambayo itaanza kutimua vumbi Novemba 24 mpaka Desemba 8 jijini Kampala katika Uwanja wa Taifa wa Mandela uliopo Namboole ratiba yake sasa itapangwa Novemba 12.

 Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka nchini Uganda-FUFA ambaye pia anafanya shughuli hiyo CECAFA, Rogers Mulindwa aliwaambia waandishi wa habari jijini Kampala mabadiliko ya tarehe hiyo bila kutoa maelezo zaidi ya sababu iliyopelekea kusogezwa mbele kwa uapngwaji huo wa ratiba. 

 Wakati michuano hiyo ikianza Uganda haitakuwa ikitetea taji hilo pekee lakini pia kushinda taji kwa rekodi ya mara 13 toka michuano hiyo ianzishwe.

MVUA ya MAGOLI Jumamosi Man United v Arsenal Old Trafford??

>>ARSENAL haijashinda Old Trafford katika Mechi 8 za mwisho!!
>>RVP kuivaa Timu yake ya zamani kwa MARA ya KWANZA!!
RVP_in_RED>>PATA DONDOO na REKODI za Mechi Man United v Arsenal!
Jumamosi Novemba 3, ndani ya Uwanja wa Old Trafford, Manchester United itaikaribisha Arsenal katika moja ya Mechi za Ligi Kuu England, BPL, ambayo inangojewa kwa hamu kubwa kwani inazikutanisha Timu ambazo, kati yao, zimefunga na kufungwa jumla ya Magoli 41 katika Mechi 8 kuanzia Oktoba 20 na pia mvuto upo kumuona Nahodha wa zamani wa Arsenal, Robin van Persie, akiivaa Klabu yake ya zamani kwa mara ya kwanza tangu ahamie Man United mwanzoni mwa Msimu huu.
Bila shaka, Arsenal watakuwa na wasiwasi kumvaa Straika ambae wakiwa nae Msimu uliopita aliifungia jumla ya Magoli 37 na tangu atue Man United mtambo wake wa magoli umeendelea mtindo mmoja.
Juzi Jumanne, Arsenal walitoka nyuma kwa Bao 4-0 walipocheza kwenye Kombe la Ligi na kuifunga Reading 7-5 katika Dakika 120 za Mchezo huku Theo Walcott akipiga hetitriki.
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO Timu za juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 9]
1 Chelsea Pointi 22
2 Man United 21 [Tofauti ya Magoli 11]
3 Man City 21 [Tofauti ya Magoli 9]
4 Tottenham 17
5 Everton 16
6 Arsenal 15
7 Fulham 14
8 WBA 14
9 West Ham 14
10 Newcastle 13
MAN_UNITED-ANDO_RVP_SHINJI_EVRA+++++++++++++++++++++++WALCOTT_WILSHERE_OX
Msimu uliopita, Mwezi Agosti Mwaka jana Uwanjani Old Trafford, Arsenal walichabangwa bao 8-2 kwenye Mechi ya Ligi na Msimu huu Man United wamekuwa wakiendeleza wimbi lao la kufunga Mabao mengi kila Mechi baada ya Jumapili iliyopita kushusha kipigo cha kwanza kwenye Ligi kwa vinara wa Ligi Chelsea Uwanjani Stamford Bridge walipoifunga 3-2 lakini Siku 3 baadae, Jumatano, Chelsea walilipa kisasi kwa kuifunga Man United, iliyochezesha Kikosi cha Pili,  bao 5-4, kwenye Mechi ya Kombe la Ligi iliyochukua Dakika 120 baada ya kutoka 3-3 katika Dakika 90.
Katika Mechi 8 za mwisho kucheza Old Trafford, Arsenal hawajashinda hata moja baada ya kuchapwa na Man United katika Mechi 7 kati ya hizo na sare 1 tu.
Kimsimamo kwenye Ligi, Arsenal wapo nafasi ya 6 wakiwa na Pointi 15 na Man United wapo nafasi ya pili, Pointi moja nyuma ya vinara Chelsea, na wana Pointi 21.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
USO kwa USO-Man United v Arsenal:
-WAMECHEZA JUMLA MECHI: 214
-Arsenal: Ushindi: 78
-Man United: Ushindi 90
-Sare: 46
NYUMBANI kwa Arsenal: Mechi 101
-Arsenal: Ushindi: 57
-Man United: Ushindi 27
-Sare: 17
NYUMBANI kwa Man United: Mechi 102
-Man United: Ushindi 60
-Arsenal: 17
-Sare: 25
MATOKEO Misimu ya hivi karibuni:
2011/12:
Januari 22-Arsenal 1 Man United 2 [BPL]
Agosti 28-Man United 8 Arsenal 2 [BPL]
2010/11:
Mei 1-Arsenal 1 Man United 0 [BPL]
Machi 12-Man United 2 Arsenal 0 [FA Cup]
Desemba 13-Man United 1 Arsenal 0 [BPL]
2009/10
Januari 31-Arsenal 1 Man United 3 [BPL]
Agosti 29-Man United 2 Arsenal 1 [BPL]
2008/9:
Mei 16-Man United 0 Arsenal 0 [BPL]
Mei 5-Arsenal 1 Man United 3 [UEFA CHAMPIONZ LIGI]
Aprili 29-Man United 1 Arsenal 0 [UEFA CHAMPIONZ LIGI]
Novemba 8-Arsenal 2 Man United 1 [BPL]
2007/8:
Aprili 13-Man United 2 Arsenal 1 [BPL]
Februari 16-Man United 4 Arsenal 0
Novemba 3-Arsenal 2 Man United 2
REKODI-Mabao Mengi:
-2011/12: Man United 8 Arsenal 2
-1946/47: Arsenal 6 Man United 2
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
 

MECHI KUPIGA VITA UMASIKINI: Ronaldo & Marafiki v Zidane & Marafiki!

MATCH_AGAINST_POVERTY>>DESEMBA 19, Gremio Arena, Porto Alegre, Brazil.MATCH_AGAINST_POVERTY2
Magwiji, ambao pia ni Mabalozi maalum wa UNDP, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Ronaldo na Zidane, wamealika Marafiki zao ili kucheza Mechi maalum ya Programu ya ‘Kupiga vita Umasikini’ hapo Desemba 19 itakayochezwa Gremio Arena huko Porto Alegre, Brazil.
Katika Mechi hii ya 10 ya ‘Kupiga vita Umasikini’, Zidane na Ronaldo, ambao waliwahi kucheza pamoja Real Madrid, kila mmoja atateua Kikosi chake.
Mechi za aina zimekuwa zikichezwa kila Mwaka kuanzia Mwaka 2003, na kubarikiwa na FIFA pamoja na UEFA, huchangisha Fedha ili kusaidia vita ya kuondoa Umaskini.
Kawaida Mechi hizi huchezwa katika Miji tofauti kwa kuikutanisha Timu ya Mabalozi wa UNDP dhidi ya Timu ya Mji inapochezwa lakini safari hii huko Gremio Arena, Porto Alegre, Brazil zitakuwa ni Timu ya Ronaldo, ambae pia atashirikisha wenzake wa Brazil, dhidi ya Timu ya Zidane.
Mwaka jana 2011, Mechi kama hii ilichezwa Mjini Hamburg, Ujerumani kati ya Hamburger HSV na Timu ya UNDP ambayo walikuwemo Ronaldo na Zidane.
Wachezaji wengine waliokuwemo kwenye Mechi hiyo ni  Didier Drogba (Ivory Coast), Dida (Brazil), Serginho (Brazil), Jens Lehmann (Germany), Lucas Radebe (South Africa), Fernando Hierro (Spain), Michel Salgado (Spain), Gheorghe Popescu (Romania), Gheorghe Hagi (Romania), Luís Figo (Portugal), Fernando Couto (Portugal), Christian Karembeu (France), Steve McManaman (England), Pavel Nedved (Czech Republic), Fabio Cannavaro (Italy), na Sami Al-Jaber (Saudi Arabia).
Mapato kwenye Mechi hizi huenda katika Programu za kupiga vita Umasikini katika Nchi zaidi ya 27 za Marekani ya Kusini, Africa na Asia.
Mapato makubwa ya Mechi ya Mwaka jana ya huko Hamburg yalienda kusaidia balaa la njaa lililoikumba Kaskazini Mashariki ya Afrika, hasa Somalia.
Akiongea Zidane alitamka: “Kila tunapokutana kwa Mechi hizi tunaweza kusaidia na kuleta tofauti kwa wenye shida!”
Nae Ronaldo amesema: “Ni muhimu kuonyesha umoja ili kusaidia wale wenye janga la Umasikini!”

Stirring the pot: Manchester United fans display a banner about Clattenburg, mocking the well-known slogan Chelsea fans attach to captain John Terry, who racially abused QPR defender Anton Ferdinand

BIN HAMMAM AGONGA UKUTA CAS.

MGOMBEA wa zamani wa urais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Mohamed bin Hammam ameshindwa rufani yake ya kutengua adhabu ya siku 90 alizopewa wakati uchunguzi wa suala la rushwa dhidi yake ukiendelea.
 
 Bin Hammam ambaye ni raia wa Qatar alikata rufani kuhusu kufungiwa kwake huko akidai lilikuwa ni suala la kisiasa baada ya kujitokeza kugombea nafasi hiyo na Sepp Blatter Mei mwaka jana. 
 
 Bin Hammam ambaye pia amewahi kuwa rais wa Shirikisho la Soka barani Asia-AFC alishinda rufani yake ya kufungiwa maisha kwasababu ya kukutwa na hatia ya kuhonga wapiga kura Julai mwaka huu lakini FIFA ilianza uchunguzi mpya dhidi yake juu matumizi mabaya ya fedha wakati akiwa rais wa AFC.  
 
Baada ya kushindwa kuishawishi kamati ya rufani ya FIFA kutengua adhabu ya kufungiwa siku 90 Bin Hammam aliamua kupeleka shauri hilo katika Mahakama ya Usuluhishi ya Michezo-CAS ambako nako maegonga mwamba. 
 
 Kamati ya maadili ya FIFA ikiongozwa na wakili wa zamani wa Marekani Michael Garcia wataendelea na uchunguzi juu matumizi mabaya ya fedha aliyofanya Bin Hammam kipindi hicho akiwa rais wa AFC.

DJOKOVIC ASHINDWA KUTAMBA PARIS MASTERS.

MCHEZA tenisi nyota kutoka Serbia, Novak Djokovic ameshindwa kutamba katika michuano ya Paris Masters na kujikuta akitolewa na Sam Querrey wa Marekani katika mzunguko wa pili.  

Djokovic ambaye ana uhakika wa kumaliza mwaka akiwa katika nafasi ya kwanza ya orodha za wachezaji bora wa mchezo huo dunia alianza vyema baada ya kushinda seti ya kwanza bila kupoteza alama lakini alijikuta akishindwa kuendelea kufanya vizuri katika seti zingine na kufungwa kwa 0-6 7-6 6-4.

 Djokovic anayeshika namba mbili ambaye anatachukua nafasi ya kukaa namba moja ambayo inashikiliwa na Roger Federer pamoja na kupoteza mchezo huo ka Querrey alitinga uwanjani jijini Paris akiwa amevaa kinyago cha Vader Mask kuazimisha sherehe za Halloween.

 Katika michezo mingine ya iliyochezwa jana David Ferrer ambaye ndiye mchezaji pekee aliyekuwepo katika orodha za juu, Juan Monaco na Janko Tipsarevic walishinda michezo yao na kuinga mzunguko wa tatu wa michuano hiyo ya mwisho kwa mwaka huu.

YANGA SASA TISHA MBAYA, SIMBA CHUPUCHUPU MOROGORO

Msuva kushoto na Domayo kulia, wakimpongeza
Kavumbangu kufunga bao la pili


YANGA SC imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya jioni ya leo kuichapa Mgambo JKT ya Handeni, Tanga mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo, unaifanya Yanga sasa iwe na pointi sawa na mabingwa watetezi, Simba SC waliotoa sare ya 1-1 na Polisi mjini Morogoro leo, ingawa inazidiwa bao moja tu katika wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Hadi mapumziko, Yanga walikuwa mbele kwa mabao 2-0, yaliyotiwa kimiani na beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na mshambuliaji Didier Kavumbangu.
Cannavaro alifunga kwa kichwa akiunganisha krosi ya Oscar Joshua dakika ya pili kutoka wingi ya kulia, wakati Kavumbangu alimalizia pasi ya Hamisi Kiiza dakika ya 39.
Pamoja na kutoka uwanjani wamelowa kipindi cha kwanza, lakini Mgambo JKT walicheza soka ya kuvutia na mara mbili walikaribia kufunga kupitia kwa Juma Mwinyimvua.
Yanga walicheza vema dakika 45 za kipindi cha kwanza, tofauti sana na mechi za awali ambazo wamekuwa ‘wakichezewa’ sana na wapinzani.
Ilishuhudiwa katika kipindi hicho, Yanga wakimiliki zaidi mpira na kupeana pasi za uhakika, ingawa mashambulizi yao mengi walipitisha pembeni, hasa upande wa kulia.
Hamisi Kiiza, Msuva na Kavumbangu walicheza kwa uelewano mkubwa pale mbele na kulitia misukosuko haswa lango la Mgambo. 
Kipindi cha pili, Yanga walirudi na moto wao tena na kuendelea kuwachachafya Mgambo.
Hata hivyo, iliwachukua Yanga dakika 34 kupata bao la tatu, mfungaji akiwa ni Jerry Tegete aliyeingia dakika ya 68 kuchukua nafasi ya Kavumbangu.
Tegete alifunga bao hilo akiunganisha krosi maridadi ya beki wa kushoto, Oscar Joshua.
Pamoja na kufungwa, Mgambo waliendelea kusukuma mashambulizi langoni mwa Yanga, ingawa leo mabeki wa timu hiyo, inayofundishwa na Mholanzi, Ernie Brandts walicheza kwa uelewano mkubwa na kudhibiti hatari zote langoni mwao.  
Mgambo inayofundishwa na Mohamed Kampira, ilipata pigo dakika ya 85, baada ya beki wake wa kulia, Salum Mlima kutolewa kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwa kumchezea rafu mbaya Mbuyu Twite.
Baada ya mchezo huo, Brandts alisema dakika 10 za mwanzo timu yake ilikuwa inashindwa kumalizia vizuri mashambulizi yake, lakini baadaye ikatulia na hatimaye kupata ushindi huo, ambao ameufurahia kwani unamuweka katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Kwa upande wake, Kampira wa Mgambo alisema kufungwa ni sehemu ya mchezo, akawasifu Yanga kwa kutumia nafasi walizopata, huku akijutia nafasi walizopoteza wachezaji wake leo.
Kikosi cha Yanga leo kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Nsajigwa Shadrack/Kevin Yondan dk 46, Oscar Joshua, Mbuyu Twite, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Frank Domayo/Nurdin Bakari dk 76, Didier Kavumbangu/Jerry Tegete dk68, Hamisi Kiiza na Haruna Niyonzima.
Mgambo JKT; Godson Mmasa, Salum Mlima, Yassin Awadh, Salum Kipanga/Godfrey Komba dk80, Bakari Mtama, Ramadhani Malima, Chande Magoja, Mussa Ngunda, Issa Kandulu/Nassor Gumbo dk 60, Fully Maganga na Juma Mwinyimvua/Omar Matwiko dk76.
Katika mchezo wa utangulizi, timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Yanga, imeifunga Mgambo JKT ya vijana pia 1-0, bao hilo pekee la Clever Charles dakika ya 65.
Katika mechi nyingine, Simba ilitoka sare ya 1-1 Polisi kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, wenyeji wakitangulia kupata bao dakika ya 35 kupitia kwa Mokili Rambo kabla ya Amri Kiemba kusawazisha dakika ya 57.

 



SIRI YA BUNJAK KUFUKUZWA AZAM HII HAPA

Bunjak

WACHEZAJI wa Azam ndio waliomponza kocha Mserbia, Boris Bunjak kufukuzwa kazi jana, baada ya kuuandikia barua uongozi, wakisema hawaridhishwi na ufundishaji wa kcoha huyo na hawamtaki.
Pamoja na kumchongea kwa uongozi Mserbia huyo, habari za ndani kutoka Azam zimesema kwamba, ni wachezaji hao hao waliopendekeza katika barua yao kurejeshwa kwa aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Muingereza Stewart Hall.
Habari zilizopatikana jana kutoka Azam FC, zilisema kwamba, sababu za kufukuzwa kwa Mserbia huyo ni kushuka kwa kiwango cha timu, hali iliyosababisha sasa ianguke hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Tayari Bunjak amekwishapewa haki zake zote na ataondoka kesho, siku ambayo Stewart anaweza kuwasili kuanza tena kazi Azam FC.
Bunjak anaondoka Azam baada ya kuiongoza timu katika mechi 16, akifungwa nne tu, zote dhidi ya Simba ikiwemo ya juzi ya Ligi Kuu, waliyofungwa 3-1 na kutoa sare tatu.
Bunjak mwenye leseni ya Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA), alitua Azam, Agosti 7, mwaka huu akitokea FC Damac ya Saudia Arabia aliyoanza kuifundisha mwaka jana na kabla ya hapo alifundisha klabu kibao za kwao, zikiwemo FK Sloga Kraljevo, FK Javor Ivanjica, Crvena Zvezda Gnjilane, FK Radnicki Nis, FC Uralan Elista, FK Mladi Radnik, FK Crvena Zvezda Beograd, Al-Shaab, FK Hajduk Kula na Al-Nasr.
Awali, Bunjak aliyezaliwa Novemba 17, mwaka 1954 ( miaka 57), alicheza soka katika klabu za FK Sloga (Kraljevo), FK Vozdovac (Beograd), FK Radnicki (Kragujevac), FK Olimpia (Ljubljana), FK Sumadija (Arandjelovac), FK Sloga (Kraljevo), FK Borac (Cacak) na FK Sloga (Kraljevo).
Stewart alifukuzwa kwa kosa la kukaidi maagizo ya Bodi ya Ukurugenzi ya klabu hiyo, kumpanga Mrisho Khalfan Ngassa katika mechi ya fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame dhidi ya Yanga.
Mserbia huyo anakuwa kocha wa tano kufukuzwa Azam, ndani ya miaka minne tangu ianze kucheza Ligi Kuu, 2008 baada ya Stewart, Mbrazil Neider dos Santos, Sylvester Marsh na Itamar Amorin, Mbrazil mwingine.
Lakini Stewart angalau aliacha kumbukumbu ya taji na Medali Azam, baada ya kuiwezesha kutwaa Kombe la Mapinduzi Januari, kushika nafasi ya pili katika Ligi Kuu Aprili, kabla ya kushika nafasi ya pili Kombe la Urafiki na Kagame mwezi uliopita, mambo ambayo bila shaka yamemfanya afikiriwe tena.
Stewart ana sifa ya kutokuwa mbinafsi na mwenye kuwaamini watu wa chini yake, kwa mfano namna ambavyo alikuwa akimpromoti Kali Ongala. Alimkuta Kali kama mchezaji, lakini kwa sababu ya umri kumtupa mkono, akashauriana naye awe Kocha Msaidizi na mshambuliaji huyo wa zamani wa Yanga, akakubali.
Chini ya Stewart, Kali alikuwa akiachiwa timu aiongoze ili kumjengea kujiamini zaidi na mwezi uliopita aliachiwa timu kwenye Kombe la Urafiki, akaifikisha fainali, ambako ilifungwa na Simba kwa penalti kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90.  
REKODI YA BORIS BUNJAK AZAM
Azam 2-1 Polisi                   (BancABC)
Azam 1-2 Simba B              (BancABC)
Azam 8-0 Trans Camp        (Kirafiki)
Azam 1-0 Prisons               (Kirafiki)
Azam 2-0 Coastal Union     (Kirafiki)
Azam 2-3 Simba SC           (Ngao ya Jamii)
Azam 1-0 Kagera Sugar     (Ligi Kuu)
Azam 2-2 Toto African        (Ligi Kuu)
Azam 3-0 JKT Ruvu           (Ligi Kuu)
Azam 1-0 Mtibwa Sugar     (Ligi Kuu)
Azam 1-0 African Lyon       (Ligi Kuu)
Azam 2-3 Simba SC           (Kirafiki)
Azam 1-0 Polisi                  (Ligi Kuu)
Azam 0-0       Prisons         (Ligi Kuu)                                      
Azam 1-1 Ruvu Shooting   (Ligi Kuu)
Azam 1-3 Simba                (Ligi Kuu)

 

YANGA B WAITILIA UBANI YANGA A, WAYACHAPA KIDUDE MAKINDA YA MGAMBO


Timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Yanga, imeifunga Mgambo JKT ya vijana pia, bao 1-0 katika mchezo wa utangulizi, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kabla ya kuanza kwa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baina ya kaka zao, Yanga A dhidi ya Mgambo JKT ya Handeni, Tanga. Bao hilo pekee lilitiwa kimiani na Clever Charles dakika ya 65.
Zuberi Amiri wa Yanga B, akichuana na Charles Domayo wa JKT Mgambo

Joseph Banda wa Yanga B (25) akipasua ukuta wa Mgambo

Meshack Ramadhani wa Yanga kushoto akigombea mpira na beki wa Mgambo

Banda akifumua shuti mbele ya mabeki wa Mgambo, mmoja akijaribu kuzuia

Notikel Masasi wa Yanga B akiwa chini ya ulinzi wa mabeki wa Mgambo

Kocha Ernie Brandts akifuatilia vipaji Yanga B ikicheza na Mgambo

Notikel Masasi wa Yanga B, akichuana na mchezaji wa Mgambo

Clever Charles, mfungaji wa bao la Yanga B leo, akiwa benchi baada ya kupumzishwa. Kulia kwake ni Said Manduta.

LIGI KUU YA VODACOM SASA KWENYE MTANDAO

MILIONEA SEIF MAGARI AKUBALI KUGOMBEA UENYEKITI DRFA

Seif Ahmad 'Magari'


KIGOGO wa Yanga, Seif Ahmad ‘Magari’ amekubali kugombea Uenyekiti wa Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA), baada ya kuombwa na wazee na wadau wa soka mkoani Dar es Salaam.
Wadau wa soka Dar es Salaam tangu wiki iliyopita wamekuwa wakimbembeleza Seif kuchukua fomu za kugombea nafasi hiyo, wakiahidi kumuunga mkono mfanyabiashara huyo wa magari na fedha za kigeni kwa asilimia 100 ashinde nafasi hiyo.
Seif amesema leo kwamba amekubali wito huo wa wana Dar es Salaam na atachukua fomu ya kuwania nafasi hiyo.
Lini? “Itakapokuwa tayari nitakuambia, ila jambo la msingi tu nimekubali,”alisema Seif. Seif amekuwa kwenye Kamati za Yanga tangu wakati wa uongozi wa Francis Mponjoli Kifukwe miaka saba iliyopita na pia amewahi kuwa mmiliki mshiriki wa klabu ya Moro United iliyokuwa Ligi Kuu.
Seif ameendelea kuwa ndani ya Kamati za Yanga katika zama za viongozi waliomfuatia Kifukwe katika klabu hiyo, Imani Madega, Lloyd Nchunga na sasa Yussuf Manji.
Iwapo Seif atachukua fomu, kuna uwezekano mpinzani wake mkuu akawa, Mwenyekiti wa zamani wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Evans Aveva ambaye naye pia ana uzoefu wa kutosha katika uongozi wa soka.
Aveva, aliyekuwa Meneja wa Hoteli ya Embassy na sasa mfanyabiashara mwenye maduka kibao ya simu, amekuwa kwenye Kamati mbalimbali za uongozi Simba tangu enzi za Yussuf Hazali, Mwenyekiti wa klabu hiyo na ameendelea pia hata katika zama za viongozi waliofuatia akina Juma Salum (sasa marehemu) na Hassan Daalal.
Aveva pia amewahi kuwa mmoja wa viongozi wa iliyokuwa Tanzania Stars, timu iliyokuwa ikiundwa na wachezaji wakongwe nchini, ambayo mwaka 1998 na 1999 ilicheza Kombe la Washindi Afrika.
Uchaguzi wa DRFA utafanyika Desemba 8, mwaka huu na fomu za kugombea nafasi mbalimbali zilianza kutolewa tangu jana, wakati Novemba 4 hadi 8, Kamati ya Uchaguzi, chini ya Mwenyekiti wake, Juma Simba itapitia fomu za walioomba uongozi.
Novemba 9 hadi 13 utakuwa muda wa pingamizi kwa wagombea, ambazo zitajadiliwa Novemba 14 hadi 16, wakati Novemba 17 hadi 19 watatoa fursa ya kukata rufaa, ambazo zitasikilziwa Novemba 20 hadi 24 na baada ya hapo, Novemba 25 yatatangazwa majina ya wagombea waliopitishwa.
Uchaguzi wa DRFA utafanyika siku chache tu kabla ya uchaguzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), mwishoni mwa Desemba, mwaka huu.  

 

FA YASUBIRI TAARIFA KUTOKA SERBIA JUU YA KUFUNGIWA WACHEZAJI WAKE KUTOKANA NA VURUGU.

CHAMA cha Soka nchini Uingereza-FA kimethibitisha kuwa hawajapewa taarifa juu ya uamuzi wa maofisa wa polisi nchini Serbia kuwahusisha wachezaji wawili wa timu ya taifa chini ya miaka 21 ya Uingereza kwa vurugu.
 Shirikisho la Soka nchini Serbia liliwafungia viungo Nokla Ninkovic na mshambuliaji Ognjen Mundrinski kucheza katika timu za taifa lakini mamlaka ya kisheria ilitangaza kuwashitaki watu 12 katika vurugu hizo yakiwemo majina mawili ya Uingereza.
 Katika taarifa ya FA ilithibitisha kuwa hawajapata taarifa rasmi zozote kuhusu kufungiwa kwa wachezaji wake na shirikisho la soka ya Serbia na kwamba wanasubiri maelezo zaidi kuhusiana na sakata hilo. 
 Taarifa hiyo ilimalizwa kwa kusema FA itawapa msaada wachezaji pamoja na viongozi waliokumbana na sakata hilo nchini Serbia wiki mbili zilizopita.

DJOKOVIC AJIHAKIKISHIA KUMALIZA NAMBA MOJA.

MCHEZA tenisi nyota kutoka Serbia, Novak Djokovic amejihakikishia nafasi ya kumpita mpinzani wake Roger Federer na kumaliza mwaka 2012 akiwa kinara katika orodha za ubora duniani kwa upande wa wanaume.

 Djokovic alipoteza nafasi yake hiyo kwa Federer mwenye umri wa miaka 31 baada ya kunyakuwa michuano ya Wimbledon lakini Federer ambaye anatoka Switzerland hataweza kutetea taji la Paris Masters.

 Kutokuwepo kwa Federer katika michuano hiyo mikubwa ya dunia ya mwisho kwa mwaka huu ambayo itafanyika Novemba 5 kunampa nafasi Djokovic kurejea katika kiti chake. 

 Djokovic mwenye umri wa miaka 25 anakuwa nyota wa kwanza kumaliza mwaka katika nafasi ya kwanza mfululizo toka Federer alipofanya hivyo kuanzia mwaka 2004 mpaka 2007.

 

CAPITAL ONE CUP: MECHI YA MIGOLI 12, Arsenal yashinda 7-5!!


ARSENE_WENGER-13>>THEO WALCOTT APIGA HETITRIKI!!
Katika Mechi za Raundi ya 4 ya Mtoano ya CAPITAL ONE CUP zilizochezwa Jumanne Usiku, Mechi ya ajabu na vuta nikuvute ni ile iliyochezwa Uwanja wa Madejski ambapo Reading waliongoza 4-0, mapumziko kuwa 4-1 mbele lakini Arsenal wakasawazisha na kuifanya gemu iwe 4-4 hadi Dakika 90 na katika Dakika 30 za nyongeza Arsenal walikwenda mbele 5-4, Reading wakarudisha na kuwa 5-5 na hatimae Arsenal kuibuka Mshindi 7-5 huku Theo Walcott akipiga hetitriki.
+++++++++++++++++++++++++
CAPITAL ONE CUP-MATOKEO:
RATIBA RAUNDI ya 4:
Jumanne Oktoba 30
Sunderland 0 Middlesbrough 1
Swindon 2 Aston Villa 3
Wigan 0 Bradford 0 [Baada Dakika 120, Mshindi Bradford 4-2 kwa Mikwaju ya Penati]
Leeds 3 Southampton 0
Reading 4 Arsenal 4 [Baada Dakika 120, Mshindi Arsenal Bao 7-5]
+++++++++++++++++++++++++
READING 5 ARSENAL 7
MAGOLI:
Reading
-Jason Roberts, 12
-Koscielny, 19
-Leigertwood, 20
-Hunt, 37
-Pogrebnyak, 115
Arsenal
-Walcott, 45, 90 & 120
-Giroud, 64
-Koscielny, 89
-Chamakh, 103 & 120
VIKOSI:
Reading: Federici, Gunter, Gorkss, Morrison, Shorey, Tabb, McCleary, Leigertwood, Robson-Kanu, Roberts, Hunt
Akiba: Stuart Taylor, Pearce, Pogrebnyak, Le Fondre, McAnuff, Church, Harte.
Arsenal: Martinez, Jenkinson, Koscielny, Djourou, Miquel, Arshavin, Frimpong, Coquelin, Walcott, Chamakh, Gnabry
Akiba: Shea, Giroud, Squillaci, Bellerin, Eisfeld, Meade, Yennaris.
Refa: Kevin Friend
WIGAN 0 BRADFORD 0
Bradford washinda kwa Penati 4-2 baada ya sare ya 0-0 katika Dakika 120.
VIKOSI:
Wigan: Al Habsi, Ramis, Watson, Lopez, Stam, Fyvie, Jones, Redmond, Gomez, Boselli, McManaman
Akiba: Pollitt, Kone, Maloney, Beausejour, Golobart, Kiernan, Orsula.
Bradford: Duke, Darby, McHugh, McArdle, Meredith, Hines, Thompson, Doyle, Atkinson, Wells, Hanson
Akiba: McLaughlin, Connell, Gary Jones, Baker, Brown, Bass, Swain.
Refa: Roger East
SUNDERLAND 0 MIDDLESBROUGH 1
MFUNGAJI: McDonald, 39
VIKOSI:
Sunderland: Westwood, Bardsley, O'Shea, Cuellar, Colback, Johnson, Cattermole, Vaughan, Sessegnon, Fletcher, Saha
Akiba: Mignolet, Campbell, Wickham, McFadden, Kilgallon, Meyler, McClean.
Middlesbrough: Steele, Hoyte, Hines, Bikey, Friend, Ledesma, Leadbitter, Bailey, Haroun, Miller, McDonald
Akiba: Leutwiler, Zemmama, Halliday, Parnaby, Park, Reach, Smallwood.
Refa: Phil Dowd
SWINDON 2 ASTON VILLA 3
MAGOLI:
Swindon
-Sorey, 78 & 81
Villa
-Benteke, 30 & 90
-Agbonlahor, 39
VIKOSI:
Swindon: Foderingham, Devera, McCormack, Flint, McEveley, Ritchie, Miller, Ferry, Roberts, Benson, Collins
Akiba: Bedwell, Archibald-Henville, Nathan Thompson, Williams, Louis Thompson, Storey.
Aston Villa: Given, Lowton, Herd, Vlaar, Lichaj, Weimann, Ireland, El Ahmadi, Bannan, Agbonlahor, Benteke
Akiba: Guzan, Bent, Albrighton, Holman, Delph, Stevens.
Refa: Stuart Attwell
LEEDS 3 SOUTHAMPTON 0
MAGOLI:
-Tonge, 35
-El Hadj Diouf, 88
-Becchio, Penati, 90
VIKOSI:
Leeds: Ashdown, Peltier, Lees, Pearce, White, Byram, Austin, Brown, Tonge, Varney, Diouf
Akiba: Kenny, Drury, Green, Becchio, Pugh, Norris, Gray.
Southampton: Kelvin Davis, Butterfield, Hooiveld, Seaborne, Reeves, Mayuka, Chaplow, De Ridder, Ward-Prowse, Lee, Do Prado
Akiba: Gazzaniga, Shaw, Stephens, Chambers, Hoskins, Sinclair, Isgrove.
Refa: Chris Foy
+++++++++++++++++++++++++
CAPITAL ONE CUP
RATIBA RAUNDI ya 4:
Mechi kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku, Bongo Taimu
Jumatano Oktoba 31
Norwich v Tottenham
Liverpool v Swansea [SAA 5 Usiku]
Chelsea v Manchester United
+++++++++++++++++++++++++

 

MASHINDANO YA FDL KESHO NI KIMBEMBE KATIKA VIWANJA MBALI MBALI HAPA TANZANIA

 


Michuano ya ligi daraja la kwanza FDL kesho inaendelea kwa michezo kadhaa hapa nchini,kundi c kuna michezo minne ambayo itachezwa katika miji ya MARA,MANYARA,DODOMA,na MWANZA.

Kule mara polisimara vs rhino rangers katika dimba la karume ,Manyara kule kuna mechi kati ya moran vs polisi tabora katika dimba la kiteto , Dodoma pale kuna mechi kati ya polisi dodoma  vs pamba katika dimba la jamhuri na kule Kigoma kuna mechi kati ya Kanembwa vs Mwadui katika dimba la lake tanganyika kigoma.

KUNDI A 

Mbeya city vs mlale [sokoine mbeya]

Small kids vs mkamba[mandela sumbawanga]

majimaji vs burkinafaso[majimaji ruvuma ]

polisi iringa vs kurugenzi[samora iringa]

KUNDI B 

mechi itakuwepo novemba mosi mwaka huu kati ya Green warriors vs ashanti[mabatini] novemba pili polisi dar vs villa squad chamazi dar es salaam

 

NSA JOB KUTIBIWA INDIA GOTI LAKE

Mshambuliaji wa Coastal Union, Nsa Job, akivunjika goti akigongana na kipa wa JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Chamazi Jumapili Oktoba 28. 2012. Coastal ilishinda 3-0.

Madaktari wakimsaidia Nsa Job baada ya mguu kuhama kutoka kwenye maungio yake ya goti

Nsa Job akiugulia wakati akipelekwa kwenye gari la wagonjwa tayari kwa safari ya kelekea hospitalini Muhimbili

Nsa Job akiugulia baada ya kufikishwa hospitalini. PICHA ZOTE: Kwa hisani ya Gazeti la MWANANCHI
MSHAMBULIAJI wa timu ya Coastal Union ya Tanga, Nsa Job, ambaye alivunjika mguu baada ya kugongana na kipa wa JKT Ruvu juzi wakati timu hizo zilipokutana katika mchezo wa Ligi Kuu ya Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Chamazi amefungwa plasta ngumu na atakosa mechi zote tatu za mzunguko wa kwanza wa ligi zilizobakia.Kwa mujibu wa taarifa zilizoandikwa kwenye tovuti ya klabu hiyo na mkurugenzi wa timu hiyo, Nassor Bin Slum, baada ya vipimo kuonyesha kuwa goti la mshambuliaji huyo liligeuka, madaktari wa hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Moi) walifanikiwa kulirejesha katika hali ya kawaida na kumfunga plasta ngumu ili kuufanya urejee kwenye hali ya awali.
Taarifa hiyo inaongeza kuwa baada ya kupatiwa tiba hiyo, mchezaji huyo aliruhusiwa kurejea katika kambi ya timu hiyo ambayo inajiandaa na mechi yake dhidi ya Azam itakayofanyika kesho kwenye Uwanja wa Chamazi.
"Alhamdulillah ule wasiwasi tuliokuwa nao mwanzo baada ya Nsa Job kuumia sasa niseme umepungua kwani baada ya kumfikisha hospitali na kupigwa X-ray ilionekana tatizo ni 'dislocation of joint' (viungo kupishana katika maungio) na madaktari wamefanya kazi ya ziada kulirudisha goti lake katika sehemu yake na ameshafungwa POP, na hivi sasa amerudi kulala hotelini na wenzake. Inshaallah apone haraka aje kutimiza malengo aliyojiwekea " alisema Nassor katika taarifa aliyoitoa.

Habari zaidi zinasema mshambuliaji huyo wa zamani wa Yanga na Simba atakwenda India kwa matibabu zaidi.Mechi nyingine atakayoikosa mshambuliaji huyo aliyeisaidia timu yake kushika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ni dhidi ya Polisi Morogoro na dhidi ya mabingwa wa mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), Yanga ambayo ni ya kufunga mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo itakayofanyika Novemba 11 jijini Tanga.
Daktari wa Coastal Union, Dk. Francis Mganga alisema hali ya kiungo wao Mkenya Jerry Santo aliyeumia pia katika mechi hiyo ya juzi ni mbaya na hawatarajii acheze katika mechi zilizobaki za mzunguko wa kwanza na kwamba mchezaji Joseph Malubo pia ni majeruhi wa uvimbe wa goti. (Habari kutoka


Mshambuliaji wa Coastal Union ya Tanga, Nsa Job akiwa amefungwa bandeji gumu (POP) baada ya kuvunjika goti wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara dhidi ya JKT Ruvu uliofanyika juzi kwenye Uwanja wa Chamazi Complex jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo Coastal Union ilishinda 3-0. 

KAVUMBANGU 100% YANGA


DIDIER Fortine Kavumbagu yuko fiti kuichezea klabu yake, Yanga SC katika mechi ya kesho ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Mgambo JKT, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mrundi huyo alivimba mguu baada ya mechi dhidi ya JKT Oljoro na kushindwa kufanya mazoezi jana, lakini amefanya mazoezi na kumpa moyo kocha Mholanzi, Ernie Brandts kwamba anaweza kutumika kesho.
Beki Kevin Patrick Yondan na mshambuliaji Said Rashid Bahanuzi nao wapo fiti kabisa na leo pia wamefanya mazoezi na wenzao kwa ukamilifu Uwanja wa sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam.
Kipa Said Mohamed Kasarama na kiungo Juma Seif Dion ‘Kijiko’ wanasumbuliwa na Malaria na hawatashiriki mechi hiyo ya kesho, wakati mabeki Salum Abdul Telela, Juma Jaffar Abdul na Ibrahim Job Isaac wote bado majeruhi.
Yanga iliyovuna pointi tatu kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Oljoro, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha na kupanda nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kutimiza pointi 20 katika mechi 10, kesho inatarajiwa kuendeleza mawindo yake.
Yanga sasa iko nyuma kabisa ya wapinzani wao wa jadi, Simba SC wanaoongoza Ligi Kuu kwa pointi zao 22, baada ya kucheza mechi 10 pia.
Mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, wanaweza kupanda kileleni kesho, iwapo Simba itatoa sare au kufungwa na Polisi mjini Morogoro katika mchezo mwingine wa Ligi Kuu.
Mgambo JKT pamoja na kwamba imepanda Ligi Kuu msimu huu, lakini imeonyesha ni timu ya ushindani baada ya kutoa sare ya bila kufungana na Simba SC, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Kwa sababu hiyo, Yanga wamechukua tahadhari ya kutosha kuelekea mchezo huo na tangu juzi Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Abdallah Ahmad Bin Kleb amekuwa ‘akienda mbio’ kuhakikisha timu inashinda keshokutwa.  
Kurejea kwa Yondan na Bahanuzi kunaongeza matumaini ya ushindi kwa Yanga katika mchezo huo, ingawa upande mwingine ni mtihani kwa Brandts, kwani katika kipindi ambacho wachezaji hao wako ‘wadini’, walioshika nafasi zao wamekuwa wakifanya vizuri.    
Mbuyu Twitwe aliyehamishwa kutoka beki ya kulia hadi beki ya kati tangu Yondan aumie Oktoba 3, amekuwa akifanya vizuri sawa na Jerry Tegete aliyempokea Bahanuzi Oktoba 8, alipoumia naye amekuwa akifanya vizuri pia.
Kwa kuzingatia Twite alikuwa ‘uchochoro’ alipokuwa akicheza pembeni, watu wanasubiri kuona kama Brandts atamrudisha huko huko baada ya Yondan kurejea, au ataamua mmoja kati yao na Nadir Haroub ‘Cannavaro’ ataanzia benchi.
Upande wa Tegete na Bahanuzi, kuna uwezekano mmoja wao atakuwa anaanzia benchi kwa sasa na mwingine kumpokea mwenzake baadaye. 

SIMBA WAWAFUATA KIBABE MAAFANDE WANYONGE MOROGORO

SIMBA SC tangu inaondoka leo Dar es Salaam kwenda Morogoro tayari kwa mchezo wao dhidi ya Polisi mjini Morogoro katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kesho, wakitoka kushinda mabao 3-1 dhidi ya Azam FC Jumamosi na kujiimarisha kileleni.
Mabingwa hao watetezi juzi na jana walifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Kinesi, Urafiki, Manzese, Dar es Salaam na kwa ujumla timu vizuri kuelekea mchezo huo wa tatu kucheza nje ya Uwanja wa Taifa, msimu huu baada ya awali kucheza mechi mbili Tanga dhidi ya Coastal Union na Mgambo JKT ambazo zote walilazimishwa sare ya bila kufungana.
Simba imeshinda mechi zake zote Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kutoa sare mbili tu, dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Yanga 1-1 na 2-2 dhidi ya Kagera Sugar ya Bukoba.
Wekundu hao wa Msimbazi, wapo kileleni mwa Ligi Kuu kwa pointi zao 22 baada ya kucheza mechi 10, wakifuatiwa na wapinzani wao wa tangu enzi za bibi na babu, Yanga SC wenye pointi 20 katika nafasi ya pili.
Beki Juma Said Nyosso na kiungo Haruna Moshi Shaaban ‘Boban’ wanaendelea kutumikia adhabu zao za kusimamishwa, lakini wachezaji wote wengine wapo fiti kabisa, ukiondoa Obadia Mungusa aliyefukuzwa mapema tu kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu.
Simba itamenyana na Polisi iliyorejea Ligi Kuu msimu huu, ambayo inashika mkia katika ligi hiyo, ikiwa haijashinda hata mechi moja tangu kuanza kwa ligi hiyo zaidi ya kutoa sare mbili.
Lakini hiyo haiifanyia Simba idharau mechi hiyo na kocha Mserbia, Milovan Cirkovick ameanza maandalizi ya mapema kwa ajili ya mechi hiyo.
Hofu kubwa kwa Simba ni hali ya Uwanja wa Jamhuri, Morogoro- ni mbaya na kulingana na uzoefu walioupata wa kucheza kwenye Uwanja mwingine mbovu wa Mkwakwani, Tanga wanajua watakuwa na shughuli pevu keshokutwa.
Hadi sasa Simba ndio timu pekee katika Ligi Kuu, ambayo haijapoteza mechi, ikiwa imeshinda mechi sita na kutoa sare nne, wakati Yanga imefungwa mechi mbili na Azam FC na Coastal Union zinazoifukuzia timu hiyo, zimefungwa mechi moja moja.  

MIGAMBO WAIFUATA YANGA NA VIRUNGU VILIVYOITULIZA SIMBA MKWAKWANI



TIMU ya soka ya Mgambo JKT ya mjini Handeni mkoani Tanga, imeondoka leo mjini Tanga, ilikokuwa imeweka kambi kwenda Dar es salaam ambako kesho itashuka dimbani kwenye Uwanja wa Taifa kucheza na wenyeji Yanga katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Mgambo inayoshika nafasi ya 10 kwenye msimamo wa Ligi Kuu hadi sasa kwa kuwa na pointi 10 ikiwa imecheza michezo tisa, imeondoka na wachezaji wake 22 na viongozi watatu kwa ajili ya pambano hilo ambalo timu hiyo ilisema kuwa inalichukulia kwa umakini mkubwa ili waweze kuibuka na ushindi kutokana na kujiandaa vilivyo.
Kocha Mkuu wa timu hiyo Mohamed Kampira, alisema jana mjini hapa kwamba, Yanga waailichukulie kuwa watawafunga kirahisi katika mchezo huo badala yake wategemee kupata upinzani hasa kutokana na kwamba timu hiyo ya Mgambo imejiandaa kuibuka na ushindi ili waweze kukaa katika nafasi nzuri katika mzunguko huu wa kwanza.
"Tunaondoka kesho asubuhi (leo) kwenda Dar es salaam, kama timu tumejiandaa vizuri na tunatarajia kuwapa wakati mgumu Yanga na kuishinda, wasitarajie mteremko, sisi ni timu na tunaamini kwamba tutaibuka na pointi zote tatu," alisema kwa kujiamini Kampira aliyevaa viatu vya aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo Stephen Matata aliyetimuliwa baada ya timu hiyo kuanza vibaya kwa kufungwa michezo mitano mfululizo tangu kuanza kwa ligi hiyo.
Kampira alisema hadi sasa wachezaji wake wamekuwa na ari kubwa ya kuibuka na ushindi na hakuna majeruhi wote wapo katika hali nzuri ya kupambana na timu hiyo inayousaka ubingwa mwaka huu kwa udi na uvumba na kwamba amewata mashabiki wa timu hiyo kuiamini kwa wachezaji watafanya kazi iliyokusudiwa.
Mgambo JKT ambayo baada ya kumtimua kocha ilikuwa imeshikwa na kocha msaidizi Josepj Lazaro ambaye aliipa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Morogoro, akaifunga Mtibwa Sugar bao 2-1 kwenye uwanja wa Manungu, ikaifunga Toto African bao 2-0 na ikatoka sare ya 0-0 na Simba mchezo ambao Kampira ilikuwa ni mchezo wake wa kwanza kukaa kwenye benchi la timu hiyo.
Wakati huo huo, mashabiki wa klabu ya Coastal Union ya Jijini hapa, wameipongeza timu yao kwa ushindi walioupata juzi walipoifunga JKT Ruvu bao 3-0 katika mchezo uliofanyika kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es salaam hatau ambayo walisema inatia faraja na wamewataka wacheji wazidi kuongeza bidii ili lengo la kumaliza ikiwa nafasi za juu litimie.
Mmoja wa mashabiki hao Fred Tayasar alisema wamejisikia furaha ushindi huo lakini pia umewapa majonzi makubwa kwa mchezaji wao Nsa Job kuvunjika mguu katika pambano hilo hatua ambayo alisema wapenzi wa timu hiyo wanaangalia uwezekano wa kumchangia fedha kwa ajili ya kumpa ili aweze kujikimu katika kipindi atakachokuwa nje ya uwanja.


BUNJAK ATUPIWA VIRAGO AZAM, KOCHA USHINDI AREJESHWA KAZINI



KOCHA Mserbia wa Azam FC, Boris Bunjak amefukuzwa rasmi leo na sasa aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Muingereza Stewart Hall anarudishwa kazini.
Habari kutoka ndani ya Azam FC zimesema kwamba, sababu za kufukuzwa kwa Mserbia huyo ni kushuka kwa kiwango cha timu, hali iliyosababisha sasa ianguke hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu.
Tayari Bunjak amekwishapewa haki zake zote na ataondoka Alhamisi, siku ambayo Stewart atawasili kuanza tena kazi Azam FC.
Bunjak anaondoka Azam baada ya kuiongoza timu katika mechi 16, akifungwa nne tu, zote dhidi ya Simba ikiwemo ya juzi ya Ligi Kuu, waliyofungwa 3-1 na kutoa sare tatu.
Bunjak mwenye leseni ya Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA), alitua Azam, Agosti 7, mwaka huu akitokea FC Damac ya Saudia Arabia aliyoanza kuifundisha mwaka jana na kabla ya hapo alifundisha klabu kibao za kwao, zikiwemo FK Sloga Kraljevo, FK Javor Ivanjica, Crvena Zvezda Gnjilane, FK Radnicki Nis, FC Uralan Elista, FK Mladi Radnik, FK Crvena Zvezda Beograd, Al-Shaab, FK Hajduk Kula na Al-Nasr.
Awali, Bunjak aliyezaliwa Novemba 17, mwaka 1954 ( miaka 57), alicheza soka katika klabu za FK Sloga (Kraljevo), FK Vozdovac (Beograd), FK Radnicki (Kragujevac), FK Olimpia (Ljubljana), FK Sumadija (Arandjelovac), FK Sloga (Kraljevo), FK Borac (Cacak) na FK Sloga (Kraljevo).
Stewart alifukuzwa kwa kosa la kukaidi maagizo ya Bodi ya Ukurugenzi ya klabu hiyo, kumpanga Mrisho Khalfan Ngassa katika mechi ya fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame dhidi ya Yanga.
Mserbia huyo anakuwa kocha wa tano kufukuzwa Azam, ndani ya miaka minne tangu ianze kucheza Ligi Kuu, 2008 baada ya Stewart, Mbrazil Neider dos Santos, Sylvester Marsh na Itamar Amorin, Mbrazil mwingine.
Lakini Stewart angalau aliacha kumbukumbu ya taji na Medali Azam, baada ya kuiwezesha kutwaa Kombe la Mapinduzi Januari, kushika nafasi ya pili katika Ligi Kuu Aprili, kabla ya kushika nafasi ya pili Kombe la Urafiki na Kagame miezi miwili iliyopita, mambo ambayo bila shaka yamemfanya afikiriwe tena.
Stewart ana sifa ya kutokuwa mbinafsi na mwenye kuwaamini watu wa chini yake, kwa mfano namna ambavyo alikuwa akimpromoti Kali Ongala. Alimkuta Kali kama mchezaji, lakini kwa sababu ya umri kumtupa mkono, akashauriana naye awe Kocha Msaidizi na mshambuliaji huyo wa zamani wa Yanga, akakubali.
Chini ya Stewart, Kali alikuwa akiachiwa timu aiongoze ili kumjengea kujiamini zaidi na mwezi uliopita aliachiwa timu kwenye Kombe la Urafiki, akaifikisha fainali, ambako ilifungwa na Simba kwa penalti kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90.  
WASIFU WA BORIS BUNJAK:
JINA KAMILI: Boris Bunjak
KUZALIWA: Novemba 17, 1954 (Miaka 57)
KLABU ALIZOCHEZEA:
1967- 1975: FK Sloga (Kraljevo)
1975- 1978  FK Vozdovac (Beograd)
1978- 1979  FK  Radnicki (Kragujevac)
1979- 1980  FK Olimpia (Ljubljana)
1980- 1981  FK  Sumadija (Arandjelovac)
1981- 1985  FK  Sloga (Kraljevo)
1985- 1986  FK  Borac (Cacak)
1986- 1990  FK  Sloga (Kraljevo)
KLABU ALIZOFUNDISHA:
1990-1993:   FK Sloga (Kraljevo)
1995-1996:   FK Javor (Ivanjica)
1996-1997:   Crvena Zvezda (Gnjilane)
1999:                      FK Radnicki (Nis)
2000:                      FC Uralan Elista (Urusi)
2000-2002:   FK Mladi (Radnik)
2002-2004:   FK Crvena Zvezda (Beograd)
2004:                      Al-Shaab (UAE)
2005:                      FK Hajduk (Kula)
2006-2007:   Al-Nasr (Oman)
2009:                      Al Oruba Sur (Oman)
2011:                      FC Damac (Saudi Arabia)
2011:                      AL NASER (Oman)
  
REKODI YA BORIS BUNJAK AZAM
Azam 2-1 Polisi                   (BancABC)
Azam 1-2 Simba B              (BancABC)
Azam 8-0 Trans Camp        (Kirafiki)
Azam 1-0 Prisons               (Kirafiki)
Azam 2-0 Coastal Union     (Kirafiki)
Azam 2-3 Simba SC           (Ngao ya Jamii)
Azam 1-0 Kagera Sugar     (Ligi Kuu)
Azam 2-2 Toto African        (Ligi Kuu)
Azam 3-0 JKT Ruvu           (Ligi Kuu)
Azam 1-0 Mtibwa Sugar     (Ligi Kuu)
Azam 1-0 African Lyon       (Ligi Kuu)
Azam 2-3 Simba SC           (Kirafiki)
Azam 1-0 Polisi                  (Ligi Kuu)
Azam 0-0       Prisons         (Ligi Kuu)                                      
Azam 1-1 Ruvu Shooting    (Ligi Kuu)
Azam 1-3 Simba                 (Ligi Kuu)


TFF YASAKA MILIONI 225 ZA KUIPELEKA MOROCCO SERENGETI BOYS



RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Chillah Tenga amesema kwamba timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys inahitaji zaidi ya Sh Milioni 225 kwa ajili ya kampeni yake iliyobakia ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika mwakani nchini Morocco.
Akizungumza na Waandishi wa Habari makao makuu ya TFF, Ilala, Dar es Salaam, Tenga alisema kwamba shirikisho lake kwa sasa halina fedha hizo, kwa sababu hiyo haina mdhamini, zaidi ya kutegemea misaada ya wadau.
Tenga alisema tayari Kamati ya Vijana ya TFF imekwishakutana kuweka mikakati ya kuiwezesha Serengti kushiriki vema kampeni hizo, ikiwemo kuunda Kamati ya kuisaidia timu hiyo.
Hata hivyo, Tenga hakuitaja Kamati iliyoundwa kwa sababu bado hawajazungumza na Wajumbe walioteuliwa.
Alisema kocha wa timu hiyo, Mdenmark Jacob Michelsen ameomba mechi za kujipima nguvu kabla ya kucheza na Kongo Brazaville kuwania tiketi ya Morocco na Kamati ya Vijana inahangaikia suala hilo kwa sasa.
Alisema tayari kuna mwaliko kutoka Botswana wa Serengeti kwenda kucheza, lakini kutokana na ukosefu wa fedha wanashindwa hadi sasa kutoa jibu.
Kikosi cha wachezaji 25 cha Serengeti Boys kipo kambini mjini Dar es Salaam tangu Oktoba 21, mwaka huu kujiandaa na mechi hiyo, ya kwanza ikichezwa nyumbani Novemba 17, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, wakati mechi ya marudiano itachezwa wiki mbili baadaye.
Tanzania imefuzu bila jasho hadi kufika hatua hiyo, baada ya wapinzani wake wa awali, Kenya na Misri kujitoa katika Raundi ya Kwanza na ya Pili.
Kama Tanzania itafuzu kushiriki Fainali hizo za mwakani, itapoza machungu ya mwaka 2005 walipofuzu kucheza Fainali za Vijana wa umri huo kwa kuzitoa Rwanda, Zambia na Zimbabwe, lakini baadaye kwa sababu ya ‘kufoji’ umri wa Nurdin Bakari, ikaondolewa mashindanoni.
Zaidi ya Fainali za Mataifa ya Afrika 1980 na CHAN 2009, katika soka ya wanaume, Tanzania haijashiriki fainali nyingine zozote za Afrika tangu iingie kwenye soka ya kimataifa.

UCHAGUZI DRFA JIRANI KABISA NA UCHAGUZI WA TFF

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA), Juma Simba ‘Gadaffi’ (katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari leo, kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) juu ya uchaguzi wa chama hicho. Simba amesema uchaguzi wa DRFA utafanyika Desemba 8, mwaka huu na fomu za kugombea nafasi mbalimbali zitaanza kutolewa kesho. Novemba 4 hadi 8, Kamati yake itapitia fomu za walioomba uongozi, Novemba 9 hadi 13 utakuwa muda wa pingamizi kwa wagombea, ambazo zitajadiliwa Novemba 14 hadi 16, wakati Novemba 17 hadi 19 watatoa fursa ya kukata rufaa, ambazo zitasikilziwa Novemba 20 hadi 24 na baada ya hapo, Novemba 25 yatatangazwa majina ya wagombea waliopitishwa. Tarehe hii mpya ya uchaguzi wa DRFA inaufanya usogeleane na uchaguzi wa TFF, ambao utafanyika pia Desemba.   


TENGA ACHEMSHA VITA YA RUSHWA TFF



RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Chillah Tenga amesema kwamba vita dhidi ya rushwa katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ni ngumu na inahitaji sapoti kubwa ya wadau na wapenzi wa mchezo wenyewe ili kuifanikisha.
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo, makao makuu ya TFF, Ilala mjini Dar es Salaam, Tenga alisema kwamba pamoja awali kuwepo kwa mazingira ya ushahidi wa rushwa, lakini wanashindwa kwa sababu wao wana mipaka yao.
“Hili la rushwa kwa kweli ni gumu, ni gumu kwa sababu sisi tuna mipaka yetu, lazima tupate ushirikiano na vyombo husika. Lazima tupate ushirikiano wa wapenzi wenyewe wa mpira,”alisema Tenga.
Beki huyo wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, alisema wakati mwingine inakuwa vita hiyo inakuwa ngumu zaidi anaposikia hata Waandishi wa Habari wanahusika.
“Mimi sijathibitisha, lakini watu wananiambia viongozi wenyewe wanashiriki mchezo huu. Tena nasikia hadi nyinyi Waandishi wa Habari wakati mwingine mnatumiwa kupenyeza rushwa, kwa kweli inasikitisha,”alisema Tenga.
Kuhusu vipimo vya dawa za kulevya katika Ligi Kuu, Tenga alisema kwamba mchakato wa zoezi hilo unaendelea na walichokifanya kwa sasa ni kuwataaribu na kuwapa muda wahusika waache taratibu.
Alisema wamewapa nusu msimu watumiaji wa mihadarati katika soka ya Tanzania kujiondoa taratibu na tayari wamekwishawaambia hadi  viongozi wa klabu zote, ili zoezi hilo likianza liende vizuri.
“Hatutaki kuwaadhiri vijana wetu, ndiyo maana tumewaambia mapema, ili wale ambao wanavuta bangi kwa mfano, waanze taratibu kula chwingamu waache bangi, ili wakati utakapofika, hakutokuwa na mzaha,”alisema Tenga.

SIMBA SC HAKUNA KULALA, INAUA MMOJA INAWINDA MWINGINE

Wachezaji wa Simba SC

SIMBA SC tangu jana wameendelea na mazoezi kujiandaa na mchezo wao ujao dhidi ya Polisi mjini Morogoro katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, wakitoka kushinda mabao 3-1 dhidi ya Azam FC Jumamosi na kujiimarisha kileleni.
Mabingwa hao watetezi jana walifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Kinesi, Urafiki, Manzese, Dar es Salaam na kwa ujumla timu vizuri kuelekea mchezo huo wa tatu kucheza nje ya Uwanja wa Taifa, msimu huu baada ya awali kucheza mechi mbili Tanga dhidi ya Coastal Union na Mgambo JKT ambazo zote walilazimishwa sare ya bila kufungana.
Simba imeshinda mechi zake zote Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kutoa sare mbili tu, dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Yanga 1-1 na 2-2 dhidi ya Kagera Sugar ya Bukoba.
Wekundu hao wa Msimbazi, wapo kileleni mwa Ligi Kuu kwa pointi zao 22 baada ya kucheza mechi 10, wakifuatiwa na wapinzani wao wa tangu enzi za bibi na babu, Yanga SC wenye pointi 20 katika nafasi ya pili.
Beki Juma Said Nyosso na kiungo Haruna Moshi Shaaban ‘Boban’ wanaendelea kutumikia adhabu zao za kusimamishwa, lakini wachezaji wote wengine wapo fiti kabisa, ukiondoa Obadia Mungusa aliyefukuzwa mapema tu kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu.
Simba inatarajiwa kuondoka kesho Dar es Salaam kwenda Morogoro kwa ajili ya mchezo dhidi ya Polisi ambayo inashika mkia katika ligi hiyo, ikiwa haijashinda hata mechi moja tangu kuanza kwa ligi hiyo zaidi ya kutoa sare mbili.
Lakini hiyo haiifanyia Simba idharau mechi hiyo na kocha Mserbia, Milovan Cirkovick ameanza maandalizi ya mapema kwa ajili ya mechi hiyo.
Hofu kubwa kwa Simba ni hali ya Uwanja wa Jamhuri, Morogoro- ni mbaya na kulingana na uzoefu walioupata wa kucheza kwenye Uwanja mwingine mbovu wa Mkwakwani, Tanga wanajua watakuwa na shughuli pevu keshokutwa.
Hadi sasa Simba ndio timu pekee katika Ligi Kuu, ambayo haijapoteza mechi, ikiwa imeshinda mechi sita na kutoa sare nne.

YONDAN, BAHANUZI WARUDI RASMI KAZINI YANGA

Bahanuzi


BEKI Kevin Yondan na mshambuliaji Said Bahanuzi waliokuwa nje ya Uwanja kwa zaidi ya wiki mbili kutokana na kusumbuliwa na majeruhi, leo wanatarajiwa kuanza programu rasmi ya mazoezi na wenzao baada ya kupata ahueni ya kutosha.
Wachezaji hao wamekuwa wakifanya mazoezi mepesi kwa zaidi ya wiki moja baada ya kupata ahueni kidogo na sasa wamepona kabisa na leo kocha Mholanzi, Ernie Brandts anatarajiwa kuwajumuisha kwenye programu yake kamili, Uwanja wa sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam.
Yanga imerejea kutoka Arusha, ambako Jumamosi ilivuna pointi tatu kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji JKT Oljoro, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid na kupanda nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, wakitimiza pointi 20 baada ya kucheza mechi 10.
Yanga sasa iko nyuma kabisa ya wapinzani wao wa jadi, Simba SC wanaoongoza Ligi Kuu kwa pointi zao 22, baada ya kucheza mechi 10 pia.
Mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame sasa wanajiandaa na mchezo wao ujao wa ligi hiyo, dhidi ya Mgambo JKT Jumatano Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mgambo JKT pamoja na kwamba imepanda Ligi Kuu msimu huu, lakini imeonyesha ni timu ya ushindani baada ya kutoa sare ya bila kufungana na Simba SC, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Kwa sababu hiyo, Yanga wamechukua tahadhari ya kutosha kuelekea mchezo huo na tangu jana Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Abdallah Ahmad Bin Kleb amekuwa ‘akienda mbio’ kuhakikisha timu inashinda keshokutwa.   
Kurejea kwa Yondan na Bahanuzi kunaongeza matumaini ya ushindi kwa Yanga katika mchezo huo, ingawa upande mwingine ni mtihani kwa Brandts, kwani katika kipindi ambacho wachezaji hao wako ‘wadini’, walioshika nafasi zao wamekuwa wakifanya vizuri.     
Mbuyu Twitwe aliyehamishwa kutoka beki ya kulia hadi beki ya kati tangu Yondan aumie Oktoba 3, amekuwa akifanya vizuri sawa na Jerry Tegete aliyempokea Bahanuzi Oktoba 8, alipoumia naye amekuwa akifanya vizuri pia.
Kwa kuzingatia Twite alikuwa ‘uchochoro’ alipokuwa akicheza pembeni, watu wanasubiri kuona kama Brandts atamrudisha huko huko baada ya Yondan kurejea, au ataamua mmoja kati yao na Nadir Haroub ‘Cannavaro’ ataanzia benchi.
Upande wa Tegete na Bahanuzi, kuna uwezekano mmoja wao atakuwa anaanzia benchi kwa sasa na mwingine kumpokea mwenzake baadaye. 

COASTAL WAISHUSHA TENA AZAM FC MBIO ZA UBINGWA LIGI KUU

Azam FC
USHINDI wa mabao 3-0 wa Coastal Union dhidi ya JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam jana, umebadilisha kabisa taswira ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya Wagosi hao wa Kaya kupanda hadi nafasi ya tatu wakiiengua Azam.
Mapinduzi katika Ligi Kuu yalianza Jumamosi, baada ya Yanga kupanda hadi nafasi ya pili kutokana na ushindi wao wa bao 1-0 dhidi ya JKT Oljoro, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha huku Azam FC ikifungwa na Simba SC mabao 3-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kushuka nafasi ya tatu.
Lakini Coastal jana imeishusha Azam kwa nafasi moja zaidi, na sasa mbio za ubingwa wa Ligi Kuu zinaonekana kuwa za farasi watatu, lakini Azam si miongoni mwao, bali Simba, Yanga na Coastal.
Mwishoni mwa wiki ijayo, Yanga itacheza na Azam FC, mechi ambayo itatengeneza taswira ya namna mzunguko wa kwanza utakavyomalizika.
Azam ikishinda inaweza kurudi nyuma ya Simba SC, lakini tofauti na hapo watu watasubiri kuona kati ya watani hao wa jadi, nani atamaliza mzunguko wa kwanza akiwa kileleni.    
Kabla ya kucheza na Azam, Yanga itacheza Mgambo Shooting Jumatano, wakati Azam itacheza na Coastal Union Chamazi.
Ligi Kuu sasa inazidi kunoga baada ya juzi Simba kuzinduka kutoka kwenye wimbi la sare, baada ya kufanikiwa kuichapa Azam FC mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo, unaifanya Simba izidi kujitanua kileleni mwa ligi hiyo kwa kufikisha pointi 22, baada ya kucheza mechi 10, wakati Azam FC inapromoka hadi nafasi ya nne kwa pointi zake 18, baada ya kucheza mechi tisa, ikiipisha Coastal yenye pointi 19 katika nafasi ya tatu na Yanga sasa ni ya pili kwa pointi zake 20.
Mechi nyingine za ligi hiyo juzi, African Lyon ilitoka sare ya 1-1 Kagera Sugar Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam na Ruvu Shooting ikaifunga 2-1 Polisi Morogoro Uwanja wa Mabatini, Mlandizi.
Mechi kati ya Mgambo JKT na Prisons iliyokuwa ichezawe juzi Uwanja wa Mkwakwani, Tanga imeahirshwa kutokana na wachezaji wa Prisons kupata ajali wakiwa njiani kuelekea Tanga.
JKT Ruvu jana ilifungwa 3-0 na Coastal Union Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam na Toto Africans ilitoka sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Waamuzi wa soka ,Italia  na washika vibendera watakuwa na wakati mgumu sana katika ratiba ya wiki ijayo ambapo  watakuwa katika ulinzi mkali kuliko wakati mwingine wowote baada ya kufanya vibaya mwishoni mwa juma  Serie A  Ndio ligi peke barani ulaya ambayo inatumia washika vibendera zaidi ya wawili utaratibu unaopendwa zaidi na Rais wa shirikisho la soka barani ulaya  UEFA  Michel Platini, ambapo walishindwa kufanya maamuzi sahihi katika mechi kati ya   Catania na  Lazio vile vile  AS Roma Juventus  Aidha  viongozi wa  Juventus na wameingia matatani katika utetezi baada ya kuonekana wakimshawishi mwamuzi kutoa maamuzi ambayo sio sahihi  .
Rais wa Catania  Antonio Pulvirenti alikuwa na hasira pale timu yake ilipokataliwa goli sahihi dhidi ya  Juventus, ambao walishinda goli kwa sifuri   1-0  dhidi  Arturo Vidal kabla ya mapunziko
ambapo rais wa   Juventus  Andrea Agnelli,  ambaye ijumaa hii alisema shirikisho la soka la italia  lilitakiwa kuipora  Catania alama tatu muhimu kama mfano wa kuchezesha soka kwa mchezo wa haki ilikotoa funzo kwa timu nyingine 
juma hili kumetokea na tabia ya kuwatiahoma waamuzi kufanya maamuzi yasiyo sahihi katika ligi ya italia ambapo tuhuma hizi zimeperekwa zaidi katika benchi la timu ya soka ya juventus kwa kuwashinikiza waamuzi kufanya maamuzi yasiyo sahihi. 


 Senghor aliendelea kusema kuwa ataitisha mkutano wa dharura kesho kwa wajumbe 23 wa kamati ya utendaji waliobakia ili kuziba pengo la wajumbe wanne waliojiuzulu.

SIMBA SC YAMUWEKEA NYOSSO MTEGO WA MWANA UKOME

Juma Nyosso
SIMBA SC inamsubiri kwa hamu beki wake Juma Said Nyosso na pendekezo lake la kuvunja mkataba na klabu hiyo, lakini itamkata maini na jibu moja tu.
Jibu gani hilo? Atatakiwa kuilipa klabu hiyo fedha za kuvunja mkataba.
“Sheria ziko wazi na mkataba wake uko wazi, kabla ya kuusaini aliusoma vizuri, akauelewa akasaini, kwa kuwa yeye ameamua kuvunja mkataba, basi atatakiwa kutulipa fedha za kuvunja mkataba,”alisema kiongozi mmoja wa Simba ambaye hakutaka kutajwa jina gazetini.
Kimsingi Simba imekubali kuvunja mkataba na beki wake huyo iliyedumu naye tangu mwaka 2007, kulingana na maombi yake, na imemtaka afike kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Poppe kujadili suala hilo.
Habari za ndani kutoka Simba SC, zimesema kwamba Nyosso amewasilisha maombi ya kuvunja mkataba na klabu hiyo, baada ya kushushwa kikosi cha pili, akidaiwa kiwango chake kimeshuka hivyo amepewa fursa ya kwenda kukiboresha.
Lakini Nyosso mwenyewe ameona kama hastahili kushushwa timu ya pili na ameomba asitishiwe mkataba wake aondoke, jambo ambalo uongozi wa klabu umelikubali.
Nyosso si kama anatuhumiwa kuhujumu timu, bali anaambiwa uwezo wake umeshuka mno na kwamba amekuwa akiigharimu timu katika siku za karibuni, hivyo amepewa fursa ya kwenda kupandisha kiwango chake.
Adhabu kama hii amewahi kupewa mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina, Carlos Tevez katika klabu ya Manchester City ya England msimu uliopita na aliitumikia vizuri hadi aliporejeshwa tena kikosi cha kwanza, ambako aliisaidia timu kumalizia msimu vizuri kwa kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu.  
Mbali na Nyosso, kiungo Haruna Moshi Shaaban amesimamishwa kwa wiki tatu kwa tuhuma za utovu wa nidhamu na katika kipindi hicho atakuwa akipokea nusu mshahara.
Boban ameamua kurudi nyumbani kwake kupumzika na mkewe hadi adhabu hiyo iishe ajue mustakabali wake, ila amesema anaonewa kwa sababu hakupewa nafasi ya kujibu tuhuma zake kabla ya hatua kuchukuliwa, ingawa amechukulia poa tu.
Wakati huo huo, habari zaidi kutoka ndani ya Simba, zimesema kwamba Mwinyi Kazimoto Mwitula, Ramadhan Suleiman Chombo na Mrisho Khalfan Ngassa nao wanaangaliwa kwa ‘jicho la tatu’ juu ya mwenendo wao kwenye timu hiyo na kwa nyakati tofauti wote wamekwishaitwa kuhojiwa masuala mbalimbali.   

WACHEZAJI WAVIVU YANGA WAWEKEWA MTEGO WA KUTEMWA, TIMU IKO SAWA KWA GWARIDE LA OLJORO KESHO

Brandts akiwaongoza vijana wake mazoezini
UONGOZI wa Yanga umemshauri kocha Ernie Brandts kutumia wachezaji wote badala ya kuwasahau kabisa wengine benchi, ili uweze kubaini wachezaji ambao hawana msaada katika timu na kuweza kuwatema katika dirisha dogo Januari, mwakani.
Katika mechi za karibuni, Yanga ikiwatumia wachezaji tofauti wakiwemo wale ambao wamekuwa benchi kwa muda mrefu kama Nahodha Nsajigwa Shadrack, Nurdin Bakari na Rashid Gumbo.
Yanga imeweka mtego kwa wachezaji ambao wanaridhika kupewa mishahara bure bila kufanya kazi na Januari watatupiwa virago.
Chanzo cha habari kutoka Yanga kimesema kwamba, klabu inataka wachezaji washindani wa namba, ili kuongeza hamasa katika timu, badala ya kuwa na wachezaji wengi wa mazoezi tu.
Yanga wanaonekana kucharuka sasa dhidi ya wachezaji wao kwa ujumla, kuanzia suala la nidhamu na uwajibikaji pia, baada ya kuona wanawekeza fedha nyingi katika usajili, lakini bado timu haichezi soka ya kuvutia, jambo ambalo wanaona linatokana na wahezaji kubweteka.
Juzi Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Abdallah Ahmed Bin Kleb ‘aliwawakia’ wachezaji wa mbele wa timu hiyo kwa uchoyo wa pasi na kukemea tabia inayoonekana kuanza kujitokeza, wachezaji wa timu hiyo kutopendana.
Bin Kleb aliingia ‘kwa hasira’ chumba cha kubadilishia nguo cha Yanga na kuanza kufoka juu ya tabia hiyo, akisema timu inatengeneza nafasi nyingi, lakini kwa uchoyo wa baadhi ya wachezaji kutoa pasi kwa wenzao walio kwenye nafasi nzuri zaidi, inaambulia mabao machache.
Bosi huyo alifanya hivyo baada ya mechi dhidi ya Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ambayo Yanga ilishinda 3-0.
Lakini pia Bin Kleb alimuuliza kocha Mkuu, Mholanzi Ernie Brandts kwa nini timu haichezi vizuri pamoja na kushinda. Brandts alitumia hekima kukwepa kujibu swali mbele ya wachezaji, lakini baadaye alimvuta pembeni Bin Kleb wakazungumza.
Tayari kuna dalili za mgawanyiko ndani ya Yanga baina ya wachezaji na hilo lilijidhihirisha wakati Hamisi Kiiza alipofunga bao lake lililokuwa la tatu katika ushindi wa 3-0, hakwenda kushangilia na wachezaji wenzake, bali alimkimbilia kipa wa akiba, Mghana Yawe Berko kushangilia naye juzi.
Ingawa hajawahi kulalamika, lakini ukiifuatailia Yanga tangu baada ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, Kiiza ndiye ambaye mara nyingi amekuwa hapewi pasi na wenzake anapokuwa kwenye nafasi nzuri, ingawa yeye amekuwa anawapa tu wenzake pasi za mabao.
Pamoja na hayo, hali hiyo inaonekana kidogo kuathiri uchezaji wa Kiiza, anayeonekana kuwa mnyonge na asiye na raha uwanjani na haikushangaza alipotolewa nje kipindi cha kwanza kwenye mechi dhidi ya Simba, Oktoba 3, mwaka huu.
Lakini Kiiza amekuwa akicheza kwa kiwango cha juu mno katika timu yake ya taifa, Uganda, The Cranes pamoja na ‘kusuasua’ Yanga. 
Yanga iko Arusha tangu jana na imefikia katika hoteli ya Joshmal, huku ikifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid tayari kwa mechi yao ya Ligi Kuu dhidi ya wenyeji JKT Oljoro kesho kwenye Uwanja huo.
Yanga inashika nafasi ya tatu katika Ligi Kuu, ikiwa na pointi 14, baada ya kucheza mechi tisa, nyuma ya Azam FC yenye pointi 18, baada ya kucheza mechi nane, wakati mabingwa watetezi Simba SC, wapo kileleni kwa pointi zao 19. Simba na Azam zitacheza kesho.  

AZAM FC WAKO KAMILI, WAPANIA KUIPIGA SHOTI SIMBA KESHO

Azam FC
AZAM FC wamepania kuifunga Simba SC kesho katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ili kupanda kileleni mwa ligi hiyo.
Kocha Boris Bunjak kutoka Serbia amekuwa akiwaandaa vizuri vijana wake kwa mazoezi na kisaikolojia pia kuelekea mchezo huo, unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua.
Azam ipo kambini kwake, Chamazi ikijifua vikali na wachezaji wameweka kambi hapo, kwa ajili ya Ligi Kuu.
Kiboko ya nyavu za Simba na Yanga, John Raphael Bocco ‘Adebayor’ yuko fiti kupita maelezo na kiungo bora Afrika Mashariki na Kati kwa sasa, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ aliyekuwa majeruhi mwanzoni mwa msimu sasa amepona kabisa.
Kiungo Abdulhalim Humud aliyekuwa anasumbuliwa na maumivu katika mechi tatu zilizopita kwa sasa yuko fiti kabisa na habari njema zaidi ni kwamba, kiungo mwingine  Mzanzibari Abdi Kassim ‘Babbi’ amerudi kwenye fomu na anafumua mashuti makali na ya mbali ya hatari.
Viungo washambuliaji kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tcheche na Kipre Michael Balou wote wapo fiti sawa na makipa Deo Munishi ‘Dida’, Mwadini Ally, mabeki Ibrahim Shikanda, Erasto Nyoni, Said Mourad na Aggrey Morris.
Kwa ujumla Azam iko tayari kwa mechi hiyo ya kesho ambayo wamepania kushinda ili kulipa kisasi cha kufungwa na Simba katika Kombe la BancABC Sup8R.
Simba yenyewe inaendelea vizuri na kambi yake visiwiani Zanzibar kujiandaa na mchezo huo na inatarajiwa kurejea kesho mchana na moja kwa moja kuelekea uwanjani kukipiga.   

SIMBA TAYARI KULAMBA KONI ZA AZAM KESHO

Kikosi cha Simba

WEKUNDU wa Msimbazi, Simba SC wanatarajiwa kurejea kesho Dar es Salaam wakitokea Zanzibar ambako waliweka kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo wa kesho wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Azam FC, Uwanja wa Taifa.
Pamoja na Juma Nyosso na Haruna Moshi kusimamishwa, lakini wachezaji waliobaki wana morali ya hali ya juu na wamepania kushinda mechi ya kwanza kati ya nne, baada ya sare tatu mfululizo.  
Kwa kawaida Simba SC huenda Zanzibar katikati ya Ligi Kuu kuweka kambi linapokaribia pambano dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Yanga SC lakini kwa kitendo cha kwenda kujichimbia huko kwa ajili ya Azam, maana yake wanaipa uzito huo mechi hiyo.
Simba ilienda Zanzibar Jumanne, siku moja baada ya kurejea kutoka Tanga, ambako ililazimishwa sare ya bila kufungana na wenyeji Mgambo JKT Jumapili katika mfululizo wa ligi hiyo.
Matokeo hayo, yaliifanya Simba ifikishe pointi 19, baada ya kucheza mechi tisa na kuendelea kuongoza Ligi Kuu.
Awali ya hapo, Simba ilitoka 2-2 na Kagera Sugar Uwanja wa Taifa na 0-0 na Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani.
Baada ya sare ya Jumapili, Mwenyekiti wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage amewataka wanachama na wapenzi wa klabu hiyo kuwa watulivu na wasikatishwe na tamaa na sare tatu mfululizo za timu hiyo katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kwani safari bado ni ndefu.
Rage amesema kwamba, hadi sasa timu yao haijafungwa katika Ligi Kuu kuashiria kwamba bado ni timu bora na matokeo ya sare hizo tatu mfululizo pia ni kutokana na uimara wa timu yao.
Rage ameonya wanachama wenye desturi ya kutoa maneno ya uchochezi timu inapoyumba kidogo, waache kufanya hivyo kwa sababu wanaweza kuvuruga amani iliyopo sasa klabuni.

Wenger ajadili kuporomoka kwa Arsenal

>>ASEMA kufungwa na Schalke ni AJALI tu!!
ARSENE_WENGER-13Kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka Klabuni Arsenal uliofanyika jana mjadala mkali ulizuka baada ya Wadau wa Klabu hiyo kucharuka wakionyesha kukerwa na matokeo mabovu yaliyoiandama hivi karibuni na kusababisha Mwenyekiti Peter Hill-Wood Mtendaji Mkuu Ivan Gazidis na Mwanahisa Mkubwa Stan Kroenke wazomewe wakati wakihutubia hali ambayo ilimfanya Meneja Arsene Wenger asimame na kutoa maelezo yaliyopunguza munkari kwenye Mkutano huo.
Akielezea hali halisi, Wenger alisema fomu ya Timu hivi karibuni imeanguka kidogo lakini ameipa Timu yake changamoto kushinda Mechi ya Jumamosi ya Ligi Kuu England dhidi ya Queens Park Rangers itayochezwa Uwanja wa Emirates.
Arsenal walishika kasi baada ya sare kadhaa Msimu huu ulipoanza lakini katika Mechi zao mbili zilizopita zote wamefungwa wakianza kwa kichapo cha Ligi na Norwich City walipofungwa 1-0 na kuwafanya wawe Pointi 10 nyuma ya vinara Chelsea na kikaja kichapo kutoka kwa Schalke cha bao 2-0 kilichowafanya wapokonywe uongozi wa Kundi lao kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Akiongea kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Arsenal, Wenger alisema anaamini Kikosi chake kitarudia hali yake.
Wenger alisema: “Tulipokuwa West Ham tulicheza vizuri, tulikuwa hatari tukishambulia lakini zikaja hizi Mechi mbili na tumecheza ovyo. Ni ngumu kuelezea. Tumegonga ukuta katika Mechi hizi mbili. Lakini inabidi turudie umakini wetu, tucheze gemu yetu ya kawaida na tusikubali kufungwa kizembe. Tunao Wachezaji wazuri, ushindi utakuja tu!”
Aliongeza: “Kilichotokea Jumatano lazima tukikubali, tunajua hatukucheza vizuri Mechi na Schalke, tumepoteza Mechi moja katika Mechi 43 za Ulaya. Ajali kama hii inaweza kutokea! Kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI bado tupo kwenye nafasi nzuri. Ni muhimu kwenye Ligi tupate matokeo mazuri ili twende juu.”
Akiongelea Kikosi chake, Wenger amesema Wachezaji majeruhi ni Kieran Gibbs (Paja) naTheo Walcott (Kifua) lakini Alex Oxlade-Chamberlain, Jack Wilshere na Bacary Sagna sasa wako fiti na wanaweza kujumuishwa kwenye Kikosi kitakachoivaa QPR.
++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi, Oktoba 27, 2012
[SAA 8 Dak 45 Mchana]
Aston Villa v Norwich City
[SAA 11 Jioni]
Arsenal v Queens Park Rangers
Reading v Fulham
Stoke City v Sunderland
Wigan Athletic v West Ham United
[SAA 12 na Nusu Jioni]
Manchester City v Swansea City
Jumapili, Oktoba 28, 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Liverpool
[SAA 12 Jioni]
Newcastle United v West Bromwich Albion
Southampton v Tottenham Hotspur
[SAA 1 Usiku]
Chelsea v Manchester United
++++++++++++++++++++++

BPL: Wikiendi MOTO, BIGI MECHI-Chelsea v Man United Stamford Bridge!


>>JUMAPILI DABI ya LIVERPOOL ya 219: Everton v Liverpool!
>>KAGAWA nje WIKI 4!!
 
Shinji Kagawa of Manchester United feels the pain of an injury
Shinji Kagawa of Manchester United feels the pain of an injury
>>JUA MAREFA wa KILA MECHI!!
Timu zote 20 za Ligi Kuu England zitashuka dimbani kwa Mechi za Ligi Jumamosi na Jumapili kwa kucheza Mechi 10 lakini kati ya hizo, bila shaka, BIGI MECHI itakuwa ile ya Stamford Bridge ambayo vinara wa Ligi Chelsea wataivaa Manchester United iliyo nafasi ya pili na Mechi ya mvuto ni ile DABI ya Jiji la Liverpool Uwanjani Goodison Park kati ya Everton na Liverpool.
++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi, Oktoba 27, 2012
[SAA 8 Dak 45 Mchana]
Aston Villa v Norwich City
[SAA 11 Jioni]
Arsenal v Queens Park Rangers
Reading v Fulham
Stoke City v Sunderland
Wigan Athletic v West Ham United
[SAA 12 na Nusu Jioni]
Manchester City v Swansea City
Jumapili, Oktoba 28, 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Liverpool
[SAA 12 Jioni]
Newcastle United v West Bromwich Albion
Southampton v Tottenham Hotspur
[SAA 1 Usiku]
Chelsea v Manchester United
++++++++++++++++++++++
BPL_LOGOLakini, Manchester United watatinga huko Stamford Bridge huku wakiwa na habari mbaya za kumkosa Kiungo wao mahiri kutoka Japan, Shinji Kagawa, ambae atalazimika kuwa nje ya Uwanja kwa Wiki 3 hadi 4 akiuguza goti aliloumia kwenye Mechi na Braga iliyochezwa majuzi Jumanne.
Wakati, Sir Alex Ferguson anathibitisha kukosekana kwa Kagawa pia alithibitisha kurudi tena Uwanjani kwa Chris Smalling ambae alivunjika kidole cha mguu.
Msimu huu, Chelsea wamepoteza Pointi 2 tu kwenye Ligi  na hawajafungwa hata Mechi moja na wako Pointi 4 mbele ya Man United na wakiwa na Wachezaji hatari Eden Hazard, Juan Mata na Oscar wamekuwa tishio katika mashambulizi yao.
Hilo linatambulika kwa Ferguson ambae amesema: “Siku zote ni gemu ngumu kwa Chelsea na Man United. Unazo Timu nzuri. Wote wapo juu baada ya kuanza vyema na Chelsea wanatumia mfumo wa kuvutia na hilo lazima tulikabili. Wamewaleta Oscar na Hazard ni Wachezaji wazuri. Wamemwingiza Mata ambae anafana uchezaji na kina Oscar ambao wanacheza nyuma tu ya Straika wao mmoja. Si mfumo rahisi kuukabili lakini lazima tutafute njia. Kwa sasa hawana Drogba tena na wamebidi wabadilike. Walipokuwa na Drogba walikuwa wanaweza kucheza mipira mirefu au kupitia kati. Sasa hayupo, ni moja kwa moja wanapitisha mipira kupitia kati kwenye Kiungo.”
DABI: Everton v Liverpool
Tangu enzi hii ni mojawapo ya Dabi inayoheshimika Duniani yenye ushindani mkali na hii ni Dabi ya 219 ambapo Liverpool wameshinda mara 87, Everton mara 66 na sare 65.
Katika Mechi 11 za Ligi Kuu ambazo Everton wamekutana na Liverpool wameshinda Mechi 1 tu, sare 3 na kufungwa 7.
Lakini, safari hii, Everton watajiona kama wana nafasi kubwa kuifunga Liverpool hasa kwa vile wao wameanza Msimu vizuri na wapo nafasi ya 4 kwenye Msimamo wa Ligi wakiwa na Pointi 15 huku Liverpool wakiwa nafasi ya 12 na wana Pointi 9 tu.
MAREFA kwa MECHI za WIKIENDI:
Jumamosi Oktoba 27
Aston Villa v Norwich
Refa: P Dowd
Refa Wasaidizi: A Garratt, A Halliday
Refa wa Akiba: M Oliver
Arsenal v Queens Park Rangers
Refa: A Taylor
Refa Wasaidizi: J Collin, J Brooks
Refa wa Akiba: L Mason
Reading v Fulham
Refa: M Jones
Refa Wasaidizi: P Bankes, A Holmes
Refa wa Akiba: L Probert
Stoke City v Sunderland
Refa: M Halsey
Refa Wasaidizi: D Bryan, M Wilkes
Refa wa Akiba: D Drysdale
Wigan Athletic v West Ham United
Refa: J Moss
Refa Wasaidizi: R Ganfield, G Beswick
Refa wa Akiba: G Eltringham
Manchester City v Swansea City
Refa: M Atkinson
Refa Wasaidizi: S Burt, J Flynn
Refa wa Akiba: S Attwell
Jumapili Oktoba 28
Everton v Liverpool
Refa: A Marriner
Refa Wasaidizi: S Ledger, S Bennett
Refa wa Akiba: P Dowd
Newcastle United v West Bromwich Albion
Refa: C Foy
Refa Wasaidizi: H Lennard, R West
Refa wa Akiba: M Halsey
Southampton v Tottenham Hotspur
Refa: L Mason
Refa Wasaidizi: D England, D C Richards
Refa wa Akiba: R East
Chelsea v Manchester United
Refa: M Clattenburg
Refa Wasaidizi: M McDonough, S Long
Refa wa Akiba: M Jones
 

LA LIGA: Mabao zaidi kwa Radamel Falcao??

RADAMEL_FALCAOJumapili kwenye La Liga Atletico Madrid watakuwa wenyeji wa Timu iliyo mkiani Osasuna na Straika wao hatari, Radamel Falcao, ana uhakika wa kufunga mabao baada ya kufunga Bao 16 katika Mechi zake 10 zilizopita alizoichezea Atletico Madrid au Timu yake ya Taifa Colombia.
+++++++++++++++++++++++
WAFUNGAJI BORA LA LIGA:
1 Lionel Messi [Barcelona] Mabao 11
2 Cristiano Ronaldo [Real Madrid] 9
Radamel Falcao [Atlético Madrid] 9
4 Aritz Aduriz          [Athletic Bilbao] 6
Álvaro Negredo [Sevilla FC] 6
Tomer Hemed [Mallorca]  6
+++++++++++++++++++++++
Kwenye La Liga, Mabao ya Falcao yameiinua Atletico Madrid na kuifikisha nafasi ya Pili kwenye Msimamo wa Ligi wakiwa Pointi sawa na vinara Barcelona ambao wamewazidi kwa ubora wa tofauti ya Magoli.
Msimu huu, Atletico Madrid imeshinda Mechi zao zote 11 zilizopita.
Atletico Madrid, ambao mara ya mwisho kutwaa Ubingwa wa Spain ni Msimu wa 1995/6, jana Alhamisi waliichapa Academica de Coimbra ya Portugal bao 2-1 kwenye Mechi ya Kundi la EUROPA LIGI.
RATIBA:
Jumamosi Oktoba 27
Espanyol v Málaga [Cornellà - El Prat]
Real Betis v Valencia [Estadio Manuel Ruiz de Lopera]
Celta Vigo v Deportivo La Coruña [Estadio Balaídos]
Rayo Vallecano v Barcelona [Campo de Fútbol de Vallecas]
Jumapili Oktoba 28
Athletic Bilbao v  Getafe [Estadio San Mamés]
Atlético Madrid v Osasuna [Vicente Calderon]
Levante v Granada [Ciudad de Valencia]
Mallorca v Real Madrid [Estadio Son Moix]
Real Zaragoza v Sevilla FC [Estadio La Romareda]
v Real Sociedad [Estadio Nuevo José Zorrilla]
Jumatatu Oktoba 29
Valladolid v Real Sociedad [Estadio Nuevo José Zorrilla]

EUROPA LIGI: Liverpool, Newcastle zatungua, Spurs sare!

EUROPA_LIGI_CUPBao la Dakika ya 53 la Steve Downing limewapa Liverpool ushindi wao bao 1-0 walipocheza na Anzhi Makhachkala ya Urusi wakati Newcastle, wakiwa nyumbani St James Park, waliifunga Club Brugge ya Belgium bao 1-0 kwa bao la Gabriel Obertan huku Tottenham, wakicheza ugenini, walitoka 1-1 na  Maribor ya Slovenia.
Nae Rodrigo Palacio alifunga katika Dakikaya 88 na kuipa Inter Milan ushindi dhidi ya Partizan Belgrade, huku wenzao Lazio wakitoka 1-1 na Panathinaikos, Napoli kuchapwa 3-1 na Dnipro Dnipropetrovsk na Udinese wakipigwa 3-1 na Young Boys kwa hetitriki ya Raul Bobadilla.
Mabingwa watetezi Atletico Madrid wamepata ushindi wao wa tatu mfululizo walipoichapa Academica Coimbra bao 2-1 huku Timu nyingine ya Spain, Athletic Bilbao, Washindi wa Pili Msimu uliopita, wakichapwa 2-1 na Olympique Lyon.

MATOKEO-MECHI DEI 3:

Alhamisi, Oktoba 25
Liverpool FC 1 FC Anzhi Makhachkala 0
BSC Young Boys 3 Udinese Calcio 1
Club Atlético de Madrid 2 A. Académica de Coimbra 1
Hapoel TelvAviv FC 1 FC Viktoria Plzen 2
VfL Borussia Mönchengladbach 2 Olympique de Marseille 0
AEL Limassol FC 0 Fenerbahçe SK 1
Newcastle United FC 1 Club Brugge KV 0
CS Marítimo 1 FC Girondins de Bordeaux 1
FC Steaua Bucuresti 2 Molde FK 0
VfB Stuttgart 0 FC København 0
PSV Eindhoven 1 AIK 1
FC Dnipro Dnipropetrovsk 3 SSC Napoli 1
Videoton FC 2 FC Basel 1
KRC Genk 2 Sporting Clube de Portugal 1
FC Rubin Kazan 1 Neftçi PFK 0
FC Internazionale Milano 1 FK Partizan 0
AC Sparta Praha 3 Hapoel Kiryat Shmona FC 1
Olympique Lyonnais 2 Athletic Club 1
Panathinaikos FC 1 S.S. Lazio 1
NK Maribor 1 Tottenham Hotspur 1
Rosenborg BK 1 FC Metalist Kharkiv 2
SK Rapid Wien 0 Bayer 04 Leverkusen 4
Helsingborgs 1 Hannover 2
Levante UD 3 FC Twente 0
BSC Young Boys 3 Udinese 1
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Novemba 8
FC Anzhi Makhachkala v Liverpool FC
Udinese Calcio v BSC Young Boys
A. Académica de Coimbra v Club Atlético de Madrid
FC Viktoria Plzen v Hapoel TelvAviv FC
Olympique de Marseille v VfL Borussia Mönchengladbach
Fenerbahçe SK v AEL Limassol FC
Club Brugge KV v Newcastle United FC
FC Girondins de Bordeaux v CS Marítimo
Molde FK v FC Steaua Bucuresti
FC København v VfB Stuttgart
AIK v PSV Eindhoven
SSC Napoli v FC Dnipro Dnipropetrovsk
FC Basel 1893 v Videoton FC
Sporting Clube de Portugal v KRC Genk
Neftçi PFK v FC Rubin Kazan
FK Partizan v FC Internazionale Milano
Hapoel Kiryat Shmona FC v AC Sparta Praha
Athletic Club v Olympique Lyonnais
S.S. Lazio v Panathinaikos FC
Tottenham Hotspur FC v NK Maribor
FC Metalist Kharkiv v Rosenborg BK
Bayer 04 Leverkusen v SK Rapid Wien
Hannover 96 v Helsingborgs IF
FC Twente v Levante UD

 

RATIBA YA NAKUNDI ULAYA YASOGEZWA MBELE.

SHIRIKISHO la Soka barani Ulaya-UEFA limeamua kusogeza mbele upangwaji wa ratiba ya michuano ya Ligi ya Mabingwa na Europa League hatua ya mtoano.
 Shughuli hiyo kwa kawaida ilitakiwa kufanyika Desemba 14 mwaka huu lakini wamesogeza mbele kwa siku sita zaidi kwa sababu ambazo hazijawekwa wazi.  
Katika taarifa ya UEFA iliyotumwa katika mtandao imesema kuwa ratiba ya hatua ya mtoano ya michuano hiyo ya Ulaya 2012-2013 ambayo kwa kawaida hufanyika Desemba 14 sasa imesogezwa mbele mpaka Alhamisi Desemba 20 katika makao makuu ya shirikisho hilo jijini Nyon, Switzerland.  
Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya itafanyika katika Uwanja wa Wembley jijino London Uingereza May 25 mwakani huku fainali ya Europa League yenyewe itafanyika jijini Amsterdam, Uholanzi katika Uwanja wa ArenA 10 siku kumi baadae.

NITASHIKANA MIKONO NA TERRY - ROBERTS.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Reading Jason Roberts amesema kuwa atashikana mikono na John Terry lakini amekataa kuweka wazi kama anafikiri nahodha huyo wa Chelsea ni mbaguzi. 
 Terry ambaye ni nahodha wa zamani wa Uingereza amefungiwa mechi nne na kutozwa faini ya paundi 220,000 baada ya kukutwa na hati ya kumfanyia vitendo vya kibaguzi Anton Ferdinand wa Queens Park Rangers mwaka jana.
 Akihojiwa kuhusiana na suala hilo Roberts amesema kuwa atashikana mikono na Terry lakini alipoulizwa kama anadhani beki huyo ni mbaguzi alikwepa swali hilo na kurudia sentensi yake ya kwanza.
 Ikiwa ni mwaka mmoja umepita toka kutokea kwa tukio hilo la Terry lakini kumekuwa na muendelezo wa matukio ya aina hiyo sehemu tofauti likiwemo tukio la mwezi ambapo beki wa timu ya vijana wa miaka chini ya 21 ya Uingereza Danny Rose alianyiwa vitendo vya kibaguzi wakati wa mechi nchini Serbia. 
 Roberts aliungana na wachezaji wengine weusi nchini Uingereza wakiwemo Rio na Anton Ferdinand kutovaa tisheti za kampeni ya kutokomeza ubaguzi michezoni wakidai kusuasua kwa juhudi za kupiga vita suala hilo.

VETTEL AJITENGENEZEA NAFASI NZUR YA KUNYAKUWA TAJI LA INDIAN GRAND PRIX.

DEREVA nyota wa mbio za magari za Langalanga, Sebastian Vettel amefanikiwa kupata nafasi ya kwanza kabla ya kuanza kwa michuano ya Indian Grand Prix nafasi ambayo imemuweka katika nafasi nzuri ya kushinda mashindano hayo kwa mara ya nne mfululizo Jumapili.  
Vettel mwenye umri wa miaka 25 raia wa Ujerumani kutoka timu ya Redbull ambaye anaongoza orodha ya madereva bora kwa alama sita zaidi ya Fernando Alonso wa timu ya Ferrari alitumia muda mzuri wa dakika moja na sekunde 27.
 Dereva wa timu ya MacLaren Jenson Button alishika nafasi ya pili katika mbio hizo huku Alonso akikamata nafasi ya tatu na nafasi ya nne kwenda kwa Lewis Hamilton wakati tano bora ilifungwa na dereva mwenzake Vettel wa timu ya Redbull Mark Webber.  
Mashindano hayo yatafanyika ramsi Jumapili huku Vettel akipambana vilivyo kuhakikisha anashinda na kujiongezea alama ili aweze kuwa bingwa wa dunia mwishoni mwa msimu huu ambao kumebakiwa na mshindano manne pekee.


TANZIA NGUMI.

KOCHA Emanuel Steward ambaye amewafundisha mabondia nguli kama Thomas Hearns, Lennox Lewis na Wladimir Klitschko amefariki dunia akiwa na miaka 68. 
 Alianza kujizolea umaarufu wakati alipokuwa akifundisha jijini Detroit ambapo Hearns aliyekuwa mwanafunzi wake alipokuwa bingwa wa dunia mwaka 1980. Steward ambaye ni raia wa Marekani ndio bondia aliyefundisha mabondia wengi zaidi ambao ni mabingwa wa dunia kuliko kocha yoyote wa mchezo huo na alifanya kazi na bingwa wa uzito wa juu Klitschko Julai mwaka huu. 
 Klitschko alituma salamu zake za rambirambi kwa Steward akimuelezea kama mwalimu bora wa mchezo huo kupata kutokea na kwamba ulimwengu wa masumbwi umempoteza mtu muhimu. 
 Steward ambaye alikuwa akisumbuliwa na kansa ya utumbo pia aliwafundisha mabondia wakubwa kama Wilfred Benitez, Julio Cesar Chavez, Oscar de la Hoya, Evander Holyfield, Mike McCallum na James Toney. 

SEREA AMGARAGAZA TENA AZARENKA.

MCHEZAJI nyota anayeshika namba moja katika orodha za ubora duniani kwa upande wa wanawake mwanadada Victoria Azarenka amebakia katika mashaka kama atamaliza mwaka huu katika nafasi hiyo baada ya kufungwa na Serena Williams kwa mara ya tano katika vipindi tifauti walivyokutana mwaka huu.
 Azarenka ambaye anatoka Belarus alikubali kufungwa kwa 6-4 6-4 naWilliams kutoka Marekani katika michuano ya WTA inayofanyika jijini Istabul ambapo sasa itabidi ahakikishe anamfunga Li Na bingwa wa zamani wa michuano ya wazi ya Ufaransa kutoka China ili aweze kujihakikishia nafasi hiyo.  
Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Williams amesema kuwa alifanya mazoezi ya nguvu ili aweze kucheza vyema na anatarajia ataendlea kufanya vyema na kama ikishindikana atajaribu kufanya hivyo tena mwakani.
 Azarenka ambaye alifungwa na Williams katika michuano ya wazi ya Marekani mwezi uliopita alianza vyema mchezo huo kwa kuongoza katika seti ya kwanza lakini Williams ambaye naye alikuwa akicheza chini ya kiwango alikuja juu na kuhakikisha hapotezi mchezo huo muhimu.
 

TIMU AMBAYO IMESHACHUKUA KOMBE LA LIGI KUU TANGU MWAKA 1965 
  •  

 

Year
Best scorers Team Goals
2004 Tanzania Abubakar Ally Mkangwa Mtibwa Sugar FC 20
2005 Somalia Cisse Aadan Abshir Simba SC 19
2006
n/a n/a
2007 United States Mashiku SC United FC 17
2007/08 Tanzania Michael Katende Kagera Sugar
2008/09 Kenya Boniface Ambani Young Africans FC 18
2009/10 Tanzania Musa Hassan Mgosi Simba SC 18
2010/11 Tanzania Mrisho Ngasa Azam FC 18
2011/12 Tanzania John Bocco Azam FC 19

 MWAKA 2009/2010 TIMU AMBAZO ZILISHUKA DARAJA NI



 ENGLAND: Nini kinawakabili Chelsea, Man United, Man City, Arsenal 6 ZIJAZO!


WALCOTT_WILSHERE_OX>>BAADA ‘VAKESHENI’ Timu kukabiliwa na LIGI, CHAMPIONS LIGI & CAPITAL ONE CUP!!
Ligi Kuu England, rasmi kama Barclays Premier League, BPL, imerudi toka ‘vakesheni’ iliyopisha Mechi za Kimataifa ambazo zipo kwenye Kalenda ya FIFA na hadi Ligi hii inasimama, Mabingwa wa Ulaya, Chelsea, ndio wapo kileleni wakiwa na Pointi 19 na hawajapoteza hata Mechi moja katika 7 huku wakiwa wametoka sare Mechi moja tu.
Timu iliyo nafasi ya pili ni Manchester United yenye Pointi 15 wakifuatia Mabingwa watetezi Manchester City ambao pia wana Pointi 15 lakini wamezidiwa kwa ubora wa magoli.
Mkiani wapo QPR ambao wana Pointi 2 tu.
+++++++++++++++++++++++++++++

MECHI ZINAZOFUATA ZA TIMU VIGOGO KWA MASHINDANO YOTE:
++NI LIGI KUU ENGLAND ISIPOKUWA INAPOTAJWA.
CHELSEA MAN CITY MAN UNITED ARSENAL
Oktoba 20
Spurs v Chelsea
Oktoba 23
Shakhtar v Chelsea [UCL]
Oktoba 28
Chelsea v Man Utd
Oktoba 31
Chelsea v Man Utd
[COC]
Novemba 3
Swansea v Chelsea
Novemba 11
Chelsea v L’pool


Oktoba 20
WBA v Man City
Oktoba 24
Ajax v Man City [UCL]
Oktoba 27
M City v Swansea
Novemba 3
West Ham v M City
Novemba 11
M City v Spurs
Oktoba 20
Man United v Stoke
Oktoba 23
Man U v Braga [UCL]
Oktoba 28
Chelsea v Man Utd
Oktoba 31
Chelsea v Man Utd
[COC]
Novemba 3
Man U v Arsenal
Novemba 10
Villa v Man United
Oktoba 20
Norwich v Arsenal
Oktoba 24
Arsenal v Schalke [UCL]
Oktoba 27
Arsenal v QPR
Oktoba 30
Reading v Arsenal
[COC]
Novemba 3
Man U v Arsenal
Novemba 10
Arsenal v Fulham
++UCL==UEFA CHAMPIONZ LIGI
++COC==CAPITAL ONE CUP
+++++++++++++++++++++++++++++

BPL:
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumamosi, Oktoba 20, 2012
[Saa za Bongo]
[Saa 8 Dak 45 Mchana]
Tottenham Hotspur v Chelsea [White Hart Lane]
[Saa 11 Jioni]
Fulham v Aston Villa [Craven Cottage]
Liverpool v Reading [Anfield]
Manchester United v Stoke City [Old Trafford]
Swansea City v Wigan Athletic [Liberty Stadium]
West Bromwich Albion v Manchester City [The Hawthorns]
West Ham United v Southampton [Upton Park]

[Saa 1 Dak 30 Usiku]
16:30  Norwich City v Arsenal [Carrow Road]
Jumapili, Oktoba 21, 2012
[Saa 9 Dak 30 Mchana]
12:30  Sunderland v Newcastle United [Stadium of Light]
[Saa 12 Jioni]
15:00  Queens Park Rangers v Everton [Loftus Road]

 

JASON ROBERTS asimama ‘KAMILI GADO’ kupinga UBAGUZI!


JASON_ROBERTS>>HATAVAA TISHETI “KICK IT OUT”
>>ADAI TERRY AMECHELEWA MWAKA MMOJA KUUNGAMA!
Jason Roberts ametangaza hatavaa Tisheti ya “KICK IT OUT” ambayo ni ya Kitengo kinachoendesha harakati kufuta Ubaguzi kwenye Soka, ambacho Wiki hii kina Kampeni yake ya msisitizo, kwa vile hajaridhika na nguvu inayotumiwa na mamlaka husika kufuta tatizo hilo na pia amesema Wachezaji wenzake wa rangi nyeusi wanaunga mkono hilo.
Roberts, ambae ni Straika wa Reading, moja ya Timu za Ligi Kuu England ambazo Wikiendi hii zimeombwa Wachezaji wao kuvaa Tisheti zenye Nembo ya “KICK IT OUT” ili kuunga mkono harakati za kuondoa Ubaguzi wa rangi kwenye Soka, amesema hatavaa Tisheti hizo kwa sababu wao wameangushwa na jinsi Ubaguzi unavyochukuliwa.
Alisema: “Sitaivaa. Wametuangusha!”
Roberts amedai John Terry, aliehukumiwa Kifungo cha Mechi 4 na Faini ya Pauni 220,000 na FA kwa tukio lililotokea Tarehe 23 Oktoba 2011,  na jana kukubali kutumikia adhabu na kuomba radhi ni kitendo kilichochelewa.
Roberts amesema: “Kuungama kwake kumechelewa Mwaka mmoja!”
Jumamosi, Reading inasafiri hadi Anfield kucheza na Liverpool ambayo pia ilikumbwa na mkasa wa Ubaguzi baada ya Straika wao Luis Suarez kumkashifu Beki wa Manchester United Patrice Evra kwenye Mechi ya Tarehe 15 Oktoba 2011 na kufungiwa Mechi 8 na Faini Pauni 40,000.
 

LIGI za ULAYA: Zarudi tena kilingeni!


BORUSSIA_DORTMUND_JUKWAA>>LA LIGA, SERIE A & BUNDESLIGA ni moto Wikiendi!!
Kufuatia ‘vakesheni’ ya Wiki mbili ya Ligi huko Barani Ulaya kupisha Mechi za Kimataifa kwa mujibu wa Kalenda ya FIFA, Ligi Vigogo, zile za La Liga, Serie A na Bundesliga, zitarudi tena kilingeni Wikiendi hii na Bundesliga itakuwa ya kwanza dimbani kwa Mechi pekee ya Ijumaa Oktoba 19 kati ya TSG Hoffenheim na SpVgg Greuther Fürth ndani ya Rhein-Neckar-Arena.
ZIFUATAZO ni RATIBA na MISIMAMO ya Ligi hizo:
LA LIGA
[Kwenye Mabano Jina la Uwanja]
Jumamosi Oktoba 20
Málaga v Valladolid [Estadio La Rosaleda]
Real Madrid v Celta Vigo [Estadio Santiago Bernabéu]
Valencia v Athletic Bilbao [Estadio Mestalla]
Deportivo La Coruña v Barcelona [Estadio Riazor]
Jumapili Oktoba 21
Getafe v Levante [Coliseum Alfonso Perez]
Espanyol v Rayo Vallecano [Cornellà - El Prat]
Granada v Real Zaragoza [Estadio Los Cármenes]
Osasuna v Real Betis [Estadio El Sadar]
Real Sociedad v Atlético Madrid [Estadio Anoeta]
Monday, October 22, 2012
Sevilla FC v Mallorca [Estadio Ramon Sanchez Pizjuan]
================================


MSIMAMO:
[Timu za juu tu]
[Kila Timu imecheza Mechi 7]
1 Barcelona Pointi 19
2 Atletico Madrid 19
3 Malaga 14
4 Real Betis 12
5 Real Madrid 11
6 Real Mallorca 11
7 Sevilla 11
8 Real Valladoid 10
9 Getafe 10
10 Rayo Vallecano 10

================================
SERIE A
[Kwenye Mabano Jina la Uwanja]
Jumamosi Oktoba 20
Juventus v Napoli [Juventus Stadium]
Lazio v AC Milan [Stadio Olimpico]
Jumapili Oktoba 21
Cagliari v Bologna [Sant'Elia]
Atalanta v Siena [Atleti Azzurri d'Italia]
Chievo Verona v Fiorentina [Bentegodi]
Inter Milan v Catania [Stadio Giuseppe Meazza]
Palermo v Torino [Renzo Barbera]
Parma v Sampdoria [Ennio Tardini]
Udinese v US Pescara [Stadio Friuli]
Genoa v AS Roma [Luigi Ferraris]
MSIMAMO:
[Timu za juu tu]
[Kila Timu imecheza Mechi 7]
1 Juventus Pointi 19
2 Napoli 19
3 Lazio 15
4 Inter Milan 15
5 AS Roma 11
6 Fiorentina 11
7 Catania 11
8 Sampdoria 10 [Wamekatwa Pointi 1]
9 Genoa 9
10 Torino 8 [Wamekatwa Pointi 1]
11 AC Milan 7
================================

BUNDESLIGA
[Kwenye Mabano Jina la Uwanja]
Ijumaa Oktoba 19
TSG Hoffenheim v SpVgg Greuther Fürth [Rhein-Neckar-Arena]
Jumapili Oktoba 20
Bayer Leverkusen v Mainz [BayArena]
Borussia Dortmund v Schalke 04 [Signal-Iduna-Park]
Eintracht Frankfurt v Hannover 96 [Commerzbank-Arena]
Fortuna Düsseldorf v Bayern Munich [LTU Arena]
VfL Wolfsburg v SC Freiburg [Volkswagen Arena]
Werder Bremen v Borussia Monchengladbach [Weserstadion]
Jumapili Oktoba 21
Nurnberg v FC Augsburg [EasyCredit-Stadion]
Hamburg SV v VfB Stuttgart [HSH Nordbank Arena]
=================================

MSIMAMO:
[Timu za juu tu]
[Kila Timu imecheza Mechi 7]
1 Bayern Munich Pointi 21
2 Eintracht Frankfurt 16
3 Schalke 14
4 Borussia Dortmund 12
5 Hannover 11
6 Bayer Leverkusen 11
7 Fortuna Dusseldorf 10
8 Hamburger 10
9 Mainz 10
10 Borussia Dortmund 9
=================================

CAF CHAMPIONZ LIGI: Nani Fainali kujulikana Wikiendi hii!!


>>SAMATTA: Ataibeba Mazembe ugenini kuwafurahisha Wabongo?
NUSU FAINALI:
[MARUDIANO]
[SAA za BONGO]
Jumamosi Oktoba 20         
22:30 Espérance Sportive de Tunis v TP Mazembe [Stade El Menzah]
Jumapili Oktoba 21         
20:30 Al Ahly v Sunshine Stars [Cairo International Stadium]
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Baada ya sare katika Mechi zote mbili za kwanza za Nusu Fainali za kusaka Klabu Bingwa Afrika, CAF CHAMPIONZ LIGI, Mabingwa watetezi Eseperance ya Tunisia na Vigogo Al Ahly wote wako nyumbani huku macho, masikio na dua za Watanzania wengi zikimwombea mwenzao Straika shupavu Mbwana Ally Samatta apate mafanikio kwa kuivusha Klabu yake Tout Poissant Mazembe ya Congo DR ugenini watakaporudiana na Esperance.
Wiki mbili zilizopita, TP Mazembe ikicheza nyumbani Lubumbashi ilitoka 0-0 na Esperance na safari hii huko Tunisia hamna budi ila magoli yapatikane ili kupata Mshindi atakaesonga Fainali.
Mazembe, ambao tegemezi lao ni Straika Samatta na Mputu, wataingia kwenye Mechi hii bila Stoppila Sunzu ambae ana Kadi na huenda wakawakosa majeruhi Rainford Kalaba na Hichani Himonde, wote wanatoka Zambia.
Tegemezi kubwa kwa Esperance ni Straika wa Ghana Harrison Afful, ambae Msimu uliopita ndie aliwapa Ubingwa kwa kufunga bao la ushindi kwenye Fainali, na Youssef Msakni.
Katika Mechi nyingine itakayochezwa bila ya Watazamaji huko Cairo, Misri, Al Ahly watakuwa nyumbani kuwakaribisha Sunshine Stars ambayo walitoka nayo sare ya bao 3-3 huko Ijebu Ode, Nigeria.
NUSU FAINALI:
MATOKEO:
Jumamosi Oktoba 6        
Sunshine Stars [Nigeria] 3 Al Ahly [Egypt] 3
Jumapili Oktoba 7         
TP Mazembe [Congo, DR] 0 Espérance Sportive de Tunis [Tunisia] 0

 

VPL: Wikiendi Taifa ni Yanga v Ruvu Shooting, Simba v Mgambo Tanga!

>>BONGO, KENYA-Sisi Sote ni Ndugu wapyaaa!
>>SIMBA v KAGERA: Watazamaji 9,842 watengeneza Milioni 58!!
RATIBA:
Jumamosi Oktoba 20
Yanga v Ruvu Shootings
Coastal Union v Mtibwa Sugar [Mkwakwani, Tanga]
Jumapili Oktoba 21
JKT Ruvu v JKT Oljoro [Azam Complex, Dar es Salaam]
Mgambo JKT v Simba [Mkwakwani, Tanga]
Tanzania Prisons v Toto Africans [Sokoine, Mbeya]
++++++++++++++++++++++++++
VPL_LOGOLIGI KUU VODACOM itanguruma tena Wikiendi hii na Jumamosi Vigogo Yanga, ambao sasa wameafikiana na Wadhamini VODACOM kuhusu Nembo kwenye Jezi zao, wapo nyumbani Uwanja wa Taifa, Dar es Saalam kucheza na Ruvu Shooting na Mahasimu wao Simba watacheza ugenini Jumapili huko Mkwakwani na Timu ‘íliyofufuka’ kwa kushinda Mechi 3 mfululizo, Mgambo JKT.
Wakati huo huo, Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, na Shirikisho la Soka Kenya,FKF, wamefikia makubaliano ya kushirikiana katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kuinua kiwango cha mpira wa miguu katika nchi hizo.
TAARIFA YA TFF:
Release No. 171
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Oktoba 18, 2012


TFF, FKF ZAANZISHA USHIRIKIANO MPYA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Kenya (FKF) wamefikia makubaliano ya kushirikiana katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kuinua kiwango cha mpira wa miguu katika nchi hizo.
Akizungumza baada ya mkutano uliowakutanisha vinara wa mashirikisho hayo Dar es Salaam jana, Rais wa TFF, Leodegar Tenga amesema wameamua kurejesha uhusiano huo uliokuwepo zamani baada ya kuwepo utulivu katika uendeshaji mpira wa miguu nchini Kenya.
Amesema maeneo ya ushirikiano ambayo wameagiza yafanyiwe kazi na sekretarieti za pande zote (TFF na KFF) ili baadaye yaingizwe katika Hati ya Makubaliano (MoU) ni mafunzo, waamuzi, mechi za timu za Taifa za wakubwa, vijana na wanawake, na Ligi Kuu.
Rais Tenga pia amesema wameamua kuwepo ziara za mafunzo (study tours) katika maeneo mbalimbali ambapo kwa Kenya wao Ligi Kuu yao iliingia katika mfumo wa kampuni mapema, hivyo itakuwa fursa nzuri kwa Bodi ya Ligi Kuu ambayo iko kwenye mchakato wa kuanzishwa kupata uzoefu kwa wenzao wa Kenya.
Naye Rais wa FKF, Sam Nyamweya aliyefuatana na Makamu wake wa Rais, Robert Asembo amesema ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya ni wa kihistoria, hivyo wameamua kuuanzisha upya kwa faida ya nchi hizo.
Amesema hivi karibuni FKF ilichukua waamuzi kutoka Tanzania waliochezesha mechi ya kirafiki kati ya Kenya (Harambee Stars) na Afrika Kusini (Bafana Bafana), hivyo wameamua kubadilishana waamuzi kwa lengo la kuwaongezea uzoefu.
“Waamuzi wa Tanzania walichezesha vizuri mechi ile. Unajua kwetu kuna upinzani mkubwa katika klabu kama AFC Leopards na Gor Mahia, ukipanga refa utasikia wengine wanalalamika, mara huyo ni Mjaluo. Hata akichezesha vizuri bado watalalamika tu kutokana na upinzani uliopo katika klabu hizo,” amesema.
Rais Nyamweya ameongeza kuwa ili kuondoa malalamiko katika mechi za aina hiyo wanaweza kuchukua waamuzi kutoka Tanzania, na vilevile waamuzi kutoka Kenya wakachezesha mechi za aina hiyo nchini Tanzania.
Amesema vilevile wamepanga kuangalia uwezekano wa kuwa na mechi za kuandaa timu kabla ya kuanza Ligi Kuu za nchi hizo ambapo washindi watatu au wanne wa kwanza katika ligi hizo kushindana.
Kwa upande wa mafunzo, wamekubaliana kuwa kwa vile kila nchi ina wakufunzi wanaotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na la Afrika (CAF) watawatumia kuandaa mafunzo ya mara kwa mara kwa waamuzi, makocha, madaktari wa tiba ya michezo na viongozi badala ya kusubiri mafunzo ya aina hiyo kutoka kwa mashirikisho hayo ya kimataifa.



PAMBANO LA SIMBA, KAGERA SUGAR LAINGIZA MIL 58/-
Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Kagera Sugar lililochezwa jana (Oktoba 17 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya mabao 2-2 limeingiza sh. 58,505,000.
Watazamaji 9,842 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo iliyochezwa kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000, na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 11,013,785.54 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 8,924,491.53.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni posho ya msimamizi wa kituo sh. 120,000, kamishna wa mechi sh. 250,000, waamuzi sh. 440,000, mtathimini wa waamuzi sh. 254,000, mwamuzi wa akiba sh. 70,000, usafi na ulinzi wa uwanja sh. 2,350,000 na Wachina (stadium technical support) sh. 2,000,000.
Umeme sh. 300,000, maandalizi ya uwanja (pitch preparation) sh. 400,000, ulinzi wa mechi sh. 3,500,000 wakati tiketi ni sh. 3,183,890. Gharama za mchezo sh. 3,671,261.85, uwanja sh. 3,671,261.85, Kamati ya Ligi sh. 3,671,261.85, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,202,757.11 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,468,504.74.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
++++++++++++++++++++++++++


MSIMAMO VPL:
1 Simba Mechi 8 Pointi 18
2 Azam FC Mechi 7 Pointi 17
3 JKT Oljoro Mechi 8 Pointi 13
4 Kagera Mechi 8 Pointi 12
5 Yanga SC Mechi 7 Pointi 11
6 Coastal Mechi 7 Pointi 10
7 JKT Ruvu Mechi 8 Pointi 10
8 Prisons Mechi 7 Pointi 9
9 Ruvu Shooting Mechi 7 Pointi 9
10 JKT Mgambo Mechi 8 Pointi 9
11 Mtibwa Sugar Mechi 6 Pointi 8
12 Toto African Mechi 8 Pointi 7
13 African Lyon Mechi 8 Pointi 7
14 Polisi Moro Mechi 8 Pointi 2

VPL: Simba, Azam zote sare!

>>NI SARE ya PILI mfululizo kwa Simba!!
>>NDFA yafafanua waliofariki ajalini Mashabiki si Wachezaji Rusumo FC!
MATOKEO:
Jumatano Oktoba 17
Tanzania Prisons 0 Azam 0
Polisi Morogoro 0 JKT Ruvu 2
Simba 2 Kagera Sugar 2
Mgambo JKT 2 Toto Africans 0
JKT Oljoro 0 African Lyon 0
+++++++++++++++++++++++
VPL_LOGOKwenye Mechi za Ligi Kuu Vodacom zilizochezwa leo, Mabingwa watetezi Simba wameendelea kubaki Nambari Wani kwenye msimamo wa Ligi licha ya kutoka sare 2-2 na Kagera Sugar katika Mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambayo Simba waliongoza kwa bao 2-0 na Kagera kusawazisha bao zote ndani ya Dakika mbili.
Hii ni Mechi ya pili mfululizo Simba kutoka sare kufuatia ile ya 0-0 hivi juzi huko Mkwakwani, Tanga na Coastal Union.
Bao za Simba zilifungwa na Felix Sunzu na Mrisho Ngassa na zile za Kagera kufungwa na Themi Felix na Salum Kanoni kwa Penati.
Kwenye mechi nyingine zilizochezwa leo, Azam FC, ambao wako nafasi ya pili, walitoka sare 0-0 huko Mbeya na Prisons na Mgambo KT, Timu iliyoanza Ligi kwa kudorora, leo imeshinda Mechi yake ya 3 mfululizo kwa kuitandika Toto africans bao 2-0 huko Mkwakwani Tanga.

WAKATI HUO HUO, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Soka cha Wilaya ya Ngara, NDFA, Seif Omary, amefafanua kuwa waliofariki kwenye ajali ya Gari huko Ngara iliyotokea Jumapili Oktoba 14 si Wachezaji wa Rusumo FC bali ni Mashabiki wao waliokuwa kwenye Gari la Polisi lenye namba za usajili PT 2007 lililokuwa limewabeba wakitokea Kabanga katika mchezo wa Ligi ya Polisi Jamii wilayani Ngara.
Awali TFF ilisambaza Taarifa ya kutoa rambirambi za Vifo vya Wachezaji wa Rusiumo FC kwenye ajali iliyokea Oktoba 16.


IFUATAYO NI TAARIFA TOKA NDFA:
Chama cha Soka wilaya ya Ngara, NDFA, kimepokea kwa faraja kubwa Rambirambi kutoka TFF kufuatia vifo vya mashabiki watano wa Timu ya Rusumo Fc kufuatia ajali ya Gari la polisi lenye namba za usajili PT 2007 lililokuwa limewabeba wakitokea Kabanga katika mchezo wa ligi ya polisi jamii wilayani hapa
Pamoja na shukrani hizo napenda kufanya marekebisho kidogo hapo kuwa waliofariki sio wachezaji ni Mashabiki na ajali imetokea tarehe 14 siku ya Jumapili wakati tukitoka Kabanga katika mechi ya kigi ya Polisi Jamii
Kwa niaba ya Chama cha soka wilaya ya Ngara NDFA,Klabu ya Rusumo Fc,familia za marehemu, na familia ya mpira wa miguu kwa ujumla wilayani Ngara kutokana na mchango wa mashabiki hao katika ustawi wa mchezo huu kupitia klabu yao
Ahsante
Makamu Mwenyekiti NDFA
SEIF OMARY
++++++++++++++++++++++++++

MSIMAMO VPL:
1 Simba Mechi 8 Pointi 18
2 Azam FC Mechi 7 Pointi 17
3 JKT Oljoro Mechi 8 Pointi 13
4 Kagera Mechi 8 Pointi 12
5 Yanga SC Mechi 7 Pointi 11
6 Coastal Mechi 7 Pointi 10
7 JKT Ruvu Mechi 8 Pointi 10
8 Prisons Mechi 7 Pointi 9
9 Ruvu Shooting Mechi 7 Pointi 9
10 JKT Mgambo Mechi 8 Pointi 9
11 Mtibwa Sugar Mechi 6 Pointi 8
12 Toto African Mechi 8 Pointi 7
13 African Lyon Mechi 8 Pointi 7
14 Polisi Moro Mechi 8 Pointi 2

RATIBA:
Jumamosi Oktoba 20
Yanga v Ruvu Shootings
Coastal Union v Mtibwa Sugar [Mkwakwani, Tanga]
Jumapili Oktoba 21
JKT Ruvu v JKT Oljoro [Azam Complex, Dar es Salaam]
Mgambo JKT v Simba [Mkwakwani, Tanga]
Tanzania Prisons v Toto Africans [Sokoine, Mbeya]

VPL: Mabingwa Simba Dimbani Kesho Jumatano Taifa!


VPL_LOGO>> LIGI DARAJA LA KWANZA, FDL, KUANZA OKTOBA 24
>> REFA MBAGA kuchezesha KENYA, BAFANA BAFANA Leo Nairobi!
>> TAFCA YAONGEZA MUDA WA KUCHUKUA FOMU
Wakati Ligu Kuu Vodacom, VPL, itaendelea kesho kwa Mabingwa watetezi na Vinara Simba kuwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kucheza na Kagera Sugar, Ligi Daraja la Kwanza, FDL [First Division League], inatarajiwa kuanza Oktoba 24 kwa kushirikisha Timu 24 zilizogawanywa Makundi matatu.
IFUATAYO NI TAARIFA KAMILI TOKA TFF:
Release No. 169
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Oktoba 16, 2012


SIMBA YAANZIA RAUNDI YA NANE KWA KAGERA SUGAR
Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaingia raundi nane kesho (Oktoba 17 mwaka huu) kwa mechi tano huku vinara wa ligi hiyo Simba wakiialika Kagera Sugar kutoka mkoani Kagera kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo namba 52 itachezeshwa na mwamuzi Ronald Swai kutoka Arusha wakati waamuzi wasaidizi ni Julius Kasitu na Methusela Musebula, wote kutoka Shinyanga. Mwamuzi wa akiba ni Ephrony Ndisa wa Dar es Salaam huku mtathimini wa waamuzi akiwa Charles Mchau kutoka Moshi.
Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Tanzania Prisons inayofundishwa na Jumanne Chale na Azam iliyo chini ya kocha Boris Bunjak kutoka Serbia. Nayo Polisi Morogoro iliyopanda msimu huu itakuwa mwenyeji wa JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Jamhuri.
Mgambo Shooting ambayo imepata ushindi mara mbili mfululizo itakuwa nyumbani Uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga ikiikaribisha Toto Africans katika mechi itakayochezeshwa na Geofrey Tumaini wa Dar es Salaam. Oljoro JKT inayonolewa na Mbwana Makata itakuwa nyumbani Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha dhidi ya African Lyon.


LIGI DARAJA LA KWANZA KUANZA OKTOBA 24
Michuano ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ya Tanzania Bara inaanza rasmi Oktoba 24 mwaka huu kwa timu 18 kati ya 24 kujitupa kwenye viwanja tisa tofauti katika ligi hiyo inayochezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.
Mechi za raundi ya kwanza za kundi A zitakazochezwa Oktoba 24 mwaka huu ni Burkina Faso dhidi ya Mbeya City (Jamhuri, Morogoro), Mlale JKT na Small Kids (Majimaji, Songea) na Kurugenzi Mufindi dhidi ya Majimaji (Uwanja wa Wambi, Mufindi mkoani Iringa).
Mkamba Rangers na Polisi Iringa zitakamilisha raundi ya kwanza kwa kundi hilo Oktoba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Mechi za raundi ya pili kwa kundi hilo zitachezwa Oktoba 27 mwaka huu kwa Polisi Iringa vs Mbeya City (Samora, Iringa), Majimaji vs Small Kids (Majimaji, Songea), Burkina Faso vs Mkamba Rangers (Jamhuri, Morogoro) na Kurugenzi Mufindi vs Mlale JKT (Wambi, Mufindi).
Raundi ya tatu ni Oktoba 31 mwaka huu kwa mechi kati ya Mbeya City vs Mlale JKT (Sokoine, Mbeya), Small Kids vs Mkamba Rangers (Nelson Mandela, Sumbawanga), Majimaji vs Burkina Faso (Majimaji, Songea) na Polisi Iringa vs Kurugenzi Mufindi (Samora, Iringa).
Kundi B Oktoba 24 mwaka huu ni Ndanda vs Transit Camp (Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara), Villa Squad vs Moro United (Mabatini, Pwani) wakati Oktoba 25 mwaka huu ni Green Warriors vs Tessema (Mabatini, Pwani) na Polisi Dar es Salaam vs Ashanti United (Chamazi, Dar es Salaam).
Raundi ya pili kwa kundi hilo ni Oktoba 27 mwaka huu Ndanda vs Green Warriors (Nangwanda Sijaona, Mtwara), Villa Squad vs Tessema (Mabatini, Pwani) wakati Oktoba 28 mwaka huu ni Ashanti United vs Transit Camp (Mabatini, Pwani) na Oktoba 29 mwaka huu ni Moro United vs Polisi Dar es Salaam (Chamazi, Dar es Salaam).
Novemba 1 mwaka huu ni Green Warriors vs Ashanti United (Mabatini, Pwani), Novemba 2 mwaka huu ni Polisi Dar es Salaam vs Villa Squad (Chamazi, Dar es Salaam), Novemba 4 mwaka huu ni Tessema vs Ndanda (Chamazi, Dar es Salaam) na Transit Camp vs Moro United (Mabatini, Pwani).
Kundi C ni Oktoba 24 mwaka huu Kanembwa FC vs Polisi Dodoma (Lake Tanganyika, Kigoma), Mwadui vs Morani (Kambarage, Shinyanga), Pamba vs Polisi Mara (Kirumba, Mwanza) na Rhino Rangers vs Polisi Tabora (Ali Hassan Mwinyi, Tabora).
Raundi ya pili ni Oktoba 27 mwaka huu; Polisi Tabora vs Polisi Dodoma (Ali Hassan Mwinyi, Tabora), Mwadui vs Polisi Mara (Kambarage, Shinyanga), Kanembwa FC vs Morani (Lake Tanganyika, Kigoma) na Pamba vs Rhino Rangers (Kirumba, Mwanza).
Oktoba 31 mwaka huu ni raundi ya tatu; Polisi Mara vs Rhino Rangers (Karume, Musoma), Morani vs Polisi Tabora (Kiteto, Manyara), Polisi Dodoma vs Pamba (Jamhuri, Dodoma) na Kanembwa FC vs Mwadui (Lake Tanganyika, Kigoma).


MBAGA AZICHEZESHA KENYA, BAFANA BAFANA
Mwamuzi Oden Mbaga wa Tanzania anayetambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ndiye anayechezesha mechi ya kirafiki kati ya Kenya (Harambee Stars) na Afrika Kusini (Bafana Bafana).
Mechi hiyo inachezwa leo Uwanja wa Kimataifa wa Moi Kasarani jijini Nairobi. Mbaga anasaidiwa na waamuzi wasaidizi wa FIFA, John Kanyenye kutoka Mbeya na Erasmo Jesse wa Morogoro.
TFF imeteua waamuzi hao baada ya kupata maombi kutoka kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kenya (FKF) ambao ndiyo waandaaji wa mechi hiyo ambayo ni moja ya vipimo kwa kocha mpya wa Harambee Stars, Henry Michel kutoka Ufaransa.


TAFCA YAONGEZA MUDA WA KUCHUKUA FOMU
 Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) imeongeza muda kwa wagombea kuchukua fomu kwa ajili ya uchaguzi wa chama hicho ambao sasa utafanyika Novemba 25 mwaka huu.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TAFCA, Ramadhan Mambosasa, jana ndiyo ilikuwa mwisho wa kuchukua fomu lakini mwitikio wa wagombea bado umekuwa mdogo ambapo ni watano tu waliojitokeza.
Hivyo, amesema wameongeza muda wa kuchukua na kurudisha fomu ambapo mwisho itakuwa ni Oktoba 19 mwaka huu saa 10 kamili alasiri. Fomu zinapatikana ofisi za TAFCA ambazo ziko Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.
Nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF, Mhazini na wajumbe watatu wa Kamati ya Utendaji.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

LEO TOKA TFF: 13 WAPITISHWA KUGOMBEA UONGOZI TWFA


Toleo la kuchapisha
TFF_LOGO>> PONGEZI KWA UONGOZI MPYA ARFA
IFUATAYO NI TAARIFA KAMILI:
Release No. 168
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Oktoba 15, 2012
13 WAPITISHWA KUGOMBEA UONGOZI TWFA
Wagombea 13 kati ya 15 waliojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) wamepitishwa baada ya usaili uliofanyika juzi.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TWFA, Ombeni Zavala, waliopitishwa kwenye nafasi ya uenyekiti ni Isabellah Huseein Kapera, Joan Ndaambuyo Minja na Lina Paul Kessy.
Makamu Mwenyekiti ni Rose Kisiwa wakati wanaowania nafasi ya Katibu Mkuu ni Amina Ali Karuma na Cecilia Oreste Makafu. Mgombea pekee wa nafasi ya Katibu Msaidizi, Macky Righton Mhango naye amepita kwenye usaili huo. Aliyepitishwa kwenye nafasi ya Mhazini ni Rose Stewart Msamila.
Furaha Francis na Zena Chande wamepitishwa kuwania nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wakati waliopita kuwania ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya TWFA ni Triphonia Ludovick Temba, Rahim Salum Maguza na Sophia James Charles.
Hivi mchakato wa uchaguzi wa TWFA uko katika kipindi cha kukata rufani ambapo ni kuanzia Oktoba 15-17 mwaka huu. Rufani zinatakiwa zifike kwa Katibu Mkuu wa TFF kabla ya saa 10 kamili jioni ya Oktoba 17 mwaka huu.
Wagombea wawili ambao hawakupitishwa kwa ajili ya uchaguzi huo
unaotarajiwa kufanyika Novemba 4 mwaka huu ni Julliet Mndeme na Jasmin Soud walioomba ujumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF. Wagombea hao ambao pia walikuwa wamewekewa pingamizi hawakufika kwenye usaili.


PONGEZI KWA UONGOZI MPYA ARFA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Oktoba 14 mwaka huu).
Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa COREFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Pwani.
TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya COREFA chini ya uenyekiti wa Hassan Othman Hassan ambaye amechaguliwa tena kuongoza chama hicho.
Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu mkoani Pwani kwa kuzingatia katiba ya COREFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.
Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya COREFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za wanachama wa TFF.
Viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Hassan Othman Hassan (Mwenyekiti), Riziki Majala (Katibu), Geofrey Irick Nyange (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF), Juma Haruna Kisoma (Mwakilishi wa Klabu TFF) na Abubakar Allawi (Mhazini).
Waliochaguliwa kuwa Wajumbe wa Kamati ya Utendaji katika uchaguzi huo uliofanyika kisiwani Mafia ni  Musa Bakari Athumani, Godfrey Magnus Haule na Gwamaka Oden Mlagila. Mwakilishi wa Wanawake ni Florence Ambonisye.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

VPL: Simba bado ipo juu lakini Azam yaja!!


VPL_LOGOKwenye Ligi Kuu Vodacom, baada ya Simba kuvutwa shati ilipotoka sare na Coastal Union ya 0-0 Uwanjani Mkwakwani huko Tanga na Azam FC kuitungua Polisi Moro huko Morogoro, Mechi zote zikichezwa Jumamosi, Simba bado wapo kileleni wakiwa na Pointi 17 lakini Azam wamebaki nafasi ya Pili, Pointi moja nyuma, huku wakiwa na Mechi moja mkononi.
Nafasi ya 3 imeshikwa na JKT Oljoro wakiwa na Pointi 12 wakifuata Yanga wenye 11.
Ligi itaendelea tena Jumatano.


MSIMAMO:
1 Simba Mechi 7 Pointi 17
2 Azam FC Mechi 6 Pointi 16
3 JKT Oljoro Mechi 7 Pointi 12
4 Yanga SC Mechi 7 Pointi 11 [Tofauti ya Magoli 3]
5 Kagera Sugar Mechi 7 Pointi 11 [Tofauti ya Magoli 2]
6 Coastal Mechi 7 Pointi 10
7 Prisons Mechi 7 Pointi 9 [Tofauti ya Magoli 0]
8 Ruvu Shooting Mechi 7 Pointi 9 [Tofauti ya Magoli -1]
9 Mtibwa Sugar Mechi 6 Pointi 8
10 Toto African Mechi 7 Pointi 7 [Tofauti ya Magoli -2]
11 JKT Ruvu Mechi 7 Pointi  [Tofauti ya Magoli -7]
12 JKT Mgambo Mechi 7 Pointi 6 [Tofauti ya Magoli -4]
13 African Lyon Mechi 7 Pointi 6 [Tofauti ya Magoli -6]
14 Polisi Moro Mechi 7 Pointi 2


RATIBA:
Jumatano Oktoba 17
Tanzania Prisons v Azam [Sokoine, Mbeya]
Polisi Morogoro v JKT Ruvu [Jamhuri, Morogoro]
Simba v Kagera Sugar [National Stadium, Dar es Salaam]
Mgambo JKT v Toto Africans [Mkwakwani, Tanga]
JKT Oljoro v African Lyon [Sheikh Amri Abeid, Arusha]
Jumamosi Oktoba 20
Yanga v Ruvu Shootings [Azam Complex, Dar es Salaam]
Coastal Union v Mtibwa Sugar [Mkwakwani, Tanga]
Jumapili Oktoba 21
JKT Ruvu v JKT Oljoro [Azam Complex, Dar es Salaam]
Mgambo JKT v Simba [Mkwakwani, Tanga]
Tanzania Prisons v Toto Africans [Sokoine, Mbeya]

REBELO APUUZA SHUTUMA JUU YA MAANDALIZI YA KOMBE LA DUNIA BRAZIL.

Aldo Rebelo.
WAZIRI wa Michezo wa Brazil, Aldo Rebelo amepuuza shutuma juu ya maandalizi ya ya Kombe la Dunia kwamba matatizo yaliyotokea katika michuano ya Olimpiki jijini London yameonyesha kwamba ni vigumu kuandaa tukio kubwa la michezo kama hilo bila kutokea matatizo.  
Wakati Shirikisho la Soka Duniani-FIFA lilipotembelea viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia Kusini mwa nchi hiyo , waziri huyo alitoa mifano kadhaa ya jinsi mambo yalivyokwenda isivyotakiwa katika michuano ya London. Rebelo amesema kuwa alilazimika kufuta baadhi ya mahojiano aliyotaka kufanyiwa kutokana na foleni kali iliyokuwepo kipindi huku rais wa mamlaka ya olimpiki jijini Rio de Janeiro naye aliibiwa wakati akiwa jijini humo. 
Waziri huyo alisema mbali na matatizo hayo lakini pia kulikuwa na tatizo kubwa la mawasiliano pamoja na watu kupoteza mizigo yao lakini hakuna yoyote aliyewashutumu waandaaji au kusema kuwa mashindano hayo hayakufanikiwa kutokana na matukio hayo.
 Rebelo amekiri kuwa ni kweli ujenzi wa miundo mbinu na viwanja kwa ajili ya Kombe la Dunia unakwenda taratibu lakini aliwahakikishia wakaguzi hao kutoka FIFA kuwa kila kitu kitakamilika kwa wakati.

UEFA KUZICHUKULIA HATUA YA KINIDHAMU SERBIA NA UINGEREZA.

SHIRIKISHO la Soka barani Ulaya-UEFA limefungua mashtaka ya kinidhamu kwa nchi za Serbia na Uingereza na kuamuru uchunguzi wa polisi juu ya tuhuma za ubaguzi zilizotokea katika mchezo wa baina ya nchi hizo wa vijana chini ya miaka 21.
  Wenyeji wa mchezo Serbia wamefunguliwa mashtaka na UEFA juu ya matukio ya ubaguzi wa rangi yaliyoonyesha na mashabiki wake kwenda kwa wachezaji weusi wa Uingereza kabla ya mchezo huo uliochezwa Jumanne usiku. 
Lakini pia vyama vya soka vya nchi zote mbili navyo vimeshtakiwa kwa kushindwa kuzuia vurugu ambazo zilitokea uwanjani mara baada ya mchezo huo kumalizika ambapo Uingereza ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0. Mashtaka hayo yanatarajiwa kusikilizwa na bodi ya nidhamu ya UEFA Novemba 22 mwaka huu.

AYEW APEWA SIKU SABA ZA KUOMBA RADHI.

MCHEZAJI nyota wa timu ya taifa ya Ghana, Andre Ayew amepewa siku saba za kuomba msamaha na Shirikisho la Soka la nchi hiyo-GFA baada ya kutupa kitambaa cha mkononi kuonyesha hasira zake kwa kutolewa katika mchezo dhidi ya Malawi mwishoni mwa wiki. 
  Akihojiwa na redio moja nchini Ghana rais wa GFA Kwesi Nyantakyi amesema katika kikao walichokaa walifikia maamuzi ya kumpa wiki moja Ayew aombe radhi kwa uma kutokana na kitendo chake hicho na kama hata fanya hivyo watamchukulia hatua zinazohusika. 
Waandishi waliokuwa wakiripoti mchezo huo wamebainisha kwamba mara baada ya kutolewa mchezaji huyo alionyesha kukasirika kwani alishindwa hata kuwa mkono wachezaji wenzake waliokuwepo katika benchi la wachezaji wa akiba ingawa mwenye hajasema lolote kuhusiana na hilo. 
Kocha wa timu hiyo Kwesi Appiah pamoja na benchi lake la ufundi nao pia hawajazungumzia lolote kuhusiana na tukio la mchezaji huyo kwa kuwaachia GFA watoe uamuzi wanaouona ni sahihi.


KUUMIA KWA ARBELOA NA SILVA KUMECHANGIA SARE - DEL BOSQUE.

KOCHA wa timu ya taifa ya Hispania, Vicente del Bosque anaamini kuumia kwa nyota wake Alvaro Arbeloa na David Silva ndio kulichangia nchi hiyo kutoa sare ya bao 1-1 dhidi ya Uafaransa katika mchezo wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2014.
 Silva ambaye anacheza katika klabu ya Manchester City ya Uingereza alilazimika kutolewa nje katika dakika 13 ya mchezo huo kutokana na kupata matatizo ya misuli wakati Arbeloa ambaye ni beki wa Real Madrid naye aliumia muda mfupi baadae.
 Del Bosque amesema kuwa kuumia kwa wachezaji hao kulisababisha kikosi chake kushindwa kucheza kama walivyozoea hivyo kusababisha mchezo huo kuwa mgumu lakini pia aliwasifu wapinzani wao kwa kuonyesha soka safi. Hispania inakabiliwa na mechi zingine za kufuzu michuano hiyo Machi 22 mwaka 2013 ambapo wataikaribisha Finland kabla ya kusafiri kuifuata Ufaransa kwa ajili ya mchezo wa marudiano siku nne baadae. 

SJIUZULU NG'O - SENGHOR.

RAIS wa Shirikisho la Soka nchini Senegal-FSF, Augustin Senghor ametangaza kuwa kamati yake ya utendaji haitajiuzulu pamoja na wadau wengi wa soka nchini humo kuwataka kufanya hivyo kufuatia timu ya taifa ya nchi hiyo kushindwa kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika mwakani. Senghor alijibu mashambulizi ya wapinzani wake na kuwaita wahujumu wa maendeleo ya soka la nchi hiyo na kutangaza kuwa FSF imetoa malalamiko dhidi ya mtu asiyejulikana aliyechangia kuvurugika kwa mchezo wao dhidi ya Ivory Coast katika dakika ya 76. Rais huyo aliendelea kutamba kuwa wamechaguliwa kushikilia wadhifa huo kwa kipindi cha miaka minne hivyo hawawezi kujiuzulu kwa ajili ya tukio la vurugu lililotokea Jumamosi na wale wanaotaka wajiuzulu wanapoteza muda wao. Nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya nchi hiyo El Hadji Diouf alimwambia rais wa FSF na kamati yake ya utendaji kuwa wanatakiwa kujiuzulu na kumtaja mwenyekiti wa zamani wa klabu ya Olympique Marseille Pape Diouf kuchukua nafasi hiyo ili kusuka upya mfumo wa soka nchini humo. Mapema Jumatatu FSF ilimtuhumu ingawa sio moja kwa moja Diouf kulipia tiketi zaidi ya 1,000 na kuzigawa kwa wahuni ili wavuruge mchezo wa Jumamosi iliyopita shutuma ambazo zilipingwa vikali na nyota huyo.

 

SIMBA YASHIKWA TENA, AZAM NA PRISONS 0-0, MGAMBO WASHINDA MECHI YA TATU MFULULIZO

Mshambuliaji wa Simba, Felix Sunzu akitafuta mbinu za kumtoka beki wa Kagera Sugar, Benjamin Effe katika mchezo wa leo Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliofanyika leo kwenye Uwanja Taifa, Dar es Salaam. Timu hizo zimetoka sare ya 2-2.


SIMBA SC imetoa sare ya pili mfululizo katika Ligi Kuu hya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kutoka 2-2 na Kagera Sugar jioni hii kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwa matokeo hayo, Simba imefikisha pointi 18 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu, kutokana na Azam FC kulazimishwa sare ya bila kufungana na Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
Hadi mapumziko, Simba SC walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililotiwa kimiani na mshambuliaji wa kimataifa wa Zambia, Felix Mumba Sunzu Jr. dakika ya nane, akiunganisha kwa kichwa krosi ya Nassor Masoud ‘Chollo’ kutoka wingi ya kulia.
Kwa ujumla kipindi cha kwanza timu zote zilishambuliana kwa zamu, ingawa ni Simba walioonekana kufanya mashambulizi ‘yenye akili’ zaidi.
Kipindi cha pili Simba ilirudi na moto tena na katika dakika ya 51, Mrisho Khalfan Ngassa aliifungia timu hiyo bao la pili kwa shuti kali lililowababatiza mabeki wa timu hiyo na kutinga nyavuni.
Hilo lilikuwa bao la tatu kwa Ngassa tangu ajiunge na Simba katika mechi tisa alizoichezea timu hiyo ya Mtaa wa Msimbazi.
Baada ya hapo, Kagera walizinduka na kuanza kulishambulia lango la Simba kupitia pembeni na katika dakika ya 64 Themi Felix aliunganisha kwa kichwa krosi ya George Kavilla na kuifungia Kagera bao la kwanza.
Bao liliwazindua Kagera, ambao waliongeza kasi ya kulishambulia lango la Simba na katika dakika ya 66, Juma Nyosso alimkwatua kwenye eneo la hatari Paul Ngwai na Salum Kanoni akaenda kumtungua Juma Kaseja, akiisawazishia Kagera.
Baada ya hapo timu zilianza kushambuliana kwa zamu na mpira ulinoga zaidi kutokana na mashambulizi ya pande zote mbili.
Katika mechi nyingine, Mgambo imeshinda mechi ya tatu mfululizo, baada ya kuifunga Toto African 2-0 kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. JKT Ruvu imezinduka baada ya kuifunga Polisi Morogoro 2-0 kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro na JKT Oljoro imetoka 0-0 na African Lyon.
Simba SC; Juma Kaseja (Nahodha), Nassor Masoud ‘Chollo’/Uhuru Suleiman, Amir Maftah, Paschal Ochieng, Juma Nyosso, Mwinyi Kazimoto/Edward Christopher, Amri Kiemba, Haruna Moshi/Jonas Mkude, Felix Sunzu, Emmanuel Okwi na Mrisho Ngassa.
Kagera Sugar; Andrew Ntala, Salum Kanoni, Martin Muganyizi, Amandus Nesta (Nahodha), Benjamin Effe/Themi Felix, Malegesi Mwangwa, Daudi Jumanne/Kamana Salum, George Kavilla, Shijja Mkinna, Enyinna Darlington na Wilfred Ammeh/Paul Nwai.
Katika mchezo wa awali, Simba B iliifunga Moro United mabao 3-0 katika mchezo wa utangulizi kabla ya mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Simba na Kagera Sugar, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.   
Mabao ya Simba B inayofundishwa na Suleiman Matola, akisaidiwa na Amri Said ‘Stam’ yalipatikana yote kipindi cha pili, wafungaji Ramadhan Salum dakika ya 65 na 70 na Miraj Athumani dakika ya 85.  Moro United inajiandaa na Ligi Daraja la Kwanza, inayotarajiwa kuanza Oktoba 24, mwaka huu.

VITOTO VYA SIMBA B NI NOMA VYAIKUNG'UTA MORO UNITED YA DARAJA LA KWANZA 3-0 TAIFA

Simba B imeifunga Moro United mabao 3-0 katika mchezo wa utangulizi kabla ya mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Simba na Kagera Sugar, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.    Mabao ya Simba B inayofundishwa na Suleiman Matola, akisaidiwa na Amri Said ‘Stam’ yalipatikana yote kipindi cha pili, wafungaji Ramadhan Salum dakika ya 65 na 70 na Miraj Athumani dakika ya 85.  Moro United inajiandaa na Ligi Daraja la Kwanza, inayotarajiwa kuanza Oktoba 24, mwaka huu.
Benchi la Ufundi la Simba, Matola, Msaidizi wake, Amri na Meneja Patrick 

Ramadhan Salum akiwapa shughuli mabeki wa Moro United

Ramadhani Salum na Abdallah Seseme, wakimpongeza Miraj Athumani kufunga bao la tatu


MSIBA MZITO FAMILIA YA SOKA TANZANIA



SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za vifo vya wachezaji watano wa timu ya Rusumo FC ya mkoani Kagera vilivyotokea jana jioni (Oktoba 16 mwaka huu).
Ofisa Habari wa TFF, Boniphace Wambura Mgoyo AMESEMA leo kwamba Rusumo FC ilikuwa ikitoka kwenye mechi ya michuano ya Polisi Jamii Wilaya ya Ngara ambapo ikiwa njiani kurudi Rusumo kutoka mjini Ngara ilipata ajali ya gari na wachezaji watano kufariki papo hapo.
Alisema wachezaji wengine ambao ni majeruhi wamelazwa Hospitali ya Wilaya ya Ngara ya Murugwanza huku wawili hali zao zikiwa mbaya.
Alisema msiba huo ni pigo kwa familia za marehemu, klabu ya Rusumo FC, Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Ngara (NDFA), Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera (KRFA) na familia ya mpira wa miguu kwa ujumla nchini kutokana na mchango wa wachezaji hao katika ustawi wa mchezo huu kupitia klabu yao.
“TFF inatoa pole kwa familia za marehemu, Rusumo FC, NDFA na KRFA na kuwataka kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Kutokana na msiba huo, mechi zote za Ligi Kuu ya Vodacom zinazochezwa leo (Oktoba 17 mwaka huu) kutakuwa na dakika moja ya maombolezo ili kutoa heshima kwa marehemu hao. Mungu aziweke roho za marehemu mahali pema peponi,”alisema Wambura.
Wakati huo huo: Wambura amesema kwamba Kocha Mkuu wa timu ya taifa, Taifa Stars, Mdenmark Kim Poulsen wikiendi hii ataanza ziara ya Zanzibar kuangalia Ligi Kuu ya Zanzibar.
Alisema Kim anatarajia kushuhudia mechi zilizopungua tano akianzia kisiwani Pemba ambapo kati ya Oktoba 19 na 21 atashuhudiwa mechi mbili zitakazochezwa kwenye Uwanja wa Gombani. Mechi hizo ni kati ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Grand Malta, Super Falcon ambao watacheza na vinara wa ligi hiyo Bandari, na baadaye mechi kati ya Duma na Bandari.
“Baadaye atakwenda Unguja kwenye Uwanja wa Amaan ambapo baadhi ya mechi alizopanga kushuhudia ni kati ya Mtende na Chipukizi, Mundu na Jamhuri na KMKM dhidi ya Zimamoto,”alisema Wambura.

No comments:

Post a Comment