Tuesday, July 2, 2013

MAANDAMANO YACHELEWESHA KUTANGAZWA KWA BEI ZA TIKETI ZA KOMBE LA DUNIA.


SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limechelewa kutangaza bei za tiketi kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia 2014 kufuatia maandamano yasiyokoma yanayoendelea nchini Brazil. FIFA ilikuwa imepanga kutoa bei na maelezo kuhusiana na tiketi kwa ajili ya michuano hiyo Jumatatu lakini wameghairisha mpaka Julai 19 mwaka huu. Katibu Mkuu wa FIFA Jerome Valcke amedai kuwa wamefikia uamuzi huo ili kuepusha kuongeza vurugu zaidi za maandamano nchini humo ambapo maelfu ya watu wamekuwa wakiponda hatua ya serikali kutumia fedha nyingi kujenga viwanja na kuboresha miundo mbinu wakati kuna huduma nyingi za kijamii zilitakiwa kupewa kipaumbele. Pamoja na maandamano hayo rais wa FIFA Sepp Blatter alisifu michuano ya Kombe la Sgirikisho iliyomalizika Jumapili kwamba ilikuwa na mafanikio makubwa kimichezo na kuwashukuru wote waliofanikisha hilo.

EBHANA VIJANA W AKIBRAZIL WAANZA KUULA ULAYA NA HATIMAYE POULINHO ASAINISHWA NA AVB ,AMWAGA MACHOZI NA KILIO JUU AKITANGAZWA RASMI KUHAMIA SPURS


KLABU ya Tottenham imeshinda mbio za kuwania saini ya kiungo Mbrazil, Paulinho baada ya kuthibitisha atajiunga na timu hiyo kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 17.
Mchezaji huyo kwa kiasi kikubwa alitarajiwa kuondoka klabu ya Brazil kutua England baada ya Fainali ya Kombe la Mabara Jumapili kama ilivyowahi kuandika BIN ZUBEIRY.
Na katika Mkutano na Waandishi wa Habari, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alijikuta akilia wakati anaelezea uhamisho huo.
Emotional: Paulinho in tears at Corinthians press conference announcing he is to join Tottenham
Hisia: Paulinho akimwaga machozi katika Mkutano na Waandishi wa Habari, Corinthians kutangaza kuhamia kwake Tottenham
Paulinho
"Ni vigumu kusema chochote mapema namna hii, lakini uhakika hiyo ilikuwa miaka ya ajabu katika maisha yangu ya soka, na mataji mengi,"alisema.
"Kitu nachopenda kusema kwa mashabiki wa Corinthians, bodi na viongozi ni! Tutaona muda mfupi! - Nitarudi katika wakati usiojulikana, kutokana na yote waliyonifanyia.
"Mataji yangu binafsi yote ni shukrani kwa klabu, Corinthians itabakia moyoni mwangu katika wote wa maisha yangu,".
Mkurugenzi wa Soka wa Corinthians, Roberto de Andrade amemsifu mchezaji huyo aliyeng'ara katika kikosi ch Brazil kilichoifunga Hispania 3-0 mjini Rio Jumapili.
Signing off: Paulinho helped Brazil win the Conferderations CUp as they beat Spain 3-0 in the final
Amesaini: Paulinho ameisaidia Brazil kutwaa Kombe la Mabara kwa kuifunga Hispania 3-0 kwenye Fainali
Paulinho of Brazil celebrates
"Nataka kumshukuru Paulinhokwa kila kitu alichoifanyia Corinthians,"alisema.
"Hatutamsahau - jinsi alivyo mtu babu kubwa - na taji la timu yake ya taifa (Kombe la Mabara aliloshinda na Brazil) ilistahili.
"Corinthians inajivunia kuwa na mchezaji kama yeye. Ni halali kuhamishia masha yake katika klabu ya English, kujua utamadunia mpya.".

WENGER HATAKI MASIHALA AMSAINISHA YAYA ATUA ARSENAL, WENGER ASEMA AMEPATA KIFAA CHA UHAKIKA


IMEWEKWA JULAI 2, 2013 SAA 12:05 ALFAJIRI
KLABU ya Arsenal imethibitisha katika tovuti yake kwamba mwanasoka kinda wa kimataifa wa Ufaransa, Yaya Sanogo amesaini Mkataba wa muda mrefu kwao.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 20 amejiunga kwa ada ndogo tu baada ya kumaliza Mkataba wake klabu ya Daraja la Kwanza Ufaransa, Auxerre.
Sanogo kwa sasa yupo na timu ya taifa ya vijana ya Ufaransa chini ya umri wa miaka 20, katika Kombe la Dunia la U-20, akiwa amefunga mabao mawili kati ya matatu ya timu yake nchini Uturuki, na amefunga mabao tisa  katika mechi 13 katika msimu alioandamwa na majeruhi Ufaransa.
Target man: Sanogo has built an excellent reputation for himself in France
Mlengwa: Sanogo amefanya vitu adimu Ufaransa
More to come? Higuain (left) and Rooney (right) are also thought to be on Wenger's wishlist
Wengi waja? Higuain (kushoto) na Rooney (kulia) nao pia wanafikiriwa kuwa katika orodha ya wachezaji anaowataka Wenger

Gonzalo Higuain na Wayne Rooney ni washambuliaji wengine walioripotiwa kutakiwa The Gunners msimu huu, lakini Wenger anavutiwa mno na uwezo wa Sanogo.
"Sanogo ni usajili mzuri wa kinda kwetu,"aliiambia Arsenal.com. "Ameonyesha uwezo wake siku za karibuni akiwa na Auxerre na poa kikosi cha vijana chini ya miaka 20 cha Ufaransa.
"Tunasonga mbele kwa Yaya kujiunga nasi na kuendeleza kukuza kiwango chake,"alisema Wenger.
Zoezi hilo lipo kwenye kukamilisha taratibu za kawaida za usajili na Sanogo atajiunga na wenzake baada ya mashindano ya Uturuki.

BRANDTS AREJEA NA LEO ANAANZA KUISUKA YANGA MPYA MABIBO


KOCHA Mholanzi, Eernie Brandts amerejea nchini usiku wa jana na asubuhi hii anaelekea Uwanja wa sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam kuanza kukinoa kikosi chake kwa ajili ya msimu mpya.
Beki huyo wa kimataifa wa zamani wa Uholanzi, anatarajiwa kukutana na sura mpya mazoezini leo, akiwemo mshambuliaji aliyesajiliwa kutoka kwa mahasimu, Simba SC, Mrisho Ngassa na kipa Deo Munishi ‘Dida’ aliyesajiliwa kutoka Azam FC.
Kijana mpya; Mrisho Ngassa atakuwepo mazoezini Loyola leo

Ngassa aliyekuwa Mwanza kwa mapumziko, amerejea Jumapili na leo atakuwepo Loyola kuanza rasmi kazi katika klabu aliyojiunga nayo tena majira haya ya joto baada ya kuiacha kwa misimu mitatu akienda Azam FC misimu miwili na msimu wa mwisho Simba SC.
Brandts aliyeipa Yanga SC ubingwa wa Bara msimu ulioisha atainoa timu hiyo kwa siku tatu tu na baada ya hapo itakwenda katika ziara ya mechi za kirafiki Kanda ya Ziwa, katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Tabora.
Yanga itacheza na KCC ya Uganda Julai 6 Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza na Julai 7 itarudiana na timu hiyo ya Kampala mjini Shinyanga kabla ya kuelekea Tabora, ambako Julai 11, itamenyana na Rhino FC iliyopanda Ligi Kuu msimu huu.
Mazoezi ya leo yanatarajiwa kuhusisha wachezaji wote wa Yanga, wakiwemo wapya, ukiondoa waliotemwa akina Said Mohamed, Nurdin Bakari, Nsajigwa Shadrack na Godfrey Taita.

DROGBA KUMBE 'DHULUMATI', MAHAKAMA YAMKUTA NA HATIA NA KUMUAMURU ALIPE EURO 450,000


Didier Drogba
IMEWEKWA JULAI 2, 2013 SAA 5:19 ASUBUHI

MAHAKAMA Ufaransa imemuagiza mwanasoka wa kimataifa wa Ivory Coast, Didier Drogba kulipa Euro 450,000 kwa kampuni ya ujenzi ya mjini Corsica baada ya kutoilipa kwa kumfanyia kazi mjini mjini Abidjan.
Kampuni ya Acqua Viva ilimfikisha kortini mshambuliaji huyo wa zamani wa Chelsea Mei kwa kugoma kulipa salio la malipo baada ya kujengewa nyumba ya kifahari iliyokamilika mwaka 2009.
Kampuni hiyo imelalamika pia wafanyakazi wake kuzuiwa kufika eneo la nyumba hiyo waliyojenga, kitu ambacho Jaji amesema si haki na kwamba kilitokana na maelekezo ya Drogba na mkewe, raia wa Mali, Lala Diakite.
Wakati mchezaji huyo wa zamani wa Marseille mwenye umri wa miaka 35, aliyejiunga na Galatasaray ya Uturuki mapema mwaka huu, ameamua kukata rufaa, lazima alipe fedha hizo mapema ili kutekeleza amri ya Mahakama.

KIJANA MACHACHARI NEYMAR, ALBA KUFANYIWA UPASUAJI.


MSHAMBULIAJI mpya wa Barcelona, Neymar na beki Jordi Alba wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa kuondoa mafindofindo Ijumaa na wanatarajiwa kupona baada ya siku 10. Upasuaji huo ulipangwa kufanyika baada ya fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho iliyofanyika jijini Rio de Janeiro Jumapili iliyopita ambapo Brazil iliisambaratisha Hispania kwa mabao 3-0. Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo Neymar anatarajiwa kufanyiwa upasuaji huo huko Rio na baadhi ya madaktari wa Barcelona wanakuwepo kusaidia. Wakati Alba mwenye miaka 24 yeye atafanyiwa upasuaji wake siku hiyohiyo lakini katika kliniki iliyopo karibu na jiji la Barcelona na wote wanatarajiwa kupona ndani siku 10 baada ya upasuaji huo.