Monday, December 31, 2012

MATUKIO YA MWAKA 2012 NAMALIZIA KUKUPA TUKIO HILI LA SIMBA KUIFUNGA YANGA BAO 5-0,,,,,GOLI LA TANO LIKIFUNGWA NA MAREHEMU PATRICK MUTESA MAFISANGO INGIA UONE

UHAMISHO WA JANUARI ULAYA NDIO HUO SASA UMEWADIA. NANI ANAKWENDA WAPI NA NANI MWENYE KISU KIKALI. SNEIJDER, BEMBA BA, THEO WALCOTT, DAVID VILLA, MOROUANE FELLAINI, BALOTELLI, ZAHA, BENAT NA GOMIS WOTE SAFARINI.


Inavyo onekana mara baada ya dirisha dogo la usajili la mwezi Januari 2013 kufunguliwa mwezi January, hakutakuwa na uhaba wa upatikanaji wa vipaji.

Mwezi January sasa umefika ambapo dirisha dogo la usajili litakuwa likifunguliwa tena barani ulaya.  Kumekuwepo na majina mengi makubwa ambayo yamekuwa yakihusishwa na kutaka kuhama kutoka upande mmoja kuelekea upande mwingine, ambapo vilabu vikubwa katika bara hilo la Ulaya navyo vikihaha kusaka vipaji vipya.

Kwa msaada wa mtandao wa Goal.com hebu tuangalie majina hayo yanayotajwa kuwa huenda wakahama kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine mwezi huu wa January.

Wesley Sneijder, Inter
 Kiungo mchezeshaji huyo raia wa Uholanzi amekuwa hana nafasi tena katika kikosi cha kwanza San Siro. Sneijder ametamka waziwazi kuwa itakuwa vema kwake kama ataondoka katika klabu yake katika dirisha hili la usajili, kiasi kuviweka vilabu vikubwa barani humo kukaa mkao wa kumsubiri.

Taarifa za awali zinasema kuwa Sneijde ameshakubaliana katika mambo fulani ya msingi na klabu ya Tottenham na kwamba mpango huo umefikia hatua nzuri ambapo pia kuna vilabu kadhaa vya ligi kuu ya England vikimtamani kama vile Manchester City, Liverpool na Manchester United.

Pia Anzhi Makhachkala ya Russia pia iko katika mpango huo.

Demba Ba, Newcastle
 Mshambuliaji huyu ni raia wa Senegal ambaye amekuwa mfungaji mkubwa wa Newcastle, akiifungia magoli 29 katika jumla ya michezo 54 aliyocheza klabu hiyo.

Ba, amevutia vilabu vingi vikubwa ambapo Chelsea na Arsenal ni vilabu ambavyo kuna tetesi zinasema wanamtaka Ba mwenye umri wa miaka 27,

Kuondoka kwake kunaweza kumfanya meneja Alan Pardew kuwasajili Mathieu Debuchy na Loic Remy.


Theo Walcott, Arsenal
 Kwa hali ya mambo ilivyo ni kwamba mkataba wa Theo Walcott katika klabu yake ya Arsenal uko katika hali ya sintofahamu ambapo kwa kwasasa umekuwa unaangaliwa na vilabu vingi vikubwa barani Ulaya wakisubiri majaaliwa yake.

Wakati mkataba huo ukitarajiwa kumalizika mwisho wa msimu huu, vilabu mbalimbali sasa vimekodoa macho wakirubiri hatma yake mwezi January.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa England mwishoni mwa juma alipiga bao tatu “hat trick” katika mchezo dhidi ya Newcastle ambayo kwa kweli imeongeza thamani yake katika mpango wake ujao usajili wa nyongeza kama washika mitutu watashawishika kumsajili tena Walcott na kwa vyovyote vile itakuwa ni busara kumsajili tena kuliko kumuacha akiondoka kama mchezaji huru majira ya kiangazi.

Kuna tetesi kuwa Chelsea na Manchester United wanamtaka nyota wa England, wakati ambapo Juventus na Paris Saint-Germain wakiwa mbioni kumnasa.

David Villa, Barcelona.
 Kama ilivyo kwa Sneijder, Villa pia ni jina kubwa ambaye amekosa nafasi ya kikosi cha kwanza katika klabu yake ya Barcelona lakini akionekana kuwa kivutio katika klabu kubwa za ligi kuu ya England “Premier League”

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 amekuwa katika kikosi kilicho anza cha Barcelona katika michezo 6 tu kati ya michezo 17 ambayo Barcelona imecheza ya ligi kuu ya Hispania ‘La Liga’ msimu huu ambapo sasa ameondoshwa rasmi katika orodha ya wachezaji wa kikosi cha kwanza moja kwa moja.

Meneja wa Chelsea Rafa Benitez inasemekana anataka kuwaunganisha wachezaji watatu wa timu ya taifa ya Hispania,Villa,Fernando Torres na Juan Mata katika kikosi chake, lakini Liverpool na Arsenal huenda wakaingia vitani kutaka saini yake. Pia huenda El Guaje akasalia Camp Nou kupigania nafasi msimu huu na kusubiri uhamisho wa majira ya kiangazi.


Marouane Fellaini, Everton

Nyota huyu raia wa Belgian alikuwa ni miongoni mwa wachezaji waliofanya vizuri msimu huu katika ligi kuu ya soka nchini England ‘Premier League’ anasifika kwa kipaji, akili na hata umbile la kisoka ikiwa ni pamoja na uwezo wa kumaliza mipira ya mwisho akitoa msaada mkubwa katika sehemu ya kiungo ya Everton maarufu  “Toffee”.

Fellaini alisaini mkataba wa miaka mitano mwaka uliopita lakini inasemekana anataka kuondoka Goodison Park, ambapo vilabu mbalimbali vikiwa vinataka huduma yake.

Real Madrid ni moja kati ya klabu kubwa inayo muawania mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye anasubiri kuona kama Everton itafuzu klabu bingwa Ulaya msimu huu na kuamua hatma yake.

 

Mario Balotelli, Manchester City
 Baada ya kuwepo taarifa kwa muda mrefu kuwa huenda akaondoka katika klabu yake ya Manchester City, Super Mario Balotelli huenda akatimiza azma hiyo hivi karibuni  baada ya dirisha kufunguliwa.

Akiwa amefunga goli moja msimu huu, mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 22 uwanjani ameonekana kutokuwa na thamani hususani kutokana na kuzongwa na matatizo mengi ya nje ya uwanja.

Itategemea na taarifa ipi utakayo amini juu ya habari za Balotteli lakini ukweli ni kwamba meneja Roberto Mancini huenda akamuondosha kikosini ama akampa nafasi ya mwisho kutegemeana na vile anaona inafa.

Kutokana pia na City kuwa na azina kubwa ya washambuliaji, City huenda ikalazimika kukubali taarifa za tetezi kwamba Milan ilikuwa ikimtaka kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni could be forced to accept a rumored 20.


 

Wilfried Zaha, Crystal Palace
 Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 20 amekuwa akivutia na kusisimua sana katika timu inayoshiriki ligi ndogo ya pili kwa ukubwa nchini England(Championship) ya Crystal Palace.

 Ana mambo mengi yan kuvutia ikiwemo nguvu na kipaji kiasi kupelekea kuitwa katika kikosi cha hivi karibuni cha timu ya taifa England.

Zaha ameonyesha wazi kutaka kuihama klabu yake mwezi januari ambapo tayari kuna klabu kama Liverpool, Arsenal, Manchester United, Tottenham, Chelsea na hata Real Madrid zikiwa zinamnyemelea na inaonekana wazi Palace haina ubavu wa kumzuia kiungo waliomsajili kwa pauni milioni 15.


Benat Etxeberria, Real Betis
 Kiungo huyu ana umri wa miaka 25 raia wa hispania amekuwa anacheza soka la kupendeza katika klabu ya Betis na kumekuwepo na taarifa za uwezekano mkubwa wa kuihama klabu yake mwezi huu wa januari dirisha litakapo funguliw.

Kiungo huyo wa zamani wa Bilbao hivi karibuni aliitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Hispania na kuna taarifa kuwa amekuwa akitakiwa na Barcelona.

Spartak Moscow na Wolfsburg pia zimetajwa kumuhitaji kama ilivyo kwa vilabu vya England ambavyo ni Tottenham, Liverpool Arsenal.


Bafetimbi Gomis, Lyon.
 Nyota wa kimataifa wa Ufaransa amekuwa katika kiwango kizuri katika msimu huu akiifungia magoli 11 katika ligi kikosi cha Les Gones. Kwasasa klabu yake ya Lyon ya nchini Ufaransa imefulia kiunchumi na inalazimika kumuuza mlinda mlango wake nyota Hugo Lloris kwenda Tottenham majira ya kiangazi.

Gomis mwenye umri wa miaka 27 huenda akajiunga na Chelsea na Liverpool ambao wote wako mawindoni kumsaka mshambuliaji huyo aliyethaminishwa kwa pauni milioni 15.

UHAMISHO: CHELSEA KUNASA KADHAA LAKINI BA…??

>>STURRIDGE KUTUA LIVERPOOL??
>>NEWCASTLE YAMPATA BEKI WA KIMATAIFA WA FRANCE!!
BENITEZ-CHELSEAULE mpango wa Demba Ba kuhamia Chelsea unaelekea umekwama baada ya kuibuka tetesi kuwa Wawakilishi wa Mchezaji huyo wa Newcastle hawakufikia makubaliano na Chelsea lakini zipo ripoti nyingine kuwa Chelsea wako mbioni kuwanasa Kiungo wa Metalist Kharkiv, Taison, na Mchezaji wa Corinthians Paulinho.DEMBA_BA
Chelsea walikuwa na nia ya kumnunua Demba Ba ili awe anatoa sapoti kwa Straika wao Fernando Torres baada ya kukosa kumchukua Radamel Falcao wa Atletico Madrid katika Dirisha la Uhamisho la Januari baada ya Klabu hiyo ya Spain kung’ang’ania kuwa hawezi kuhama sasa labda mwishoni mwa Msimu.
Kuhusu Demba Ba, kikwazo kikubwa ni kuwa Meneja wa Newcastle, Alan Pardew, hapendezewi kumuuza Straika ambae amefunga Bao 13 kwenye Ligi na pia Mkataba wa Mchezaji huyo una kipengele kuwa Uhamisho wowote ule lazima uambatane na Malipo ya Pauni Milioni 7.5.
Na habari toka ndani ya Klabu ya Chelsea zimedokeza kuwa Liverpool watailipa Chelsea Pauni Milioni 12 ili kumnunua Daniel Sturridge ambae imeripotiwa alishapimwa afya yake huko Liverpool na Uhamisho rasmi unasubiri Januari 1 wakati Dirisha la Uhamisho litakapofunguliwa.
Nae Meneja wa muda wa Chelsea Rafa Benitez amekataa kuzungumza lolote kuhusu Ba pale aliposema: “Hatuzungumzii shughuli zetu hadharani. Yeye ni Mchezaji wa Klabu nyingine na huwa siongelei Wachezaji wengine!”
NEWCASTLE KUMSAINI MATHIEU DEBUCHY TOKA LILLE
Newcastle imefikia makubaliano kumsaini Beki wa Kimataifa wa France, Mathieu Debuchy, kutoka Klabu ya Ufaransa, Lille.
Beki huyo wa kulia mwenye Miaka 27 alichezea Mechi zote 4 za France kwenye EURO 2012 na inasadikiwa Ada yake ya Uhamisho ni Pauni Milioni 5.
Debuchy anakuwa Mchezaji wa pili kusainiwa na Newcastle kutoka Lille hivi karibuni baada ya Klabu hiyo pia kumchukua Kiungo Yohan Cabaye Juni 2011.

PATRICK LIEWING MFARANSA MPYA WA SIMBA ATUA SIMBA MCHANA WA LEO TU


Katibu wa Simba, Evodius Mtawala (kushoto) akiongozana na kocha mpya wa klabu hiyo, Patrcik Liewig baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam mchana huu. 

Mtawala na Liewig

Liewig, Mwenyekiti mpya wa Kamati ya Ufundi, Dani Manembe na Mtawala

Anazungumza na Waandishi

Anapanda kibasi

Ndani ya kibasi

Wanachama waliokuja kumlaki

SEKIETE APORWA MAMILIONI YA SIMBA JUZI KATIKA MGAWO WA MECHI YA SIMBA NA TUSKER

Zaidi ya Sh. milioni 10 za klabu ya Simba zimeporwa baada ya Mhasibu wa klabu hiyo, Erick Sekiete (28) kudai kuvamiwa na majambazi sita katika mtaa wa Sinza kwa Remmy na kuporwa kiasi hicho cha pesa juzi saa 3:20 usiku.

  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela amesema kuwa Sh. milioni 7.59 na dola za Marekani 2,000 ambazo Simba walizipata baada ya makato ya mapato ya mechi yao dhidi ya Tusker FC ya Kenya iliyomalizika kwa wenyeji Simba kuchapwa 3-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

“Simba ilipata mgawo wa Sh. milioni 10.6 na dola za Marekani 2,000 (Sh. milioni tatu) kutokana na mapato ya kiingilio cha mechi yao dhidi ya Tusker. Baada ya makato, walibakiwa na Sh. milioni 7.59 ambazo Sekiete alikabidhiwa,” alisema Kamanda Kenyela.

 Amesema kuwa baada ya kukabidhiwa fedha hizo, Sekiete na mwenzake Stanley Phillipo (23) ambaye alidaiwa kuwa ni mwanafunzi, walipanda kwenye gari aina ya Toyota Premio yenye namba za usajili T869 BKS lililokuwa likiendeshwa na Said Pamba na kwamba walipofika eneo hilo, dereva aliwashusha na kwamba wakaanza kutafuta teksi.

Aliendelea kueleza kuwa muda mfupi baada ya kushushwa, Sekiete na Philipo waliamua kuvuka upande wa pili wa barabara iendayo Kijitonyama ili wachukue teksi lakini ghafla walitekwa na watu sita walioshuka kutoka kwenye pikipiki tatu.

“Mmoja wa watu walioshuka kwenye pikipiki alikuwa na bastola na alifyatua risasi hewani wakati wenzake wakipora begi lenye fedha kutoka kwa mhasibu,” alisema Kenyela.

Aliendelea kufafanua kuwa wakati watu hao wakimnyang’anya begi Sekiete walikuwa wakitamka maneno ya kejeli kwa uongozi wa Simba.

Aliyanukuu maneno hayo kwa kusema; “Mnafungwa halafu mnazingua, na kwa kuwa viongozi wenu wanakula pesa za klabu, nasi hizi tunaziiba.”

Kamanda Kenyela alisema kuwa baada ya watu hao kupora fedha hizo, walitokomea kusikojulikana na hadi sasa, Jeshi la Polisi linawashikilia watu watatu akiwamo Sekiete kuhusiana na tukio hilo.

Watu wengine wanaoshikiliwa na jeshi hilo katika Kituo cha Polisi Magomeni ni Pamba na Philipo ambao walikuwa pamoja na Sekiete kwenye gari.

“Sisi (Jeshi la Polisi) tulishaonya watu kusafirisha kiasi kikubwa cha fedha bila ulinzi, tunawashikilia watu hawa watatu kwa sababu huenda walipanga kuiba fedha hizo,” aliongeza.

“Mazingira ya kuporwa kwa fedha hizo yanatia shaka huenda kuna kitu kilikuwa kimepangwa ili fedha hizo ziibwe. Iweje mtu akahifadhi nyumbani kwake kiasi kikubwa cha fedha kama hicho?” alihoji Kamanda Kenyela.

“Kwa sasa mtu yeyote atakayeripoti kuporwa fedha kiasi kikubwa kama hiki na alikuwa akisafirisha pasipo na ulinzi, tutaanza naye.

“Tunawashikilia watatu kwa uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo. Tunaomba ushirikiano kuto
ka watu wenye taarifa juu ya waliohusika na tukio hili.”

Mwenyekiti wa Simba, Aden Rage aliliambia gazeti hili jana kuwa amesikitishwa na taarifa za kuporwa kwa fedha za klabu yao.

“Mhasibu wetu anaishi Sinza. Alizichukua zile fedha za klabu akazihifadhi nyumbani kwake ili leo (jana) azipeleke benki,” alisema Rage.

AFCON 2013: IVORY COAST YATAJA 23, DROGBA, YAYA, GERVINHO NDANI!


AFCON_2013_LOGOKOCHA wa Ivory Coast, Sabri Lamouchi, ametangaza Kikosi chake cha Wachezaji 23 kwa ajili ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2013 yatakayochezwa Nchini Afrika Kusini kuanzia Januari 19 hadi Februari 10 na Kikosi hicho kimesheheni Majina makubwa katika Soka wakiwemo Yaya Toure, Mchezaji Bora Afrika, na Straika hatari Didier Drogba.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
AFCON 2013
MAKUNDI:
KUNDI A: South Africa, Cape Verde, Morocco, Angola
KUNDI B: Ghana, DR Congo, Niger, Mali
KUNDI C: Zambia, Ethiopia, Nigeria, Burkina Faso
KUNDI D: Ivory Coast, Togo, Tunisia, Algeria
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
KIKOSI KAMILI:
MAKIPA: Copa Barry (Lokeren/Belgium), Daniel Yeboah (Hana Klabu), Badara Sangaré (Sewe San Pedro)
MABEKI: Abib Kolo Touré (Manchester City/England), Souleyman Bamba (Trabzonspor/Turkey), Emmanuel Eboué (Galatasaray/Turkey), Siaka Tiéné (PSG/France), Arthur Boka (Stuttgart/Germany), Ismaël Traoré (Brest/France), Igor Lolo (FC Kuban/Russia)
VIUNGO: Didier Zokora (Trabzonspor/Turkey), Cheik Tioté (Newcastle/England), Yaya Gnégnéri Touré (Manchester City/England), Max Gradel (Saint-Etienne/France), Romaric N'Dri (Saragosse/Spain), Abdul Razak (Manchester City/England), Didier Ya Konan (Hanovre/Germany)
WASHAMBULIAJI: Salomon Kalou (Lille/France), Gervinho (Arsenal/England), Didier Drogba (Shanghaï Shenhua/China), Wilfried Bony (Vitesse Arnhem/Netherlands), Lacina Traoré (Anzhi Makhachkala/Russia), Arouna Koné (Wigan/England)

CHELSEA NA EVERTON JANA TAREHE 30/12/2012 WALIUAGA MWAKA WA 2012 KWA MECHI YA UGENINI KW AKUPIGISHWA KWATA NA HWA JAMAAA==WANAJUA WASHIKAJI

MESSI W ALIVERPOOL SUAREZ AIPIGIA BAO MBILI TIMU YAKE IKIIUA QPR 3 BILA


Bao 3 ndani ya Dakika 28 za kwanza leo zimewapa Liverpool, waliocheza bila Meneja wao Brendan Rodgers ambae ni mgonjwa, ushindi wa 3-0 na kuzidi kuwadidimiza mkiani mwa Ligi Kuu England QPR huku Liverpool wakipanda nafasi moja na kumaliza Mwaka 2012 wakiwa nafasi ya 9.
Ushindi wa Liverpool ulipatikana kwa Bao za Luis Suarez, Bao 2, na Daniel Agger.
VIKOSI:
QPR: Julio Cesar, Onuoha, Nelsen, Hill, Traore, Mackie, Diakite, Mbia, Wright-Phillips, Taarabt, Cisse
Akiba: Green, Derry, Ferdinand, Granero, Da Silva, Hoilett, Faurlin.
Liverpool: Reina, Johnson, Skrtel, Agger, Jose Enrique, Allen, Henderson, Downing, Gerrard, Sterling, Suarez
Akiba: Gulacsi, Assaidi, Coates, Lucas, Carragher, Fernandez Saez, Shelvey.
Refa: Anthony Taylor

BPL: MECHI ZA KUANZA 2013 ni JUMANNE JANUARI 1!

BPL_LOGO>>ARSENAL KUCHEZA KIPORO NA WEST HAM JANUARI 23!!
BPL, Barclays Premier League, itafungua Mwaka mpya 2013 kwa Mechi 7 Jumanne Januari Mosi na Mechi 3 Jumatano Januari 2 huku Mabingwa watetezi Manchester City, ambao wako nafasi ya pili, kucheza nyumbani na Stoke City na Vinara wa Ligi, Manchester United, kuwa ugenini kuivaa Wigan.
Mechi za Ligi Kuu England kwa Mwezi Januari zitakuwa zikipisha Mechi za FA CUP kwa Wikiendi ya kuanzia Januari 5 ambapo Raundi ya 3 ya FA CUP itachezwa, Raundi ambayo Timu za Ligi Kuu England ndipo zinaanza Mashindano hayo na pia Wikiendi ya Januari 26 ambapo Raundi ya 4 ya FA CUP itachezwa.
+++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Brom v Fulham
[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke City
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Southampton v Arsenal
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
+++++++++++++++++++++++
Kimsimamo, Manchester United wako mbele kileleni kwa Pointi 7 wakifuatiwa na Man City na Timu ya 3 ni Chelsea, wenye Mechi moja mkononi, wakiwa Pointi 4 nyuma ya Man City.
Nafasi ya 4 inakamatwa na Tottenham lakini Arsenal wana nafasi ya kuikamata nafasi hiyo kwa vile wana Mechi moja mkononi baada ya Mechi yao na West Ham iliyokuwa ichezwe Desemba 26 kuahirishwa na sasa itachezwa Januari 23.
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO:
=Tofauti ya Magoli inatajwa kwa Timu zilizofungana Pointi
1 Man United Mechi 20 Pointi 49
2 Man City Mechi 20 Pointi 42
3 Chelsea Mechi 19 Pointi 38
4 Tottenham Mechi 20 Pointi 36
5 Arsenal Mechi 19 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 18]
6 Everton Mechi 20 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 8]
7 WBA Mechi 20 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 3]
8 Stoke Mechi 20 Pointi 29
9 Liverpool Mechi 20 Pointi 28 [Tofauti ya Magoli 5]
10 Swansea Mechi 20 Pointi 28 [Tofauti ya Magoli 5]
11 Norwich Mechi 20 Pointi 25 [Tofauti ya Magoli -9]
12 West Ham Mechi 19 Pointi 23
13 Sunderland Mechi 20 Pointi 22
14 Fulham Mechi 20 Pointi 21
15 Newcastle Mechi 20 Pointi 20
16 Wigan Mechi 20 Pointi 18 [Tofauti ya Magoli -13]
17 Aston Villa Mechi 20 Pointi 18 [Tofauti ya Magoli -24]
18 Southampton Mechi 19 Pointi 17
19 Reading Mechi 20 Pointi 13
20 QPR Mechi 20 Pointi 10
+++++++++++++++++++++++
WAFUNGAJI BORA:
Robin van Persie MAGOLI 14
Demba Ba 13
Miguel Michu 13
Luis Suarez 13
Jermain Defoe 10
Gareth Bale 9
Edin Dzeko 8
Marouane Fellaini 8
Steven Fletcher 8
Rickie Lambert 8
Theo Walcott  8
Sergio Aguero 7
Santi Cazorla 7
Juan Mata 7
Wayne Rooney 7
Carlos Tevez 7
Fernando Torres  7
+++++++++++++++++++++++
RATIBA MECHI ZIJAZO-LIGI KUU ENGLAND:
**WIKIENDI YA JANUARI 5 MECHI ZA RAUNDI YA 3 FA CUP
Jumamosi 12 Januari 2013
[SAA 12 Jioni]
Aston Villa V Southampton
Everton V Swansea
Fulham V Wigan
Norwich V Newcastle
Reading V West Brom
Stoke V Chelsea
Sunderland V West Ham
Jumapili 13 Januari 2013
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Man United V Liverpool
[SAA 1 Usiku]
Arsenal V Man City
Jumatatu 14 Januari 2013
[SAA 5 Usiku]
QPR V Tottenham
Jumamosi 19 Januari 2013
[SAA 12 Jioni]
Liverpool V Norwich
Man City V Fulham
Newcastle V Reading
Swansea V Stoke
West Ham V QPR
Wigan V Sunderland
[SAA 2 na Nusu Usiku]
West Brom V Aston Villa
Jumapili 20 Januari 2013
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Chelsea V Arsenal
[SAA 1 Usiku]
Tottenham V Man Utd
Jumatatu 21 Januari 2013
[SAA 5 Usiku]
Southampton V Everton
Jumatano 23 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Arsenal V West Ham
**WIKIENDI YA JANUARI 26 MECHI ZA RAUNDI YA 4 FA CUP
Jumanne 29 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Aston Villa V Newcastle
Norwich V Tottenham
QPR V Man City
Stoke V Wigan
Sunderland V Swansea
[SAA 5 Usiku]
Reading V Chelsea
Jumatano 30 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Arsenal V Liverpool
Everton V West Brom
Fulham V West Ham
[SAA 5 Usiku]
Man United V Southampton

GAZETI LA ;daily mail

 
Streka wa Newcastle United  Demba Ba, 27, yupo karibu kujiunga na chelsea kwa euro  £7.5m-january kw akusaini miaka mitatu kuichezea timu ya chelsea katika dimba la t Stamford Bridge.
Demba Ba
Demba Ba has scored BA ameshafunga bao 13 msimu huu kwa newcastle
Midfielder wa Liverpool Joe Cole, 31, anatarajia kujiunga na timu ya QPR january na wapo katika mazungumzo ya kumuuza QPR kwa bossi Harry Redknapp
Kocha wa zamani wa timu ya Taifa ya Italy  Marcello Lippi wameshakubaliana na AC Milan kumsainisha  mshambuliaji wa Shanghai Shenhua na mshambuliaji wa -Chelsea  Didier Drogba, 34.
QPR january watampa  manager wao  Harry Redknapp £20m kwa ajili ya kumsainisha  midfielder wa Rennes ya Ufaransa Yann M'Vila, 22, na Mshambuliaji  wa Marseille  Loic Remy, 25, na  midfielder wa West Ham united  Mohamed Diame, 25.

SEHEMU NYINGINE

Midfielder wa Real Madrid ya Hispania na midfielder wa zamani wa  Liverpool  Xabi Alonso, 31, anataka kurudi   Premier League.
Klabu ya Arsenal imempa mshambuliaji wao  Theo Walcott, 23,weeks 2 ili asaini mkataba mpya wa kalabu hiyo.


MCHEZAJI BORA CHALLENGE ATUA AZAM LEO


Umony
MCHEZAJI bora wa Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge, Brian Umony anatarajiwa kuwasili leo mjini Dar es Salaam kujiunga na klabu yake mpya, Azam FC.
Umony anawasili siku mbili tu, baada ya wachezaji wengine wapya wa Azam, kutoka Kenya, beki Joackins Atudo na kiungo Humphrey Mieno kuwasili Dar es Salaam kujiunga na klabu yao hiyo mpya.
Nyota hao wote watatu, watakuwemo kwenye kikosi kitakachokwenda visiwani Zanzibar kesho kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi.
Brian amerejea nyumbani Uganda mwaka huu na kujiunga na KCC baada ya kumaliza mkataba wake katika klabu ya Becamex Binh Duong F.C. ya Vietnam.
Mwaka 2009, ilikuwa aje kuichezea Simba SC ya Dar es Salaam, lakini Wekundu hao wa Msimbazi wakazidiwa kete na SuperSport United ya Afrika Kusini.
Umony aliichezea Supersport United hadi 2010 alipohamia University of Pretoria ya Afrika Kusini pia hadi mwaka 2011 alipohamia Portland Timbers ya Marekani kwa mkopo na mwaka huu akatua Becamex Binh Duong F.C. kabla ya kurejea Uganda na sasa anakuja kuanza maisha mapya Azam FC 2012.
Kwa upande wa Atudo na Mieno, wao walianza kuichezea Azam katikati ya mwezi huu na walikuwepo kwenye kikosi cha timu hiyo kilichotwaa Kombe la Hisani la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), linaloandaliwa na FECOFA, Shirikisho la Soka la DRC wiki iliyopita, baada ya kuwachapa wenyeji, Dragons FC kwa penalti 4-2 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90.
Azam iliingia fainali, baada ya kufanikiwa kuitoa kwa mikwaju ya penalti 5-4 Shark FC ya DRC Ijumaa, kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90 kwenye Uwanja wa Martyrs.
Kikosi kizima cha Azam kilichoshiriki mashindano hayo ni Kipre Tchetche, Seif Abdallah, Kipre Balou, Zahor Pazi, Jackson Wandwi, Malika Ndeule, Uhuru Suleiman, Omar Mtaki, Jabir Aziz, Ibrahim Mwaipopo, Gaudence Mwaikimba, Abdi Kassim, Luckson Kakolaki, Samih Hajji Nuhu, Mwadini Ally, Himid Mao, David Mwantika, Waziri Salum, Humphrey Mieno na Joackins Atudo.
Katika mashindano hayo, Gaudence Mwaikimba aliibuka mfungaji bora kwa mabao yake matatu, ukiachilia mbali mawili ya penalti. Mchezaji mwingine wa kigeni wa Azam, Brian Umony wa Uganda, atajiunga na timu hiyo baada ya sikukuu pia.
Azam wamepangwa Kundi B, katika Kombe la Mapinduzi pamoja na Mtibwa Sugar ya Morogoro, Coastal Union  ya Tanga na Miembeni ya Unguja.
Kundi A lina timu za Simba SC, Tusker FC ya Kenya, Bandari ya Unguja na Jamhuri ya Pemba.
Michuano ya Kombe la Mapinduzi, ambayo ni maalum kwa ajili ya kuherehekea Mapinduzi matukufu ya Zanzaibar, inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Januari 2, hadi kilele cha miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Januari 12, mwakani, huku ikishirikisha timu kutoka ndani na nje ya Tanzania.

KOCHA WA SIMBA AWASILI LEO SAA SABA NA NUSU UWANJA WA NDEGE WA JK


Liewig
WAKATI kocha mpya wa Simba, Mfaransa Patrick Liewig anatarajiwa kuwasili leo saa 7.25 mchana, kikosi cha Wekundu hao wa Msimbazi kinatarajiwa kuondoka leo kwenda visiwani Zanzibar kushiriki Kombe la Mapinduzi.
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kwamba, Liewig ambaye ni kocha wa zamani wa Akademi ya Paris Saint Germain (PSG) ya Ufaransa, ASEC Mimosas ya Ivory Coast na Club Africain ya Tunisia, atakapofika atasaini mkataba na kuanza kazi mara moja.
Kaburu alisema kocha huyo mwenye Stashahada ya Juu ya ukocha na Shahada ya tatu ya ualimu wa soka ya vijana aliyotunukiwa na Mkurugenzi wa Ufundi wa Ufaransa, Gerard Houiller, atakwenda na timu Zanzibar.
Liewig pia amehudhuria kozi za ufundishaji mazoezi ya viungo Juni mwaka 1999 katika Chuo Kikuu cha Dijon.
Kwa upande wa uzoefu, Liewig alifanya kazi PSG kuanzia mwaka 1989 hadi 1999 kama Kocha Mkuu wa akademi na kuna wakati alikuwa akishirikishwa pia katika programu za timu A, ingawa majukumu yake zaidi yalikuwa ni kwa Under 20, Under 18 aliowawezesha kutwaa Kombe la French Junior Gambardella na Under 16.
Kuanzia mwaka 1989 hadi 1990:  alikuwa Meneja Mkuu wa Tomislav IVIC, 1990 hadi 1991 alikuwa Msaidizi wa Henri Michel, 1991 hadi 1994 alikuwa Msaidizi wa Artur Jorge, 1994 hadi 1996 alikuwa Msaidizi wa Luis Fernandez, 1996 hadi 1998: alikuwa Msaidizi wa Ricardo Gomez, 1998 hadi 1999 alikuwa Msaidizi wa Alain Giresse.
Liewig pia alifundisha Al Wahda FC ya Abu Dhabi kuanzia 1999 hadi 2001, ambayo aliipa ubingwa wa Ligi Kuu ya nchi hiyo na Kombe la Ligi.
Januari mwaka 2003 alikuwa Msimamizi wa Chama cha Soka UAE katika fainali za Afrika za U20 nchini Burkina Faso.
Kuanzia mwaka 2004 hadi 2009 alikuwa Kocha wa ASEC Mimosas ya Ivory Coast aliyoipa mataji matatu ya Ligi Kuu ya nchini humo mfululizo, 2004, 2005 na 2006, Super Cup ya nchini humo 2005, 2007, 2008 na 2009 na akaiwezesha kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa mara tatu, mara moja akiifikisha Nusu Fainali.
Amekuwa Kocha bora wa Ivory Coast miaka mitatu mfululizo, 2004, 2005 na 2006 na tangu Septemba mwaka jana hadi Juni mwaka huu, alikuwa kocha wa Club Africain ya Tunisia.

YANGA WAANZA MAZOEZI LEO ULAYA


Hoteli waliyofikia Yanga inavyoonekana, wanakula raha aje?
YANGA SC, wanatarajiwa kuanza mazoezi leo katika viwanja vya hoteli ya Fame mjini Antalya, Uturuki, baada ya kuwasili jana majira ya saa 10:30 jioni, kwa saa za Afrika Mashariki.
Mabingwa mara tano wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, wapo nchini humo kwa uenyeji wa kampuni ya Utalii ya Team Travel ya nchini humo na watakuwa huko kwa wiki mbili kuanzia jana.
Vinara hao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, wamefikia katika hoteli ya Fame Residence Lara & Spa kilomita chahce kutoka katika Uwanja wa ndege wa Antalya, ambako hoteli ya Fame Residence ipo mwambaoni mwa bahari ya Mediteranian.
Yanga iliondoka Dar es Salaam Alfajiri ya jana, saa 10:30 na kikosi kizima pamoja na benchi la ufundi kamili.
Waliopo Uturuki ni makipa; Ally Mustafa 'Barthez', Said Mohamed na Yussuf Abdul, mabeki Juma Abdul, Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Stefano Mwasyika, Oscar Joshua, Mbuyu Twite, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Ladisalus Mbogo na Kelvin Yondani.
Viungo ni Athumani Iddi ‘Chuji’, Frank Domayo, Haruna Niyonzima, Kabange Twite, Nurdin Bakari, Omega Seme, Simon Msuva, Rehani Kibingu, Nizar Khalfani na David Luhende wakati washambuliaji ni Didier Kavumbagu, Said Bahanunzi, Jerry Tegete, George Banda na Hamisi Kiiza.
Upande wa benchi la ufundi ni Kocha Mkuu Mholanzi, Ernie Brandts, Kocha Msaidizi Freddy Felix Minziro na Kocha wa makipa, Razak Ssiwa, na Maofisa wengine ni Daktari wa timu, Sufiani Juma, Meneja Hafidh Saleh, Ofisa Habari, Baraka Kizuguto Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Mohammed Nyenge.
Mwandishi wa Gazeti la Mwanaspoti, Michael Momburi aliondoka jana usiku, yeye akigharamiwa na kampuni yake.
Ziara ya mwisho katika nchi ya maana kwa Yanga, ilikuwa mwaka 2008 nchini Afrika Kusini, ambako iliweka kambi ya zaidi ya wiki mbili wakati huo ikiwa chini ya Profesa Dusan Savo Kondic, raia wa Serbia.
Zaidi ya hapo, mwaka huu Yanga ilikwenda Kigali, Rwanda kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu ya Bara, kwa mwaliko wa rais wa nchi hiyo, Paul Kagame.  Yanga pia imewahi kufanya ziara Brazil mwaka 1974 na Romania 1979. 
Yanga SC ni klabu kongwe Tanzania ambayo kati ya zinazoshiriki Ligi Kuu kwa sasa, yenyewe ndio yenye umri mkubwa zaidi.
Ingawa historia inasema Yanga ilizaliwa mwaka 1935 na Simba mwaka 1936, lakini ukizama ndani utagundua kwamba, huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa utani na upinzani wa jadi, baina ya miamba hiyo ya soka nchini.
Kulikuwa kuna timu inaitwa New Youngs, ambayo mwaka 1938 ilisambaratika na baadhi ya wachezaji wake wakaenda kuunda timu iliyokuwa ikiitwa Sunderland, ambayo hivi sasa inajulikana kama Simba.
Kabla ya kutokea vurugu zilizoisambaratisha New Youngs, vijana wa Dar es Salaam walikuwa wana desturi ya kukutana viwanja vya Jangwani kufanya mazoezi na baada ya muda wakaamua kuunda timu yao, waliyoipachika jina Jangwani.
Ndani ya kipindi kifupi tu, timu hiyo iliteka hisia za wengi, waliojitokeza kujiandikisha uanachama wa klabu hiyo. Miongoni mwa waliovutika na uanachama wa klabu hiyo ni Tarbu Mangara (sasa marehemu) na ilipofika mwaka 1926, walifanya mkutano wa kwanza katika eneo ambalo hivi kuna shule ya sekondari ya Tambaza.
Miongoni mwa yaliyojadiliwa kwenye mkutano huo ni kuiboresha timu hiyo, ambayo wachezaji wake wengi walikuwa wafanyakazi wa Bandarini na mashabiki wake wengi walikuwa wabeba mizigo wa bandarini.
Baada ya mkutano huo, timu hiyo ilibadilishwa jina na kuwa Navigation, iliyotokea kuwa moto wa kuotea mbali katika timu za Waafrika enzi hizo, kabla ya uhuru wa Tanganyika. Timu kama Kisutu, Kitumbini, Gerezani na Mtendeni zilikuwa hazifui dafu kwa wana Jangwani hao.
Ikiwa inatamba kwa jina la Navigation, wanachama wa timu hiyo walikuwa wakitembea kifua mbele na kuwatambia wapinzani, kwamba wao ndiyo zaidi. Kwa sababu katika kipindi hicho, Italia ilikuwa inatamba kwenye ulimwengu wa soka, wanachama wa timu hiyo nao waliamua kuibadilisha jina timu yao na kuiita Taliana.
Taliana ilipata mafanikio ya haraka na haikushangaza ilipopanda hadi Ligi Daraja la Pili Kanda ya Dar es Salaam, mwanzoni mwa miaka ya 1930. jina la Taliana waliamua kuachana nalo mapema, kabla ya kuingia kwenye ligi hiyo, hivyo wakaanza kujiita New Youngs.
Lakini kila ilipokuwa ikibadilisha jina, ilikuwa ikifanya vitu pia, kwani wakiwa na jina la New Youngs, waliweza kutwaa Kombe la Kassum, lililoshirikisha timu mbalimbali za Dar es Salaam.
Hatimaye ukawadia mwaka mbaya kwa New Youngs, 1938 wakati baadhi ya wachezaji walipojitoa na kwenda kuanzisha Sunderland. Kwa sababu hiyo, waliobaki wakaamua kubadili jina na kuwa Young Africans, jina ambalo mashabiki wake wengi walishindwa kulitamka vizuri hivyo kujikuta wakisema Yanga. Safari njema Yanga SC.