Thursday, December 20, 2012

RONALDO DE LIMA XI vs ZIDANE ZIZOU XI 3-2 TIMU YA ZIDANE YAFUNGWA NA TIMU YA AKINA RONALDO RICHA YA ZIDANE KUIFUNGIA TIMU YAKE GOLI KATIKA MECHI DHIDI ya UMASIKIN


 

  RHINO RANGERS WAZIDI KUJIIMARISHA LIGI DARAJA LA KWANZA

 

Timu ya maafande wa jeshi la wananchi ya mkoani tabora RHINO RANGERS imeendelea kujiimarisha katika ligi daraja la kwanza kwa kucheza michezo kadhaa na timu za mkoani tabora ili kujiimarisha katika mzunguko wa pili wa ligi daraja la kwanza FDL.

Timu hiyo leo imecheza mchezo wa kirafiki na timu ya LEEDS UNITED katika dimba la ALLY HASSAN MWINYI na imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 ,mabao ya rhino rangers hii leo yamefungwa na shija mongo dk ya 17 ,maganda machembe mchezaji mpya iliyemsajili alifunga dk ya 32,na bao la ushindi lilifungwa mnamo dk ya 52 ya kipindi cha pili na msafiri maiko.

Pia timu hiyo ya rhino rangers inatarajia kucheza mchezo mmoja w akirafiki na timu ya simba B kutoka dar es salaam ili iwape mazoezi ya kutosha kuelekea mzunguko wa pili wa ligi daraja la kwanza FDL.

Kuelekea mzunguko w apili wa ligi daraja la kwanza rhino rangers imeendelea kuimarisha kikosi chake kwa kusajili wachezaji watano ili kuongeza nguvu katika kikosi,wachezaji iliowasajili ni ayoub iddy ,na josephy mapunda nafasi ya beki,doi mobby,mganda mchembe washambuliaji,na emanuely noely nafasi ya kiungo.

wachezaji wa zamani ni abdukarim mtumwa,iddy kihulya,charles mpinuki,james mwambembe,julius masunga,abass mohamedy,stanslaus mwakitosi,steven madhanda,shija sanju,shija mongo,salum mamro,salum majid,usi makame,na frank koe.

wengine ni josephy salaganda,victor hangaya,bakary mahadhi,said kipanga,issa mohamedy,stanley mlai,samwely mwamasangula,omary magesa,msafiri maiko,ramadhani shabyeji na ally rumba na kuhitimisha idadi ya wachezaji 30 katika klabu hiyo inayonolewa na kocha wa zaman wa mafunzo ya zanzibar akisaidiwa na kocha mongo.

 

 

UCHAGUZI W AMKOA W ATABORA TAREFA KUFANYIKA KESHO KATIKA UKUMBI WA TUWASA KUANZIA SAA NNE ASUBUHI .


 MWENYEKITI wa kamati ya uchaguzi mkoa wa tabora TAREFA bw.MKAMA BWIRE leo ametibitisha    kuwa uchaguzi w amkoa w atabora utafanyika kesho december 22 ya mwaka huu katika ukumbi  wa idara ya maji mkoani tabora TUWASAkutafuta viongozi watakaochaguliwa kuwakilisha mkoa wa tabora TAREFA.


Majina yaliyopitishwa LEO  2112/2012  katika nafasi ya MWENYEKITI.

1.Musa Ntimizi

2.Yusuph kitumbo.

3.Laurent paul

-===NAFASI YA MAKAMU MWENYEKITI

1.A laija Mwiga

===NAFASI YA KATIBU

1.Albert sitta

2.Fatteh Dewj

===NAFASI YA KATIBU MSAIDIZI

,,,,,,HAKUNA MGOMBEA

====NAFASI YA MWEKA HAZINA=AMEJIONDOA KUTOKANA NA KUONGEZEWA MAJUKUMU KATIKA UTENDAJI WA KAZI W AUHASIBU MKOA W ATABORA BW.

1.Mussa Msananga

===NAFASI YA MWEKA HAZINA MSAIDIZI

,,,,HAKUNA MGOMBEA

===NAFASI YA MJUMBE MKUTANO MKUU TFF

1.Dick Mlimuka

2.Milambo Kamili

3.Ramadhani Maghembe

4.Charles Mwakambaya

===NAFASI YA MWAKILISHI WA VILABU

1.Achery manjori

2.Razack j.Kumba

3. Lwamba yussa

===NAFASI YA UJUMBE KAMATI YA UTENDAJI

1.Stanslaus Sizya

2.Abdul mohamed Aman

3.James Erick Kabepele

===NAFASI YA MWAKILISHI WA MPIRA WA MIGUU KWA UPANDE WA WANAWAKE NI-janeth michael


 

LULU AACHIWA KWA DHAMANA

Lulu katika siku za mwanzo za kesi yake, akifikishwa Mahakama ya Kisutu
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, leo asubuhi imemuachia kwa dhamana msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayetuhumiwa kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba ‘The Great’ baada ya kupitia vifungu vya sheria.
Hatua hiyo inakuja baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kubadilisha mashitaka ya mwanadada huyo kutoka kesi ya mauaji hadi kuua bila kukusudia.
Kutokana na mabadiliko hayo, hata kama atashindwa kesi, Lulu hatapewa hukumu ya kunyongwa kwa kuwa anatuhumiwa kwa kesi ya kuua bila kukusudia na kwa mujibu wa kifungu cha sheria, anaweza kufungwa maisha au miaka kadhaa.
Lulu anakabiliwa na tuhuma za kumuua The Great Kanumba aliyefariki dunia, Aprili 7, mwaka huu nyumbani kwake Vatican, Sinza Dar es Salaam.
Lulu aliyecheza filamu kadhaa na marehemu Kanumba waliyeibuka naye katika kundi la Kaole, Magomeni, anadaiwa alimsukuma Kanumba nyumbani kwake Sinza Vatican, ambaye pia inadaiwa alikuwa mpenzi wake.
Inaelezwa baada ya tukio hilo, Lulu alikimbia nyumbani kwa Kanumba na mdogo wa The Great, Sethi Bosco akaenda kuchukua gari kumpeleka kaka yake hospitali ya Muhimbili, ambako alipofika iligundulika amekwishafariki dunia.
Sethi alikaririwa akisema kwamba siku ya tukio, Lulu alikwenda kwao usiku wa manane na alipofika yeye (Sethi) alimuacha aongee na kaka yake. Sethi alidai aliwaacha sebuleni akaingia chumbani kwake na baadaye akasikia wameingia chumbani (kwa Kanumba).
Sethi alisema baada ya muda alisikia kelele za dalili ya ugomvi na baada ya muda Lulu alitoka kumwambia (Sethi) juu ya hali ya Kanumba kubadilika na kuwa mbaya.
Sethi alidai aliposikia hivyo akashituka na kwenda chumbani ambako alimkuta kaka yake katika hali mbaya, povu likimtoka mdomoni hivyo kuchukua hatua ya kumuita daktari wake, kabla ya kumkimbiza Muhimbili.
Lulu alikamatwa asubuhi ya kuamkia siku ya tukio hilo, linalodaiwa kutokea usiku wa manane na kuwekwa kizuizini katika kituo cha Polisi Oysterbay, Kinondoni, Dar es Salaam, kabla ya kufikishwa mahakamani.
Uchunguzi wa madaktari katika hospitali ya Rufaa ya Muhimbili ulisema pombe kali aina ya Jackie Daniels ilisababisha kifo cha mwigizaji huyo. 
Kifo cha Kanumba kiliwaumiza wengi, kwani msanii huyo alikuwa mahiri na kipenzi cha wapenzi wa filamu nchini.
Wapembuzi wa mambo wanasema huu ni msiba wa kwanza kuteka hisia za watu wengi zaidi, tangu kifo cha baba wa taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Oktoba mwaka 1999.

RAUL: AFUNGIWA MECHI KUMI NA MOJA

Mchezaji wa zamani na  kiungo wa  klabu ya Liverpool na  Chelsea  Raul Meireles amefungiwa mechi kumi na moja baada kutuhumiwa kumtemea mate mwamuzi  .

 Mchezaji huyo wa mwenye miaka 29-anayechezea  Fenerbahce , alitolewa nje kwa kadi Nyekundu siku ya mechi dhidi ya  Galatasaray,
ambayo mechi hiyo walipoteza kwa mabao mawili kwa moja aidha Raul Amekataa tuhuma hizo. 

Japokuwa shirikisho la soka la uturuki limeshutumu mwamuzi huyo  Halis Ozkahya's kwa kukiri na kuidhinisha adhabu hiyo . 

 Meireles amesema : "Nitachukua hatua za kisheria dhidi yake  kuonyesha kuwa nimechukizwa na siku fanya kitendo hicho." pia alikata kuwa alifamnyia ishara za kumdharau mwamuzi huyo ,

"Sijui ishara yoyote  ya kituruki kuwa nilimuonyesha mwamuzi kuwa yeye ni shoga huyu mwamuzi ni kigeugeu na anasikiliza sana kelele za mashabiki  ,"Aliongeza mreno huyo    

 "Tazam mtindo wangu wa Nywele 'Nilichovaa mimi sio mtu wa aina hiyo ishara ya mkono wangu haiku ya maana hiyo au kitendo mnaachokiita cha kishoga  
Mwamuzi huyu anatoa tuhuma za kudharirishana na ni kashfa hii mimi nina mtoto wa miaka nane sasa itakuwaje watooto wakisema kuwa baba yenu kamtemea mate mwamuzi au kamtukana 
 
Meireles alichezea misimu mwili klabu ya za ligi ya uingereza akitokea porto akijiunga na  Liverpool na badae kwenda  Chelsea 2011. 

 Alijiunga  mwezi kenda na Fenerbahce kwa ada ya pauni  £8m . 


HATUTADHARAU MECHI "KATONGO "

Christopher Katongo nahodha wa timu ya Taifa ya Zambia akieleza mikakati ya ushindi hapo kesho dhidi ya timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars mchezo utakaopigwa kesho katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Christopher Katongo (30), ambaye pia ni Mwanasoka Bora wa Afrika wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) mwaka huu, amesema kuwa mipango endelevu ya kulea wachezaji vijana na nidhamu ya wachezaji ndiyo chanzo cha mafanikio yao.

 Amesema kwamba hata katika mechi ya timu yake dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi, wachezaji wenye umri mdogo ndiwo watakaopewa kipaumbele katika kikosi cha Chipolopolo.

 “Nidhamu, kujituma na kufuata taratibu ndiyo siri ya mafanikio yetu. Nadhani umeona mazoezi yetu, tunafanya kazi kwa umoja na kila mchezaji ana ari ya kufanya kile anachoelekezwa na mwalimu,” .

Kocha wa kikosi wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa stars Kim Poulsen alikielezea namna atakavyotumia nafasi ya kesho ya kucheza na timu bora ya Afrika Zambi hapo kesho, ambapo ameeleza kuwa anamatumaini ya kushinda katika mchezo huo licha ya kuwakosa wachezaji wake wawili muhimu Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu.
 “
KIBIRA AFUNGIWA CHANETA
Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limemuondolea adhabu ya kifungo cha muda usiojulikana katibu mkuu wa zamani wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta), Anna Kibira kufuatia baraza hilo kubaini kuwa hana hatia yoyote.

Taarifa kutoka ndani ya BMT zimeeleza kuwa sasa, Kibira yuko huru na kwamba, akitaka anaweza kujitosa katika kuwania uongozi wakati wa uchaguzi mkuu wa Chaneta utakaofanyika hivi karibuni.

  Mwenyekiti wa BMT, Dioniz Malinzi, amesema Kibira yuko huru na kwamba kuanzia sasa anaweza kugombea nafasi yoyote anayoitaka kutokana na ukweli kwamba hana hatia inayomzuia kugombea katika uchaguzi mkuu wa chama hicho.

 Amesema kuanzia sasa, Kibira na wanamichezo wengine wenye nia ya kugombea wanapaswa kujiandaa kwa uchaguzi mkuu wa chama hicho.

 Aliongeza kuwa Kibira anatarajiwa kufika kwenye ofisi za BMT kuanzia leo kupata maelekezo kutokana na adhabu aliyokuwa amepewa awali na kamati ya utendaji ya CHANETA, ambayo iliashiria kufungiwa kwake kwa muda usiojulikana.

 Aidha, Kibira amesema kuwa bado hajapata taarifa yoyote kuhusiana na kufungiwa kwake Chaneta, lakini amefurahishwa na uamuzi wa kuondolewa adhabu na kwamba atakuwa tayari kutangaza nia yake pale atakapopata uthibitisho rasmi kuwa yuko huru kugombea katika uchaguzi huo.

 "Nimefurahi kusikia hivyo. Lakini nasubiri taarifa rasmi kutoka kwa BMT ili nijihakikishie kama kweli ninaruhusiwa kugombea," amesema Kibira.

 Aliongeza kuwa, katika muda wote wa kusimamishwa kwake CHANETA, amekuwa akijishughulisha na michezo mingine kutokana na ukweli kuwa michezo iko damuni.

Licha ya kufungiwa kwa muda usiojulikana, Kibira alikuwa hajawahi kupewa barua yoyote hadi BMT ilipoeleza jana kuwa yuko huru na kwamba sasa anaweza kujishughulisha na CHANETA

REAL MADRID VS MAN UNITED: RONALDO "SITOSHANGILIA GOLI ENDAPO NITAFUNGA DHIDI YA UNITED"

Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo amesisitiza kwamba hatoweza kushangilia ikiwa atafunga katika hatua ya 16 ya UEFA Champions league dhidi ya Manchester United.

 Nahodha huyo wa Ureno ambaye alicheza kwa mafanikio makubwa akiwa na United katika kipindi cha miaka 6 kabla ya kuondoka na kujiunga Los Blancos katika kipindi cha kiangazi mwaka 2009 kwa ada iliyovunja rekodi ya dunia ya £80 million.

"Sitoshangilia goli nikiweza kufunga dhidi ya Man United," Ronaldo alikaririwa akisema siku ya alhamisi na mtandao wa AS.


Ronaldo, 27, hivi karibuni alielezea hisia zake juu ya kocha wa Manchester United na kusema kocha huyo raia wa Scotland amecheza part kubwa katika kumfanya mchezaji ambaye alivyo sasa.

"Ferguson ni mtu mzuri sana. Mwanadamu mwema. Amenifundisha vitu vingi," Ronaldo aliiambia The Sun.


"Kama nilivyosema huko nyuma, Fergie ni kama baba yangu kwenye soka. Nammisi sana yeye na mahusiano tuliyokuwa nayo."


HIVI NDIVYO TUZO YA BALLON D'OR INAVYOTENGENEZWA - RONALDO, MESSI, AU INIESTA NANI KUIBUKA KIDEDEA WIKI 2 ZIJAZO????

RONALDO, INIESTA OR MESSSI

Golden balls: The world's oldest jewellers have a team of six working on the Ballon d'Or trophy
Timu ya masonara sita ndio wanashughulikia utengenezwaji wa tuzo ya Ballon d'Or

Golden balls: The world's oldest jewellers have a team of six working on the Ballon d'Or trophy
Utengenezaji wa Ballon d'Or ukiendelea

Golden balls: The world's oldest jewellers have a team of six working on the Ballon d'Or trophy
Ufaransa ndio imekuwa nchi inayotengeneza tuzo tangu mwaka 1956.



Piece by piece: The same family-run store in Paris have built the trophy every year since 1956
Mtengenezaji akiweka kipande kimojawapo kwenye tuzo hiyo

Craftsman: All the finishing touches are applied by hand... but who will get their hands on the trophy?
Craftsman: All the finishing touches are applied by hand... but who will get their hands on the trophy?

 

 

 

 

 

UEFA CHAMPIONZ LIGI: BAADA ya DROO, NINI WAMESEMA!!

>>RATIBA KAMILI YATOKA!!
>>REAL v MAN UNITED ni FEBRUARI 13
>> FERGIE: ‘NDIO BIGI MECHI RAUNDI YA TIMU 16!!’
+++++++++++++++++++
RATIBA:
[Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku]
Jumanne 12  Februari 2013
Celtic v Juventus
Valencia v Paris St Germain
Jumatano 13  Februari 2013
Real Madrid v Manchester United
Shakhtar Donetsk v Borussia Dortmund
Jumanne 19  Februari 2013
Arsenal v Bayern Munich
FC Porto v Malaga
Jumatano 20  Februari 2013
Galatasaray v FC Schalke
AC Milan v Barcelona
Jumanne 5 Machi 2013
Borussia Dortmund v Shakhtar Donetsk
Man United v Real Madrid
Jumatano 6 Machi 2013
Juventus v Celtic
Paris St George v Valencia
Jumanne 12 Machi 2013
Barcelona v AC Milan
Schalke v Galatasaray
Jumatano 13 Machi 2013
Bayern Munich v Arsenal
Malaga v FC Porto
+++++++++++++++++++
FERGIE_n_MOURINHOMara baada ya kumalizika kwa Droo ya kupanga Mechi za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI hapo jana huko Nyon, Uswisi, Wadau mbalimbali waliibuka kutoa maoni yao kuhusu Ratiba hiyo na Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, alisema pambano la Real Madrid na Manchester United ndio ‘mpambano’ wa Raundi hiyo.
Real Madrid na Manchester United hawajakutana kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI tangu Robo Fainali ya Mwaka 2003 ambayo Real walishinda kwa jumla ya Mabao 6-5 baada ya kushinda Mechi ya kwanza 3-1 huko Santiago Bernabeu na kufungwa 4-3 Uwanjani Old Trafford huku Ronaldo de Lima akipiga Hetitriki.
Mbali ya pambano kuwa zito, Mechi hii itakuwa na mvuto kwani Cristiano Ronaldo atarudi Old Trafford kwa mara ya kwanza tangu aihame Man United na kwenda Real Madrid Juni 2009 kwa Dau la Pauni Milioni 80.
Mara ya mwisho kwa Sir Alex Ferguson kumvaa Jose Mourinho ilikuwa kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI Mwaka 2009 wakati Man United ilipoibwaga Inter Milan kwenye Robo Fainali baada ya kutoka 0-0 na kuifunga 2-0 Old Trafford kwa Bao za Vidic na Ronaldo.
Ferguson amesema: “Ni nafasi nzuri kwa Mashabiki wetu kumuona Ronaldo tena na mimi kukutana na Jose-itabidi niagize Mvinyo safi!”
+++++++++++++++++++
Man United v Real Madrid
-1957: European Cup-Nusu Fainali: Real washinda 3-1Madrid, sare 2-2 na Real kushinda Jumla ya Bao 5-3
-1968: European Cup-Nusu Fainali: Man United washinda 1-0 Old Trafford, sare 3-3 ugenini na Man United washindi Jumla ya Bao 4-3
-2000: European Cup-Robo Fainali: Sare 0-0 huko Bernabeu, Man United wafungwa 3-2 nyumbani
-2003: European Cup-Robo Fainali: Real washinda 3-1 nyumbani, Man United washinda 4-3 nyumbani, Real wapita Jumla ya Mabao 6-5.
+++++++++++++++++++
YAFUATAYO ni NINI KILISEMWA KUTOKA KWA WADAU MBALIMBALI:
Real Madrid
Mkurugenzi wa Real Madrid, Emilio Butragueno, aliewahi kuwa Straika wao zamani:  "Tungependa kucheza na Man United baadae lakini hata wao hawakufurahia!"
Barcelona
Makamu wa Rais wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu "AC Milan ni Klabu kubwa Ulaya, inaheshimika. Kwa sasa hawachezi vizuri lakini mpira hubadilika Siku hadi Siku."
Bayern Munich
Mwenyekiti wa Bayern Karl-Heinz Rummenigge "Tunaijua Arsenal vizuril. Tunaridhika na Droo hii lakini hatuwadharau!"
Paris St Germain
Mkurugenzi wa Soka, Leonardo: "Siku zote ni ngumu kusema ni Droo nzuri au siyo!"
Valencia
Mkurgenzi wa Valencia, Fernando Giner: "Kama tumefika hapa basi sisi ni moja ya Timu Bora 16 Ulaya!"

SALUM KINJE WA SIMBA MGONJWA, ASHINDWA KUFANYA MAZOEZI


KIUNGO wa Simba Salim Kinje leo alishindwa kufanya mazoezi ya asubuhi na wenzake kutokana na kuugua malaria

Simba ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu wanafanya mazoezi ya ufukweni  Coco Beach jijini Dar es Salaam wakijiandaa na mzunguko wa pili.

Akizungumza nleo jijini wakati wenzake wakiwa mazoezini Kinje alisema kuwa ugonjwa huo ulimuanza tangu juzi na kwamba anaendelea kutumia dawa.

"Sijajumuika na wenzangu kwani naumwa na malaria ambayo yalinianza jana(juzi) lakini hata hivyo naendelea vizuri kwani dawa ninazotumia zinanisaidia," alisema.

Wakati huo huo wachezaji wa kikosi hicho wamefurahishwa kumuona kiungo mchezeshaji Haruna Moshi 'Boban' akijumuika nao katika mazoezi hayo.

Mbiyavanga, Salum Kinje wawa kivutio mazoezini Simba

Ramadhani Chombo 'Redondo' alisema kuwa Haruna Moshi ni mchezaji muhimu sana na kwamba kikosi chao kitazidi kuimarika.

"Sisi hatuna kubwa la kuongea zaidi ya kufurahi kumuona akijumuika nasi katika mazoezi,hii inaashiria kuwa timu inazidi kuimarika," alisema.

Mara baada ya mazoezi hayo kumalizika majira ya saa 2:56 asubuhi Boban alipanda gari yake aina ya Toyota Corola yenye namba za usajili T4920 CAT na kuondoka.

Boban alisimamishwa na uongozi wa timu hiyo baada ya kudanganya kuwa ni mgonjwa na kuachwa katika safari ya kwenda Tanga kupambana na Mgambo Shooting.

Hata hivyo kesho yake wakati Simba ikikwaana na Mgambo katika uwanja wa Mkwakwani Boban alionekana jijini Dar es Salaam akicheza mpira wa mchangani maarufu kama 'Ndondo'.

 

AZAM KUTINGA FAINALI LEO DRC?

Mwaikimba ataendelea kucheka na nyavu leo?
AZAM FC inashuka dimbani leo kumenyana na Shark FC katika Nusu Fainali ya Kombe la Hisani mjini hapa, kwenye Uwanja wa Martyrs.
Awali, Shirikisho la Soka Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo (DRC), liliitaka Azam FC kucheza mechi moja zaidi, baada ya kufuzu Nusu Fainali, lakini baada ya majadiliano, mpango huo umefutwa na leo Wana Lamba Lamba wanacheza Nusu Fainali moja kwa moja.
Azam iliingia Nusu Fainali juzi baada ya kuilaza Real de Kinshasa kwenye Uwanja huo huo wa Martyrs, shukrani kwao, washambuliaji Gaudence Mwaikimba na Seif Abdallah waliofunga mabao hayo, moja kila kipindi.
Ikiongezewa nguvu na nyota wake watatu, Kipre Tchetche, Kipre Balou raia wa Ivory Coast na Mkenya, Joackins Atudo waliochelewa mechi mbili za awali, Azam juzi ilitawala mchezo na kama si rafu za wapinzani wao, ingevuna ushindi mtamu.
Hadi mapumziko, tayari Azam walikuwa mbele kwa bao 1-0, lililotiwa kimiani na Mwaikimba dakika ya 21, ambaye aliunganisha pasi nzuri ya Kipre kutoka wingi ya kushoto.
Hilo lilikuwa bao la pili kwa Mwaikimba, mshambuliaji wa zamani wa Kahama United, Ashanti United, Yanga, Prisons na Kagera Sugar katika mechi tatu za mashindano haya alizocheza, awali alifunga katika sare ya 1-1 na Dragons.
Kipre Tchetche alilazimika kutoka nje ya Uwanja dakika ya 43 kutokana na rafu za wachezaji wa Real, nafasi yake ikichukuliwa na Samih Hajji Nuhu.
Real walikuwa wakipiga kiatu haswa na kiungo Waziri Salum aliungana na Kipre Tchetche kuuacha Uwanja kabla ya filimbi ya kuugawa mchezo, ingawa nafasi yake ilichukuliwa na Uhuru Suleiman dakika ya kwanza ya kipindi cha pili.
Awali ya hapo, refa Madila Achille alimtoa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 43 beki Muipalayi Igongo kwa kumchezea rafu mbaya Gaudence Mwaikimba, ambayo chupuchupu naye imtoe nje, kiasi cha kulazimika kumalizia mechi akichechemea.
Kipindi cha pili, Azam waliendelea kuwafundisha soka Real na katika dakika ya 73, kazi nzuri ya Mwaikimba ilisaidia kupatikana bao la pili. Mpira mrefu uliopigwa na kipa Mwadini Ally, Mwaikimba aliumiliki vema, akatoa pasi pembeni kushoto kwa Hajji Nuhu ambaye aliingia ndani kidogo na kukata krosi maridadi iliyounganishwa kimiani na Seif.
Humphrey Mieno alikuwa mwathirika mwingine wa rafu za Real, baada ya kulazimika kutoka nje dakika ya 77, akimpisha Abdi Kassim ‘Babbi’.
Azam walionekana kuridhika baada ya kuwa wanaongoza mabao 2-0 na wakafanya uzembe uliowapa bao la kufutia machozi Real, lililofungwa na Bisole Panzu dakika ya 78.
Katika mechi zake mbili za awali za Kundi B, Azam ilitoka 1-1 na Dragons na ikafungwa 2-0 na Shark FC.
Nusu Fainali nyingine itachezwa kesho wakati Fainali na mechi ya kusaka mshindi wa tatu zitachezwa Jumapili na Azam itaondoka hapa Jumatatu kurejea nyumbani.

KIIZA AWASILI YANGA

Kiiza

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Hamisi Kiiza ‘Diego’ amewasili jana Dar es Salaam jana kujiunga na timu yake, Yanga SC baada ya mapumziko kufuatia mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge.
Kiiza aliyeiongoza Uganda kutwaa ubingwa mjini Kampala, Uganda aliomba mapumziko baada ya Kombe la Challenge na jana amerejea rasmi kazini.
Yanga inatarajiwa kwenda kuweka kambi Uturuki, Desemba 28, mwaka huu kujiandaa na Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame pamoja na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Kikosi kizima cha Yanga kipo kambini Dar es Salaam, kikijifua vikali chini ya kocha wake Mkuu, Mholanzi Ernie Brandts.
Yanga imepania kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu pamoja na kutetea Kombe la Kagame, michuano ambayo itafanyika Januari mwakani mjini Kigali, Rwanda.       

UMONY AOMBA UDHURU AZAM

Umony

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Brian Umony atajiunga na klabu yake mpya, Azam FC baada ya sikukuu za Krisimasi na mwaka mpya, imeelezwa.
Katibu wa Azam FC, Nassor Idrisa alisema jana  kwamba, Umony ameomba aje kuanza kazi baada ya sikukuu na uongozi umemkubalia.
Azam inatarajiwa kuondoka hapa mapema Jumatatu kurejea Dar es Salaam baada ya kumalizika kwa mashindano ya Kombe la Hisani mjini hapa Jumapili.
Nassor amesema timu ikirejea Dar es Salaam wachezaji watapewa mapumziko ya siku mbili kwa ajili ya sikukuu na baada ya hapo, watarudi kambini tayari kwa safari ya Zanzibar kwenye Kombe la Mapinduzi.
A
zam ambao ndio mabingwa watetezi wa Kombe la Mapinduzi, leo watacheza mechi ya Nusu Fainali na Shark FC Uwanja wa Martyrs na Jumapili watacheza mechi ya mwisho, iwe ya kusaka mshindi wa tatu au ubingwa, itategemea na matokeo ya leo.

KIUNGO AZAM NJE WIKI MBILI

Waziri akisaidiwa na makipa wa timu yake kutoka uwanjani
KIUNGO Waziri Salum wa Azam FC, atakuwa nje ya Uwanja kwa wiki mbili kufuatia kuumia katika mchezo wa juzi dhidi ya Real de Kinshasa kwenye Uwanja wa Martyrs mjini hapa.
Daktari wa Azam FC, Mjerumani Paulo Gomez alisema jana toka  mjini kishansa kwamba Waziri ameumia mfupa wa pembeni wa paja la kushoto na kwa sababu hiyo atakuwa nje kwa muda wiki mbili akipata matibabu.
Kocha Muingereza Stewart Hall amepokea kwa masikitiko taarifa hizo, akisema Waziri ni mchezaji ambaye anainukia vizuri Azam na kumkosa katika mashindano haya litakuwa pigo kwake.
Hata hivyo, Stewart alisema atatumia wachezaji wengine wakati akimsubiri kiungo huyo Mzanzibari apate ahueni.
Waziri amecheza mechi zote tatu za Azam katika mashindano haya hadi juzi alipoumia dakika ya 43 na kutoka nje.
Kiungo huyo amekuwa akionyesha soka maridadi katika mashindano haya na kuashiria kwamba ataibeba Azam katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho mwakani.
Wachezaji wengine majeruhi Azam ni kiungo Mzanzibari pia, Abdulhalim Humud anayesumbuliwa na maumivu ya nyama za paja na mshambuliaji John Bocco, ambao wamebaki Dar es Salaam. 


YAYA TOURE NI BORA AFRIKA 2012

>>WACHEZAJI wa NDANI AFRIKA: MSHINDI ABOUTRIKA!!
>>TIMU BORA: ZAMBIA, KOCHA BORA wa ZAMBIA: HERVE RENARD!!
>>TUZO ya NGULI: KOCHA EL-GOHARY, MCHEZAJI RIGOBERT SONG!
>>GABON YAFUTIWA USHINDI KOMBE LA DUNIA 2014!!
YAYA_TOURE-BORA_CAFKIUNGO WA MANCHESTER CITY, na Mchezaji wa Ivory Coast, Yaya Toure, ameshinda Tuzo ya CAF ya Mchezaji Bora Afrika kwa mara ya pili mfululizo baada ya kuwabwaga Didier Drogba, alietwaa nafasi ya pili, na Alex Song kukamata nafasi ya tatu.
++++++++++++++++
WACHEZAJI BORA AFRIKA MIAKA ya KARIBUNI:
-2006 Didier Drogba
-2007 Frederic Kanoute
-2008 Emmanuel Adebayor
-2009 Didier Drogba
-2010 Samuel Eto'o
-2011 Yaya Toure
-2012 Yaya Toure
++++++++++++++++
Yaya Toure alishinda kufuatia Kura zilizopigwa na Makocha Wakuu au Wakurugenzi wa Ufundi wa Vyama Wanachama wa CAF.
Hadi sasa Mchezaji anaeongoza kwa kutwaa Tuzo nyingi za Mchezaji Bora Afrika ni Samuel Eto’o wa Cameroun.
Pamoja na Toure, Zambia ilichaguliwa kuwa ndio Timu Bora ya Mwaka na Kocha wao Herve Renard kutwaa Tuzo ya Kocha Bora kwa Mwaka 2012.
Tuzo ya Klabu Bora Afrika ilikwenda kwa Al Ahly ya Misri baada ya kutwaa CAF CHAMPION LIGI Mwaka huu likiwa ni Taji lao la 7.
Kwa upande wa Wachezaji wanaocheza ndani ya Afrika, Tuzo ya Mchezaji Bora ilichukuliwa na Gwiji wa Al Ahly Mohamed Aboutrika.
Kwa upande wa Vijana wanaochipukia, Mchezaji wa Egypt, Mohamed Salah, Miaka 23, alitunukiwa Tuzo ya Kipaji kinachoinukia kwa kuifungia Egypt katika Mechi 3 kati ya 4 walizocheza huko London Mwaka huu kwenye Michezo ya Olimpiki.
Watu waliotunukiwa Tuzo za kuwa Manguli, Utumishi uliotukuka, ni Kocha veterani wa Egypt, Mahmoud El-Gohary, Miaka 74, kwa kuzipa ushindi Barani Afrika Klabu na Nchi yake katika utumishi wake.
Nae Veterani wa Cameroun, Rigobert Song, alitawazwa kuwa Nguli wa Afrika.
Kwa upande wa Kinamama, Timu Bora imetajwa kuwa ni Equatorial Guinea baada ya kutwaa Ubingwa wa Afrika kwa Kinamama walipoitoa Banyana Banyana ya Afrika Kusini.
Mchezaji Bora kwa Kinamama ni Genoveva Anonman wa Equatorial Guinea ambae alipachika Bao 6 kwenye Fainali za Wanawake na ambae anang’ara huko kwenye Ligi ya German Bundesliga kwa Kinamama.


 GABON YANYANG'ANYWA USHINDI KWA KUMCHEZESHA MCHEZAJI ASIYESTAHILI YAPEWA  NIGER
WAKATI HUO HUO, FIFA imeipa ushindi Niger wa Bao 3-0 katika Mechi ya Mchujo ya Bara la 
img Afrika kuwania kucheza Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka 2014 baada ya Gabon kumchezesha Mchezaji asiestahili.
FIFA imeamua kuwa Charly Moussono hakustahili kuichezea Gabon kwa vile aliiwakilisha Cameroun kwenye Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2006 za Soka la Bichi.
Kufuatia uamuzi huo, FIFA imeyafuta matokeo ya 0-0 kati ya Niger na Gabon kwenye Mechi iliyochezwa huko Niamey, Niger Mwezi Juni.
FIFA imethibitisha kuwa uamuzi huu utabaki kama ulivyo kwa vile Gabon ilishindwa kukata Rufaa katika muda uliostahili.
Kufuatia uamuzi huu Msimamo wa KUNDI E ambalo lina Timu za Congo, Burkina Faso, Niger na Gabon ni kama ifuatavywo baada ya Mechi mbili:
1 Congo Pointi 4
2 Gabon 3
3 Niger 3
4 Burkina Faso 1

HII NI MARA YA PILI kwa FIFA kuzipora Pointi Timu za Afrika ya kwanza ikiwa ni Sudan. SOMA RIPOTI ya awali:
FIFA imeinyang’anya Sudan ushindi wake wa Bao 2-0 walioifunga Zambia kwenye Mechi ya Kundi D ya Mechi za Mchujo kuwania kucheza Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Brazil baada ya kumchezesha Mchezaji mmoja ambae hakustahili kucheza Mechi hiyo.
Kamati ya Nidhamu ya FIFA imeamua kuwa Mchezaji Saif Ali hakutakiwa kucheza Mechi hiyo waliyoshinda Sudan Mjini Khartoum hapo Juni 2 Mwaka huu baada ya kuwa na Kadi za Njano alizopata katika Mechi za nyuma ikiwemo ile ambayo Zambia waliichapa Sudan kwenye Robo Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2012, iliyochezwa huko Gabon na Equatorial Guinea.
FIFA imeamua sasa kuipa Pointi 3 Zambia na goli 3-0 na pia kukitwanga Faini ya Dola 6,340 Chama cha Soka cha Sudan.
Uamuzi huu wa FIFA unaifanya Zambia sasa iongoze Kundi D ikiwa na Pointi 6 kwa Mechi mbili ikifuatiwa na Ghana wenye Pointi 3, Sudan nafasi ya 3 wakiwa na Pointi 1 na Lesotho wako mkiani wakiwa na Pointi 1.
MSIMAMO KUNDI D:
1 Zambia Mechi 2 Pointi 6
2 Ghana Mechi 2 Pointi 3
3 Sudan Mechi 2 Pointi 1
4 Lesotho Mechi 2 Pointi 1

MECHI DHIDI ya UMASIKINI: RONALDO XI yaichapa ZIDANE XI

>>ILIPIGWA Grêmio Arena, Porto Alegre, Brazil, MASHABIKI: 50,000!!
MATCH_AGAINST_POVERTYMbele ya Mashabiki zaidi ya 50,000 waliofurika ndani ya Grêmio Arena huko Mjini Porto Alegre, Brazil Kikosi cha Ronaldo kilikifunga Kikosi cha Zinédine Zidane Bao 3-2 katika Mechi ya Kampeni ya Kupiga Vita Umaskini Duniani, rasmi kama MATCH AGAINST POVERTY.MATCH_AGAINST_POVERTY-PICTURE
Wakiwa Mabalozi wa Programu ya Maendeleo ya Umoja wa Mataifa, UNDP, Ronaldo wa Brazil na Zinedine Zidane wa France waliongoza Kombaini zao wakiwa Manahodha katika Mechi ya kila Mwaka, hii ikiwa mara ya 10 kuchezwa, kuhamasisha Ulimwengu katika Vita dhidi ya Umasikini.
Bao la ushindi kwa RONALDO XI lilifungwa na Leandro Damiao katika Dakika za mwisho huku Mabao yao mengine yakifungwa na Cacá Ferrari na Bebeto.
Bao za ZIDANE XI zilifungwa na Zidane na Falcao.
Mechi hii ilichezeshwa na Refa ambae anasifika kuwa ndie alikuwa Bora kupita wote, Pierluigi Collina wa Italy.
Akiongea baada ya Mechi Zidane alisema: “Kucheza Brazil, kwenye Moyo wa Soka, kwa mara ya kwanza na kukutana tena na Rafiki yangu Ronaldo ni kitu cha furaha kubwa! Lakini tukumbuke lengo letu ni kuhamasisha Vita dhidi ya Umasikini!”
Mapato ya Mechi hiyo, kupitia Tiketi, Udhamini na Matangazo ya TV na Radio, yatagawanywa kwenye Programu mbili za kusaidia Vijana Nchini Brazil na Cape Verde, Afrika.
Mechi nyngine zilizopita, chini ya usimamizi wa UNDP na udhamini wa UEFA, zilichezwa katika Miji ya Basle, Madrid, Dusseldorf, Marseille, Malaga, Fez, Lisbon, Athens na Hamburg, na mapato yake kwenye Miradi ya kupiga Vita Umasikini sehemu mbalimbali Duniani.
VIKOSI:
RONALDO XI:
Danrlei, Dida, Cafú, Serginho, Réver, Junior Baiano, Roque Junior, Roberto Carlos, William, Lucas, Juninho Paulista, Zinho, Djalminha, Roger, Zico, Denilson, Ronaldo, Neymar, Leandro Damião, Bebeto, Cacá Ferrari, Edmundo, Paulinho.
KOCHA: Carlos Alberto Parreira

ZIDANE XI:
Vítor Baía, Juliano Belletti, Diego Cavalieri, Emerson, Fernando Hierro, Míchel Salgado, Fernando Couto, Juan Pablo Sorín, Paolo Montero, Carlos Gamarra, Hidetoshi Nakata, Zinédine Zidane, Deco, Santiago Solari, Fredrik Ljungberg, Juan Román Riquelme, Christian Karembeu, Alex de Souza, Pedro Pauleta, Sebastián Abreu, Falcão, Mário Jardel.
KOCHA: Luiz Felipe Scolari

NGOMA MPYA YA Diamond- Kesho

MECHI YA CHELSEA NA CORITHIANS KUCHEZA BILA DROGBA NDO YALIWASIBU CHELSEA EBU ANGALIA MADUDU YA TORRES NA MOSES

CHELSEA WATAMKUMBUKA SANA DIDIER DROGBA KWANI ALIKUWA NI MTU PEKEE ALIYEIWEZESHA KUTWAA KOMBE LA UEFA CHAMPIONZ SHIP KWA MARA YA KWANZA,,,EBU TUJIKUMBUSHE UMUHIMU WAKE PALE DARAJANI

LEEDS UNITED NA CHELSEA JANA KATIKA CAPITAL ONE CUP;MOSES APIGA BONGE LA GOLI NJE YA 18 INGIA ULIONEE


 

EUROPA LIGI: DROO RAUNDI YA TIMU 32 HIYOOO!

EUROPA_LIGI_CUP>>MABINGWA wa ULAYA Chelsea v SPARTA PRAGUE!!
>> ZENIT V LIVERPOOL, NEWCASTLE V METALIST KHARKIV, SPURS V LYON
DROO ya Mechi za EUROPA LIGI kwa Raundi ya Mtoano ya Timu 32 imefanyika leo huko Nyon, Uswisi na sambamba na hiyo kila Timu inajua ikifuzu Raundi hiyo na kuingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16 nani watakuwa Wapinzani.
DROO KAMILI:
RAUNDI ya MTOANO TIMU 32:
BATE Borisov v Fenerbache
Inter Milan v Cluj
Levante v Olympiakos
Zenit St Petersburg v Liverpool
Dynamo Kiev v Bordeaux
Bayer Leverkusen v Benfica
Newcastle v Metalist Kharkiv
Stuttgart v Genk
Atletico Madrid v Rubin Kazan
Ajax v Steaua Bucharest
Basel v Dnipro
Anzhi Makhachkala v Hannover
Sparta Prague v Chelsea
Borussia Monchengladbach v Lazio
Tottenham v Lyon
Napoli v Viktoria Plzen
RATIBA ya MECHI:
Mechi ya 1=14 Februari 2013
Mechi ya 1=21 Februari 2013
RAUNDI ya MTOANO TIMU 16:
Napoli au Viktoria Plzen v BATE Borisov au Fenerbache
Leverkusen au Benfica v Dynamo Kiev au Bordeaux
Anzhi Makhachkala au Hannover v Newcastle au Metalist
Stuttgart au Genk v Monchengladbach au Lazio
Tottenham au Lyon v Inter Milan au Cluj
Levante au Olympiakos v Atletico Madrid au Rubin Kazan
Basel au Dnipro v Zenit St Petersburg au Liverpool
Ajax au Steaua Bucharest v Sparta Prague au Chelsea
RATIBA ya MECHI:
Mechi ya 1=7 Machi 2013
Mechi ya 2=14 Machi 2013
+++++++++++++++++++
RATIBA HATUA YA MTOANO
RAUNDI YA TIMU 32:
Mechi ya 1=14 Februari 2013
Mechi ya 1=21 Februari 2013
RAUNDI YA TIMU 16:
Mechi ya 1=7 Machi 2013
Mechi ya 2=14 Machi 2013
ROBO FAINALI:
Mechi ya 1=4 Aprili 2013
Mechi ya 2=11 Aprili 2013
NUSU FAINALI
Mechi ya 1=25 Aprili 2013
Mechi ya 2=2 Mei 2013
FAINALI
15 Mei 2013
UWANJA wa AMSTERDAM ARENA

 

NUSU FAINALI UHAI KESHO



MECHI za Nusu fainali ya michuano ya Kombe la Uhai 2012 inayoshirikisha timu za vijana wenye umri chini ya miaka 20 za klabu za Ligi Kuu ya Vodacom zitachezwa kesho (Desemba 21 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.
Nusu fainali ya kwanza ya michuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya Said Salim Bakhresa kupitia maji Uhai itazikutanisha timu za Mtibwa Sugar ya Morogoro na Azam na itafanyika kuanzia saa 2 kamili asubuhi.
Simba na Coastal Union zitacheza nusu fainali ya pili kuanzia saa 10 kamili jioni kwenye uwanja huo huo. Mtibwa Sugar imepata tiketi ya nusu fainali baada ya kuichapa African Lyon mabao 3-1 wakati Simba iliilaza Oljoro JKT mabao 2-0.
Nayo Azam iliindoa JKT Ruvu kwenye robo fainali kwa bao 1-0 huku Coastal Union ikipata ushindi wa penalti 4-3 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye mechi ya mwisho ya robo fainali.
Mechi ya fainali na ile ya kutafuta mshindi wa tatu zitachezwa Jumapili (Desemba 23 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam. Mechi ya mshindi wa tatu itaanza saa 2 kamili asubuhi wakati ya fainali itakuwa saa 10 kamili jioni.

TFF YAWAPONGEZA ZEN C NA WENZAKE TWFA


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) linaupongeza uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Desemba 19 mwaka huu) hoteli ya Midlands mjini Morogoro.
Ushindi aliopata Lina Kessy aliyechaguliwa tena kuwa Mwenyekiti pamoja na wajumbe wengine wa Kamati ya Utendaji unaonesha jinsi ambavyo wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TWFA walivyo na imani kwao.
TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya TWFA, na kwamba ina changamoto kubwa ya kuhakikisha inaendesha shughuli za chama hicho kwa kuzingatia katiba na kanuni.
Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya TWFA chini ya Mama Ombeni Zavala na Kamati ya Uchaguzi ya TFF inayoongozwa na Deogratias Lyatto kwa kuhakikisha uchaguzi huo unafanyika kwa utulivu na kwa kuzingatia Katiba ya TWFA na Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
Safu mpya ya uongozi wa DRFA inaundwa na Lina Kessy (Mwenyekiti), Rose Kissiwa (Makamu Mwenyekiti), Amina Karuma (Katibu), Zena Chande (Mwakilishi wa Mkutano Mkuu wa TFF) wakati mjumbe wa Kamati ya Utendaji ni Triphonia Temba.

TENGA ATOA NOTISI KWA MUJIBU WA KATIBA

Tenga

RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ambaye ndiye Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho hilo tayari ametoa notisi ya mkutano huo utakaofanyika Februari 23 na 24 mwakani jijini Dar es Salaam.
Mkutano huo utafanyika Februari 23 mwakani na kufuatiwa na ajenda ya uchaguzi siku inayofuata. Ajenda ya uchaguzi iko chini ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF.
Notisi hiyo imetumwa kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu ambao ni kutoka vyama vya mpira wa miguu vya mikoa, vyama shiriki, klabu za Ligi Kuu ya Vodacom na wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF.
Ajenda za Mkutano Mkuu zitatumwa kwa wajumbe siku 15 kabla ya mkutano huo wenye wajumbe zaidi ya 100.

KIM NA WAANDISHI KESHO

Kim Poulsen
MAKOCHA wa Tanzania (Taifa Stars), Kim Poulsen na Zambia (Chipolopolo) watakuwa na mkutano na waandishi wa habari utakaofanyika kesho (Desemba 21 mwaka huu) kuzungumzia pambano lao litakalochezwa Jumamosi (Desemba 22 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mkutano huo utafanyika saa 5 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Makocha hao watazungumzia maandalizi yao ya mwisho kabla ya pambano hilo litakalochezeshwa na mwamuzi Sylvester Kirwa kuanzia saa 10 kamili jioni.
Pia makocha hao watajibu maswali kutoka kwa waandishi wa habari kuhusu pambano hilo litakalokutanisha timu hizo ambazo zimefanya vizuri kwenye orodha ya viwango vya ubora vya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) vilivyotolewa jana (Desemba 19 mwaka huu).
Wakati Zambia ambao ni mabingwa wa Afrika wamepanda juu kwa viwango vya ubora kwa nafasi nne, Taifa Stars ambayo katika mchezo uliopita iliifunga Kenya (Harambee Stars) bao 1-0 imepanda kwa nafasi nne.
Taifa Stars ambayo inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini tangu Desemba 12 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo kubwa ya kirafiki inayotarajiwa kuwa ya kuvutia.

MWINGINE AMWAGA MPUNGA MKUTANO TASWA, ITAKUWAJE SIKU HIYO?

Mhando, katibu wa TASWA
KAMPUNI ya Msama Promotions inayoandaa Tamasha la Pasaka imeahidi kutoa Sh. Milioni 1.5 kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) utakaofanyika Bagamoyo mkoani Pwani wiki ijayo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama ambaye ndiye Mkurugenzi wa kampuni hiyo amesema ushirikiano wake  na wanahabari umemsukuma kusaidia kiasi hicho cha fedha.
Msama ameahidi kuendelea kushirikiana na TASWA kadri awezavyo na kwamba mafanikio ya Tamasha la Pasaka yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na wanahabari.
“Kampuni yangu ya Msama Promotions kupitia Tamasha la Pasaka tumeamua kuungana na wanahabari katika kufanikisha mkutano wenu, tunaamini uhusiano wetu utaendelea kuwa wa kupigiwa mfano,” ilisema sehemu ya taarifa ya TASWA jana ikimkariri Msama.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa TASWA, Amir Mhando alishukuru kwa udhamini huo na kuomba wengine wenye moyo wajitokeze kuwasaidia kwani bajeti yao ni Sh. Milioni 20. Tayari kampuni ya simu za mkononi ya Zantel imeshatangaza udhamini wa Sh. Milioni sita.
Mhando alisema maandalizi ya Mkutano Mkuu wa TASWA utakaofanyika wiki ijayo Bagamoyo mkoani Pwani yanaendelea vizuri na kwamba zaidi ya wanachama 100 wa TASWA na wadau wengine wa TASWA wamethibitisha kushiriki.
Wakati huo huo: TASWA imewapongeza wanachama wake Benny Kisaka na Zena Chande kwa kufanikiwa kuwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Kisaka alishinda wadhida huo wiki iliyopita kupitia uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), wakati Chande alishika Jumatano katika uchaguzi wa Chama cha Mpira wa Miguu Wanawake Tanzania (TWFA).
“Tunaamini wajumbe wa Mkutano Mkuu DRFA na wale wa TWFA hawakufanya makosa, wamefanya uamuzi sahihi na wamepata watu sahihi na makini na michango yao itakuwa yenye tija kubwa kwa maendeleo la mpira wa miguu hapa nchini. Tunawatakia kila la heri wanachama wetu hao katika changamoto mbalimbali watakazokutana nazo kwenye nafasi zao hizo walizopata,”amesema Amir Mhando, Katibu Mkuu TASWA.

MESSI CHALI TUZO YA MWANASOKA BORA

ULIZA kikundi cha watu ni mtu gani wanaamini kuwa ndiye mwanamichezo bora duniani, jina la Lionel Messi ndilo utakalolisikia mara nyingi.
Isipokuwa kikundi hicho kikiwa kinaundwa na waandishi wa habari wa Argentina,ambao hawaoni kama Messi ni bora hata kwa nchini mwao tu. Wala nafasi ya piliwanaona hashiki.Ila ni nafasi ya tatu aliyoshika nyota huyo wa Barcelona nyuma ya bondia Sergio Martinez na mpiganaji wa taekwondo, Sebastian Crismanich. 

Pretty good year: Sergio Martinez with his trophy after beating Sebastian Chrismanich and Lionel Messi to the award
Sergio Martinez akiwa na tuzo yake baada ya kumshinda Sebastian Chrismanich na Lionel Messi 
Ready for it: Martinez will fight British boxer Martin Murray in April 2013
Niko tayari: Martinez atapambana na bondia wa Uingereza Martin Murray Aprili 2013

Mafanikio bab'kubwa aliyonayo Messi mwaka huu ya kuvunja rekodi iliyodumu kwa miaka 40 bada ya kufunga magoli 90 hadi sasa haikutosha kumpa tuzo hiyo.Martinez alishinda taji la Olimpia de Oro baada ya kumchapa  Mmexico Julio Cesar Chavez Jr katika taji la ubingwa wa WBC mapema mwaka huu. Atapigana na bondia  Muingereza Martin Murray Aprili 2013.

What, not me? Lionel Messi finished third in the poll of Argentine journalists
What, not me? Lionel Messi amemaliza wa tatu katika tuzo ya waandishi wa habari ya mwanamichezo bora wa Argentina.

Crismanich, yeye, alikuwa mtu pekee wa Argentina aliyeshinda medali ya dhahabu katika michezo ya Olimpiki ya London 2012."Ni heshima kubwa kushinda tuzo hii ambayo ilikuwa ikiwaniwa na wanamichezo kama Sebastian Crismanich na Leo Messi," Martinez alisema katika sherehe ya tuzo hizo Jumanne usiku.
Lakini kwa kuwa alishashinda tuzo hiyo ya Argentina mwaka 2011 na kwa kuwa anapewa nafasi kubwa zaidi ya kubeba kwa mara ya nne mfululizo tuzo ya Ballon d'Or ya Mwanasoka Bora wa Dunia 2012, Messi hawezi kuwa amefadhaishwa sana.