Monday, January 14, 2013

SELEMBE AISUBILIA KWA HAMU JKT MGAMBO



Selembe aisubiri kwa hamu JKT Mgambo
Kiungo mshambulia wa pembeni wa timu ya Taifa ya Zanzibar na klabu ya soka ya Coastal Union ya Tanga, Suleiman Kassim amesema kuwa, klabu yake itaifunga kwa mara nyingine timu ya JKT Mgambo inayotokea, wilaya ya Muheza, mkoani humo katika mchezo wa mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom, Tanzania Bara.
” Tuliwafunga, Mgambo kwa bao 1-0 katika mchezo wa kwanza, hatutaishia hapo bali tutawafunga tena katika mchezo wa tarehe 27″ anasema, kiungo huyo wa zamani wa Azam FC, na African Lyon, wakati akiteta na tovuti ya kandanda..
Selembe, ambaye ana uwezo mzuri katika kukimbia na mipira, kutoa pasi za mwisho na kufunga wakati mwingine. Lakini vitu hivyo hufanya sasa akiwa na timu ya Taifa. ” Unajua mimi mara nyingi huwa natengeneza nafasi za kufunga magoli kwa wenzangu, hiyo imekuwa ni kama tabia yangu, lakini ikitokea nafasi ya kufunga basi mara moja nafanya hivyo” anaongeza kiungo huyo ambaye amekuwa akiingia na kutoka katika timu ya Taifa ya Tanzania ( Taifa Stars)

YANGA KUONJESHA LADHA ZA UTURUKI JUMAPILI DHIDI YA TIMU LA BONDENI


Kikosi cha Yanga SC
MABINGWA wa soka Afrika Mashariki na Kati, Yanga SC ya Dar es Salaam Jumapili hii watashuka kwenye Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam kumenyana na Black Leopard ya Polokwane, Limpopo nchini Afrika Kusini.
Katibu wa Yanga, Lawrence Mwalusako amesema leo kwamba kikosi cha Yanga kilichokuwa Uturuki baada ya kurejea leo Alfajiri wachezaji watapumzika kwa siku mbili kabla ya Jumatano kuanza mazoezi.
Mwalusako alisema kuhusu lini timu hiyo itawasili, bado hawajajulishwa na Waratibu wa mechi hiyo, kampuni ya Prime Time Promotions.
Yanga ilikuwa Uturuki kwa wiki mbili kwa kambi ya mazoezi na imerejea leo Alfajiri nchini. Katika ziara yake hiyo, ilicheza mechi tatu za kujipima nguvu na kufungwa mbili na kutoka sare moja.
Katika mchezo wake wa kwanza, ilitoka sare ya 1-1 Ariminia Bielefeld ya Daraja la Tatu (sawa na la nne) Ujerumani kabla ya kufungwa 2-1 na Denizlispor FC ya Daraja la Kwanza Uturuki na baadaye 2-0 na Emmen FC ya Ligi Daraja la Kwanza Uholanzi.
Yanga iliweka kambi katika hoteli ya Fame Residence Lara & Spa kilomita chahce kutoka katika Uwanja wa Ndege wa Jiji la Antalya, iliyopo ufukweni mwa bahari ya Mediteranian.
Kikosi cha wachezaji 27 kilikuwa kambini nchini Uturuki, ambacho ni makipa; Ally Mustafa 'Barthez', Said Mohamed na Yussuf Abdul, mabeki Juma Abdul, Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Stefano Mwasyika, Oscar Joshua, Mbuyu Twite, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Ladisalus Mbogo na Kelvin Yondani.
Viungo ni Athumani Iddi ‘Chuji’, Frank Domayo, Haruna Niyonzima, Kabange Twite, Nurdin Bakari, Omega Seme, Simon Msuva, Rehani Kibingu, Nizar Khalfani na David Luhende wakati washambuliaji ni Didier Kavumbagu, Said Bahanunzi, Jerry Tegete, George Banda na Hamisi Kiiza na Kocha Mkuu Mholanzi, Ernie Brandts, Kocha Msaidizi, Freddy Felix Minziro na Kocha wa makipa na Razak Ssiwa.
Hiyo inakuwa mara ya tatu kihistoria Yanga kufanya ziara nje ya Afrika baada ya Brazil mwaka 1975 na Romania mwaka 1978. Yanga pia imewahi kuweka kambi Afrika Kusini mwaka 2008.
Leopards ilirejea Ligi Kuu ya Afrika Kusini mwaka juzi tangu ishuke 2008 na msimu uliopita iliponea chupuchupu kushuka tena, baada ya kushika nafasi ya 14 katika Ligi ya timu 16, na kwa msimu huu hadi sasa ipo nafasi ya 12.

MSIMAMO WA LIGI KUU AFRIKA KUSINI:

PosTeamPWDLGFGAGDPts
1Kaizer Chiefs16105131112035
2Orlando Pirates1610422391434
3Platinum Stars1610152618831
4Free State Stars166731413125
5Maritzburg Utd166641814424
6University of Pretoria165831814423
7Bloem Celtic166371618-221
8SuperSport United1631121915420
9Bidvest Wits164751417-319
10Mamelodi Sundowns164661215-318
11Moroka Swallows165292327-417
12Black Leopards163851924-517
13Golden Arrows164481520-516
14Ajax Cape Town164391526-1115
15Chippa United162771320-713
16AmaZulu16268823-1512
Print

MAN U, ARSENAL, SPURS NA LIVERPOOL ZAWASUKIA BONGE LA ZENGWE MAN CITY NA CHELSEA



Martin Samuel on the attempted coup...

Fair play? To the gang of four that means a ban on dreamers like Jack Walker - click HERE for our Chief Sports Writer's column
A breakaway group of elite clubs are attempting to curb the spending power of Manchester City and Chelsea.
A letter, signed by Manchester United, Liverpool, Tottenham Hotspur and Arsenal and published on Arsenal-headed notepaper, was circulated at a Premier League meeting before Christmas.
Addressed to Richard Scudamore, the Premier League chief executive, it called for UEFA’s financial fair play controls to be implemented strictly — a step on from the regulations currently under consideration.
Moneybags: Man City have splashed the cash in their bid for Premier League domination
Moneybags: Man City have splashed the cash in their bid for Premier League domination
Rolling in it: Chelsea have spent hundreds of millions under Roman Abramovich
Rolling in it: Chelsea have spent hundreds of millions under Roman Abramovich
In a clear attack on high-spending owners such as Roman Abramovich at Chelsea and Manchester City’s Sheik Mansour, the letter reads: 'Thank you for your continued work on the vital subject of Financial Regulation for the Premier League.
'However, we do not feel that the latest proposals go far enough to curb the inflationary spending which is putting so much pressure on clubs across the entire League.
'We continue to believe that to be successful and have the best chance of gaining at least the 14 votes necessary, any proposals for Financial Regulation must include meaningful measures to restrict the owner funding of operating losses.
FFP plans: The letter with the Arsenal header which says the proposed regulations do not go far enough
FFP plans: The letter with the Arsenal header which says the proposed regulations do not go far enough
Part two of the letter
'The owners, controlling shareholders and chief executives of Arsenal Football Club, Liverpool Football Club, Manchester United Football Club, and Tottenham Hotspur Football Club, continue to believe that the best way of achieving this will be a strict adoption of the UEFA Financial Fair Play rules.
'We already have seven clubs each season who are competing in Europe under these rules and, by proposing below some amendments to phase in FFP measures and make concessions to future new owners and promoted clubs, we believe there is a strong chance of achieving the necessary consensus.
'In summary, we would together make the following proposal:
  • Clubs will agree to break even over a rolling three-year period;
  • Break even result to be calculated strictly in accordance with UEFA FFP rules.'
The letter was followed up by a 10-minute speech from Manchester United chief executive David Gill, who advocated handing over control of the new regulations directly to UEFA — a move that would as good as make UEFA president Michel Platini the head of English club football.

TENGA AACHIA NGAZI YA URAIS TFF ASEMA AMALIZA AJENDA ZAKE NA KUWAACHIA SOKA LENYE KICHWA


Tenga akizungumza leo TFF

RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amesema kwamba amekamilisha ajenda yake ya kulijenga shirikisho hilo kuwa taasisi, kwa kuweka mifumo bora ya uendeshaji ikiwemo kutengeneza katiba mpya na kanuni, hivyo hatagombea tena wadhifa huo katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Februari 24 mwaka huu.
Akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye ofisi za TFF leo, Rais Tenga amesema wakati anaingia kwenye uongozi mwaka 2004 ajenda ilikuwa na kuijenga TFF kama taasisi kwa kuweka mifumo ya uendeshaji ikiwemo kutengeneza katiba na kanuni, jambo ambalo limefanyika.
“Wajumbe wamekuwa wakiniuliza Rais vipi? Mimi hapana. Nilishafika pale pa kufika. Tulipoanza wakati ule ilikuwa ni kujenga taasisi. Na kazi hiyo tumeifanya. Tulipoingia mwaka 2004 hiyo ndiyo ilikuwa ajenda,” amesema Rais Tenga.
Amesema walitengeneza Katiba, vyombo huru vya kufanya uamuzi, kuongeza wigo wa wapiga kura ambapo hivi sasa kwenye mpira wa miguu hakuwezi kutokea migogoro, hata ikitokea kuna mfumo wa kuidhibiti.
Rais Tenga ameishukuru Sekretarieti ya TFF, Kamati ya Uchaguzi ya TFF, kamati za uchaguzi za wanachama wa TFF na vyama wanachama wa TFF kwa hatua iliyofikiwa katika uchaguzi ambapo mikoa yote imekamilisha uchaguzi na kubaki vyama shiriki pekee.
Ametoa mwito kwa wadau kujitokeza kugombea uongozi TFF, kwani baada ya kujenga taasisi ajenda iliyobaki ni mpira wa miguu wenyewe ikiwemo nini kifanyika ili mpira uchezwe katika maeneo mbalimbali.
“Tumeshatengeza mfumo, sasa ni kuangalia jinsi ya kuendeleza mpira. Changamoto ni tufanye nini ili mpira uendelee. Tunataka watu wengine wabebe hiyo ajenda ili tuangalie tunakwendaje mbele,” amesema.
Pia amesema ushirikiano ambao amepata kwa wapenzi na wadau wa mpira wa miguu ni wa ajabu. Vilevile ameishukuru vyombo vya habari, Serikali, klabu, wadhamini na wafadhili kwa mchango wao katika uendeshaji wa mpira wa miguu nchini.
Wakati huo huo, wadau 19 wamechukua fomu kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) unaotarajiwa kufanyika Februari 24 mwaka huu.
Fomu hizo zimeanza kutolewa leo (Januari 14 mwaka huu) ambapo wawili wamechukua nafasi ya Makamu wa Rais wakati waliobaki wanaomba ujumbe wa Kamati ya Utendaji wakiwakilisha kanda mbalimbali.
Waliochukua fomu za umakamu wa rais ni Wallace Karia na Ramadhan Nassib. Wote ni wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF inayomaliza muda wake.
Waliochukua fomu za Ujumbe ni Shaffih Dauda, Athuman Kambi, Hussein Mwamba, Stewart Masima, Yusuph Kitumbo, Mugisha Galibona, Vedastus Lufano, Twahili Njoki, Charles Mugondo, Elley Mbise, Farid Nahdi, Ayubu Nyaulingo, Nazarius Kilungeja, Epaphra Swai, Khalid Abdallah, James Mhagama na Selemani Bandiho. 
Katika hatua nyingine, TFF imeupongeza uongozi mpya wa Chama cha Soka Katavi (KAREFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Januari 13 mwaka huu).
Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa KAREFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Katavi.
TFF imeahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya KAREFA chini ya ukatibu wa Peter Hella aliyeibuka mshindi katika uchaguzi huo uliofanyika ukumbi wa DC mjini Mpanda kwa kumshinda Emmanuel Chaula kwa kura sita dhidi ya mbili.
TFF imesema uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu mkoani Katavi kwa kuzingatia katiba ya KAREFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.
TFF pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya KAREFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
Viongozi waliochaguliwa ni Hella (Katibu), Elias Mande (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF) na Deo Bakuba (Mwakilishi wa Klabu TFF). Nafasi ya Mwenyekiti haikuwa na mgombea wakati Mawazo Maso aliyekuwa mgombea pekee wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti alipata kura nyingi za hapana. Nafasi zilizo wazi zitajazwa katika uchaguzi mdogo.

PONGEZI UONGOZI MPYA KATAVI


 
 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Katavi (KAREFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Januari 13 mwaka huu).
Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa KAREFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Katavi.
TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya KAREFA chini ya ukatibu wa Peter Hella aliyeibuka mshindi katika uchaguzi huo uliofanyika ukumbi wa DC mjini Mpanda kwa kumshinda Emmanuel Chaula kwa kura sita dhidi ya mbili.
Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu mkoani Katavi kwa kuzingatia katiba ya KAREFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.
Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya KAREFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
Viongozi waliochaguliwa ni Hella (Katibu), Elias Mande (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF) na Deo Bakuba (Mwakilishi wa Klabu TFF). Nafasi ya Mwenyekiti haikuwa na mgombea wakati Mawazo Maso aliyekuwa mgombea pekee wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti alipata kura nyingi za hapana. Nafasi zilizo wazi zitajazwa katika uchaguzi mdogo.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

19 WACHUKUA FOMU ZA UONGOZI TFF UCHAGUZI MKUU,,,MWENYEKITI W ATAREFA YUSUPH KITUMBO ACHUKUA FOMU NAYE YA UJUMBE


 
Wadau 19 wamechukua fomu kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) unaotarajiwa kufanyika Februari 24 mwaka huu.
Fomu hizo zimeanza kutolewa leo (Januari 14 mwaka huu) ambapo wawili wamechukua nafasi ya Makamu wa Rais wakati waliobaki wanaomba ujumbe wa Kamati ya Utendaji wakiwakilisha kanda mbalimbali.
Waliochukua fomu za umakamu wa rais ni Wallace Karia na Ramadhan Nassib. Wote ni wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF inayomaliza muda wake.
Waliochukua fomu za ujumbe ni Shaffih Dauda, Athuman Kambi, Hussein Mwamba, Stewart Masima, Yusuph Kitumbo, Mugisha Galibona, Vedastus Lufano, Twahili Njoki, Charles Mugondo, Elley Mbise, Farid Nahdi, Ayubu Nyaulingo, Nazarius Kilungeja, Epaphra Swai, Khalid Abdallah, James Mhagama na Selemani Bandiho.  

ULAYA: BARCA YAZIDI KUPAA YAMALIZA MZUNGUKO WA KWANZA BILA KUFUNGWA , JUVE YANASA, YAKARIBIWA NA LAZIO & NAPOLI ,BPL MAN U NA MAN CITY BALAAA WASHINDA DARBY KUBWA JANA!

BARCA_v_REALSERIE A
MATOKEO:
Jumapili Januari 13
Torino FC 3 Siena 2
SS Lazio 2 Atalanta 0
Parma 1 Juventus 1
Udinese 3 Fiorentina 1
Napoli 3 Palermo 0
Cagliari 2 Genoa 1
Catania 1 AS Roma 0
Sampdoria 0 AC Milan 0

Wakati Mabingwa watetezi na Vinara wa Serie A, Juventus, wakitoka sare, Lazio na Napoli zilishinda Mechi zao na kuisogelea Juventus.

MSIMAMO-Timu za JUU:
[Kila Timu imecheza Mechi 20]
1 Juventus Pointi 45
2 Lazio 42
3 Napoli 40
4 Inter Milan 38
5 Fiorentina 35
6 AS Roma 32
7 AC Milan 31

Juventus, wakicheza ugenini, walifunga Bao kwanza kwa frikiki ya Andrea Pirlo lakini Nicola Sansone akaisawazishia Parma na Mechi kumalizika 1-1.
Lazio waliifunga Atalanta Bao 2-0 na kujichimbia nafasi ya pili wakiwa Pointi 3 nyuma ya Juventus.
Bao za Lazio zilifungwa na Sergio Floccari na Davide Brivio, aliejifunga mwenyewe, na vile vile Atalanta kumaliza Mechi hiyo wakiwa Mtu 10 baada ya Beki Carlos Carmona kupewa Kadi za Njano mbili na kutolewa kwa Kadi Nyekundu.
Napoli waliichapa Palermo 3-0 kwa Bao za Christian Maggio, Gokhan Inler na Lorenzo Insigne.
LA LIGA
RATIBA/MATOKEO:
Jumapili Januari 13
Real Betis 2 Levante 0
Real Sociedad 1 Deportivo La Coruna 1
Atletico de Madrid 2 Real Zaragoza 0
Malaga CF 1 FC Barcelona 3
Jumatatu Januari 14
Getafe CF v Granada CF

Lionel Messi aliifungia Barcelona Bao la Kwanza katika Dakika ya 27 na kumtengenezea Cesc Fabregas, aliefunga Bao la Pili na Thiago kufunga la tatu, na kuwapa Barcelona ushindi wa Bao 3-1 dhidi ya Malaga ambao walifunga Bao lao pekee Dakika ya mwisho ya mchezo kupitia Diego Buonanotte.
Ushindi huo umewafanya Barca wawe Pointi 11 mbele ya Timu ya Pili Atletico Madrid ambao nao waliifunga Real Zaragoza 2-0 na kujivuta kuwa Pointi 7 mbele ya Timu ya 3 Real Madrid ambao Jumamosi walitoka 0-0 na Osasuna.
Bao za Atletico Madrid zilifungwa na Tiago na Radamel Falcao kwa Penati.
 
ARSENAL 0 MAN CITY 2
MANCINI_n_WENGERKwa mara ya kwanza katika Miaka 37, Manchester City wamefanikiwa kuifunga Arsenal nyumbani kwao na kuwakaribia Vinara wa Ligi Manchester United na kuwa Pointi 7 nyuma yao baada ya kushinda 2-0 katika Mechi ambayo Arsenal walibakia Mtu 10 kuanzia Dakika ya 10.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
MSIMAMO-Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 22 isipokuwa inapotajwa]
1 Man United Mechi 22 [Tofauti ya Magoli 27] Pointi 55
2 Man City  [Tofauti ya Magoli 24] Pointi  48
3 Chelsea  Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 24] Pointi 41
4 Tottenham [Tofauti ya Magoli 22] Pointi 40
5 Everton [Tofauti ya Magoli 22] Pointi 37
6 Arsenal Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 16] Pointi 34
7 West Brom [Tofauti ya Magoli 1] Pointi 33
8 Liverpool [Tofauti ya Magoli 7] Pointi 31
9 Swansea [Tofauti ya Magoli 5] Pointi 30
10 Stoke [Tofauti ya Magoli -3] Pointi 29

Sentahafu wa Arsenal Laurent Koscielny alitolewa nje katika Dakika ya 10 kwa kumshika Edin Dzeko ambae alipiga Penati ya kosa hilo lakini Kipa Szczesny aliokoa baada ya mpira kupiga posti.
Kosa kosa hiyo ilizidisha munkari wa Man City ambao walizidisha presha na James Milner kuwafungia Bao la kwanza Dakika ya 21 na Dzeko kuongeza la pili Dakika ya 32.
Kipindi cha Pili Nahodha wa Man City Vincent Kompany alipewa Kadi Nyekundu na Refa Mike Dean kwa kumrukia miguu miwili Jack Wilshere.
VIKOSI:
Arsenal: Szczesny, Sagna, Koscielny, Vermaelen, Gibbs, Diaby, Wilshere, Cazorla, Oxlade-Chamberlain, Podolski, Walcott
Akiba: Mannone, Mertesacker, Andre Santos, Giroud, Ramsey, Coquelin, Jenkinson.
Man City: Hart, Zabaleta, Kompany, Nastasic, Clichy, Javi Garcia, Barry, Milner, Silva, Tevez, Dzeko
Akiba: Pantilimon, Lescott, Sinclair, Kolarov, Suarez, Rekik, Balotelli.
Refa: Mike Dean

BPL, BARCLAYS PREMIER LEAGUE
RATIBA:
Jumatano Januari 16
[SAA 4 DAK 45 Usiku]
Chelsea v Southampton
Jumamosi Januari 19
[SAA 12 Jioni]
Liverpool v Norwich
Man City v Fulham
Newcastle v Reading
Swansea v Stoke
West Ham v QPR
Wigan v Sunderland
[SAA 2 na Nusu Usiku]
West Brom v Aston Villa
Jumapili Januari 20
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Chelsea v Arsenal
[SAA 1 Usiku]
Tottenham v Man United
  MANCHESTER UNITED 2 LIVERPOOL 1
>>UNITED WAKO POINTI 10 MBELE, KILELENI!
BPL_LOGOManchester United leo wamezidi kupaa kileleni baada ya kuwachapa Mahasimu wao wakubwa Liverpool Bao 2-1 Uwanjani Old Trafford na kukwea juu kileleni mwa BPL, Barclays Premier League, wakiwa Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Man City ambao muda mfupi baadae leo wana kibarua kigumu Uwanjani Emirates watakapoivaa Arsenal.RVP-BAO_NA_LIVERPOOL

MAGOLI:
Man United 2
-Van Persie Dakika ya 19
-Vidic 54
Liverpool 1
-Sturridge Dakika ya 57

Man United, ambao walitawala kabisa Kipindi cha Kwanza, walifunga Bao lao la kwanza kupitia Robin van Persie kufuatia pasi murua kati ya Danny Welbeck, Tom Cleverley, Shinji Kagawa na Patrice Evra kumtilia pasi ya chini Van Persie aliepachika wavuni kiakili.
Frikiki ya Robin van Persie iliunganishwa kwa kichwa na Patrice Evra na kumparaza Nemanja Vidic na kutinga wavuni na kuwapa Man United Bao la Pili.
Lakini, Dakika chache baadae, makosa ya Man United yaliwapa Liverpool Bao laini baada ya shuti la Steven Gerrard kutemwa na Kipa David De Gea na kutua njiani kwa Mchezaji mpya Daniel Sturridge alieunganisha vizuri na kufunga Bao lake la kwanza kwenye BPL kwa Timu yake mpya na Bao lake la pili baada ya pia kuifungia kwenye FA CUP walipoichapa Mansfield 2-1 kwenye Mechi yake ya kwanza kabisa hivi majuzi.
VIKOSI:
Manchester United: De Gea, Da Silva, Ferdinand, Vidic, Evra, Carrick, Cleverley, Young, Kagawa, Welbeck, van Persie
Akiba: Amos, Jones, Valencia, Anderson, Giggs, Smalling, Hernandez.
Liverpool: Reina, Wisdom, Skrtel, Agger, Johnson, Lucas, Downing, Gerrard, Allen, Sterling, Suarez
Akiba: Jones, Henderson, Sturridge, Carragher, Borini, Shelvey, Robinson.
Refa: Howard Webb

BPL, BARCLAYS PREMIER LEAGUE
RATIBA:
Jumapili 13 Januari 2013
[SAA 1 Usiku]
Arsenal v Man City
Jumatano Januari 16
[SAA 4 DAK 45 Usiku]
Chelsea v Southampton
Jumamosi Januari 19
[SAA 12 Jioni]
Liverpool v Norwich
Man City v Fulham
Newcastle v Reading
Swansea v Stoke
West Ham v QPR
Wigan v Sunderland
[SAA 2 na Nusu Usiku]
West Brom v Aston Villa
Jumapili Januari 20
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Chelsea v Arsenal
[SAA 1 Usiku]
Tottenham v Man United