Monday, October 8, 2012

MILOVAN ASEMA AKUFFO TATIZO KIWANGO NDIO MAANA BENCHI

Daniel Akuffo mbele ya Mrisho Ngassa

KOCHA Mkuu wa Simba SC, Profesa Milovan Cirkovick amesema kwamba mshambuliaji mpya kutoka Ghana, Daniel Akuffo anatakiwa aongeze juhudi na kupandisha kiwango chake, ili apate nafasi kwenye kikosi cha kwanza, lakini kwa sasa ataendelea kuanzia benchi kwa kuwa anazidiwa uwezo na wachezaji wanaoanza.
 
 
Akizungumza baada ya mechi dhidi ya JKT Oljoro juzi, Mserbia huyo alisema kwamba Akuffo anaanzia benchi kwa sasa kwa sababu kuna wachezaji walio vizuri mno zaidi yake na ndio wanapewa nafasi. “Ajitahidi, atakapokuwa vizuri atapata nafasi ya kuanza, ila kwa sasa anazidiwa na wanaoanza,”alisema Milovan.
 
 
Daniel Akuffo aliyesajiliwa msimu huu kutoka ASEC Mimosa ya Ivory Coast, aliingia kwa kishindo      Simba akifunga katika mechi nne mfululizo, lakini baada ya hapo kasi yake imezimika na amefikisha jumla ya mechi 10, akiwa amefunga mabao matano tu, katika ligi bao moja tu. Katika mabao hayo matano aliyofunga jumla hadi sasa mshambuliaji huyo mrefu, mawili ni ya penalti.
 
 
Simba SC juzi ilizidi kujiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kufuatia ushindi wa mabao 4-1 ilioupata kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha, ambayo ilimaliza pungufu ya wachezaji wawili baada ya kipa wake Shaibu Issa na mshambuliaji Meshack Nyambele kutolewa kwa kadi nyekundu kipindi cha pili.
 
 
Katika mechi hiyo iliyochezeshwa na refa Amon Paul wa Mara, aliyesaidiwa na Anold Bugabo wa Singida na Charles Simon wa Dodoma, hadi mapumziko Simba walikuwa tayari mbele kwa mabao 2-1, mabao yake yote yakitiwa kimiani na kiungo Amri Ramadhan Kiemba katika dakika za 16 na 44, wakati la Oljoro lilifungwa na Paul Nonga dakika ya 29.
 
 
Kiemba alifunga bao la kwanza akiunganisha krosi pasi ya Christopher Edward, wakati bao la pili lilitokana na krosi ya Nassor Masoud ‘Chollo’, yote kutokana na mashambulizi ya upande wa kulia.
 
 
Ilikuwa rahisi kwa Kiemba kufunga mabao yote akiwa kwenye eneo la hatari, kutokana na mabeki wa Oljoro kumuwekea ulinzi zaidi Felix Sunzu.
Nonga naye alifunga bao lake baada ya kupewa pasi ndefu na kumpiga chenga kipa na Nahodha wa Simba, Juma Kaseja upande wa kulia mwa Uwanja na kuutumbukiza mpira nyavuni kiulaini.
 
 
Bao hilo lilitokana na beki Paul Ngalema kupokonywa mpira wakati amepanda kusaidia mashambulizi na Oljoro wakafanya shambulizi la haraka.
Kipindi cha pili Simba walirudi vizuri zaidi uwanjani na kuuteka zaidi mchezo- jambo ambalo liliwafanya Oljoro wawapunguze kasi kwa kuwachezea rafu. Hilo liliwagharimu kupoteza wachezaji wao wawili kabla ya filimbi ya mwisho na kufungwa mabao mawili zaidi.
 
 
Dakika ya 83 Mganda Emanuel Okwi aliifungia Simba bao la tatu na katika dakika ya tatu ya muda wa nyongeza baada ya kutimu dakika 90 za mchezo, Okwi akiwa anaelekea kufunga tena, alikwatuliwa na kipa wa Oljoro Shaibu Issa na refa akaamuru penalti sambamba na kumtoa nje kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja mlinda mlango huyo.
 
 
Awali ya hapo, Oljoro ilimpoteza mchezaji mwingine, Nyambele dakika ya 78, ambaye alionyeshwa njano ya pili kwa rafu aliyomchezea Jonas Mkude. Nahodha Kaseja alitaka kwenda kupiga, lakini akazuiwa na Felix Mumba Sunzu akaenda kufunga bao la nne kwa mkwaju wa penalti.
 
 
Kwa ushindi huo, Simba imefikisha pointi 16 baada ya kucheza mechi sita, hivyo kuendelea kuongoza Ligi Kuu, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 13, ingawa imecheza mechi tano.

YANGA WAWASHIKA 'UCHAWI' SIMBA SC KIPIGO CHA KAGERA

Yanga SC katika moja ya mechi zao, ambazo wanadai eti Simba wanatia mkono


YANGA SC imesema kwamba wamegundua Simba SC ‘wanatia mkono’ kwenye mechi zao na ndio maana zinakuwa ngumu, ila kuanzia sasa na wao wanaanza ‘fitina’.
 
Madai hayo yanakuja, baada ya jana kuchapwa bao 1-0 na Kagera Sugar katika mchezo wake wa sita wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, uliopigwa Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.
“Simba ilituma watu Bukoba watie mkono mechi yetu, sisi tuliwashitukia hao watu baadaye sana, lakini tunashangaa kwa nini wanafanya hivi, wakati sisi tulizungumza nao tukakubaliana haya mambo tuyaache, tucheze mpira, sasa wao wanatuzunguka wanaendeleza mchezo mchafu,”alisema kiongozi Mjumbe mmoja wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, ambaye hakutaka kutajwa jina.
Mjumbe huyo alisema kwamba wao walijua baada ya makubaliano na Simba kutofanyiana fitina, waliamini mambo hayo hayatakuwapo, lakini baada ya kugundua wenzao wamewageuka sasa na wao wanaanza ‘mchezo huo’.
“Na sisi sasa tunaanza kuzicheza mechi zao, wakumbuke tu wao ndio walichokoza nyuki, sasa subirini kuanzia mechi yao na Coastal, wakishinda wao wanaume, na pamoja na kuzicheza mechi zao, tunajizatiti katika mechi zetu. Uzuri watu wote wanaowatumia tumekwishawajua, ni wale wale waliokuja Morogoro, na wale wale waliokuja Bukoba. Tumekwishawajua,”alisema Mjumbe huyo.   
Bao pekee la Themi Felix katika dakika ya 67, jana liliwapa Kagera Sugar ushindi wa 1-0 dhidi ya Yanga SC, kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Felix aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Mnigeria, Enyinna Darlington kwa kumtungua bao hilo, kipa Mghana wa Yanga, Yaw Berko, ameendeleza rekodi yake kuvifunga vigogo, Simba na Yanga katika Uwanja huo.
Hiyo inakuwa mechi ya pili Yanga kufungwa ndani ya mechi sita walizocheza hadi sasa na mbili wametoka sare- maana yake inabaki na pointi zake nane na kuzidi kujipunguzia matumaini ya ubingwa msimu huu, ikiwa sasa inazidiwa pointi nane na vinara wa ligi hiyo Simba SC.
Aidha, hii ni mechi ya pili Yanga inacheza chini ya kocha wake mpya, Mholanzi Ernie Blandts aliyerithi mikoba ya Mbelgiji, Tom Saintfiet na katika mechi hizo mbili ameambulia pointi moja kutokana na sare dhidi ya Simba Jumatano.  
Kwa ujumla Yanga haijashinda hata mechi moja ya ugenini kati ya tatu ilizocheza hadi sasa, ilitoka 0-0 na Prisons, ikafungwa 3-0 na Mtibwa na jana imechapwa 1-0 na Kagera Sugar, wakati Alhamisi itacheza na Toto African mjini Mwanza.
Katika mechi hiyo ya jana, Yanga ilipata pigo dakika ya 23 baada ya mshambuliaji wake mahiri na tegemeo, Said Bahanuzi ‘Spider Man’ kuchanika nyama za paja dakika ya 23, baada ya kugongana na beki Benjamin Effe wa Kagera Sugar na kushindwa kuendelea na mchezo, nafasi yake ikichukuliwa na Jerry Tegete.
Tangu ajiunge na Yanga akitokea Mtibwa Sugar msimu huu, leo Bahanuzi amecheza mechi ya 13 kwa dakika hizo 23 na ameifungia timu hiyo jumla ya mabao 12, matatu kati ya hayo kwa penalti. 
Katika mechi zilizochezwa juzi za ligi hiyo, Simba SC ilizidi kujiimarisha kileleni kufuatia ushindi wa mabao 4-1 ilioupata kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha, ambayo ilimaliza pungufu ya wachezaji wawili baada ya kipa wake Shaibu Issa na mshambuliaji Meshack Nyambele kutolewa kwa kadi nyekundu kipindi cha pili.
Katika mechi hiyo iliyochezeshwa na refa Amon Paul wa Mara, aliyesaidiwa na Anold Bugabo wa Singida na Charles Simon wa Dodoma, hadi mapumziko Simba walikuwa tayari mbele kwa mabao 2-1, mabao yake yote yakitiwa kimiani na kiungo Amri Ramadhan Kiemba katika dakika za 16 na 44, wakati la Oljoro lilifungwa na Paul Nonga dakika ya 29.
Kiemba alifunga bao la kwanza akiunganisha krosi pasi ya Christopher Edward, wakati bao la pili lilitokana na krosi ya Nassor Masoud ‘Chollo’, yote kutokana na mashambulizi ya upande wa kulia.
Ilikuwa rahisi kwa Kiemba kufunga mabao yote akiwa kwenye eneo la hatari, kutokana na mabeki wa Oljoro kumuwekea ulinzi zaidi Felix Sunzu.
Nonga naye alifunga bao lake baada ya kupewa pasi ndefu na kumpiga chenga kipa na Nahodha wa Simba, Juma Kaseja upande wa kulia mwa Uwanja na kuutumbukiza mpira nyavuni kiulaini.
Bao hilo lilitokana na beki Paul Ngalema kupokonywa mpira wakati amepanda kusaidia mashambulizi na Oljoro wakafanya shambulizi la haraka.
Kipindi cha pili Simba walirudi vizuri zaidi uwanjani na kuuteka zaidi mchezo- jambo ambalo liliwafanya Oljoro wawapunguze kasi kwa kuwachezea rafu. Hilo liliwagharimu kupoteza wachezaji wao wawili kabla ya filimbi ya mwisho na kufungwa mabao mawili zaidi.
Dakika ya 83 Mganda Emanuel Okwi aliifungia Simba bao la tatu na katika dakika ya tatu ya muda wa nyongeza baada ya kutimu dakika 90 za mchezo, Okwi akiwa anaelekea kufunga tena, alikwatuliwa na kipa wa Oljoro Shaibu Issa na refa akaamuru penalti sambamba na kumtoa nje kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja mlinda mlango huyo.
Awali ya hapo, Oljoro ilimpoteza mchezaji mwingine, Nyambele dakika ya 78, ambaye alionyeshwa njano ya pili kwa rafu aliyomchezea Jonas Mkude. Nahodha Kaseja alitaka kwenda kupiga, lakini akazuiwa na Felix Mumba Sunzu akaenda kufunga bao la nne kwa mkwaju wa penalti.
Kwa ushindi huo, Simba imefikisha pointi 16 baada ya kucheza mechi sita, hivyo kuendelea kuongoza Ligi Kuu, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 13, ingawa imecheza mechi tano.
Katika mechi nyingine za jana, Mgambo imepata ushindi wake wa kwanza baada ya kuichapa Polisi Morogoro 1-0, wakati Toto African imeichapa JKT Ruvu 2-1 na Prisons imelazimishwa sare ya bila kufungana na Mtibwa Sugar.

ZANZIBAR YAJITOA MICHUANO YA CAF 2012



WAWAKILISHI wa Zanzibar katika michuano ya Afrika mwakani, Super Falcon waliofuzu kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika na Jamhuri waliofuzu kucheza Kombe la Shirikisho wamejitoa kwenye michuano hiyo.
 
 
Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Rais wa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), Aman Ibrahim Makungu, zimesema kwamba timu hizo zimeamua kujitoa katika michuano hiyo kwa sababu hazina fedha, ambapo kila timu ilihitaji kiasi cha dola za 
 
Kimarekani 30,000, zaidi ya Sh. Milioni 45 kwa ajili ya maandalizi ya ushiriki wa michuano hiyo.
 
 
Kufuatia hatua hiyo ZFA, iko katika mazungumzo na baadhi ya klabu za Ligi Kuu ili kuona kama kuna uwezekano wa kupata timu zitakazochukua nafasi hizo.
Mwaka huu Zanzibar iliwakilishwa na timu ya Mafunzo katika ligi ya Mabingwa Afrika, huku Jamhuri wakipata nafasi ya kushirki katika kombe la Shirikisho.
Hata hivyo timu zote zilishindwa kufanya vizuri baada ya kuondolewa katika hatua ya mwanzo katika michuano hiyo.

KOMBE la DUNIA 2014: FIFA yaipora Sudan Pointi Mechi iliyoifunga Zambia!

Jumanne, 09 Oktoba 2012 08:55
   
>>FA Sudan Faini Dola 6,340!
BRAZIL_2014_BESTFIFA imeinyang’anya Sudan ushindi wake wa Bao 2-0 walioifunga Zambia kwenye Mechi ya Kundi D ya Mechi za Mchujo kuwania kucheza Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Brazil baada ya kumchezesha Mchezaji mmoja ambae hakustahili kucheza Mechi hiyo.


Kamati ya Nidhamu ya FIFA imeamua kuwa Mchezaji Saif Ali hakutakiwa kucheza Mechi hiyo waliyoshinda Sudan Mjini Khartoum hapo Juni 2 Mwaka huu baada ya kuwa na Kadi za Njano alizopata katika Mechi za nyuma ikiwemo ile ambayo Zambia waliichapa Sudan kwenye Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2012, iliyochezwa huko Gabon na Equatorial Guinea.


FIFA imeamua sasa kuipa Pointi 3 Zambia na goli 3-0 na pia kukitwanga Faini ya Dola 6,340 Chama cha Soka cha Sudan.


Uamuzi huu wa FIFA unaifanya Zambia sasa iongoze Kundi D ikiwa na Pointi 6 kwa Mechi mbili ikifuatiwa na Ghana wenye Pointi 3, Sudan nafasi ya 3 wakiwa na Pointi 1 na Lesotho wako mkiani wakiwa na Pointi 1.


MSIMAMO KUNDI D:
1 Zambia Mechi 2 Pointi 6
2 Ghana Mechi 2 Pointi 3
3 Sudan Mechi 2 Pointi 1
4 Lesotho Mechi 2 Pointi 1


RATIBA/MATOKEO:
01/06/12: Ghana 7-0 Lesotho
02/06/12: Sudan 2-0 Zambia [Matokeo yamefutwa sasa ni Sudan 0 Zambia 3]
12/06/12: Zambia 1-0 Ghana
10/06/12: Lesotho 0 Sudan 0
22-26/03/13: Ghana v Sudan; Lesotho v Zambia
07-11/06/13: Sudan v Ghana; Zambia v Lesotho
14-18/06/13: Lesotho v Ghana; Zambia v Sudan
06-10/09/13: Ghana v Zambia; Sudan v Lesotho

VPL: Yanga yafa Kagera!

Jumatatu, 08 Oktoba 2012 20:11
   
>>KIPIGO CHAIPOROMOSHA HADI NAFASI YA 8!!
MATOKEO:
Jumatatu Oktoba 8
Kagera Sugar 1 Yanga 0 (Uwanja wa Kaitaba, Bukoba)
++++++++++++++++++++++++++
VPL_LOGOYanga leo huko Uwanja wa Kaitaba, Bukoba walipigwa bao 1-0 na Kagera Sugar na kuporomoshwa hadi nafasi ya 8 katika Mechi pekee ya Ligi Kuu Vodacom huku ushindi huo ukiupaisha Kagera Sugar hadi nafasi ya 3 kwa kufikisha Pointi 10 wakiwa nyuma ya Azam wenye Pointi 13 na vinara Simba wenye 16.

 Bao la ushindi kwa Kagera Sugar lilifungwa katika Dakika ya 68 na Themi Felix.

Mechi hii ya Kagera Sugar na Yanga ilikuwa ichezwe jana lakini kutokana na Uwanja wa Kaitaba kuwa na shughuli nyingine za kijamii ikaahirishwa hadi leo.


Mechi ifuatayo kwa Yanga ni huko Mwanza dhidi ya Toto Africans Siku ya Alhamisi Oktoba 11.


MSIMAMO:
1 Simba Mechi 6 Pointi 16
2 Azam FC Mechi 5 Pointi 13
3 Kagera Sugar Mechi 6 Pointi 10
4 Prisons Mechi 6 Pointi 9 [Tofauti ya Magoli 1]
5 Coastal Mechi 6 Pointi 9 [Tofauti ya Magoli 0]
6 JKT Oljoro Mechi 6 Pointi 9 [Tofauti ya Magoli 0]
7 Mtibwa Sugar Mechi 5 Pointi 8 [Tofauti ya Magoli 3]
8 Yanga SC Mechi 6 Pointi 8 [Tofauti ya Magoli 1]
9 Toto African Mechi 6 Pointi 7 [Tofauti ya Magoli 0]
10 Ruvu Shooting Mechi 6 Pointi 6 [Tofauti ya Magoli -2]
11 African Lyon Mechi 6 Pointi 6 [Tofauti ya Magoli -5]
12 JKT Ruvu Mechi 6 Pointi 6 [Tofauti ya Magoli -7]
13 JKT Mgambo Mechi 6 Pointi 3
14 Polisi Moro Mechi 6 Pointi 2

FALCON, JAMHURI zajitoa Michuano ya CAF 2013!

Jumatatu, 08 Oktoba 2012 19:50
   
>>RIPOTI na Ally Mohammed, COCONUT FM 88.2, Zenji
Wawakilishi wa Zanzibar katika Michuano ya Kimataifa kwa Vilabu Barani Afrika kwa Mwaka 2013, Falcon na Jamhuri, wamejitoa katika michuano hiyo.


Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu Visiwani Zanzibar, ZFA, Aman Ibrahim Makungu, ni kuwa Timu ya Super Falcon ambao ni Mabingwa watetezi katika Ligi Kuu ya Zanzibar, ambao walikuwa waiwakilishe Zanzibar katika Ligi ya Mabingwa Barani Afrika Mwakani pamoja na Timu ya Jamhuri ambao ni Makamo Bingwa wa Ligi Kuu ya Zanzibar na ambao walikuwa waiwakilishe Zanzibar katika Kombe la Shirikisho hapo mwakani kwa pamoja wameamua kujitoa katika michuano hiyo.
Chanzo cha Timu hizo kujitoa inasemekana ni ukata wa fedha, ambapo kila timu ilihitaji Dola 30,000 kwa ajili ya maandalizi ya ushiriki wa michuano hiyo.


Kufuatia hatua hiyo ZFA, iko katika mazungumzo na baadhi ya Vilabu vya Ligi Kuu ili kuona kama kuna uwezekano wa kupata Timu zitakazochukua nafasi hizo.


Mwaka huu Zanzibar iliwakilishwa na timu ya Mafunzo katika Ligi ya Mabingwa Barani Afrika, huku Jamhuri wakipata nafasi ya kushirki katika Kombe la Shirikisho.


Hata hivyo Timu zote zilishindwa kufanya vizuri baada ya kuondolewa katika hatua ya mwanzo katika michuano hiyo.

MECHI za KIMATAIFA: Kurindima kuanzia Ijumaa!!

Jumatatu, 08 Oktoba 2012 19:31
 
BRAZIL_2014_BEST>>ULAYA na kwingineko ni MCHUJO KOMBE la DUNIA 2014
>>AFRIKA ni kuwania Fainali AFCON 2013 huko Afrika Kusini!!
Ijumaa Oktoba 16, Mechi za Kimataifa zitaanza kuchezwa na Barani Ulaya, Marekani ya Kusini na kwingineko ni Mechi za Mchujo kuwania kufuzu kucheza Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Brazil lakini kwa Afrika, hapo Jumamosi na Jumapili, kutakuwa na Mechi za marudiano za Raundi ya Mwisho ya Mchujo kupata Timu 15 zitakazoungana na Wenyeji Afrika Kusini kucheza Fainali za AFCON 2013, Kombe la Mataifa ya Afrika, Januari 2013.


RATIBA MECHI ZOTE:
ULAYA-Mechi za Makundi Kombe la Dunia 2014
[Saa za Bongo]
Ijumaa Oktoba 12
1800 Russia v Portugal
1830 Finland v Georgia
1900 Armenia v Italy
1900 Faroe Islands v Sweden
1900 Kazakhstan v Austria
2000 Albania v Iceland
2000 Czech Republic v Malta
2030 Liechtenstein v Lithuania
2030 Turkey v Romania
2100 Belarus v Spain
2100 Bulgaria v Denmark
2100 Moldova v Ukraine
2115 Slovakia v Latvia
2130 Estonia v Hungary
2130 Netherlands v Andorra
2130 Serbia v Belgium
2145 Greece v Bosnia-Hercegovina
2145 Rep of Ireland v Germany
2145 Wales v Scotland
2200 England v San Marino
2200 Luxembourg v Israel
2230 Macedonia v Croatia
2230 Switzerland v Norway
2245 Slovenia v Cyprus


Jumanne Oktoba 16
Albania v Slovenia
Andorra v Estonia
Belarus v Georgia
Belgium v Scotland
Bosnia-Hercegovina v Lithuania
Czech Republic v Bulgaria
Hungary v Turkey
Iceland v Switzerland
Israel v Luxembourg
Latvia v Liechtenstein
Macedonia v Serbia
Portugal v Northern Ireland
Romania v Netherlands
Russia v Azerbaijan
San Marino v Moldova
Slovakia v Greece
Spain v France
Ukraine v Montenegro
2000 Cyprus v Norway
2100 Faroe Islands v Rep of Ireland
2130 Austria v Kazakhstan
2130 Croatia v Wales
2145 Germany v Sweden
2145 Italy v Denmark
2200 Poland v England


FAHAMU:
-ULAYA yapo Makundi 9
-Washindi 9 wa kila Kundi wataingia Fainali moja kwa moja na Washindi wa Pili 8 bora wenye rekodi nzuri dhidi ya Timu zilizomaliza nafasi za Kwanza, Tatu, Nne na Tano kwenye Kundi lao watapelekwa kwenye Droo kupanga Mechi 4 za Mchujo, zitakazochezwa nyumbani na ugenini, ili kupata Timu nne zitakazoingia Fainali.
++++++++++++++++++++++++++++++
AFCON 2013=Kombe la Mataifa ya Afrika
[Fainali Afrika Kusini-Januari 2013]
[Kwenye Mabano Matokeo Mechi za kwanza]


Jumamosi Oktoba 13
Malawi v Ghana [0-2]
Botswana v Mali [0-3]
Nigeria v Liberia [2-2]
Uganda v Zambia [0-1]
E.Guinea v Congo DR [0-4]
Senegal v Cote d'Ivoire [2-4]
Tunisia v Sierra Leone [2-2]
Morocco v Mozambique [0-2]


Jumapili Oktoba 14
Algeria v Libya [1-0]
Cameroon v Cape Verde [0-2]
Togo v Gabon [1-1]
Angola v Zimbabwe [1-3]
Niger v Guinea [0-1]
Ethiopia v Sudan [3-5]
Burkina Faso v Central African Republic [0-1]
FAHAMU: Washindi 15 wa Mechi hizi watajumuika na Wenyeji Afrika Kusini kwenye Fainali zitakazochezwa Afrika Kusini Januari 2013.
++++++++++++++++++++++++++++++
MAREKANI ya KUSINI-Mechi za Makundi Kombe la Dunia 2014


MSIMAMO:
1 Argentina Mechi 7 Pointi 14
5 Colombia Mechi 7 Pointi 13
3 Ecuador Mechi 7 Pointi 13
4 Uruguay Mechi 7 Pointi 12
2 Chile Mechi 7 Pointi 12
6 Venezuela Mechi 8 Pointi 11
7 Peru Mechi 7 Pointi 7
8 Bolivia Mechi 7 Pointi 4
9 Paraguay Mechi 7 Pointi 4


FAHAMU: Timu 4 za juu zinatinga Fainali Brazil moja kwa moja na ile ya 5 itaenda Mechi ya Mchujo.


Ijumaa Oktoba 12
Colombia v Paraguay
Ecuador v Chile
Bolivia v Peru
Argentina v Uruguay


Jumanne Oktoba 16
Bolivia v Uruguay
Venezuela v Ecuador
Paraguay v Peru
Chile v Argentina
++++++++++++++++++++++++++++++
CONCACAF [Nchi za Marekani ya Kati, Kaskazini na Carribean]- Mechi za Makundi Kombe la Dunia 2014==RAUNDI ya 3
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
KUNDI A
-USA
-Guatemala
-Jamaica
-Antigua and Barbuda

KUNDI B
-Mexico
-El Salvador
-Costa Rica
-Guyana

KUNDI C
-Panama
-Honduras
-Canada
-Cuba



FAHAMU:
-Mshindi wa kila Kundi na Mshindi wa Pili wataingia Raundi ya 4 ambayo ni ya mwisho itayochezwa kwa mtindo wa Ligi ili kutoa Timu 3 zitakazoenda Fainali za Kombe la Dunia moja kwa moja na ya 4 itapelekwa Mechi ya Mchujo.
-Kundi B: Mexico wamefuzu kuingia Raundi ya 4 kwa vile tayari wana Pointi 12 wakifuatiwa na El Salvador wenye 5, Costa Rica 4 na Guyana 1 huku kila Timu imebakiza Mechi 2.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++


RATIBA:
Ijumaa Oktoba 12
Antigua and Barbuda v USA
El Salvador v Costa Rica
Canada v Cuba
Guatemala v Jamaica
Guyana v Mexico
Panama v Honduras


Jumanne Oktoba 16
Honduras v Canada
Cuba v Panama
USA v Guatemala
Jamaica v Antigua and Barbuda
Costa Rica v Guyana
Mexico v El Salvador

BPL: Likizoni hadi Oktoba 20!

Jumatatu, 08 Oktoba 2012 17:55
 
>>KILELENI BADO Chelsea, Man United!
>>BAADA ‘VAKESHENI’ Timu kukabiliwa na CHAMPIONS LIGI & CAPITAL ONE CUP!!
BPL_LOGOLigi Kuu England, rasmi kama Barclays Premier League, BPL, inaenda ‘vakesheni’ kupisha Mechi za Kimataifa ambazo zipo kwenye Kalenda ya FIFA zitakazochezwa Oktoba 12 na 16 na Ligi hii itarejea tena dimbani hapo Oktoba 20.


Hadi Ligi hii inasimama, Mabingwa wa Ulaya, Chelsea, ndio wapo kileleni wakiwa na Pointi 19 na hawajapoteza hata Mechi moja katika 7 huku wakiwa wametoka sare Mechi moja tu.


Timu iliyo nafasi ya pili ni Manchester United yenye Pointi 15 wakifuatia Mabingwa watetezi Manchester City ambao pia wana Pointi 15 lakini wamezidiwa kwa ubora wa magoli.
Mkiani wapo QPR ambao wana Pointi 2 tu.
+++++++++++++++++++++++++++++
MECHI ZINAZOFUATA ZA TIMU VIGOGO KWA MASHINDANO YOTE:
++NI LIGI KUU ENGLAND ISIPOKUWA INAPOTAJWA.
CHELSEA MAN CITY MAN UNITED ARSENAL
Oktoba 20
Spurs v Chelsea
Oktoba 23
Shakhtar v Chelsea [UCL]
Oktoba 28
Chelsea v Man Utd
Oktoba 31
Chelsea v Man Utd
[COC]
Novemba 3
Swansea v Chelsea
Novemba 11
Chelsea v L’pool


Oktoba 20
WBA v Man City
Oktoba 24
Ajax v Man City [UCL]
Oktoba 27
M City v Swansea
Novemba 3
West Ham v M City
Novemba 11
M City v Spurs
Oktoba 20
Man United v Stoke
Oktoba 23
Man U v Braga [UCL]
Oktoba 28
Chelsea v Man Utd
Oktoba 31
Chelsea v Man Utd
[COC]
Novemba 3
Man U v Arsenal
Novemba 10
Villa v Man United
Oktoba 20
Norwich v Arsenal
Oktoba 24
Arsenal v Schalke [UCL]
Oktoba 27
Arsenal v QPR
Oktoba 30
Reading v Arsenal
[COC]
Novemba 3
Man U v Arsenal
Novemba 10
Arsenal v Fulham
++UCL==UEFA CHAMPIONZ LIGI
++COC==CAPITAL ONE CUP
+++++++++++++++++++++++++++++
BPL:
MSIMAMO:
BPLSTAND08OCT12
BPL:
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumamosi, Oktoba 20, 2012
[Saa za Bongo]


[Saa 8 Dak 45 Mchana]
Tottenham Hotspur v Chelsea [White Hart Lane]
[Saa 11 Jioni]
Fulham v Aston Villa [Craven Cottage]
Liverpool v Reading [Anfield]
Manchester United v Stoke City [Old Trafford]
Swansea City v Wigan Athletic [Liberty Stadium]
West Bromwich Albion v Manchester City [The Hawthorns]
West Ham United v Southampton [Upton Park]


[Saa 1 Dak 30 Usiku]
16:30  Norwich City v Arsenal [Carrow Road]
Jumapili, Oktoba 21, 2012
[Saa 9 Dak 30 Mchana]
12:30  Sunderland v Newcastle United [Stadium of Light]
[Saa 12 Jioni]
15:00  Queens Park Rangers v Everton [Loftus Road]

WALIMBWENDE MISS TANZANIA WATEMBELEA MLIMA KILIMANJARO


Warembo wanaoshiriki shindano la Redds Miss Tanzania 2012, wakiwa katika picha ya pamoja Oktoba 7, 2012 wakati warembo hao walipo tembelea Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro na kupata maelezo na kuzungumza na watalii na wapanda mlima huo. Warembo 29 na viongozi wa  Kamati ya Miss Tanzania wapo Kanda ya Kaskazini kutembelea vivutio vya utalii na kuhamasisha utalii wa ndani. Mbali na kutembelea hifadhi hiyo lakini warembo hao walishiriki katika tamasha la michezo kwaajili ya kuchangia fedha na vitu mbalimbali kwa watoto Yatima mjini Arusha. Oktoba 8 warembo wanaendelea na ziara yao ikiwa ni pamoja na kutembelea kituo cha Redio cha RADIO 5 cha mjini Arusha.
 Washiriki wa Redds Miss tanzania 2012 wakiwa katiak picha tofauti tofauti wakati wakiwa katika eneo la Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro KINAPA.
  Warembo wakizungumza na mmoja wa Wasaidizi wa watalii wanao panda mlima Kilimanjaro.
 baadhi ya warembo wakipiga picha na baadhi ya viongozi wa Kamati ya Miss Tanzania
  Warembo wakizungumza na mmoja wa Wasaidizi wa watalii wanao panda mlima Kilimanjaro.
 Warembo wakiwa wakiwa katika eneo la maegesho ya magari KINAPA
 Wakielekea eneo la kupata taarifa mbalimbali za Mlima Kilimanajaro
 Wakipiga picha na baadhi ya watalii waliowakuta hapo.
 Warembo wa Redds Miss Tanzania wakimsikiliza Afisa Mhifadhi wa KINAPA, Eva Malya aliyekuwa akiwapa taarifa mbalimbali juu ya mlima huo.
 Warembo wakiwa na nyuso za furaha wakiendelea kupata maelezo juu ya mlima
Hapa sasa walibeba mabegi ili wapande Mlima.

SIMBA NA OLJORO MILIONI 50 HAZIFIKI

Emmanuel Okwi wa Simba akipiga mzito katika mechi ya jana na Olljoro


MECHI ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Simba na Oljoro JKT ya Arusha lililochezwa jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa wenyeji kuibuka na ushindi wa mabao 4-1, imeingiza Sh. 46,680,000.
 
 
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniphace Wambura Mgoyo amesema  leo kwamba, watazamaji 8,081 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 8,172,396.61 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 7,120,677.97.
 
 
Amesema mgawo mwingine wa mapato hayo ni posho ya msimamizi wa kituo sh. 120,000, kamishna wa mechi sh. 193,000, waamuzi sh. 210,000, mwamuzi wa akiba (reserve referee) sh. 70,000, usafi na ulinzi wa uwanja sh. 2,350,000 na Wachina (stadium technical support) sh. 2,000,000.
 
 
Amesema umeme sh. 300,000, maandalizi ya uwanja (pitch preparation) sh. 400,000, ulinzi wa mechi sh. 3,500,000 wakati tiketi ni sh. 3,175,000. Gharama za mchezo sh. 2,724,132.20, uwanja sh. 2,724,132.20, Kamati ya Ligi sh. 2,724,132.20, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,634,479.32 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,089,652.88.
 
 
Wakati huo huo: TFF imetoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama Soka Arusha (KRFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Oktoba 7 mwaka huu).
Wambura amesema ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa ARFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Kigoma.
 
 
Amesema TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya ARFA chini ya uenyekiti wa Khalifa Mgonja ambaye amechaguliwa tena kuongoza chama hicho.
“Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu mkoani Arusha kwa kuzingatia katiba ya ARFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake. 
 
 Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya ARFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za wanachama wa TFF,”alisema Wambura.
 
 
Aliwataja viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Khalifa Mgonja (Mwenyekiti), Seif Banka (Makamu Mwenyekiti), Adam Brown (Katibu), Peter Temu (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF), Omari Walii (Mwakilishi wa Klabu TFF) na Mwalizo Nassoro (Mhazini), wakati Wajumbe wa Kamati ya Utendaji waliochaguliwa katika uchaguzi huo uliofanyika Leganga, Usa River ni Hamisi Issa, Athuman Mhando na Eliwanga Mjema.
 

Alisema bafasi ya Katibu Msaidizi iko wazi na itajazwa katika uchaguzi mdogo utakayofanyika baadaye.

RICK 'ROZAY' ROSS ATISHA FIESTA DAR - YAVUNJA REKODI KWA UMATI WA WATU

 
 
 
 Mwanamuziki kutoka nchini Marekani Rick Ross akiimba jukwaani  usiku huu mbele ya maelfu ya wakazi wa jiji la Dar na vitongoji vyake kwenye viwanja vya Lidaz Club,wakati wa tamasha la Serengeti Fiesta likirindima.
 Mkali mwingine wa miduara AT na madansa wake wakilishambulia jukwaa.
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka THT,akiimba jukwaani na shabiki wake.
 Mashabiki wakitaka kuangusha uzio uliowekwa kwa ajili ya usalama.
 Baadhi ya Askari wakijaribu kuweka usalama wa kutosha kwa Mwanamuziki Rick Ross imara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Lidaz Club,kwa ajili ya kutumbuiza kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 201.
 Viwanja vya Lidaz palikuwa hapatoshi hata kidogo.
 Mwanamuziki kutoka nchini Marekani,Rick Ross akijisikia furahaa kuwaona Watanzania wakiwa wamejitokeza kwa wingi kwa ajili ya kumshuhudia yeye akikamua stejini.
Watu kibao wakiwa ndani ya viwanja vya lidaz club usiku huu.
Msanii wa miondoko ya rusha rohoo a.k.a Miduara,Shilole akijiachia jukwaani vilivyo na madansa wake usiku huu mbele ya umati mkubwa uliofika kwenye viwanja vya Lidaz Club,katika kuhitimisha kilele cha tamasha la Serengeti Fiesta 2012.
Sehemu ya umati watu waliojitokeza kila kona jiji la Dar na kwingineko kuwashuhudia wasanii mbalimbali wakitumbuiza kwenye jukwaa la tamasha la Serengeti Fiesta 2012,akiwemo Mwanamuziki wa kimataifa kutoka nchini Marekani,Rick Ross.
Wasanii wa kundi la Wanaume TMK,likiongozwa na Mh Themba sambamba na Chege Chigunda wakilishambulia jukwaa vilivyo usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012,linaloendelea hivi sasa katika viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar.uwanja wa Lidaz Club hapatoshi kabisa usiku huu.
Nyomi la Watu ile balaa usiku huu.
Wasanii wa kikundi cha Makomando kutoka THT wakionesha umahiri wao wa kucheza jukwaa.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Dyana pichani akionesha mbwembewe zake kabla ya kukamata kipaza sauti,mbele ya umati mkubwa uliojitokeza kwa wingi usiku huu ndani ya viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar
Msaniii mahiri wa kizazi kipya,Barnaba Boya kiimba jukwaani huku Dyana na skwadi lake wakionesha mbwembwe zao kama kawa.



Msanii wa muziki wa kizazi kipya Barnaba Boy akiimba jukwaani usiku huu 
Mmoja wa wshindi wa shindano la Serengeti Supa Nyota 2012,Youk Killer akishusha mistari yake nguvi usiku huu,huku shangwe na vigele vigele vikiwa vimetawala.
Mashabiki wakishangweka usiku huu vilivyo.
Mmoja wa washindi wa shindano la Serengeti Supa Nyota 2012,Jo Maker akifloo jukwaani. .

Baadhi ya mashabiki wakijiachia vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta 2012

Mmoja wa wshindi wa shindano la Serengeti Supa Nyota 2012,NeyLee akiimba jukwaani .

Baadhi ya wasanii kutoka nyumba ya vipaji THT wakiamsha amsha usiku huu wakati tamasha la Serengeti Fiesta 2012 likiendelea huku mashabiki na wapenzi wa tamasha hilo wakiendelea kumiminika usiku huu ndani ya viwanja vya Lidaz Club,jijini Dar.
Mmoja wa wasanii chipukizi kutoka kwa THT,akiimba kwa hisia mbele ya umati mkubwa wa watu (haupo pichani),uliojitokeza kushuhudia wasanii wa hapa nyumbani na nje wakitumbuiza katika jukwaa moja usiku huu.
Mmoja wa wasanii chipukizi akinogesha jukwaa la Serengeti Fiesta 2012 usiku huu
The Wacko Jako wa bongo akifanya vitu vyake jukwaani usiku huu
Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar na vitongoji vyake wakiwa tayari ndani ya viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar usiku huu wakati wa tamasha la Serengeti Fiesta likiendelea kurindima,huku wakimsubiri kwa hamu mwanamuziki wa Kimataifa kutoka nchini Marekani,Rick Ross ambaye anatarajia kukamua usikuu huu.
Wasanii wa kikundi cha Makomando kutoka THT wakionesha umahiri wao wa kucheza jukwaa.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Dyana pichani akionesha mbwembewe zake kabla ya kukamata kipaza sauti,mbele ya umati mkubwa uliojitokeza kwa wingi usiku huu ndani ya viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar
Msaniii mahiri wa kizazi kipya,Barnaba Boya kiimba jukwaani huku Dyana na skwadi lake wakionesha mbwembwe zao kama kawa.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Barnaba Boy akiimba jukwaani usiku huu 
Mmoja wa wshindi wa shindano la Serengeti Supa Nyota 2012,Youk Killer akishusha mistari yake nguvi usiku huu,huku shangwe na vigele vigele vikiwa vimetawala.
Mashabiki wakishangweka usiku huu vilivyo.
Mmoja wa washindi wa shindano la Serengeti Supa Nyota 2012,Jo Maker akifloo jukwaani. .

Baadhi ya mashabiki wakijiachia vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta 2012

Mmoja wa wshindi wa shindano la Serengeti Supa Nyota 2012,NeyLee akiimba jukwaani .

Baadhi ya wasanii kutoka nyumba ya vipaji THT wakiamsha amsha usiku huu wakati tamasha la Serengeti Fiesta 2012 likiendelea huku mashabiki na wapenzi wa tamasha hilo wakiendelea kumiminika usiku huu ndani ya viwanja vya Lidaz Club,jijini Dar.
Mmoja wa wasanii chipukizi kutoka kwa THT,akiimba kwa hisia mbele ya umati mkubwa wa watu (haupo pichani),uliojitokeza kushuhudia wasanii wa hapa nyumbani na nje wakitumbuiza katika jukwaa moja usiku huu.
Mmoja wa wasanii chipukizi akinogesha jukwaa la Serengeti Fiesta 2012 usiku huu
The Wacko Jako wa bongo akifanya vitu vyake jukwaani usiku huu
Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar na vitongoji vyake wakiwa tayari ndani ya viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar usiku huu wakati wa tamasha la Serengeti Fiesta likiendelea kurindima,huku wakimsubiri kwa hamu mwanamuziki wa Kimataifa kutoka nchini Marekani,Rick Ross ambaye anatarajia kukamua usikuu huu.