Monday, October 1, 2012

UEFA CHAMPIONZ LIGI: Mabingwa Chelsea, Man United ugenini Jumanne!

Jumatatu, 01 Oktoba 2012 20:50
 
RATIBA:
Jumanne Oktoba 2
[Mechi zote Saa 3 Dakika 45 Usiku isipokuwa inapotajwa]
Juventus v FC Shakhtar Donetsk
FC Nordsjælland v Chelsea FC
Valencia CF v LOSC Lille
FC BATE Borisov v FC Bayern München
SL Benfica v FC Barcelona
FC Spartak Moskva v Celtic FC [SAA 1 Usiku]
CFR 1907 Cluj v Manchester United FC
Galatasaray A.S. v SC Braga
TAARIFA:
MAN_UNITED-ANDO_RVP_SHINJI_EVRAJumanne Usiku ni MECHI DEI 2 ya Mashindano ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na Timu za England ambazo zitakuwa dimbani, Mabingwa Chelsea na Manchester United, zote zitacheza ugenini kwa Chelsea kuwa huko Denmark kuivaa Timu mpya FC Nordsjælland inayotoka Mji wa Farum wenye Wakazi 18,000 tu na Manchester United kucheza huko Bucharest, Romania na Timu yenye uzoefu CFR 1907 Cluj.
Wakati Manchester United walianza MECHI DEI 1 kwa ushindi katika Mechi yao ya Kundi H kwa kuitungua Galatasaray ya Uturuki kwa Bao 1-0, Mabingwa Chelsea wakiwa nyumbani Stamford Bridge waliutupa uongozi wa bao 2-0 na kwenda sare na Mabingwa wa Italy kwa bao 2-2.
Man United
Manchester United imesafiri kwenda Romania bila ya Wachezaji Michael Carrick, Ryan Giggs, Paul Scholes na Antonio Valencia.
Ingawa inajulikana Valencia alikuwa na maumivu lakini kuachwa kwa Giggs, Scholes na Carrick kumekuwa hamna maelezo ingawa Wachezaji wote hao walicheza Mechi ya Jumamosi waliyofungwa 3-2 na Tottenham.
Miongoni mwa Kikosi cha Wachezaji 21 waliokuwemo kwenye msafara ni Chipukizi kina Michael Keane, Scott Wootton, Jesse Lingard, Nick Powell na Ryan Tunnicliffe ambao wanaungana na Darren Fletcher ambae ni hivi karibuni tu amerejea Uwanjani baada ya kuwa nje kwa Miezi 10.
Kikosi kamili:
Man United: De Gea, Lindegaard; Büttner, Evans, Evra, Ferdinand, M.Keane, Rafael, Wootton; Anderson, Cleverley, Fletcher, Lingard, Nani, Powell, Tunnicliffe; Hernandez, Kagawa, Rooney, van Persie, Welbeck.CHELSEA_ULAYA_2012
Chelsea huko Denmark
Hii ni Mechi ya kwanza kwa Chelsea kucheza ugenini kwenye hatua ya Makundi baada ya kucheza Mechi ya kwanza nyumbani ya Kundi E Stamford Bridge na kuutupa uongozi wa bao 2-0 na kwenda sare na Mabingwa wa Italy kwa bao 2-2.
Safari hii watakuwa Uwanja wa Parken Mjini Denmark kucheza na Timu ngeni na ndogo, FC Nordsjælland ambayo inatoka Mji mdogo wa Farum wenye Wakazi 18,000 tu.
FC Nordsjælland walifungwa Mechi yao ya kwanza bao 2-0 ugenini na Shakhtar Donetsk lakini pia Chelsea wana rekodi dhaifu kwa Mechi za ugenini kwani Msimu uliopita waliotwaa Ubingwa wa Ulaya kwenye hatua ya Makundi walitoka sare na Valencia na Genk na kufungwa na Bayer Leverkusen.
RATIBA:
Jumatano Oktoba 3
[Mechi zote Saa 3 Dakika 45 Usiku isipokuwa inapotajwa]
FC Dynamo Kyiv v GNK Dinamo
FC Porto v Paris Saint-Germain FC
FC Schalke 04 v Montpellier Hérault SC
Arsenal FC v Olympiacos FC
RSC Anderlecht v Málaga CF
FC Zenit St. Petersburg v AC Milan [SAA 1 Usiku]
Manchester City FC v Borussia Dortmund
AFC Ajax v Real Madrid CF

ZUNGU JIPYA LAANZA KULISHA SUMU ZA KUUA MNYAMA JANGWANI


 Wachezaji wakijifua kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao dhidi ya Simba siku ya jumatano
 Wachezaji wakijifua kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao dhidi ya Simba siku ya jumatano
  Wachezaji wa Yanga wakimsikiliza kocha wao, Emstus Wilhelmus Johannes Brandts wakati wa mazoezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Loyola jijini Dar es Salaam
Wachezaji wa Yanga wakiwa katika mazoezi ya kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Simba chini ya kocha wao mpya raia wa Uholanzi, Emstus Wilhelmus Johannes Brandts kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Loyola jijini Dar es Salaam

 

 

REFA WA MWANZA KUCHEZESHA PAMBANO LA WATANI KESHOKUTWA

Felix Sunzu wa Simba akiwa chini ya ulinzi wa mabeki wa Yanga, Nadoir Haroub 'Cannavaro' aliye karibu na msaada wa Oscar Joshua nyuma yake


REFA Mathew Akrama kutoka Mwanza ndiye atakayechezesha mechi ya kwanza ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baina ya wapinzani wa jadi nchini, Yanga na Simba itakayochezwa keshokutwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura amesema kwamba katika mechi hiyo namba 80 ya Ligi Kuu itakayoanza saa 1:00 usiku na kurushwa moja kwa moja na Televisheni ya Super Sport ya Afrika Kusini, Akrama atasaidiwa na Samuel Mpenzu kutoka Arusha na Ephrony Ndissa wa Dar es Salaam wakati refa wa mezani atakuwa Oden Mbaga pia wa Dar es Salaam.
Amesema tiketi kwa ajili ya mechi ya kwanza ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baina ya wapinzani wa jadi nchini, Yanga na Simba itakayochezwa keshokutwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, zitaanza kuuzwa kesho kwenye vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Alivitaja vituo vitakavyotumika kuuza tiketi hizo kuanzia saa 4 asubuhi ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Uwanja wa Taifa, Kituo cha Mafuta OilCom Ubungo, Mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio/Samora, Dar Live Mbagala na Kituo cha Mafuta Buguruni.
Alikumbushia viingilio, cha chini kwenye mechi hiyo ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648 kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000. Watazamaji watakaoketi kwenye viti vya rangi ya bluu ambavyo ni 17,045 watalipa sh. 7,000 kwa tiketi moja.
Sh. 10,000 ni kwa viti vya rangi ya chungwa ambavyo viko 11,897 wakati VIP C inayochukua watazamaji 4,060 itakuwa sh. 15,000. Kwa upande wa VIP B tiketi ni sh. 20,000 na VIP A yenye watazamaji 748 tu kiingilio kitakuwa sh. 30,000.

KUELEKEA PAMBANO LA WATANI; KASEJA HAYUKO VIZURI SANA, BERKO NAYE...

TZ One, Juma Kaseja 


REJEA bao alilofungwa kwenye mechi na Ruvu Shooting. Achana nalo, kumbuka bao alilofungwa kwenye mechi na Prisons. Unaona nini?
Si Kaseja yule ambaye wengi tunamjua, hodari zaidi na mwenye hesabu kali katika mipira inayotokana na mashambulizi ya watu wanaokuja moja kwa moja wakitazamana naye.
Alikuwa mzito wa kuamua na hakujishughulisha kabisa kwenye mabao yote. Alikuwa tayari kufungwa. Baada ya kumuanzia mpira Nyosso kwenye eneo la hatari na beki huyo kuchelewa kuucheza hadi akapokonywa na Seif Rashid, Kaseja hakujisumbua kwenda kumsaidia beki wake, alirudi golini kusubiri kufungwa na akafungwa.
Nasema alirudi kusubiri kufungwa, kwa sababu zile zinaitwa nafasi ambazo zinaamua uhodari wa kipa na uzembe wa mtu aliyepata nafasi. Kama Seif Rashid angepiga nje, angelaumiwa na kama Kaseja angeokoa angesifiwa.
Rejea bao la Prisons, mfungaji alipiga shuti la kawaida sana na sidhani kama hata yeye mwenyewe alikuwa ana matumaini ya kufunga- maana kwenye soka kuna neno moja linaitwa kujaribu, nadhani alikuwa anajaribu. Akafanikiwa.
Kweli mpira ulimgonga Shomary Kapombe, lakini haukuwa wenye madhara bado- kama Kaseja angekuwa makini zaidi, bado tu angeucheza ule mpira. Mabao haya mawili pekee hayatoshi kusema Kaseja hayuko vizuri kwa sasa, rejea mabao aliyofungwa na Azam kuanzia Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame hadi Ngao, bado utaendelea kukataa kwamba Juma hayuko vizuri sana kwa sasa?
Na unaweza kuona presha ya kubadilisha mabeki Simba kwa sasa, inatokana na hali ya kipa wao Kaseja- amekuwa si yule Juma ‘Mahakama ya Rufaa’ ya kufungwa bao na amekuwa kipa wa kawaida.
Berko, Yanga One
Hata hivyo, bado kuelekea mpambano wa watani wa jadi Jumatano, Kaseja anabebwa na uzoefu wake, akiwa mchezaji aliyecheza mechi nyingi zaidi za Simba na Yanga na kwa muda mrefu kwa wachezaji wa sasa wa timu hizo, tangu mwaka 2003.
Kwa misimu miwili iliyopita, Yanga walikuwa wanamlalamikia Yaw Berko anawaringia kwa sababu hawakuwa na kipa mwingine wa kushindana naye. Msimu uliopita alisajiliwa Shaaban Kado akiwa vizuri sana, lakini naye mwisho wa siku akashindwa kuufikia ubora wa Berko.
Yanga waliendelea kuumiza kichwa juu ya kipa huyo na msimu huu wamemsajili Ally Mustafa ‘Barthez’ kutoka Simba. Ni kama kuna hali fulani ya kulazimisha Barthez adake hata kama hafikii ubora wa Berko, ili kupunguza kile wanachoamini maringo ya Mghana huyo.
Na kweli, Barthez anadaka, lakini hadi mechi ya jana dhidi ya African Lyon bado vigumu kumshawishi mtu kwamba kipa huyo anaweza akaanzishwa kwenye mechi ngumu kama ya Simba, Berko akiwa mzima.
Na kama umeweza kufuatilia, katika siku za karibuni, tangu baada ya Kombe la Kagame, Berko amekuwa hodari zaidi anapopewa nafasi langoni, akiamini upinzani wa kweli umekuja hivi sasa.
Kwa nini? Katika Kombe la Kagame, Berko hakumaliza Robo Fainali dhidi ya Mafunzo aliumia na kutoka, Barthez akaenda kumalizia hadi kwenye penalti Yanga ikashinda. Berko hakurudi tena langoni hadi Yanga inatwaa ubingwa- hilo hakika kama alikuwa ana maringo kweli, basi lilimtia adabu.
Ila, pamoja na yote. Panga, pangua vikosi vyote hawa ndio makipa wanaostahili kupewa dhamana Jumatano.

SIMBA SC YATOKA SARE NA MASTAA WA ZENJI

Simba SC


SIMBA SC imetoka sare ya bila kufungana na All Stars ya Zanzibar katika mchezo wa kirafiki jana usiku uliofanyika Uwanja wa Amaan, Zanzibar kujiandaa na mechi dhidi ya watani wao wa jadi, Yanga SC.
Simba SC inaendelea vizuri na maandalizi yake ya pambano dhidi ya watani wao wa jadi, Yanga SC, Oktoba 3, mwaka huu, ikifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Chuo cha Kiislam, Kwerekwe, visiwani Zanzibar na kambi yao ipo Chukwani.
Morali ya kambi ipo juu na wachezaji wote wako fiti, wakijifua kwa shauku kubwa ili kumvutia kocha Mserbia, Milovan Cirkovick awape nafasi ya kucheza Oktoba 3, kuanzia sa 1:00 usiku.
Simba ilirejea jana Zanzibar, baada ya juzi kuendeleza wimbi lake la ushindi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kwa kuichapa Prisons ya Mbeya iliyorejea Ligi Kuu msimu huu mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mabao ya Simba yalitiwa kimiani na Felix Mumba Sunzu na Mrisho Ngassa, ambaye hilo ni bao lake la kwanza katika Ligi Kuu ndani ya mechi nne na la pili jumla tangu ajiunge na timu hiyo katika mechi saba alizocheza, wakati la Prisons lilifungwa na Elias Maguri.
Kwa ushindi huo, Simba imefikisha pointi 12 na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu, ikiizidi Azam FC pointi mbili katika nafasi ya pili, ingawa timu zote zimecheza mechi sawa, nne.

SIMBA NA YANGA ZILIVYOFUNGANA TANGU 1965 HADI 5-0 ZA MEI 6 MWAKA HUU

Haruna Nitonzima wa Yanga kulia, akijaribu kumtoka Nassor Masoud 'Chollo' wa Simba kushoto

REKODI YA SIMBA NA YANGA:
JUNI 1, 1968
Yanga v Sunderland
5-0
WAFUNGAJI:
Maulid Dilunga dk. 18 (penalti), Dilunga dk. 43, Salehe Zimbwe dk. 54, Zimbwe dk. 89, Kitwana Manara dk. 86.
MACHI 3, 1969
Yanga v Sunderland
(Yanga ilipewa pointi za chee na ushindi wa mabao 2-0, baada ya Sunderland kugoma kuingia uwanjani).
JUNI 4, 1972
Yanga v Sunderland
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Kitwana Manara dk. 19,
Sunderland: Willy Mwaijibe dk. 11.
JUNI 18, 1972
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Leonard Chitete.
JUNI 23,  1973
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Haidari Abeid 'Muchacho' dk. 68.
AGOSTI 10, 1974
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Gibson Sembuli dk. 87, Sunday Manara dk. 97.
Simba: Adam Sabu dk. 16.
(Mechi ya kihistoria iliyochezwa Uwanja wa Nyamagana mjini Mwanza).
JULAI 19, 1977
Simba v Yanga
6-0
WAFUNGAJI:
Abdallah Kibadeni dk. 10, 42 na 89, Jumanne Hassan 'Masimenti' dk. 60 na 73, Selemani Sanga alijifunga dk. 20.
OKTOBA 7, 1979
Simba v Yanga
3-1
WAFUNGAJI:
Simba: Nico Njohole dk. 3, Mohammed Bakari 'Tall' dk. 38, Abbas Dilunga dk.72. Yanga: Rashidi Hanzuruni dk. 4.
OKTOBA 4, 1980
Simba v Yanga
3-0
WAFUNGAJI: Abdallah Mwinyimkuu dk. 29, Thuwein Ally dk. 82, Nico Njohole dk. 83.
SEPTEMBA 5, 1981
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Juma Hassan Mkambi dk. 42
APRILI 29, 1982
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Rashid Hanzuruni dk 2.
SEPTEMBA 18, 1982
Yanga 3-0 Simba
WAFUNGAJI:
Omar Hussein dk. 2 na 85, Makumbi Juma dk. 62.
FEBRUARI 10, 1983
Yanga v Simba.
0-0
APRILI 16, 1983
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Charles Mkwasa dk. 21, Makumbi Juma dk. 38, Omar Hussein dk. 84, Simba; Kihwelu Mussa dk. 14.
SEPTEMBA 10, 1983,
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Lila Shomari alijifunga dk. 72, Ahmed Amasha dk. 89.
SEPTEMBA 25, 1983
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk. 75,
Simba: Sunday Juma dk. 72.
MACHI 10, 1984
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 72.
Simba: Idd Pazi kwa penalti dk 20.
JULAI 14, 1984
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 39.
Simba: Zamoyoni Mogella dk. 17
MEI 19, 1985
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 6
Simba: Mohammed Bob Chopa dk. 30.
AGOSTI 10, 1985
Yanga v Simba
2-0
MACHI 15, 1986
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 44
Simba: John Hassan Douglas dk. 20.
AGOSTI 23, 1986
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila dk. 9, Malota Soma dk. 51
Yanga: Omar Hussein dk. 5.
JUNI 27, 1987
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Edgar 'Fongo' Mwafongo dk. 36.
AGOSTI 15, 1987
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Abeid Mziba dk. 14.
APRILI 30, 1988
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Justin Mtekere dk. 28
Simba: Edward Chumila dk. 25.
JULAI 23, 1988
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila 21, John Makelele dk. 58
Yanga: Issa Athumani dk. 36.
JANUARI 28, 1989
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Issa Athumani dk. 4, Abeid Mziba dk. 85
Simba: Malota Soma dk. 30.
MEI 21, 1989
Yanga v Simba
0-0
MEI 26, 1990
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Mavumbi Omari dk 6.
OKTOBA 20, 1990
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk 33, Thomas Kipese dk. 82, Sanifu Lazaro dk. 89
Simba: Edward Chumila dk. 58.
MEI 18, 1991
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Said Sued 'Scud' dk.  7.
AGOSTI 31, 1991
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Said Sued Scud.
OKTOBA 9, 1991
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Athumani China dk. 3, Abubakar Salum 'Sure Boy' dk. 54.
NOVEMBA 13, 1991
Yanga v Simba
2-0
APRILI 12, 1992
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Kenneth Mkapa dk. 10.
SEPTEMBA 26, 1992
Simba v Yanga
2-0
OKTOBA 27, 1992
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Damian Morisho Kimti.
 MACHI 27, 1993
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Said Mwamba Kizota dk. 47 na 57
Simba: Edward Chumila dk. 75.
JULAI 17, 1993
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Dua Said dk. 69.
SEPTEMBA 26, 1993
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Dua Said dk. 13.
NOVEMBA 6, 1993
Simba v Yanga
0-0
FEBRUARI 26, 1994
Yanga v Simba
2-0
MFUNGAJI: Mohammed Hussein 'Mmachinga' na James Tungaraza 'Boli Zozo'.
JULAI 2, 1994
Simba v Yanga
4-1
WAFUNGAJI:
Simba: George Masatu, Athumani China, Madaraka Selemani, Dua Saidi Yanga; Constantine Kimanda.
NOVEMBA 2, 1994
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Madaraka Selemani dk. 71
NOVEMBA 21, 1994
Simba v Yanga
2-0
WAFUNGAJI: George Lucas dk. 18, Madaraka Selemani dk. 42.
MACHI 18, 1995
Simba v Yanga
0-0
OKTOBA 4, 1995
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Mchunga Bakari dk. 79,
Yanga: Mohamed Hussein ÔMmachingaŐ dk. 40.
FEBRUARI 25, 1996
Yanga v Simba
2-0
SEPTEMBA 21, 1996
Yanga v Simba
0-0
OKTOBA 23, 1996
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Mohamed Hussein 'Mmachinga' dk. 46
NOVEMBA 9, 1996
Yanga v Simba
4-4
WAFUNGAJI:
Yanga: Edibilly Lunyamila (penalti) dk. 28, Mustafa Hozza alijifunga dk 64, Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Sanifu Lazaro dk. 75.
Simba: Thomas Kipese dk. 7, Ahmed Mwinyimkuu dk. 43, Dua Saidi dk. 60 na 90.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)
APRILI 26, 1997
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 16
Simba: Abdallah Msamba sekunde ya. 56
AGOSTI 31, 1997
Yanga v Simba
0-0
OKTOBA 11, 1997
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 52
Simba: George Masatu dk. 89
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya)
NOVEMBA 8, 1997
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Sekilojo Chambua dk. 85
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma)
FEBRUARI 21, 1998
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Akida Makunda dk. 46
Simba: Athumani Machepe dk. 88
JUNI 7, 1998
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 28
Simba: Abuu Juma (penalti) dk. 32
MEI 1, 1999
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idd Moshi dk. 59, Kalimangonga Ongala dk. 64, Salvatory Edward dk. 70, Simba: Juma Amir dk. 12.
AGOSTI 29, 1999
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Bakari Malima dk. 49, Mohamed Hussein 'Mmachinga' dk 71
JUNI 25, 2000
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Steven Mapunda dk. 59 na 72
Yanga: Idd Moshi dk. 4.
AGOSTI 5, 2000
Yanga v Simba
2-0
MFUNGAJI: Iddi Moshi 37 na 47. (Alifunga mabao hayo, akitoka kwenye fungate ya ndoa yake)
SEPTEMBA 1, 2001
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Joseph Kaniki dk. 76
SEPTEMBA 30, 2001
Simba v Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
Simba: Joseph Kaniki dk. 65,
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 86
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza)
AGOSTI 18, 2002
Simba v Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
Simba: Madaraka Selemani 65
Yanga: Sekilojo Chambua (penalti). dk. 89
NOVEMBA 10, 2002
Simba v Yanga
0-0
SEPTEMBA 28, 2003
Simba v Yanga
2-2
WAFUNGAJI:
Simba: Emmanuel Gabriel dk. 27 na 36
Yanga: Kudra Omary dk. 42, Heri Morris dk. 55
NOVEMBA 2, 2003
Simba v Yanga
0-0
AGOSTI 7, 2004
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Shaaban Kisiga dk. 64, Ulimboka Mwakingwe dk. 76
Yanga: Pitchou Kongo dk. 48
SEPTEMBA 18, 2004
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Athumani Machuppa dk. 82
APRILI 17, 2005
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Nurdin Msiga dk. 44, Athumani Machupa dk. 64,
Yanga: Aaron Nyanda dk. 39
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)
AGOSTI 21, 2005
Simba v Yanga
2-0
MFUNGAJI: Nico Nyagawa dk. 22 na 56
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)
MACHI 26, 2006
Simba v Yanga.
0-0
OKTOBA 29, 2006
Simba v Yanga
0-0
JULAI 8, 2007
Simba v Yanga
1-1 (dakika 120)
WAFUNGAJI:
Simba: Moses Odhiambo (penalti dk. 2)
Yanga: Said Maulid (dk. 55).
(Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya sare hiyo).
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)
OKTOBA 24, 2007:
Simba Vs Yanga
1-0
Mfungaji: Ulimboka Mwakingwe
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)
APRILI 27, 2008:
Simba Vs Yanga
0-0
OKT 26, 2008
Yanga Vs Simba
1-0
MFUNGAJI: Ben Mwalala dk15.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)
APRILI  19, 2009
Simba Vs Yanga
2-2
WAFUNGAJI:
SIMBA: Ramadhan Chombo dk 23, Haruna Moshi dk 62
YANGA: Ben Mwalala dk48, Jerry Tegete dk90
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)
(Matokeo haya yanahusu mechi za Ligi ya Bara na iliyokuwa Ligi ya Muungano pekee)
OKTOBA 31, 2009
Simba Vs Yanga
1-0
MFUNGAJI: Mussa Hassan Mgosi dk 26
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)
APRILI 18, 2010
Simba Vs Yanga
4-3
WAFUNGAJI:
SIMBA: Uhuru Suleiman dk 3, Mussa Mgosi dk 53 na 74, Hillary Echesa dk 90+
YANGA: Athumani Iddi dk 30, Jerry Tegete dk 69 na 89
OKTOBA 16, 2010:
Yanga Vs Simba
1-0
MFUNGAJI: Jerry Tegete dk 70
MACHI 5, 2011
Simba Vs Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
YANGA: Stefano Mwasyika (penalti) dk 59.
SIMBA:  Mussa Mgosi dk 73.
(Refa Orden Mbaga alizua tafrani uwanjani, kwanza kwa kulikataa bao la kusawazisha la Simba, kisha akalikubali baada ya kujadiliana na msaidia wake namba moja).
OKTOBA 29, 2011
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Davies Mwape dakika ya 75
MEI 6, 2012
Simba 5-0 Yanga SC
WAFUNGAJI:
Emmanuel Okwi (dk 2 na 62), Felix Sunzu (penalti 56), Juma Kaseja (penalti dk 67) na Patrick Mafisango (penalti dk 72)
Okwi 'sterling' wa mechi iliyopita ya watani, ambayo Yanga ilikula 5-0
MECHI ZA WATANI WA JADI NJE YA LIGI KUU
KLABU BINGWA AFRIKA MASHARIKI NA KATI:
JULAI 10, 2011
Yanga 1-0 Simbam, Fainali
MFUNGAJI : Kenneth Asamoah dk 108
JANUARI 1975
Yanga Vs Simba; Fainali, 2-0
WAFUNGAJI: Gibson Sembuli na Sunday Manara
JANUARI 1992
Simba Vs Yanga; Fainali
1-1, Simba ilishinda kwa penalti 5-4
JULAI 27, 2008
Simba Vs Yanga; Mshindi wa Tatu
(Yanga haikutokea uwanjani, Simba ikapewa ushindi wa chee)
KOMBE LA HEDEX:
JUNI 30, 1996
Yanga Vs Simba 2-0
CCM Kirumba, Mwanza
WAFUNGAJI: Bakari Malima na Edibily Lunyamila
KOMBE LA HEDEX:
JULAI 13, 1996
Simba Vs Yanga 1-1, Taifa, Dsm
WAFUNGAJI:
SIMBA: Hussein Amaan Marsha kwa penalti
YANGA: Bakari Juma Malima
KOMBE LA TUSKER:
FEBRUARI 10, 2001
Yanga Vs Simba (fainali) 0-0
(Simba ilishinda kwa penalti 5-4, Uwanja wa Taifa)
MACHI 31, 2002.
Simba Vs Yanga 4-1
WAFUNGAJI:
SIMBA: Mark Sirengo dk. 3 na 76, Madaraka Selemani dk. 32 na Emanuel Gabriel dk. 83.
YANGA: Sekilojo Chambua dk 16.
(Mechi hii ya fainali iliyohudhuriwa na rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, chupuchupu ivunjike dakika ya 32, baada ya Madaraka kufunga bao ambalo kabla ya kufumua shuti lililomshinda kipa Manyika Peter, aliushika mpira kwa makusudi, ili kuuweka sawa. Rais wa Yanga wakati huo, Tarimba Abbas aliinuka na kuwaonyesha ishara wachezaji wake watoke uwanjani na hapo ndipo meza kuu aliyokuwa ameketi mzee Mwinyi, ilipoanza kushambuliwa kwa chupa za maji na mashabiki wa Yanga. Mwamuzi wa mchezo huo, Abdulkadir Omar alisubiri hadi vurugu zilipotulizwa na FFU ndipo akaendeleza mchezo. Tarimba alitoka nje na hakutaka kuendelea kushuhudia mchezo huo. Baada ya hapo, alifungiwa na Chama cha Soka Tanzania, FAT).
JULAI 2, 2005
CCM Kirumba, Mwanza. Fainali
Simba Vs Yanga, 2-0
WAFUNGAJI: Emmanuel Gabriel dk. 60, Mussa Hassan Mgosi dk. 72
AGOSTI 15, 2006
Simba Vs Yanga; Nusu Fainali, 1-1
WAFUNGAJI:
SIMBA: Emanuel Gabriel dk. 69
YANGA: Credo Mwaipopo 90
(Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 7-6)
DESEMBA 25, 2009
Yanga Vs Simba; Nusu Fainali, 2-1
WAFUNGAJI:
YANGA: Jerry Tegete dk 67, Shamte Ally dk 120
SIMBA: Hillary Echesa dk 78 (penalti)
(Uwanja wa mpya wa Taifa)
KOMBE LA MAPINDUZI:
JANUARI 12, 2011
Simba Vs Yanga; Fainali 2-0
WAFUNGAJI: Mussa Mgosi dk 33, Shijja Mkinna dk 71
(Uwanja wa Amaan, Zanzibar)
KOMBE LA AICC:
JUNI 1989
Yanga Vs Simba SC 1-0
MFUNGAJI: Joseph Machella
APRILI 20, 2003,
CCM Kirumba, Mwanza
Yanga Vs Simba 3-0
WAFUNGAJI:
Kudra Omary dk. 30, Heri Morris dk 32 na Salum Athumani dk. 47
JANUARI 19, 2003, Kombe la CCM
Simba Vs Yanga 1-1, Dsm
WAFUNGAJI:
SIMBA: Jumanne Tondolo dk. 10
YANGA: Mwinyi Rajabu dk. 20
NGAO YA JAMII:
FEBRUARI 17, 2001
Yangs Vs Simba 2-1, Dsm
WAFUNGAJI:
YANGA: Edibilly Lunyamila dk. 47, AllyYussuf 'Tigana' dk 80.
SIMBA: Steven Mapunda 'Garrincha' dk.43
AGOSTI 18, 2010
Yanga vs Simba 0-0
(Yanga ilishinda kwa penalti 3-1)
WAFUNGAJI: Geoffrey Bonny, Stefano Mwasyika na Isaac Boakye kwa upande wa Yanga na Mohamed Banka kwa Simba.
WALIOKOSA: Ernest Boakye kwa Yanga na Emanuel Okwi, Uhuru Suleiman na Juma Nyosso kwa Simba.
AGOSTI 17, 2011
Simba vs Yanga 2-0, Dar
WAFUNGAJI:
Haruna Moshi ‘Boban’ dk 15 na Felix Sunzu dk 38.
NOVEMBA 15, 2000
KOMBE LA FAT
Yanga Vs Simba 2-1
Sheikh Amri Abeid, Arusha.
WAFUNGAJI:
YANGA: Aziz Hunter 40 na Vincent Tendwa
SIMBA: Ally Yussuf 'Tigana' dk.37
NOVEMBA 12,  2000
MARUDIANO KOMBE LA FAT
Simba Vs Yanga 1-0, Dsm
MFUNGAJI:
SIMBA: Ben Luoga  dk.44      
(Matokeo ya jumla yakawa 2-2 na Yanga ikatolewa kwa mikwaju ya penalti 5-4).
Hamisi Friday Kiiza akijaribu kumtoka Nassor Masoud Chollo