Sunday, February 24, 2013

CAPITAL ONE CUP FAINALI JUMAPILI: BRADFORD CITY v SWANSEA CITY

CAPITAL_ONE_CUP-BESTUWANJA: Wembley
TAREHE : Jumapili Februari 24
SAA: 1 Usiku
Bradford City, Timu ya Daraja la chini, Ligi 2, Madaraja matatu chini ya wapinzani wao Swansea City,  inawania kutwaa CAPITAL ONE CUP na hivyo kucheza EUROPA LIGI Msimu ujao.
ZIFUATAZO NI DONDOO MUHIMU ZA FAINALI HIYO:
+++++++++++++++++++++++++++
HALI za TIMU:
Bradford City watamcheki Beki wao Rory McArdle kama yuko fiti baada ya kuwa nje kwa muda kutokana na kuumia enka lakini hawataweza kumchezesha Straika Andy Gray  kwa vile alishaichezea Leeds United kwenye Mashindano haya.
Swansea itamkosa Beki wao Chico Flores ambae ana tatizo la enka.
Meneja wa Swansea, Michael Laudrup, ameshatangaza kuwa Kipa wa Akiba Gerhard Tremmel ndia atakeacheza Fainali hii.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
WAMEFIKAJE FAINALI
SWANSEA CITY:
-RAUNDI ya 2: SWANSEA 3 BARNSLEY 1
-RAUNDI ya 3: CRAWLEY 2 SWANSEA 3
-RAUNDI ya 4: LIVERPOOL 1  SWANSEA 3
-ROBO FAINALI: SWANSEA 1 MIDDLESBROUGH 0
-NUSU FAINALI 1: CHELSEA 0 SWANSEA 2
-NUSU FAINALI 2 : SWANSEA 0 CHELSEA 0
BRADFORD CITY:
-RAUNDI ya 1: NOTTS COUNTY 0 BRADFORD 1 (Dakika 120)
-RAUNDI ya 2: WATFORD 1 BRADFORD 2
-RAUNDI ya 3: BRADFORD 3 BURTON ALBION 2 (Dakika 120)
-RAUNDI ya 4: WIGAN 0 BRADFORD 0 (Dakika 120, Penati 4-2)
-ROBO FAINALI: BRADFORD 1 ARSENAL 1 (Dakika 120, Penati 3-2)
-NUSU FAINALI 1: BRADFORD 3 ASTON VILLA 1
-NUSU FAINALI 2: ASTON VILLA 2 BRADFORD 1 (Bradford wapita 4-3]
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
BRADFORD_CITYTATHMINISWANSEA_CITY
Ni Fainali inayokutanisha Timu ya Daraja la chini, Bardford City, ambayo iko Ligi 2, ikiwa ni Madara matatu toka walipo wapinzani wao Swansea City, ambao wako BPL, Barclays Premier League.
Bradford City, chini ya Kocha Phil Parkinson, wametinga Fainali hii kwa kushinda Mechi 4 kati ya 7 kwenye Mashindano haya kwa Mechi kuchezwa Dakika 120 na mbili kati ya hizo kwa Mikwaju ya Penati 5 walipozibwaga Timu kubwa toka BPL, Wigan na Arsenal.
MICHUPia, Bradford wana historia ambayo bila shaka itaitetemesha Swansea ikiwa Mechi itafikia hatua ya kuamuliwa Mshindi kwa Mikwaju ya Penati 5 kwani wao wameshinda hatua hiyo mara 9 mfululizo.
Msimu huu Swansea, chini ya Meneja Michal Laudrup na wakiwa na Straika hatari kutoka Spain Michu, wamekuwa wakicheza Kandanda safi na kufanya vizuri kwenye Ligi Kuu England wakiwa nafasi ya 7.
USO kwa USO:
-Hii itakuwa Mechi ya kwanza kwa Bradford na Swansea kukutana katika Kikombe kikubwa.
-Swansea hawajafungwa katika Mechi 4 za Ligi walizokutana mwisho na Bradford, zote zikiwa ni za Ligi 1, lakini tatu kati ya hizo zilikuwa ni sare.
-Mara ya mwisho Bradford kuifunga Swansea ilikuwa ni Bao 5-1 Uwanjani Valley Parade kwenye Ligi 1 hapo Machi 30 Mwaka 1996.
REKODI:
Bradford City
Bradford ni Timu ya pili kutoka Darala chini, Ligi 2, kufika Fainali ya Kombe la Ligi.
Timu nyingine ilikuwa ni Rochdale Mwaka 1962 ambayo ilifungwa na Norwich iliyokuwa Daraja la Pili.
Ikiwa Bradford itanyakua Kombe, itakuwa ni Timu ya 6 kufanya hivyo bila kuwa Ligi ya juu kabisa nyingine zikiwa ni Norwich (Daraja la 2, 1962), QPR (Daraja la 3, 1967), Swindon (Daraja la 3, 1969), Aston Villa (Daraja la 2, 1975) na Sheffield Wednesday (Daraja la 2, 1991).
Swansea City
Hii ni mara ya kwanza kwa Swansea City kutinga Fainali ya Kombe hili na kabla walikuwa hawajawahi kuvuka Raundi ya 4 ya Mashindano haya.
VIKOSI VINATARAJIWA:
Bradford (Mfumo: 4-4-2): Duke; Darby, Nelson, McArdle, McHugh; Hines, G Jones, Doyle, Reid; Wells, Hanson.
Swansea (Mfumo: 4-5-1): Tremmel; Rangel, Monk, Williams, Davies; Dyer, Hernandez, Ki, De Guzman, Routledge; Michu.
Refa: Kevin Friend [Mechi: 23 Kadi Nyekundu: 1 Kadi Njano: 74]
WASHINDI WA LIGI CUP WALIOPITA:
1961 Aston Villa 0–2
1963 Birmingham City
1964 Leicester City
1965 Chelsea
1966 West Bromwich Albion
1967 Queens Park Rangers
1968 Leeds United
1969 Swindon Town
1970 Manchester City
1971 Tottenham Hotspur
1972 Stoke City
1973 Tottenham Hotspur
1974 Wolverhampton Wanderers
1975 Aston Villa
1976 Manchester City
1977 Aston Villa
1978 Nottingham Forest
1979 Nottingham Forest
1980 Wolverhampton Wanderers
1981 Liverpool
1982 Liverpool
1983 Liverpool
1984 Liverpool
1985 Norwich City
1986 Oxford United
1987 Arsenal
1988 Luton Town
1989 Nottingham Forest
1990 Nottingham Forest
1991 Sheffield Wednesday
1992 Manchester United
1993 Arsenal
1994 Aston Villa
1995 Liverpool
1996 Aston Villa
1997 Leicester City
1998 Chelsea
1999 Tottenham Hotspur
2000 Leicester City
2001 Liverpool
2002 Blackburn Rovers
2003 Liverpool
2004 Middlesbrough
2005 Chelsea
2006 Manchester United
2007 Chelsea
2008 Tottenham Hotspur
2009 Manchester United
2010 Manchester United
2011 Birmingham City
2012 Liverpool

BAYERN YAFUMUA, BARCA, REAL ZOTE USHINDI 2-1, DABI MILANO LEO!!


>> DABI MILANO: JUMAPILI NI INTER MILAN v AC MILAN
MESSI_ASHANGILIA_GOLIVINARA wa La Liga, Barcelona, wamezidi kujongelea Ubingwa, baada ya kuichapa Sevilla kwa Bao 2-1 hii ikiwa ni Mechi yao ya kwanza toka wapokee kichapo kule San Siri mikononi mwa AC Milan katika UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Sevilla ndio waliotangulia kufunga kwa Bao la Botid, Dakika ya 42, na Barca kusawazisha Dakika ya 51, kwa Bao la David Villa, na Lionel Messi kufunga Bao la pili, Dakika ya 60.
Bao 2 za Kipindi cha Pili, za Gonzalo Higuain na Kaka, zimewapa ushindi Real Madrid wa ugenini dhidi ya Deportivo La Coruna.
Deportivo ndio waliotangulia kufunga kwa Bao la Dakika ya 34 la Riki na Real kupiga Bao Dakika ya 73, Mfungaji Kaka, na Dakika ya 88 la Higuain.
Winga wa Real, Angelo Di Maria, alitolewa kwa Kadi Nyekundu Dakika ya 90 kufuatia Kadi za Njano mbili mfululizo.
Kwenye, Bundesliga, vinara, Bayern Munich, waliifumua Werder Bremen Bao 6-1 na kujichimbia kileleni wakiwa Pointi 18 mbele ya Mabingwa Borussia Dortmund ambao leo wanacheza ugenini na Borussia Mönchengladbach.
BAADA ya kuwachapa FC Barcelona, AC Milan Jumapili wana kibarua kipya kwenye Serie A watakapocheza Dabi ya Jiji la Milano “ugenini” na Mahasimu wao wakubwa Inter Milan Uwanjani San Siro, Uwanja ambao kwa Mahasimu hao wote wawili ndio Nyumbani, huku AC Milan wakikamata nafasi ya 3 wakiwa na Pointi 44 na Inter wapo nafasi ya 5 wakiwa na Pointi 43.
RATIBA/MISIMAMO:
LA LIGA
Ijumaa Februari 22
Athletic de Bilbao 1 Real Sociedad 3
Jumamosi Februari 23
Real Mallorca 1 Getafe CF 3
Real Zaragoza 2 Valencia 2
Deportivo La Coruna 1 Real Madrid CF 2
FC Barcelona 2 Sevilla FC 1
Jumapili Februari 24
Rayo Vallecano v Real Valladolid
Celta de Vigo v Granada CF
Atletico de Madrid v RCD Espanyol
Real Betis v Malaga CF
Jumatatu Februari 25
Levante v Osasuna
MSIMAMO-Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 25 isipokuwa inapotajwa]
1 Barcelona 68
2 Atletico Madrid Mechi 24 Pointi 53
3 Real Madrid 52
4 Malaga Mechi 24 Pointi 42
5 Valencia 41
6 Real Sociedad 40

SERIE A
Jumamosi Februari 23
Palermo 0 Genoa 0
Jumapili Februari 24
Sampdoria v Chievo Verona
Atalanta v AS Roma
Bologna v Fiorentina
Juventus v Siena
Parma v Catania
Cagliari v Torino FC
Inter Mila v AC Milan
Jumatatu Februari 25
Udinese v Napoli
SS Lazio v Pescara
MSIMAMO-Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 25]
1 Juventus Pointi 55
2 Napoli 51
3 AC Milan 44
4 Lazio 44
5 Inter Milan 43
6 Fiorentina 42
7 Catania 39

BUNDESLIGA
Ijumaa Februari 22
SC Freiburg 0 Eintracht Frankfurt 0
Jumamosi Februari 23
Bayern Munich 6 SV Werder Bremen 1
Hannover 5 Hamburger SV 1
VfB Stuttgart 1 FC Nuremberg 1
FSV Mainz 1 VfL Wolfsburg 1
FC Augsburg 2 TSG Hoffenheim 1
Schalke 2 Fortuna Dusseldorf 1
Jumapili Februari 24
Borussia Mönchengladbach v BV Borussia Dortmund
SpVgg Greuther Furth v Bayer 04 Leverkusen
MSIMAMO-Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 23 isipokuwa inapotajwa]
1 Bayern Munich Pointi 60
2 Borussia Dortmund Mechi 22 Pointi 42
3 Bayer Leverkusen Mechi 22 Pointi 41
4 Eintracht Frankfurt 38
5 Freiburg 35
6 Hamburger 34
7 Hannover 33
8 Mainz 32
9 Schalke

CAF SUPER CUP: AL AHLY YATWAA KOMBE!


CAF_LOGOAL AHLY ya Misri jana ilitwaa CAF SUPER CUP kwa kuifunga AC Leopards ya Congo Brazzaville Bao 2-1 katika Mechi ilitochezwa Uwanja wa Borg El Arab uliopo Ukanda wa Kitalii kando kando mwa Bahari ya Mediterranean.
Mechi hiyo ilichezwa kwenye Uwanja wa Jeshi na kushuhudiwa na Washabiki, kitu ambacho hivi sasa huko Misri ni cha nadra, kwa vile Watazamaji hawaruhusiwi kwa sababu ya kiusalama tangu yatokee mauuaji Uwanjani Port Said Februari Mwaka jana.
Hii ni mara ya 5 katika Miaka 11 kwa Al Ahly kutwaa CAF SUPER CUP ambalo hushindaniwa na Washindi wa CAF CHAMPIONS LIGI, safari hii Al Ahly, na Mshindi wa Kombe la Shirikisho, safari hi AC Leopards.
Bao za Al Ahly zilifungwa na Chipukizi Rami Rabiea, Dakika ya 55, na Mkongwe Mohamed Barakat, Dakika ya 72.
Bao pekee la AC Leopards lilifungwa Dakika ya 77 na Nahodha wao Rudi Ndey ambae pia nusura asawazishe Dakika za mwishoni lakini shuti lake likaokolewa kwenye mstari wa goli.
Al Ahly, licha ya kutwaa Kombe, pia walipewa kitita cha Dola 75,000 na AC Leopards kupewa Dola 50,000.
WASHINDI WALIOPITA:
1993 Africa Sports National
1994 Zamalek SC
1995 ES Tunis
1996 Orlando Pirates FC
1997 Zamalek SC
1998 ES Sahel
1999 ASEC Mimosas
2000 Raja CA Casablanca
2001 Hearts of Oak SC
2002 Al Ahly SC
2003  Zamalek SC
2004 Enyimba International FC
2005 Enyimba International FC
2006 Al Ahly SC
2007 Al Ahly SC
2008 ES Sahel
2009 Al Ahly SC
2010 TP Mazembe
2011 TP Mazembe
2012 Maghreb AS Fez

BPL: MAN CITY YAICHAPA CHELSEA, YAIKARIBIA UNITED POINTI 12 NYUMA!


>>MAN CITY 2 CHELSEA 0, LAMPARD AKOSA PENATI, YAYA & TEVEZ WAUA!!
>>CHELSEA 4 BORA HATARINI, SPURS WAKO POINTI 1 NYUMA, ARSENAL 2 NYUMA!!
BPL_LOGOMABINGWA watetezi wa BPL, Barclays Premier League, Manchester City, wakicheza kwao Uwanja wa Etihad, leo wameichapa Chelsea Bao 2-0 na kujichimbia nafasi ya pili na kuwasogelea Vinara wa Ligi Man United kwa kuwa Pointi 12 nyuma yao Mechi zikiwa zimebaki 11 lakini Chelsea sasa wapo hatarini kwenye 4 bora kwani wako nafasi ya 3 na nyuma yao kwa Pointi 1 tu ni Tottenham walio na Mechi 1 mkononi na wanafuatia Arsenal walio nafasi ya 5 Pointi 2 nyuma ya Tottenham.

MATOKEO:
Jumapili Februari 24
Manchester City 2 Chelsea 0
Newcastle United 4 Southampton 2

NEWCASTLE 4 SOUTHAMPTON 2
PAPISS_CISSENewcastle walitoka nyuma kwa Bao 1-0 na kuishinda Southampton, iliyo nafasi za hatari za kushushwa Daraja, Bao 4-2 katika Mechi iliyochezwa St James Park.
Ushindi huu umeipandisha Newcastle nafasi kadhaa katika Msimamo wa Ligi Kuu England na sasa wapo nafasi ya 4 wakiwa na Pointi 30 zikiwa ni Pointi ni Pointi 6 juu ya zile Timu 3 za mkiani ambayo ni sehemu ya hatari kwani ni eneo la kuporomoka Daraja mwishoni mwa Msimu.

MAGOLI:
Newcastle 4
-Sissoko Dakika ya 33
-Cisse 42
-Cabaye 67 (Penati)
-Hooiveld 79 (Kajifunga mwenyewe)
Southampton 2
-Schneiderlin Dakika ya 3
-Lambert 50

Morgan Schneiderlin aliifungia Southampton Bao la kwanza na  Moussa Sissoko kusawazisha kisha likaja shuti kali la Papiss Cisse liliowafanya Newcastle waongoze lakini Rickie Lambert akaifanya Mechi iwe 2-2.
Newcastle walipachika Bao la 3 kwa Penati iliyofungwa na Yohan Cabaye kufuatia Danny Fox kuunawa mpira na Bao la 4 alijifunga mwenyewe Jos Hooiveld ambae sasa ameifikia rekodi ya Ligi Kuu England ya kujifunga mwenyewe Bao 3 katika Msimu mmoja.
VIKOSI:
Newcastle: Elliot, Debuchy, Coloccini, Steven Taylor, Santon, Tiote, Cabaye, Sissoko, Gutierrez, Gouffran, Cisse
Akiba: Alnwick, Anita, Yanga-Mbiwa, Perch, Marveaux, Shola Ameobi, Obertan.
Southampton: Boruc, Clyne, Hooiveld, Yoshida, Shaw, Steven Davis, Schneiderlin, Cork, Lallana, Rodriguez, Lambert
Akiba: Kelvin Davis, Fonte, Ramirez, Fox, Ward-Prowse, Mayuka, Puncheon.
Refa: Chris Foy
MAN CITY 2 CHELSEA 0
Hadi Mapumziko Mechi hii ilikuwa 0-0 licha ya Man City kuitawala na Kipindi cha Pili Chelsea MANCINI_ALIAwalipata Penati katika Dakika 52 baada ya Kipa Joe Hart kumwangusha Demba Ba lakini Frank Lampard alishindwa kufunga kwa Kipa Joe Hart kuokoa.
Kwa mshangao wa wengi, licha ya Refa Andre Marriner kutoa Penati, Kipa Joe Hart hakupewa hata Kadi ya Njano.
Hiyo ilikuwa changamoto kwa Man City na Yaya Toure alifunga Bao zuri katika Dakika ya 63 akiwa katikati ya msitu wa Mabeki na Carlos Tevez, aleingizwa Kipindi cha Pili, alipachika Bao la pili katika Dakika ya 85.
VIKOSI:
Man City: Hart, Zabaleta, Toure, Nastasic, Clichy, Javi Garcia, Toure, Rodwell, Milner, Aguero, Silva
Akiba: Pantilimon, Lescott, Nasri, Dzeko, Sinclair, Kolarov, Tevez.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Luiz, Cahill, Cole, Mikel, Lampard, Ramires, Hazard, Mata, Ba
Akiba: Turnbull, Torres, Oscar, Moses, Terry, Azpilicueta, Bertrand.
Refa: Andre Marriner

RATIBA
BPL: BARCLAYS PREMIER LEAGUE
Jumatatu Februari 25
[Saa 5 Usiku]
West Ham United v Tottenham Hotspur
Jumamosi Machi 2
[Saa 12 Jioni]
Chelsea v West Bromwich Albion
Everton v Reading
Manchester United v Norwich City
Southampton v Queens Park Rangers
Stoke City v West Ham United
Sunderland v Fulham
Swansea City v Newcastle United
[Saa 2 na Nusu Usiku]
Wigan Athletic v Liverpool
Jumapili Machi 3
[Saa 1 Usiku]
Tottenham Hotspur v Arsenal
Jumatatu Machi 4
[Saa 5 Usiku]
Aston Villa v Manchester City

MSIMAMO:
[Kila Timu imecheza Mechi 27 isipokuwa inapotajwa]
1 Man United Pointi 68
2 Man City 56
3 Chelsea 49
4 Tottenham Mechi 26 Pointi 48
5 Arsenal 47
6 Everton 42
7 WBA 37
9 Liverpool 39
9 Swansea 37
10 Stoke 33
11 Fulham 32
12 Norwich 32
13 West Ham Mechi 26 Pointi 30
14 Newcastle 30
15 Sunderland 29
16 Southampton 27
17 Wigan 24

18 Aston Villa 24
19 Reading 23
20 QPR 17

VPL: SIMBA HOI, YATUNGULIWA KIMOJA NA MTIBWA!


>>SIMBA WABAKI WA TATU, HATARINI KUNG’OLEWA NA COASTAL!
>>SIMBA NJE YA LIGI KUIFATA LIBOLO, MECHI INAYOFUATA MACHI 10 NA COASTAL UNIONI!!
UWANJA_WA_TAIFA_DARBAO la Dakika ya 16 la Salvatory Ntebe leo limewapa ushindi Mtibwa Sugar wa Bao 1-0 walipocheza na Mabingwa Simba kwenye Mechi ya VPL, Ligi Kuu Vodacom, iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na wao kupanda nafasi mbili hadi ya 5 kwenye Msimamo wa Ligi na kuiacha Simba nafasi ya 3 wakiwa hatarini kung’olewa na Coastal Union walio Pointi 1 nyuma na Mechi moja mkononi.
Simba, ambao wanasafiri kwenda Angola kurudiana na Clube Recreativo de Desportivo do Libolo ambayo ilishinda 1-0 katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Awali ya CAF CHAMPIONZ LIGI, watarudi tena kwenye VPL hapo Machi 10 watakapokuwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kucheza na Coastal Union.
VPL: RATIBA/MATOKEO:
Jumapili Februari 24
SIMBA SC 0 MTIBWA SUGAR FC 1
Jumatano Februari 27
COASTAL UNION v RUVU SHOOTING [MKWAKWANI, TANGA]
YANGA v KAGERA SUGAR [UWANJA WA TAIFA,  DAR ES SALAAM]
POLISI MOROGORO v MGAMBO JKT [JAMHURI , MOROGORO]
JKT RUVU v TOTO AFRICANS [AZAM COMPLEX, DAR ES SALAAM]
MTIBWA SUGAR v TANZANIA PRISONS [MANUNGU, MOROGORO]
Jumamosi Machi 2
POLISI MOROGORO v JKT OLJORO [JAMHURI, MOROGORO]
Jumatano Machi 6
JKT OLJORO v TANZANIA PRISONS [SH. AMRI ABEID, ARUSHA]
AFRICAN LYON FC v RUVU SHOOTINGS [AZAM COMPLEX, DAR ES SALAAM]
MGAMBO JKT v MTIBWA SUGAR [MKWAKWANI, TANGA]
Alhamisi Machi 7
JKT RUVU v KAGERA SUGAR [AZAM COMPLEX, DAR ES SALAAM]
Jumamosi Machi 9
YOUNG AFRICANS v TOTO AFRICANS [UWANJA WA TAIFA, DAR ES SALAAM]
AZAM FC v POLISI MOROGORO [AZAM COMPLEX, DAR ES SALAAM]
Jumapili Machi 10
SIMBA SC v COASTAL UNION [UWANJA WA TAIFA, DAR ES SALAAM]
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
W
D
L
GD
PTS
1
YANGA
17
12
3
2
22
39
2
AZAM FC
18
11
3
4
16
36
3
SIMBA
18
8
7
3
11
31
4
COASTAL
17
8
6
3
6
30
5
MTIBWA
17
7
5
5
3
26
6
RUVU SHOOTING
15
7
3
5
3
24
7
KAGERA
16
6
6
4
2
24
8
JKT OLJORO
17
5
6
6
-1
21
10
MGAMBO
17
6
3
8
-5
21
9
PRISONS
18
4
7
7
-5
19
11
JKT RUVU
17
4
4
9
-13
16
12
TOTO
17
2
7
8
-11
13
13
LYON
17
3
3
11
-18
12
14
POLISI
16
2
5
9
-10
11