Friday, October 5, 2012

AC Milan yabembeleza Mashabiki kuona Dabi na Inter ndani ya San Siro


 
SAN_SIROAC_MILAN_MONTOLIVOIngawa Dabi ya Jiji la Milano ni moja ya Dabi kubwa Barani Ulaya lakini Mechi hiyo ya Wikiendi hii imechukua hatua mpya pale Klabu ya AC Milan kuwabembeleza Mashabiki wake kuhudhuria pambano hilo na Mahasimu wao Inter Milan litakalochezwa ndani ya Uwanja wa San Siro.
AC Milan wanaingia kwenye Dabi hii wakiwa nafasi ya 11 wakiwa na Pointi 7 zikiwa ni Pointi 5 nyuma ya Inter Milan, ambao wako nafasi ya 3, na Pointi 9 nyuma ya vinara Juventus.


Huku wakiwa wameondokewa na Wachezaji wao nyota, Zlatan Ibrahimovic na Thiago Silva, waliouzwa kwa Paris Saint-Germain, Mashabiki wa AC Milan wamekuwa wakisusa Mechi za Klabu yao.


Mpaka jana Jumatano ni Tiketi 55,000 tu zimeuzwa kwa ajili ya Dabi hiyo itakayochezwa Jumapili na miongoni mwa hizo ni Tiketi 23700 za wale Washabiki wanaokata Tiketi za Msimu mzima wakati Uwanja wa San Siro hupakia Watu 80,018.


Wiki iliyopita, kwenye Mechi ya kwanza waliyoshinda nyumbani, Watu 28,000 tu walihudhuria kushuhudia AC Milan ikiifunga Cagiari 2-0.


Msimu uliopita Mashabiki 79,612 walishuhudia Inter Milan ikiifunga AC Milan 1-0 kwa bao la Diego Milito na Mwaka juzi, Watu 80,000 walikuwepo AC Milan ilipoitwanga Inter Milan bao 3-0.


Uhafifu wa mahudhurio umeifanya AC Milan iweke Video kwenye Tovuti yake ambayo Nahodha Massimo Ambrosini na Straika Stephan El Shaarawy wanawabembeleza Mashabiki wao na kuwaambia: “Dabi bila nyie haina maana yeyote!”


Juzi, AC Milan walipata ushindi mtamu wa ugenini kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI walipoichapa Zenit St Petersburg bao 3-2.


Nae Meneja wa AC Milan, Massimiliano Allegri, ambae amekuwa akisakamwa kwa mwendo mbovu, amedai: “Ni Magazeti ndio yanyodai tupo hali mbaya. Tunaingia kwenye Dabi tukitoka kwenye ushindi mzuri…ingawa tunajua Dabi siku zote zina maajabu!”


RATIBA=Serie A
[SAA za Bongo]
Jumamosi Oktoba 6
19:00 Chievo Verona v Sampdoria
21:45 Genoa v Palermo


Jumapili Oktoba 7
13:30 AS Roma v Atalanta
16:00 Torino FC v Cagliari
16:00 Siena v Juventus
16:00 Pescara v SS Lazio
16:00 Catania v Parma
16:00 Fiorentina v Bologna
21:45 AC Milan v Inter Milan
21:45 Napoli v Udinese


Jumamosi Oktoba 20
19:00 Juventus v Napoli
21:45 SS Lazio v AC Milan

EUROPA LIGI: Liverpool 2 Udinese 3, Newcastle 3 Bordeaux 0, Panathinaikos 1 Spurs 1!

Ijumaa, 05 Oktoba 2012 07:00
   
>>MABINGWA Atletico Madrid 1 Viktoria Plzen 0!!
EUROPA_LIGI_CUPEUROPA LIGI jana Usiku iliendelea na Mechi Dei 2 kwa Mechi za pili katika hatua ya Makundi na Mabingwa watetezi Atletico Madrid kuendeleza ushindi kwa kuifunga FC Viktoria Plzen 1-0 huku Liverpool wakichapwa Uwanani kwao Anfield bao 3-2 na Udinese, Newcastle wakiichapa Bordeaux 3-0 na Spurs kutoka sare 1-1 na Panathinaikos.


MATOKEO=MECHI DEI 2
Oktoba 4
Club Atlético de Madrid 1 FC Viktoria Plzen 0
FC Anzhi Makhachkala 2 BSC Young Boys 0
Liverpool FC 2 Udinese Calcio 3
A. Académica de Coimbra 1 Hapoel Tel-Aviv FC 1
Olympique de Marseille 5 AEL Limassol FC 1
VfL Borussia Mönchengladbach 2 Fenerbahçe SK 4
Club Brugge KV 2 CS Marítimo 0
Newcastle United FC 3 FC Girondins de Bordeaux 0
Molde FK 2 VfB Stuttgart 0
FC Steaua Bucuresti 1 FC København 0
AIK 2 FC Dnipro Dnipropetrovsk 3
PSV Eindhoven 3 SSC Napoli 0
FC Basel 1893 2 KRC Genk 2
Videoton FC 3 Sporting Clube de Portugal 0
Neftçi PFK 1 Inter Milan 3
FC Rubin Kazan 2 FK Partizan 0
Hapoel Kiryat Shmona 3 Olympique Lyonnais 4
AC Sparta Prague 3 Athletic Bilbao 1
S.S. Lazio 1 NK Maribor 0
Panathinaikos FC 1 Tottenham Hotspur 1
FC Metalist Kharkiv 2 SK Rapid Wien 0
Rosenborg BK 0 Bayer 04 Leverkusen 1
Hannover 96 2 Levante UD 1
Helsingborgs IF 2 FC Twente 2


MATOKEO:
Septemba 20
BSC Young Boys 3 Liverpool FC 5
Udinese Calcio 1 FC Anzhi Makhachkala 1
Hapoel Tel-Aviv FC 0 Club Atlético de Madrid 3
FC Viktoria Plzen 3 Académica de Coimbra 1
AEL Limassol FC 0 VfL Borussia Mönchengladbach 0
Fenerbahçe SK 2 Olympique de Marseille 2
CS Marítimo 0 Newcastle United FC 0
FC Girondins de Bordeaux 4 Club Brugge KV 0
VfB Stuttgart 2 FC Steaua Bucuresti 2
FC København 2 Molde FK 1
FC Dnipro Dnipropetrovsk 2 PSV Eindhoven 0
SSC Napoli 4 AIK 0
KRC Genk 3 Videoton FC 0
Sporting Clube de Portugal 0 FC Basel 1893 0
FC Internazionale Milano 2 FC Rubin Kazan 2
FK Partizan 0 Neftçi PFK 0
Olympique Lyonnais 2 AC Sparta Praha 1
Athletic Club 1 Hapoel Kiryat Shmona FC 1
NK Maribor 3 Panathinaikos FC 0
Tottenham Hotspur FC 0 S.S. Lazio 0
SK Rapid Wien 1 Rosenborg BK 2
Bayer 04 Leverkusen 0 FC Metalist Kharkiv 0
Levante UD 1 Helsingborgs IF 0
FC Twente 2 Hannover 2

NGASSA AANZA 'KUNUKA' SIMBA, ADAIWA KUCHEZA KINAZI JUZI, KAZIMOTO, BOBAN NAO NDANI, KAPOMBE AZAWADIWA MAMILIONI

Mrisho Ngassa


MRISHO Khalfan Ngassa, kiungo mpya wa Simba aliyesajiliwa baada ya ‘kufukuzwa’ Azam FC kwa kosa la kubusu jezi ya Yanga ni miongoni mwa wachezaji wanaotuhumiwa kucheza chini ya viwango vyao katika mechi ya juzi dhidi ya mahasimu wao wa jadi, Yanga SC, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati beki Shomary Kapombe atazawadiwa Sh Milioni 2 ‘kwa kujituma ile mbaya’ kwenye mechi hiyo.
 
 
Simba ilifanya kikao jana kupitia mechi ya juzi na kuwatenganisha wachezaji katika makundi mawili, waliojituma na ambao hawakujituma kabisa na huko kiungo iliyemsajiki kwa mkopo kutoka Azam, Ngassa ndiye kinara.
 
 
Katika kundi la Ngassa wamo pia Haruna Moshi ‘Boban’, Mwinyi Kazimoto na Daniel Akuffo, wakati upande wa waliopiga ‘mzigo wa uhakika’, mbali na Kapombe, wengine ni Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Paul Ngalema, Juma Nyosso, Jonas Mkude, Amri Kiemba, Felix Sunzu na Edward Christopher, ambao pia watazawadiwa.
 
 
Chanzo chetu kutoka Simba kimesema kwamba hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya wachezaji wote ambao hawakujituma kwenye mechi hiyo, lakini si kusimamishwa wala kufukuzwa, bali kukatwa mishahara. 
 
 
“Kocha amekataa adhabu ya kufukuza mchezaji, watakatwa mishahara, ila sijui uongozi wenyewe utaenda mbali kiasi gani,”kilisema chanzo hicho.
 
 
Aidha, beki Amir Maftah na mshambuliaji Emmanuel Okwi pia nao wanaingia kwenye orodha ya wachezaji ambao hawakuwa na nia nzuri na mechi hiyo kutokana na kupewa kadi nyekundu zilizowafanya waikose mechi hiyo. “
 
Hawa wote walikuwa wana uwezo wa kuepuka zile kadi, lakini haikuwa hivyo, sasa nao uongozi unalifanyia kazi suala lao, huenda nao wakakumbwa na adhabu ya kukatwa mishahara,”kilisema chanzo hicho.
 
 
Kikao kingine kinatarajiwa kufanyika leo baina ya benchi la Ufundi na Kamati ya Ufundi na baada ya hapo hatua rasmi dhidi ya wachezaji hao zitajulikana.
 
 
Simba itafanya mazoezi leo kwenye Uwanja wa Kinesi, Urafiki, Dar es Salaam kuanzia saa 10:30 na baada ya hapo wachezaji wataingia kambini kwa ajili ya mechi ya Jumapili dhidi ya JKT Oljoro, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
 
Simba juzi ilishindwa kuendeleza ubabe wake kwa Yanga, baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na wapinzani wao hao wa jadi, katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, uliopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kuanzia saa 1:02 usiku.
 
 
Yanga ambao walimaliza mechi hiyo wakiwa pungufu baada ya Simon Msuva kutolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 77 kwa kumrudishia rafu Juma Nyosso, ndio waliohaha kusawazisha bao, baada ya kutanguliwa kwa bao la mapema la kiungo Amri Kiemba.  
 
 
Hadi mapumziko Simba walikuwa tayari mbele kwa bao 1-0, lililotiwa kimiani na kiungo Amri Kiemba dakika ya pili.
 
 
Simba walicheza vizuri kipindi chote cha kwanza wakigongeana pasi za uhakika na kuwazidi kasi uwanjani wapinzani wao, wakati Yanga pamoja na kuzinduka baada ya kufungwa bao, lakini makosa yalikuwa mengi.
 
 
Pasi zao zilikuwa nyingi hazifiki, walikuwa wanapokonyeka mipira kirahisi, wanazidiwa nguvu na wapinzani wao katika kugombea mipira na hata mashambulizi yao hayakuwa ya mpangilio, zaidi ya kuonekana kubahatisha zaidi.
Katika kubahatisha huko, Mbuyu Twite alifumua shuti zuri dakika ya 38 kutoka wingi ya kulia, ambalo lilitoka nje sentimita chache.    
 
 
Kabla hata ya dakika 45 za kipindi cha kwanza kumalizika, kocha Mholanzi Ernie Brandts alimtoa Hamisi Kiiza na kumuingiza Frank Domayo ili kuimarisha safu ya kiungo, ambayo ilionekana kuzidiwa na Simba inayofundishwa na Mserbia, Milovan Cirkovick.
 
 
Kipindi cha pili, Yanga walianza na mabadiliko, kocha Ernie Brandts akimtoa kiungo Nizar Khalfan na kumuingiza mshambuliaji Didier Kavumbangu, ambaye alikwenda kuongeza nguvu ya safu ya ushambuliaji ya timu hiyo.
Angalau, kipindi cha pili Yanga walionekana kucheza vizuri na kupeleka mashambulizi yenye uhai langoni mwa Simba, ingawa safu imara ya ulinzi ya Wekundu wa Msimbazi ilikuwa kikwazo.
 
 
Katika dakika ya 63, beki Paul Ngalema aliunawa mpira katika harakati za kuokoa na refa Mathew Akrama akaamuru penalti, ambayo ilikwamisha kimiani kiufundi na Said Bahanuzi ‘Spider Man’.
 
 
Katika dakika ya 77 Mathew Amkrama alimtoa nje kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja Simon Msuva, baada ya kumkita Juma Nyosso, aliyemkanyaga ‘kwa bahati mbaya’. Msuva alichezewa rafu na Nyosso na tayari refa alikwishapuliza filimbi na kumpa kadi ya njano beki huyo wa Simba, lakini kiungo huyo wa Yanga akaponzwa na hasira za kitoto.
 
 
Pamoja na Yanga kubaki pungufu, waliendelea kucheza vema na mashambulizi yalikuwa ya pande zote mbili. Refa Akrama alishindwa kuumudu mchezo na maamuzi yake mengi yalikuwa chungu kwa Yanga, mfano Haruna Moshi ‘Boban’ alipomchezea rafu mbaya beki Kevin Yondan hadi akashindwa kuendelea na mchezo, na nafasi yake ikachukuliwa na Juma Abdul alimpoza kwa kadi ya njano.
Hakumchukulia hatua yoyote kipa Juma Kaseja aliyeonekana kupoteza muda tangu mwanzo, na alimpa onyo tu zaidi ya mara tatu.
 
 
Alipongia Abdul alikwenda kucheza beki ya kulia na Mbuyu Twite akahamia katikati kucheza na Nadir Haroub ‘Cannavaro’.
 
 
Baada ya mchezo huo, kocha wa Simba, Milovan alisema kwamba ulikuwa mchezo mzuri na Yanga walicheza vizuri, lakini timu yake ilicheza vizuri na anajivunia. Alisema Yanga imeimarika tofauti na ilivyokuwa awali na kwamba hizo ni dalili Ligi Kuu msimu huu itakuwa ngumu.
 
 
Kwa upande wake, kocha wa Yanga, mwanzoni hawakucheza vizuri, lakini baadaye walitulia na kucheza vizuri. “Hii ni mechi ya kweli ya upinzani, unaweza kuona rafu na kadi nyingi,”alisema Brandts.