Wednesday, October 3, 2012

MATOKEO YA MECHI ZILIZOPITA ZA WATANI WA JADI;

JUNI 7, 1965
Yanga v Sunderland (Simba)
1-0
MFUNGAJI: Mawazo Shomvi dk. 15).

JUNI 3, 1966
Yanga v Sunderland (Simba)
3-2
WAFUNGAJI:
Yanga: Abdulrahman Lukongo dk. 54, Andrew Tematema dk 67, Emmanuel Makaidi dk. 83. Sunderland: Mustafa Choteka dk 24, Haji Lesso dk. 86.

NOVEMBA 26, 1966
Sunderland v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Mustafa Choteka dk. 44.

MACHI 30, 1968
Yanga v Sunderland
1-0
MFUNGAJI: Kitwana Manara dk. 28.

JUNI 1, 1968
Yanga v Sunderland
5-0
WAFUNGAJI:
Maulid Dilunga dk. 18 (penalti), Dilunga dk. 43, Salehe Zimbwe dk. 54, Zimbwe dk. 89, Kitwana Manara dk. 86.

MACHI 3, 1969
Yanga v Sunderland
(Yanga ilipewa pointi za chee na ushindi wa mabao 2-0, baada ya Sunderland kugoma kuingia uwanjani).

JUNI 4, 1972
Yanga v Sunderland
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Kitwana Manara dk. 19,
Sunderland: Willy Mwaijibe dk. 11.

JUNI 18, 1972
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Leonard Chitete.

JUNI 23, 1973
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Haidari Abeid 'Muchacho' dk. 68.

AGOSTI 10, 1974
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Gibson Sembuli dk. 87, Sunday Manara dk. 97.
Simba: Adam Sabu dk. 16.
(Mechi ya kihistoria iliyochezwa Uwanja wa Nyamagana mjini Mwanza).

JULAI 19, 1977
Simba v Yanga
6-0
WAFUNGAJI:
Abdallah Kibadeni dk. 10, 42 na 89, Jumanne Hassan 'Masimenti' dk. 60 na 73, Selemani Sanga alijifunga dk. 20.

OKTOBA 7, 1979
Simba v Yanga
3-1
WAFUNGAJI:
Simba: Nico Njohole dk. 3, Mohammed Bakari 'Tall' dk. 38, Abbas Dilunga dk.72. Yanga: Rashidi Hanzuruni dk. 4.

OKTOBA 4, 1980
Simba v Yanga
3-0
WAFUNGAJI: Abdallah Mwinyimkuu dk. 29, Thuwein Ally dk. 82, Nico Njohole dk. 83.

SEPTEMBA 5, 1981
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Juma Hassan Mkambi dk. 42

APRILI 29, 1982
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Rashid Hanzuruni dk 2.

SEPTEMBA 18, 1982
Yanga 3-0 Simba
WAFUNGAJI:
Omar Hussein dk. 2 na 85, Makumbi Juma dk. 62.

FEBRUARI 10, 1983
Yanga v Simba.
0-0

APRILI 16, 1983
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Charles Mkwasa dk. 21, Makumbi Juma dk. 38, Omar Hussein dk. 84, Simba; Kihwelu Mussa dk. 14.

SEPTEMBA 10, 1983,
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Lila Shomari alijifunga dk. 72, Ahmed Amasha dk. 89.

SEPTEMBA 25, 1983
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk. 75,
Simba: Sunday Juma dk. 72.

MACHI 10, 1984
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 72.
Simba: Idd Pazi kwa penalti dk 20.

JULAI 14, 1984
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 39.
Simba: Zamoyoni Mogella dk. 17

MEI 19, 1985
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Omar Hussein dk. 6
Simba: Mohammed Bob Chopa dk. 30.

AGOSTI 10, 1985
Yanga v Simba
2-0

MACHI 15, 1986
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Abeid Mziba dk. 44
Simba: John Hassan Douglas dk. 20.

AGOSTI 23, 1986
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila dk. 9, Malota Soma dk. 51
Yanga: Omar Hussein dk. 5.

JUNI 27, 1987
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Edgar 'Fongo' Mwafongo dk. 36.

AGOSTI 15, 1987
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Abeid Mziba dk. 14.

APRILI 30, 1988
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Justin Mtekere dk. 28
Simba: Edward Chumila dk. 25.

JULAI 23, 1988
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Edward Chumila 21, John Makelele dk. 58
Yanga: Issa Athumani dk. 36.

JANUARI 28, 1989
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Issa Athumani dk. 4, Abeid Mziba dk. 85
Simba: Malota Soma dk. 30.

MEI 21, 1989
Yanga v Simba
0-0

MEI 26, 1990
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Mavumbi Omari dk 6.

OKTOBA 20, 1990
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Makumbi Juma dk 33, Thomas Kipese dk. 82, Sanifu Lazaro dk. 89
Simba: Edward Chumila dk. 58.

MEI 18, 1991
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Said Sued 'Scud' dk. 7.

AGOSTI 31, 1991
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Said Sued Scud.

OKTOBA 9, 1991
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Athumani China dk. 3, Abubakar Salum 'Sure Boy' dk. 54.

NOVEMBA 13, 1991
Yanga v Simba
2-0

APRILI 12, 1992
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Kenneth Mkapa dk. 10.

SEPTEMBA 26, 1992
Simba v Yanga
2-0

OKTOBA 27, 1992
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Damian Morisho Kimti.

MACHI 27, 1993
Yanga v Simba
2-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Said Mwamba Kizota dk. 47 na 57
Simba: Edward Chumila dk. 75.

JULAI 17, 1993
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Dua Said dk. 69.

SEPTEMBA 26, 1993
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Dua Said dk. 13.

NOVEMBA 6, 1993
Simba v Yanga
0-0

FEBRUARI 26, 1994
Yanga v Simba
2-0
MFUNGAJI: Mohammed Hussein 'Mmachinga' na James Tungaraza 'Boli Zozo'.

JULAI 2, 1994
Simba v Yanga
4-1
WAFUNGAJI:
Simba: George Masatu, Athumani China, Madaraka Selemani, Dua Saidi Yanga; Constantine Kimanda.

NOVEMBA 2, 1994
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Madaraka Selemani dk. 71

NOVEMBA 21, 1994
Simba v Yanga
2-0
WAFUNGAJI: George Lucas dk. 18, Madaraka Selemani dk. 42.

MACHI 18, 1995
Simba v Yanga
0-0

OKTOBA 4, 1995
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Mchunga Bakari dk. 79,
Yanga: Mohamed Hussein ÔMmachingaŐ dk. 40.

FEBRUARI 25, 1996
Yanga v Simba
2-0

SEPTEMBA 21, 1996
Yanga v Simba
0-0

OKTOBA 23, 1996
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Mohamed Hussein 'Mmachinga' dk. 46

NOVEMBA 9, 1996
Yanga v Simba
4-4
WAFUNGAJI:
Yanga: Edibilly Lunyamila (penalti) dk. 28, Mustafa Hozza alijifunga dk 64, Said Mwamba 'Kizota' dk. 70, Sanifu Lazaro dk. 75.
Simba: Thomas Kipese dk. 7, Ahmed Mwinyimkuu dk. 43, Dua Saidi dk. 60 na 90.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)

APRILI 26, 1997
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 16
Simba: Abdallah Msamba sekunde ya. 56

AGOSTI 31, 1997
Yanga v Simba
0-0

OKTOBA 11, 1997
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 52
Simba: George Masatu dk. 89
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya)

NOVEMBA 8, 1997
Yanga v Simba
1-0
MFUNGAJI: Sekilojo Chambua dk. 85
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma)

FEBRUARI 21, 1998
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Akida Makunda dk. 46
Simba: Athumani Machepe dk. 88

JUNI 7, 1998
Yanga v Simba
1-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idelfonce Amlima dk. 28
Simba: Abuu Juma (penalti) dk. 32

MEI 1, 1999
Yanga v Simba
3-1
WAFUNGAJI:
Yanga: Idd Moshi dk. 59, Kalimangonga Ongala dk. 64, Salvatory Edward dk. 70, Simba: Juma Amir dk. 12.

AGOSTI 29, 1999
Yanga v Simba
2-0
WAFUNGAJI: Bakari Malima dk. 49, Mohamed Hussein 'Mmachinga' dk 71

JUNI 25, 2000
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Steven Mapunda dk. 59 na 72
Yanga: Idd Moshi dk. 4.

AGOSTI 5, 2000
Yanga v Simba
2-0
MFUNGAJI: Iddi Moshi 37 na 47. (Alifunga mabao hayo, akitoka kwenye fungate ya ndoa yake)

SEPTEMBA 1, 2001
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Joseph Kaniki dk. 76

SEPTEMBA 30, 2001
Simba v Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
Simba: Joseph Kaniki dk. 65,
Yanga: Sekilojo Chambua dk. 86
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza)

AGOSTI 18, 2002
Simba v Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
Simba: Madaraka Selemani 65
Yanga: Sekilojo Chambua (penalti). dk. 89

NOVEMBA 10, 2002
Simba v Yanga
0-0

SEPTEMBA 28, 2003

Simba v Yanga
2-2
WAFUNGAJI:
Simba: Emmanuel Gabriel dk. 27 na 36
Yanga: Kudra Omary dk. 42, Heri Morris dk. 55

NOVEMBA 2, 2003
Simba v Yanga
0-0

AGOSTI 7, 2004
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Shaaban Kisiga dk. 64, Ulimboka Mwakingwe dk. 76
Yanga: Pitchou Kongo dk. 48

SEPTEMBA 18, 2004
Simba v Yanga
1-0
MFUNGAJI: Athumani Machuppa dk. 82

APRILI 17, 2005
Simba v Yanga
2-1
WAFUNGAJI:
Simba: Nurdin Msiga dk. 44, Athumani Machupa dk. 64,
Yanga: Aaron Nyanda dk. 39
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

AGOSTI 21, 2005
Simba v Yanga
2-0
MFUNGAJI: Nico Nyagawa dk. 22 na 56
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha)

MACHI 26, 2006
Simba v Yanga.
0-0

OKTOBA 29, 2006
Simba v Yanga
0-0

JULAI 8, 2007
Simba v Yanga
1-1 (dakika 120)
WAFUNGAJI:
Simba: Moses Odhiambo (penalti dk. 2)
Yanga: Said Maulid (dk. 55).
(Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 baada ya sare hiyo).
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

OKTOBA 24, 2007:
Simba Vs Yanga
1-0
Mfungaji: Ulimboka Mwakingwe
(Mechi hii ilichezwa Uwanja wa Jamhuri, Morogoro)

APRILI 27, 2008:
Simba Vs Yanga
0-0

OKT 26, 2008
Yanga Vs Simba
1-0
MFUNGAJI: Ben Mwalala dk15.
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

APRILI 19, 2009
Simba Vs Yanga
2-2
WAFUNGAJI:
SIMBA: Ramadhan Chombo dk 23, Haruna Moshi dk 62
YANGA: Ben Mwalala dk48, Jerry Tegete dk90
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)
(Matokeo haya yanahusu mechi za Ligi ya Bara na iliyokuwa Ligi ya Muungano pekee)

OKTOBA 31, 2009
Simba Vs Yanga
1-0
MFUNGAJI: Mussa Hassan Mgosi dk 26
(Mechi hii ilichezwa Uwanja mpya wa Taifa, Dar es Salaam)

APRILI 18, 2010
Simba Vs Yanga
4-3
WAFUNGAJI:
SIMBA: Uhuru Suleiman dk 3, Mussa Mgosi dk 53 na 74, Hillary Echesa dk 90+
YANGA: Athumani Iddi dk 30, Jerry Tegete dk 69 na 89

OKTOBA 16, 2010:
Yanga Vs Simba
1-0
MFUNGAJI: Jerry Tegete dk 70

MACHI 5, 2011
Simba Vs Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
YANGA: Stefano Mwasyika (penalti) dk 59.
SIMBA: Mussa Mgosi dk 73.
(Refa Orden Mbaga alizua tafrani uwanjani, kwanza kwa kulikataa bao la kusawazisha la Simba, kisha akalikubali baada ya kujadiliana na msaidia wake namba moja)

Simba, Yanga nje ya Ligi KuuP W D L
Yanga SC 18 8 2 8
Simba SC 18 8 2 8

NJE ya mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba na Yanga zimekuwa zikikutana katika mechi zenye msisimko wakati mwingine za kuwania mataji, tena yenye thamani ya mamilioni na mvuto wake umebaki kuwa kama kawaida.
Kwa wenye kuikumbuka mechi ya fainali ya Ligi, Uwanja wa Nyamagana, mjini Mwanza mwaka 1974, hawawezi kuisahau mechi ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, kwa sasa maarufu kama Kombe la Kagame.
Kwa nini? Kwa sababu wafungaji wa mabao ya Yanga kwenye Uwanja wa Nyamagana ndio wafungaji wa mabao wa timu hiyo katika ushindi wa 2-0 visiwani Zanzibar kwenye Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati.
Hiyo ilikuwa mechi ya kwanza kubwa kuzikutanisha Simba na Yanga nje ya Ligi Kuu na Watoto wa Jangwani, chini ya kocha kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), wakati huo wakaibuka na ushindi wa mabao 2-0 na kutwaa Kombe.
Tangu wakati huo hadi Januari 12 , mwaka 2011, watani hao wa jadi katika soka ya Tanzania wamekutana kwenye mechi ambazo si za Ligi mara 18 na katika hizo, Yanga imeshinda mechi nane, Simba mechi nane na zimetoka sare mbili.
Ni mechi gani, za mashindano gani, endelea;

KLABU BINGWA AFRIKA MASHARIKI NA KATI:
JULAI 10, 2011
Yanga 1-0 Simbam, Fainali
MFUNGAJI : Kenneth Asamoah dk 108

JANUARI 1975
Yanga Vs Simba; Fainali, 2-0
WAFUNGAJI: Gibson Sembuli na Sunday Manara

JANUARI 1992
Simba Vs Yanga; Fainali
1-1, Simba ilishinda kwa penalti 5-4

JULAI 27, 2008
Simba Vs Yanga; Mshindi wa Tatu
(Yanga haikutokea uwanjani, Simba ikapewa ushindi wa chee)

KOMBE LA HEDEX:
JUNI 30, 1996
Yanga Vs Simba 2-0
CCM Kirumba, Mwanza
WAFUNGAJI: Bakari Malima na Edibily Lunyamila

KOMBE LA HEDEX:
JULAI 13, 1996
Simba Vs Yanga 1-1, Taifa, Dsm
WAFUNGAJI:
SIMBA: Hussein Amaan Marsha kwa penalti
YANGA: Bakari Juma Malima

KOMBE LA TUSKER:
FEBRUARI 10, 2001
Yanga Vs Simba (fainali) 0-0
(Simba ilishinda kwa penalti 5-4, Uwanja wa Taifa)

MACHI 31, 2002.
Simba Vs Yanga 4-1
WAFUNGAJI:
SIMBA: Mark Sirengo dk. 3 na 76, Madaraka Selemani dk. 32 na Emanuel Gabriel dk. 83.
YANGA: Sekilojo Chambua dk 16.
(Mechi hii ya fainali iliyohudhuriwa na rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, chupuchupu ivunjike dakika ya 32, baada ya Madaraka kufunga bao ambalo kabla ya kufumua shuti lililomshinda kipa Manyika Peter, aliushika mpira kwa makusudi, ili kuuweka sawa. Rais wa Yanga wakati huo, Tarimba Abbas aliinuka na kuwaonyesha ishara wachezaji wake watoke uwanjani na hapo ndipo meza kuu aliyokuwa ameketi mzee Mwinyi, ilipoanza kushambuliwa kwa chupa za maji na mashabiki wa Yanga. Mwamuzi wa mchezo huo, Abdulkadir Omar alisubiri hadi vurugu zilipotulizwa na FFU ndipo akaendeleza mchezo. Tarimba alitoka nje na hakutaka kuendelea kushuhudia mchezo huo. Baada ya hapo, alifungiwa na Chama cha Soka Tanzania, FAT).

JULAI 2, 2005
CCM Kirumba, Mwanza. Fainali
Simba Vs Yanga, 2-0
WAFUNGAJI: Emmanuel Gabriel dk. 60, Mussa Hassan Mgosi dk. 72

AGOSTI 15, 2006
Simba Vs Yanga; Nusu Fainali, 1-1
WAFUNGAJI:
SIMBA: Emanuel Gabriel dk. 69
YANGA: Credo Mwaipopo 90
(Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 7-6)

DESEMBA 25, 2009
Yanga Vs Simba; Nusu Fainali, 2-1
WAFUNGAJI:
YANGA: Jerry Tegete dk 67, Shamte Ally dk 120
SIMBA: Hillary Echesa dk 78 (penalti)
(Uwanja wa mpya wa Taifa)

KOMBE LA MAPINDUZI:
JANUARI 12, 2011
Simba Vs Yanga; Fainali 2-0
WAFUNGAJI: Mussa Mgosi dk 33, Shijja Mkinna dk 71
(Uwanja wa Amaan, Zanzibar)

KOMBE LA AICC:
JUNI 1989
Yanga Vs Simba SC 1-0
MFUNGAJI: Joseph Machella

APRILI 20, 2003,
CCM Kirumba, Mwanza
Yanga Vs Simba 3-0
WAFUNGAJI:
Kudra Omary dk. 30, Heri Morris dk 32 na Salum Athumani dk. 47

JANUARI 19, 2003, Kombe la CCM
Simba Vs Yanga 1-1, Dsm
WAFUNGAJI:
SIMBA: Jumanne Tondolo dk. 10
YANGA: Mwinyi Rajabu dk. 20

NGAO YA JAMII:
FEBRUARI 17, 2001
Yangs Vs Simba 2-1, Dsm
WAFUNGAJI:
YANGA: Edibilly Lunyamila dk. 47, AllyYussuf 'Tigana' dk 80.
SIMBA: Steven Mapunda 'Garrincha' dk.43

AGOSTI 18, 2010
Yanga vs Simba 0-0
(Yanga ilishinda kwa penalti 3-1)
WAFUNGAJI: Geoffrey Bonny, Stefano Mwasyika na Isaac Boakye kwa upande wa Yanga na Mohamed Banka kwa Simba.
WALIOKOSA: Ernest Boakye kwa Yanga na Emanuel Okwi, Uhuru Suleiman na Juma Nyosso kwa Simba.

AGOSTI 17, 2011
Simba 2-0 Yanga
WAFUNGAJI:
Haruna Moshi ‘Boban’ dk 15 na Felix Sunzu dk 38 (penalti)


NOVEMBA 15, 2000
KOMBE LA FAT
Yanga Vs Simba 2-1
Sheikh Amri Abeid, Arusha.
WAFUNGAJI:
YANGA: Aziz Hunter 40 na Vincent Tendwa
SIMBA: Ally Yussuf 'Tigana' dk.37

NOVEMBA 12, 2000
MARUDIANO KOMBE LA FAT
Simba Vs Yanga 1-0, Dsm
MFUNGAJI:
SIMBA: Ben Luoga dk.44
(Matokeo ya jumla yakawa 2-2 na Yanga ikatolewa kwa mikwaju ya penalti 5-4)

SIMBA WANGOJA ULINZI TRAFIKI WAKAPOKEE TIMU BANDARINI, TAIFA KWAANZA KUNOGA

Basi la Simba likiwa limepaki makao makuu ya Trafiki, kusubiri ulinzi kwa ajili ya kwenda kuipokea timu Bandarini, ikitokea Zanzibar


Basi la Simba likiwa limepaki makao makuu ya Trafiki, kusubiri ulinzi kwa ajili ya kwenda kuipokea timu Bandarini, ikitokea Zanzibar

Eeneo la Gerezani, karibu na BP kama unaenda Kurasini

Eneo la Gerezani, karibu na BP kama unaenda Kurasini

Jamaa amenunua na kuvaa hapo hapo jezi ya Yanga

Biashara ye jezi

Add caption

Mashabiki wa Simba wanaelekea uwanjani

Daudi Chalamila na Simba mwenzie

Zambia, Cameroon zaomba kucheza CHALENJI CUP

Mabingwa wa Afrika, Zambia, wameomba kushiriki Mashindano ya Mwaka huu ya CHALENJI CUP, Tusker CECAFA Cup, ambayo ndio hutoa Nchi Bingwa wa Afrika Mashariki na Kati ambayo yatafanyika huko Kampala, Uganda kati ya Novemba 27 na Desemba 12.


Nchi nyingine 4 ambazo pia zimeomba kushiriki ni Cameroon, Malawi, Zimbabwe na Cote D'Ivoire.
Habari za maombi ya Nchi hizo zimethibitishwa na Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicolas Musonye, ambae amesema ushiriki wa Nchi hizo utategemea uamuzi wa CECAFA ambao utatolewa baada ya Mkutano wao.


Mkutano huo wa CECAFA unategemewa kufanyika Wikiendi ijayo baada ya Mechi za Raundi ya Mwisho ya Mtoano ya AFCON 2013.


Mwaka jana, Malawi na Zimbabwe, zilishiriki kama Wageni waalikwa.
Hata hivyo, Musonye pia amesema ushiriki wa Nchi hizo ambao si Wanachama wa CECAFA utategemea pia ikiwa kama kutakuwa na Nchi Mwanachama ambayo itajitoa ingawa hadi sasa Nchi zote 12 Wanachama wa CECAFA zimethibitisha ushiriki wao.


Droo ya kupanga Ratiba ya Michuano hiyo itafanyika huko Kampala hapo November 8.
Bingwa Mtetezi wa CHALENJI CUP ni Uganda ambao pia ndio Nchi iliyotwaa Ubingwa huo mara 12 ambazo ni nyingi kupita Nchi nyingine.
 

LISTI ya FIFA UBORA DUNIANI: Spain palepale Nambari Wani, Bongo palepale 132!


@@@@KUMI BORA, Colombia yatinga, yapanda Nafasi 13!!
@@@@BRAZIL Washuka 2, Wapo wa 14!!
FIFA_LOGO_BESTSpain, ambao ndio Mabingwa wa Ulaya na Dunia, wameendelea kushika Nambari Wani kwenye Listi ya FIFA/Coca Cola ya Ubora Duniani iliyotolewa leo huku Tanzania ikibakia Nambari 132 na kwenye Kumi Bora Portugal imepanda na kushika Namba 3, England imeporomoka na sasa ipo nafasi ya 5 kutoka Namba 3.


Barani Afrika Ivory Coast ndio wapo juu na wapo nafasi ya 16 ambayo ni ile ile kama ilivyokuwa Mwezi uliopita.


Colombia wameingia Kumi Bora baada ya kupanda nafasi 13 huku Denmark na Croatia zikiporomoka kutoka Kumi Bora.


Brazil, Mabingwa wa Dunia mara 5, wameporomoka nafasi mbili na sasa wapo nafasi ya 14.
Listi nyingine mpya itatolewa Novemba 7.


KUMI BORA:
1 Spain
2 Germany
3 Portugal
4 Argentina
5 England
6 Netherlands
7 Uruguay
8 Italy
9 Colombia
10 Greece
 

BATE Borisov yaifumua Bayern, yatikisa Ulaya!!!


@@@@REKODI: Juve sare ya 8 mfululizo!!
@@@@REKODI: Celtic wavunja rekodi ya kutoshinda Mechi 20 ugenini!


MATOKEO:
Jumanne Oktoba 2
Juventus 1 Shakhtar Donetsk 1
FC Nordsjælland 0 Chelsea 4
Valencia 2 LOSC Lille 0
FC BATE Borisov 3 FC Bayern München 1
SL Benfica 0 FC Barcelona 2
FC Spartak Moskva 2 Celtic 3
CFR 1907 Cluj 1 Manchester United 2
Galatasaray 0 Braga 2
 ++++++++++++++++++++++++++++++
RVP_ROONEY_CLEVERLYKlabu ya Belarus, BATE Borisov, jana ilileta mtikiso mkubwa huko Ulaya kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa kuwatandika Bayern Munich, ambao Msimu uliopita walitinga Fainali ya michuano hii na kubwagwa kwa Penati na Chelsea, kwa kuwatandika bao 3-1 katika Mechi ya Kundi F.


Huku Bayern Munich wakitolewa nishai, Vigogo wengine wote wa Ulaya, Mabingwa Chelsea, Barcelona na Manchester United walishinda lakini Juventus walitoka sare 1-1 na Shakhtar Donetsk.


Chelsea, wakicheza ugenini huko Denmark, waliichapa Timu mpya FC Nordsjaelland 4-0, Barcelona, pia wakiwa ugenini, waliifunga Benfica 2-0 lakini walipata mkosi pale Nahodha wao Carles Puyol alipokimbizwa Hospitali baada ya kuteguka kiwiko cha mkono na Sergio Busquets kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.


Nao Manchester United, wakicheza huko Romania, walitoka nyuma kwa bao moja na kuifunga CFR Cluj kwa bao zote mbili kufungwa na Robin van Persie ambae alipiga bao hizo kwa ushirikiano mkubwa na Wayne Rooney ambae jana ilikuwa ndiyo Mechi yao ya kwanza kuanza Mechi pamoja.


Huko Turin, Italy, Wakongwe wa Ulaya Juventus jana waliweka rekodi mpya Ulaya ya kutoka sare 8 mfululizo kwenye Mashindano ya Klabu Ulaya walipotoka 1-1 na Shakhtar Donetsk.


Valencia waliifunga Lille bao 2-0 na kuifanya Klabu hiyo ya Ufaransa ifungwe mara mbili mfululizo kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu huu.


Jana Celtic walivunja ile rekodi yao ya kutoshinda ugenini katika Mechi 20 za UEFA CHAMPIONZ LIGI baada ya kuifunga Spartak Moscow 3-2 huku bao la ushindi likifungwa Dakika za mwisho na Georgios Samaras.


Braga walendeleza wimbi lao la kutofungwa ugenini kwa kuichapa Galatasaray bao 2-0 na hiyo ni Mechi yao ya 7 kutofungwa ugenini.


Huko Copenhagen, Chelsea, wakiongoza kwa bao 1-0, walimshukuru Kipa wao Petr Cech kwa kuokoa bao la wazi katika Dakika ya 73 na Dakika chache baadae Luiz akawafungia bao la pili kwa frikiki na kuwafanya Chelsea wapige bao 3 ndani ya Dakika 11 za mwisho na kushinda 4-0 kwa bao za Juan Mata, bao 2, David Luiz na Ramires.

++++++++++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumatano Oktoba 3
[Mechi zote Saa 3 Dakika 45 Usiku isipokuwa inapotajwa]
FC Dynamo Kyiv v GNK Dinamo
FC Porto v Paris Saint-Germain FC
FC Schalke 04 v Montpellier Hérault SC
Arsenal FC v Olympiacos FC
RSC Anderlecht v Málaga CF
FC Zenit St. Petersburg v AC Milan [SAA 1 Usiku]
Manchester City FC v Borussia Dortmund
AFC Ajax v Real Madrid CF
++++++++++++++++++++++++++++++


MSIMAMO:
[Kila Timu imecheza Mechi 2]
KUNDI E
Chelsea Pointi 4
Shakhtar Donetsk 4
Juventus 2
Nordsjaelland 0


KUNDI F
BATE Bprisov Pointi 6
Valencia 3
Bayern Munich 3
Lille 0


KUNDI G
Barcelona Pointi 6
Celtic 4
Benfica 1
Spartak Moscow 0


KUNDI H
Manchester United Pointi 6
CFR Cluj 3
Braga 3
Galatasaray 0

YULE REFA WA MEI 6 ALIKUWA KIBOKO, MAREFA WETU NA MECHI

 


 tano juma

JIONI ya leo kuanzia saa 11:00, nyasi za Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam zitawaka moto kwa mpambano mkali wa watani wa jadi, Simba na Yanga katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ambayo itarushwa moja kwa moja na Televisheni ya Super Sport ya Afrika Kusini.
Nakumbuka, wachambuzi na watangazaji wa SuperSport waliwahi kuiingiza mechi ya Simba na Yanga katika orodha ya mechi tatu kali za wapinzani wa jadi Afrika - nyingine zikiwa ni kati ya Orlando Pirates na Kaizer Chiefs za Afrika Kusini na Al Ahly dhidi ya Zamalek za Misri.
Lakini mimi naongeza mechi ya wapinzani wa Ghana, Hearts Of Oak na Asante Kotoko, ingawa Kenya nako upinzani wa Gor Mahia na AFC Leopard umeanza kuja juu tena, baada ya kuporomoka miaka ya karibuni, kutokana na kuyumba kwa timu zenyewe.
Hakuna ubishi upinzani wa Ahly na Zamalek huo ni dunia nzima - ni zaidi ya upinzani, lakini kwa Afrika fuatilia ligi nyingi, utagundua Simba na Yanga ni mechi yenye mvuto wa kipekee na ndiyo maana hivi sasa SuperSport wamekuwa wakionyesha mfululizo mechi za watani hao, ingawa hawana mkataba na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) wa kuonyesha mechi za Ligi Kuu.
Unaweza kutilia shaka kiwango cha soka cha timu hizo, lakini si upinzani wao kwa maana ya upinzani. Upinzani wao ni sehemu ya burudani na kama iko siku zitakuwa imara na kucheza soka ya kuvutia, basi burudani itakuwa mara mbili.
Hata hivyo kuna mambo mawili au matatu ambayo kwa kiasi fulani yamekuwa yakipunguza ladha ya mechi za watani hao wa jadi.
Awali tatizo kubwa lilikuwa Uwanja mdogo wa Uhuru, lakini tangu kukamilika kwa Uwanja wa Taifa ambao tumeshuhudia mechi zote zilizochezwa hapo, haijatokea mechi hata moja mashabiki wakajaza viti, mambo yamekuwa mazuri.
Matatizo mawili yaliyobakia ni viwango vya timu kuboreshwa, ili ifike wakati pamoja na upinzani, kukamiana lakini watazamaji washuhudie soka safi.
Tatizo la pili ni marefa, kweli ilipofikia na kama kweli lengo ni kuiongezea msisimko zaidi mechi ya watani, waamuzi wa Tanzania wawekwe kando na watumike waamuzi kutoka nje ya nchi, tena ikibidi nje kabisa ya nchi tatu za Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki.
Rejea mchezo uliopita wa Mei 6, 2012, refa alitoa penalti tatu na kadi moja nyekundu kwa Yanga, ikichapwa 5-0 na Simba.
Hii si sahihi katika mechi za wapinzani wa jadi, dhahiri refa huyu alishindwa kuumudu mchezo wa watani hata kama alifuata sheria 17. Katika mechi ya wapinzani wa jadi, ukishatoa kadi moja nyekundu kwa timu moja, unajifikiria sana kurudia kutoa kadi ya pili kwa timu hiyo hiyo.
Katika mechi za wapinzani wa jadi, ukishatoa penalti moja kwa timu moja, unajifikiria sana kutoa penalti ya pili kwa timu hiyo hiyo. Unafikiria mengi. Tena mengi sana.
Jana Ofisa Habari wa Simba SC, Ezekiel Kamwaga alizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu refa Mathew Akrama atakayechezesha pambano la leo watani wa jadi kesho, akishangaa kwamba anapewaje mechi mbili mfululizo za Yanga, wakati ndiye aliyechezesha mechi iliyopita ya Yanga na African Lyon.
“Tunajua sekretarieti ya TFF ndiyo huwa inahusika kupanga marefa, na ndiyo hii hii ambayo tunailalamikia haitutendei haki, sasa sisi tunamuomba mambo mawili makubwa Akrama, kwenye mechi ya Simba na Yanga; kuna watu huwa wanapoteza maisha wakifungwa. Kuna watu huwa wanapoteza fahamu, wanaweka rehani nyumba zao, mali zao kucheza kamari, na wanaliwa.kuna viongozi wengine wamewahi kutimuliwa madarakani kwa sababu ya kufungwa na Simba na Yanga.
Kwa hiyo, hii mechi ina mambo mengi sana, sasa sisi tunamuomba Akrama asiue watu, asifanye watu wakaliwa, asifanye watu wakapata mateso yasiyo na sababu,”alisema.
Labda Kamwaga alikuwa akizungumza kama propaganda tu siasa za soka ya nchi hii, lakini aliongea mambo mazito na yenye mantiki. Kweli Simba na Yanga zimekwishaua watu.
Lakini sitaki kuegemea upande wa Kamwaga, kuua watu kwa maumivu ya kufungwa- hapana, zinapoibuka hisia za timu fulani kuumizwa na refa, mfano ule wa kutoa penalti tatu na kadi nyekundu juu, kuna hatari ya vurugu zaidi na mauaji kutokea.
Haya ni mambo ambayo umefika wakati sasa, TFF wanapoingia kwenye mechi ya watani, wanatakiwa kuyafikiria.
Rejea mechi ya Machi 5, mwaka 2011 Uwanja wa Taifa, refa Orden Mbaga aliivuruga mno mechi hiyo, kutokana tu na pengine mchecheto ama kutaka kufanya kile ambacho kinaitwa ‘kubalansi’ mchezo au kukwepa lawama, matokeo yake anafanya madudu.
Dakika ya 58 Juma Said Nyosso alimkwatua Davies Robby Mwape kwenye eneo la hatari akawapa penalti Yanga na kilichofuatia wengi walijua beki huyo wa Simba atatolewa nje kwa kadi nyekundu, badala yake akampa kadi ya njano.
Ngumu kuamini Mbaga, refa mwenye beji ya Shrikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) hajui alipaswa kufanya nini kwa Nyosso, lakini kwa sababu ni refa wa nyumbani na aliongoza wapinzani wa jadi katika mechi ya nyumbani, alihofia kumtoa mchezaji kwa kadi nyekundu angeshushiwa lawama nzito. Marefa hufanyiwa fujo na kupigwa na mashabiki, labda alihofia hali hiyo pia.
Dakika ya 73 Simba walipata bao safi la kusawazisha lililofungwa kwa kichwa na Mussa Hassan Mgosi, aliyeuwahi mpira uliotemwa na kipa Yaw Berko  kufuatia shuti la mpira wa adhabu, lililogonga mwamba wa juu na kudondokea nyavuni kabla ya kuokolewa na mabeki wa Yanga.
Halikuwa bao lenye shaka yoyote, hakukuwa na kuotea wala dosari yoyote, lakini haieleweki kwa nini Mbaga alilikataa bao hilo awali.
Ilikuwa offside au mpira haukutinga nyavuni hadi akalikataa kwanza? Haijulikani, lakini alilikubali baada ya wachezaji wa Simba kumuambia aangalie kwenye TV iliyokuwapo uwanjani marudio ya tukio lile na baada ya hapo akaenda kujadiliana na msaidizi wake, ndipo akalikubali.
Mbaga alichemsha- lakini si Mbaga tu, marefa wengi wa Tanzania waliwahi kutokota kabla yake na nitakumbushia baadhi ya mechi.  
Machi 31, mwaka 2002 katika fainali ya Kombe la Tusker, Simba ikishinda 4-1, refa Abdulkadir Omar ‘Msomali’ aliivuruga mechi na kuvuruga amani uwanjani pia kwa madudu yake.
Kwa nini? Katika mechi hiyo ya fainali iliyohudhuriwa na rais mstaafu wa awamu ya pili ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi, chupuchupu ivunjike dakika ya 32, baada ya Madaraka Suleiman kufunga bao ambalo kabla ya kufumua shuti lililomshinda kipa Manyika Peter, aliushika mpira kwa makusudi, ili kuuweka sawa.
Rais wa Yanga wakati huo, Tarimba Abbas aliinuka na kuwaonyesha ishara wachezaji wake watoke uwanjani na hapo ndipo meza kuu aliyokuwa ameketi mzee Mwinyi, ilipoanza kushambuliwa kwa chupa za maji na mashabiki wa Yanga. Abdulkadir Omar alisubiri hadi vurugu zilipotulizwa na FFU ndipo akaendeleza mchezo. Tarimba alitoka nje na hakutaka kuendelea kushuhudia mchezo huo. Baada ya hapo, alifungiwa na Chama cha Soka Tanzania, (FAT), sasa TFF kabla ya kujiuzulu uongozi wa klabu hiyo baadaye.
Agosti 18, mwaka 2002 Simba na Yanga zikitoka sare ya 1-1 katika mechi ya Ligi Kuu, refa Victor Mwandike aliwaacha mashabiki wa Simba midomo wazi kwa kuwapa Yanga penalti dakika ya 89 na ushehe, ambayo Sekilojo Chambua aliitumia vema kuisawazishia bao timu yake, baada ya Simba kutangulia kufunga kupitia kwa Madaraka Suleiman dakika ya 65.
Oktoba 24, mwaka 2007, refa Osman Kazi alikataa mabao matatu yaliyofungwa na Yanga, yote akidai kipa Juma Kaseja alisukumwa na wachezaji wa Yanga, lakini kwa yeyote atakayerudia kuangalia DVD ya mchezo ule, hawezi kuona ukweli wa madai ya Kazi.
Awali ya hapo, Kazi aliwahi kupuliza filimbi ya kumaliza dakika 45 za kipindi cha kwanza katika Nusu Fainali ya Kombe la Tusker mwaka 2005 mjini Mwanza, wakati mchezaji wa Yanga, Said Maulid ‘SMG’ amekwishawatoka mabeki wa Simba na anakwenda na mpira mbele yake amebaki Juma Kaseja tu.
Refa ni mwamuzi wa mwisho- lakini kwa wana Yanga walijutia mno tukio lile kwenye mchezo ambao mwishowe walifungwa 2-0, kwa mabao ya kipindi cha pili ya Emmanuel Gabriel na Mussa Mgosi.
Aprili  19, mwaka 2009, Jerry Tegete aliifungia Yanga bao la kusawazisha kwa mkono na kutengeneza sare ya 2-2, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Refa makini asingeweza kukubali bao lile, hivyo kwa haya yote lazima tukubali marefa wa Tanzania hawawezi tena kuchezesha mechi za watani wa jadi.
Sababu nyingine za marefa wetu kuzishindwa mechi hizo ni mapenzi yao kwa moja ya timu hizo, kitu ambacho Misri wamekiepuka na mechi ya Zamalek na Ahly inachezeshwa na marefa kutoka nje ya nchi yao.
Nakumbuka refa kutoka Uganda, Dennis Bate aliyechezesha Nusu Fainali ya Kombe la Tusker mwaka 2009 kati ya Simba na Yanga, aliiongoza vizuri mechi hiyo na akadhibiti ujanja wote wa wachezaji kutaka kumdanganya na hatimaye aboronge.
Kuna wachezaji wanaitwa wazoefu wa mechi za Simba na Yanga na hawa wamekuwa wakiwapoteza sana marefa kwa uzoefu wa kucheza mechi hizo, lakini kama marefa watatoka nje ya Tanzania, tena wa kiwango cha beji za FIFA, uhondo wa mechi za watani utaongezeka maradufu.
Zaidi ya mara mbili sasa naandika juu ya mechi za watani wa jadi kubadilishiwa marefa, lakini wakubwa wameendelea kukaa kimya- labda wanajua wanachokifanya, ila ukweli ulivyo
kwa sasa, marefa wetu hawaziwezi tena mechi hizi.