Wednesday, January 2, 2013

KUMEKUCHA MAPINDUZI CUP ZANZIBAR, MNYAMA ANASHUKA AMAAN USIKU HUU


Wachezaji wa Azam wakiwasili Bandari ya Zanzibar jioni hii tayari kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani hapa, inayoanza leo, mabingwa wa Kenya, Tusker wameanza vyema kwa kuifunga Bandari ya hapa mabao 5-1 jioni hii Uwanja wa Amaan, na saa 2:00 usiku mabingwa wa Tanzania Bara, Simba SC watamenyana na Jamhuri ya Pemba

Wachezaji wa Tusker wakiwasili Bandari ya Zanzibar jioni hii, wakiwa na mwenyeji wao nchini, George Wakuganda kushoto tayari kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani hapa, inayoanza leo, mabingwa hao wa Kenya,  mabingwa wa Kenya, Tusker wameanza vyema kwa kuifunga Bandari ya hapa mabao 5-1 jioni hii Uwanja wa Amaan, na saa 2:00 usiku mabingwa wa Tanzania Bara, Simba SC watamenyana na Jamhuri ya Pemba

Wachezaji wa Mtibwa wakiwasili Bandari ya Zanzibar jioni hii tayari kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani hapa, inayoanza leo, mabingwa wa Kenya, Tusker wameanza vyema kwa kuifunga Bandari ya hapa mabao 5-1 jioni hii Uwanja wa Amaan, na saa 2:00 usiku mabingwa wa Tanzania Bara, Simba SC watamenyana na Jamhuri ya Pemba 

Mchezaji wa Azam, Kipre Michael balou akiwasili Bandari ya Zanzibar jioni hii tayari kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani hapa, inayoanza leo, mabingwa wa Kenya, Tusker wameanza vyema kwa kuifunga Bandari ya hapa mabao 5-1 jioni hii Uwanja wa Amaan, na saa 2:00 usiku mabingwa wa Tanzania Bara, Simba SC watamenyana na Jamhuri ya Pemba. 

Mchezaji mpya wa Azam, Brian Umony akiwasili Bandari ya Zanzibar jioni hii tayari kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi visiwani hapa, inayoanza leo, mabingwa wa Kenya, Tusker wameanza vyema kwa kuifunga Bandari ya hapa mabao 5-1 jioni hii Uwanja wa Amaan, na saa 2:00 usiku mabingwa wa Tanzania Bara, Simba SC watamenyana na Jamhuri ya Pemba

Mwenyekiti wa ZFA, Aman Ibrahim Makungu akiwa bize na simu kuwasiliana na wageni wanaowasili visiwani hapa kwa ajili ya michuano hii. 

SAJUKI KUZIKWA IJUMAA KISUTU



Waombolezaji wakiwa kwenye msiba wa Sajuki Tabata jijini Dar es Salaam leo, Januari 2, 2013. 

Msanii wa vivhekesho, Mtanga (kushoto) akiwa na waombolezaji wengine katika msiba wa Sajuki leo Januari 2, 2013.

Waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehemu Sajuki leo Januari 2, 2013.

Piga pale...! Sajuki (kulia) akiwa katika maandalizi ya filamu yake mojawapo kali wakati wa enzi za uhai wake.
Hatimaye ule utata kuhusiana na mahala pa kumzika msanii Juma Kilowoko 'Sajuki' umepatiwa jibu baada ya baba yake kukubali kuwa azikwe jijini Dar es Salaam.

Kutokana na uamuzi huo, sasa msanii huyo aliyekuwa nyota na kipenzi cha wengi enzi za uhai wake atazikwa keshokutwa Ijumaa (Januari 4) kwenye makaburi ya Kisutu.

Awali, baba wa msanii huyo alitaka mwanawe akazikwe kwao mkoani Songea. Hata hivyo, baada ya kuketi na kujadili kwa kina na familia yake, akaamua kutangaza kuwa mwanawe huyo kipenzi atazikwa jijini Dar es Salaam ili kutoa nafasi kwa rafiki zake wengi aliokuwa akishirikiana nao katika kazi zake za kila siku za kisanii kupata nafasi ya kushiriki mazishi yake.

Mzee Kilowoko ametoa msimamo huo mpya leo hoo hii, ikiwa ni muda mfupi tu baada ya kutangaza awali kuwa mwanawe atakwenda kuzikwa Songea.

Sajuki amefariki leo asubuhi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa katika wodi ya wagonjwa mahututi na kupumua kwa msaada wa mashine kabla ya kuaga dunia mishale ya saa 1:00 asubuhi.

USAJILI MBALI MBALI BARANI ULAYA UNAVYOENDELEA KWA SASA ANGALIA ILI UWEZE KUJUA NANI ANAENDA WAPI NANI ANATOKA NA NANI ANABAKI



Mlinzi wa Atalanta Federico Peluso amefanyiwa vipimo vya afya hii leo katika klabu ya Juventus na anatarajiwa kukamilisha taratibu za usajili wake hii leo

Mpango wa uhamisho wake ni wa gharama ya euro milioni 1.5 ambapo Bianconeri(Juve) wakiwa na maamuzi ya uhamisho wa kudumu baada ya msimu kumalizika.

Endapo klanbu hiyo itachagua kufanya hivyo, inamaanisha kuwa mabingwa hao wa kandanda nchini Italia watalazimika kulipa eoro milioni 3.5 kwa kupata huduma yake na huku mlinzi huyo wa kati akitarajiwa kuongeza ushindani katika sehemu ya ulinzi wa kati na ulinzi wa kushoto

Taarifa ya klabu kupitia mtandao wake imethibitisha kuwa mchezaji huyo atafanyiwa vipimo hivyo kule Turin kunako taasisi ya tiba za michezo

Peluso alijiunga Atalanta mwaka 2009 akitokea AlbinoLeffe na amekwisha itumikia timu ya taifa ya Italia michezo mitatu.


Ronaldo: Nadhani Mourinho atasalia.


Cristiano Ronaldo anaamini kuwa kocha wake Jose Mourinho atasalia katika klabu yake ya Real Madrid.

Mreno huyo ameanza kuona hatma yake katika klabu hiyo kama inamashaka hasa kutoka na gumzo lililoanza kuchomoza hususani kutokana na Madrid kuachwa kwa mbali na mahasimu wao wa soka la Hispania Barcelona kwa tofauti ya alama 16 katika msimamo wa ligi ya Hispania La Liga.

Hata hivyo, Ronaldo haoni kwamba hiyo ndiyo inaweza kuwa sababu ya kumuondosha Mourinho Santiago Bernabeu, na kusisitiza kuwa bado ni mtu sahihi wa kuendelea kuiongoza klabu hiyo.

Akinukuliwa na vyombo vya habari baada ya kuulizwa juu ya uwezekanao wa Mourinho kuondoka Ronaldo alijibu

"Sijui, itategenea na hali ya mambo itakavyokuwa ndani ya klabu, kwa upande wangu ningependa asalie kwakuwa ni kocha sahihi. Ni kocha wa kiwango cha juu katika timu ya kiwango cha juu. Nadhani atasalia lakini kila mtu ana uchaguzi wake wa mambo yake ya baadaye"

Mourinho alianza kuingia matatizoni kuanzia pale alipoamua kumuweka benchi mlinda mlango namba moja Iker Casillas na kupelekea kichapo kutoka kwa Malaga, lakini Ronaldo anasema maamuzi ya kocha ni ya mwisho.

WAKALA: Pato anaelekea kukamilisha uhamisho wake  Corinthians.

Mshambuliaji wa AC Milan Alexandre Pato anakaribia kukamilisha taratibu za uhamisho wake kuelekea Corinthians, hii ni kwa mujibu wa wakala wa mchezaji huyo Gilmar Veloz.

Kipindi cha utumishi wake wa miaka 23 katika viunga vya San Siro ulitiwa doa na majeraha ambapo taarifa zinasema sasa ameamua kurejea katika ardhi ya nyumbani.

Kuna vilabu kadhaa barani ulaya vimekuwa katika mawindo ya kumtaka Pato, lakini mwakilishi wake amesisitiza kuwa Pato atarejea nyumbani Brazil hivi karibuni.

Benitez: Torres yuko tayari kuwekwa benchi falcao anakuja.
Kocha wa muda wa Chelsea Rafael Benitez, amesisitiza kuwa Fernando Torres atamuelewa tu endapoa atalamika kumuweka benchi katika baadhi ya michezo, wakati huu ambapo klabu hiyo inataka kusajili vijana zaidi katika safu yake ya ushambuliaji katika kipindi hiki cha dirisha dogo la usajili.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Hispania alikuwa akihangaika katika kipindi kirefu kusaka kurejesha kiwango chake  tangu aliposajiliwa kutoka Liverpool januari 2012 ambapo angalau kiwango hicho kimeongezeka mara baada ya kuwasili kwa Bernitez.
Mwezi wa November, klabu hiyo kutoka kaskazini mwa jiji la London ilikuwa katika mazungumzo na mshambuliaji wa Atletico Madrid Radamel Falcao ambapo Benitez anaamini kuwa mchezaji huyo ataleta ushinda wenye afya zaidi katika safu yake ya ushambuliaji.

LEO CHELSEA, EVERTON, LIVERPOOL, QPR, SUNDERLAND & NEWCASTLE UWANJANI!!

BENITEZ-CHELSEALEO Timu 6 za BPL, Barclays Premier League, zitashuka dimbani kucheza Mechi zao za kwanza za Mwaka mpya 2013 na zifuatazo ni DONDOO MUHIMU za MECHI HIZO ZIKIWEMO HALI ZA WACHEZAJI na REKODI ZAO za USO KWA USO:
+++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
CHELSEA v QPR
Hali za Wachezaji
Kipa wa Chelsea Petr Cech ataikosa Mechi hii baada ya kuumia nyonga juzi walipocheza na Everton na nafasi yake itashikwa na Turnbull
Nae Nahodha wa Chelsea John Terry bado yupo nje akiwa ni majeruhi.
Bosi wa QPR Harry Redknapp amesema atawakosa Wachezaji watatu au wanne walioumia walipocheza juzi na Liverpool lakini amekataa kutaja Majina yao.
Uso kwa Uso
-Katika Mechi 11 za Ligi Kuu England walizokutana, QPR wameshi 2 na Chelsea 5.    -QPR hawajashinda Stamford Bridge tangu walipopata ushindi wa 2-0 Aprili 1983.
LIVERPOOL v SUNDERLAND
Hali za Wachezaji
Liverpool watamkosa Beki wao wa kushoto Jose Enrique ambae ameumia musuli za pajani na huenda Winga wao Stewart Downing akalazimika kucheza nafasi hiyo.
Beki wa Sunderland John O'Shea hatacheza baada ya kuumia walipocheza na Spurs Jumamosi iliyopita lakini Fulbeki Danny Rose atarudi kilingeni baada ya kuzuiwa kucheza dhidi ya Spurs kwa vile ndio Klabu yake na yeye yupo Sunderland kwa Mkopo.
Uso kwa Uso
-Sunderland hawajahi kuifunga Liverpool Uwanjani Anfield tangu Ligi Kuu England ianzishwe na wameshacheza Mechi 11 za Ligi hiyo.
- Sunderland wameifunga Liverpool mara 3 tu katika Mechi za Ligi Kuu England katika Mechi 23 walizocheza kati yao.
NEWCASTLE v EVERTON
Hali za Wachezaji
Newcastle hawatakuwa nae Danny Simpson alievunjika kidole cha mguu walipocheza na Arsenal hivi majuzi na ingawa Kiungo Yohan Cabaye na Beki Steven Taylor wameshaanza mazoezi baada ya kuwa majeruhi kwa kipindi sasa lakini Mechi hii ni mapema kwao kuingia dimbani.
Everton wanamkaribisha Nyota wao na Mfungaji wao Bora Marouane Fellaini ambae amemaliza Kifungo chake cha Mechi 3 lakini watamkosa Kiungo Darron Gibson ambae atakuwa nje kwa Mwezi mmoja baada ya kuumia paja.
Uso kwa Uso
-Katika Mechi 163 kati yao, kila moja imeshinda Mechi 64 na sare 35.
-Everton wameshinda Mechi 1 tu kati ya 10 walizocheza mwisho Uwanja wa St James Park nyumbani kwa Newcastle.
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO_Timu za Juu:
1 Man Utd Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 26] Pointi 52
2 Man City Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 22] Pointi 45
3 Tottenham Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 12] Pointi 39
4 Chelsea Mechi 19 [Tofauti ya Magoli 21] Pointi 38
5 Arsenal Mechi 20 [Tofauti ya Magoli 18] Pointi 34
6 Everton Mechi 20 [Tofauti ya Magoli 8] Pointi 33
7 West Brom Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 2] Pointi 33
8 Swansea Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 5] Pointi 29
9 Stoke Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 1] Pointi 29
10 Liverpool Mechi 20 [Tofauti ya Magoli 5] Pointi 28
11 West Ham Mechi 20 [Tofauti ya Magoli 0] Pointi 26
12 Norwich Mechi 21 [Tofauti ya Magoli -10] Pointi 25
13 Fulham Mechi 21 [Tofauti ya Magoli -5] Pointi 24
14 Sunderland Mechi 20 [Tofauti ya Magoli -5] Pointi 22
15 Newcastle Mechi 20 [Tofauti ya Magoli -11] Pointi 20
16 Aston Villa Mechi 21 [Tofauti ya Magoli -24] Pointi 19
17 Southampton Mechi 20 [Tofauti ya Magoli -11]  Pointi 18
18 Wigan Mechi 21 [Tofauti ya Magoli -17] Pointi 18
19 Reading Mechi 20 [Tofauti ya Magoli -17] Pointi 13
20 QPR Mechi 20 [Tofauti ya Magoli -20] Pointi 10
+++++++++++++++++++++++
RATIBA MECHI ZIJAZO:  
**WIKIENDI YA JANUARI 5 MECHI ZA RAUNDI YA 3 FA CUP
Jumamosi 12 Januari 2013
[SAA 12 Jioni]
Aston Villa V Southampton
Everton V Swansea
Fulham V Wigan
Norwich V Newcastle
Reading V West Brom
Stoke V Chelsea
Sunderland V West Ham
Jumapili 13 Januari 2013
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Man United V Liverpool
[SAA 1 Usiku]
Arsenal V Man City
Jumatatu 14 Januari 2013
[SAA 5 Usiku]
QPR V Tottenham
Jumamosi 19 Januari 2013
[SAA 12 Jioni]
Liverpool V Norwich
Man City V Fulham
Newcastle V Reading
Swansea V Stoke
West Ham V QPR
Wigan V Sunderland
[SAA 2 na Nusu Usiku]
West Brom V Aston Villa
Jumapili 20 Januari 2013
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Chelsea V Arsenal
[SAA 1 Usiku]
Tottenham V Man Utd
Jumatatu 21 Januari 2013
[SAA 5 Usiku]
Southampton V Everton
Jumatano 23 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Arsenal V West Ham
**WIKIENDI YA JANUARI 26 MECHI ZA RAUNDI YA 4 FA CUP
Jumanne 29 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Aston Villa V Newcastle
Norwich V Tottenham
QPR V Man City
Stoke V Wigan
Sunderland V Swansea
[SAA 5 Usiku]
Reading V Chelsea
Jumatano 30 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Arsenal V Liverpool
Everton V West Brom
Fulham V West Ham
[SAA 5 Usiku]
Man United V Southampton

VAN DER VAART ATENGANA NA MKEWE BAADA YA KUMSHUSHIA KIPIGO

.

KIUNGO nyota wa zamani wa klabu ya Tottenham Hotspurs na Real Madrid, Rafael van der Vaart ametengana na mkewe Sylvie baada ya nyota huyo kukiri kumpiga. Van der Vaart ambaye kwasasa anacheza katika klabu ya Hamburg ya nchini Ujerumani aliingia katika mzozo na mkewe wakatiwa shereheza kuukaribisha mwaka mpya na inaaminika kuwa alimpiga mbele ya wageni waliokuwepo katika sherehe ndogo waliyoandaa. Kiungo huyo alikiri kosa hilo na kudai kufanya jambo la kijinga na kuomba radhi wakati akihojiwa na gazeti moja nchini Ujerumani huku mke wake nae akidai kumsamehe mumwe huyo kwa kosa alilofanyiwa. Lakini pamoja na mkewe kumsamehe kiungo huyo wawili hao walitangaza kutengana baadae ikiwa ni wiki baada ya kufurahia sherehe za Noel wakiwa pamoja na mtoto wao Damian na kutuma picha ya pamoja katika mtandao wa kijamii wa Twitter.

BPL: ARSENAL YAKWAMA NAFASI YA 5!!

BPL_LOGO>>SOUTHAMPTON 1 ARSENAL 1
>>MECHI INAYOFUATA YA LIGI: ARSENAL v MAN CITY!!
+++++++++++++++++++++++
MATOKEO:
Jumanne 1 Januari 2013
West Brom 1 Fulham 2
Man City 3 Stoke 0
Swansea 2 Aston Villa 2
Tottenham 3 Reading 1
West Ham 2 Norwich 1
Wigan 0 Man United 4
Southampton 1 Arsenal 1
+++++++++++++++++++++++
Southampton leo wamejikwamua kutoka mkiani mwa Ligi Kuu England baada ya kutoka sare 1-1 na Arsenal Uwanjani na, pengine, ilikuwa bahati mbaya kwao kwa kutonyakua Pointi zote 3 kwa jinsi gemu ilivyokuwa.
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO_Timu za Juu:
1 Man Utd Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 26] Pointi 52
2 Man City Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 22] Pointi 45
3 Tottenham Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 12] Pointi 39
4 Chelsea Mechi 19 [Tofauti ya Magoli 21] Pointi 38
5 Arsenal Mechi 20 [Tofauti ya Magoli 18] Pointi 34
6 Everton Mechi 20 [Tofauti ya Magoli 8] Pointi 33
7 West Brom Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 2] Pointi 33
8 Swansea Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 5] Pointi 29
9 Stoke Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 1] Pointi 29
10 Liverpool Mechi 20 [Tofauti ya Magoli 5] Pointi 28
+++++++++++++++++++++++
Sare hii imewafanya Southampton washike nafasi ya 17 na kuwaacha Wigan, Reading na QPR mkiani.
Southampton ndio waliotangulia kufunga Bao kupitia Gaston Ramirez katika Dakika ya 34 lakini kwenye Dakika ya 41 Guly do Prado alijifunga mwenyewe akijaribu kuokoa friki ya Theo Walcott.
VIKOSI:
Southampton: Boruc, Cork, Yoshida, Fonte, Shaw, Puncheon, Steven Davis, Schneiderlin, Ramirez, Lambert, Do Prado
Akiba: Kelvin Davis, Hooiveld, Rodriguez, Ward-Prowse, Richardson, Mayuka, De Ridder.
Arsenal: Szczesny, Sagna, Koscielny, Vermaelen, Gibbs, Arteta, Wilshere, Oxlade-Chamberlain, Cazorla, Podolski, Walcott
Akiba: Martinez, Mertesacker, Rosicky, Giroud, Ramsey, Coquelin, Gervinho.
Refa: Lee Probert
+++++++++++++++++++++++
RATIBA:  
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
**WIKIENDI YA JANUARI 5 MECHI ZA RAUNDI YA 3 FA CUP
Jumamosi 12 Januari 2013
[SAA 12 Jioni]
Aston Villa V Southampton
Everton V Swansea
Fulham V Wigan
Norwich V Newcastle
Reading V West Brom
Stoke V Chelsea
Sunderland V West Ham
Jumapili 13 Januari 2013
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Man United V Liverpool
[SAA 1 Usiku]
Arsenal V Man City
Jumatatu 14 Januari 2013
[SAA 5 Usiku]
QPR V Tottenham
Jumamosi 19 Januari 2013
[SAA 12 Jioni]
Liverpool V Norwich
Man City V Fulham
Newcastle V Reading
Swansea V Stoke
West Ham V QPR
Wigan V Sunderland
[SAA 2 na Nusu Usiku]
West Brom V Aston Villa
Jumapili 20 Januari 2013
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Chelsea V Arsenal
[SAA 1 Usiku]
Tottenham V Man Utd
Jumatatu 21 Januari 2013
[SAA 5 Usiku]
Southampton V Everton
Jumatano 23 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Arsenal V West Ham
**WIKIENDI YA JANUARI 26 MECHI ZA RAUNDI YA 4 FA CUP
Jumanne 29 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Aston Villa V Newcastle
Norwich V Tottenham
QPR V Man City
Stoke V Wigan
Sunderland V Swansea
[SAA 5 Usiku]
Reading V Chelsea
Jumatano 30 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Arsenal V Liverpool
Everton V West Brom
Fulham V West Ham
[SAA 5 Usiku]
Man United V Southampton

MAN U WAUANZA MWAKA WA 2013 KWA NEEMA NA BAADA MECHI ZA MWAKA MPYA, NINI WAMESEMA!

>>PULIS: "TOFAUTI YA STOKE NA CITY NI PAUNI MILIONI 220!!"
>>RVP: “NI TIMU SPESHO! NIMEZUNGUKWA NA MABINGWA!”
>>WENGER: “GEMU YETU ILIKOSA MALENGO!”
FERGIE_n_WENGER-KICHEKOMan City 3-0 Stoke
Meneja wa Stoke Tony Pulis: "Sina malalamiko, wao walikuwa Timu bora! Kuna Mtu aliniuliza nini tofauti kati ya Stoke na City na nilijibu Pauni 220 Milioni!” 
Wigan 0-4 Man Utd
Bosi wa Manchester United Sir Alex Ferguson: "Wigan ni Timu ngumu kucheza nayo kwao, kupata ushindi wa 4-0 ni matokeo mazuri kwetu! Javier Hernandez ni Mfungaji na ni Mchezaji hatari ndani ya boksi! Van Persie ni Mchezaji wa kipekee na Goli lake la kwanza lilikuwa zuri sana! Tulijua yeye Ni mchezaji bora na atatuongezea kitu hapa na hilo ndio amefanya!"
Robin Van Persie: “Hii ni Timu spesheli! Kila Mchezaji anamsaidia mwenzake! Sisi tunakabili Gemu kwa gemu lakini kila Mtu anataka kuwa Bingwa! Nahisi nimezungukwa na Mabingwa! Wanajua namna ya kushinda na hilo hufanya kazi yangu kuwa rahisi!”
Tottenham 3-1 Reading
Meneja wa Tottenham Andre Villas-Boas: "Tumefanya vyema kwa kumaliza Kipindi hiki kigumu cha Krismasi na Mwaka mpya kwa kupata Pointi 10 katika Mechi 4."
Swansea 2-2 Aston Villa
Bosi wa Aston Villa Paul Lambert: "Zikibakia Sekunde 30 unategemea ushindi! Tuna majeruhi wengi lakini Wachezaji wanahitaji pongezi! Tumetoka kipindi kigumu na matokeo haya yana afadhali!”
Southampton 1 Arsenal 1
Bosi wa Arsenal Arsene Wenger: “Hatukutengeneza nafasi nyingi baada ya kufunga 5 na Reading na 7 na Newcastle! Gemu yetu ilikosa malengo, tulishindwa kupenya, hatukuwa na spidi-sifa zote ambazo kawaida tunazo!”

WENGER ACHOMOA KUMREJESHA HENRY EMIRATES.


MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger ameondoa uwezekano wa kumsajili tena kwa mkopo mshambuliaji nyota wa zamani wa klabu hiyo Thierry Henry. Henry mwenye umri wa miaka 35 amekuwa akifanya mazoezi na klabu hiyo ili kujiweka katika hali nzuri kufuatia kumalizika kwa msimu wa Ligi Kuu nchini Marekani-MLS akiwa na na timu ya New York Red Bulls. Wenger amesema nyota huyo hayuko fiti kwasababu ndio kwanza amerejea kutoka mapumzikoni hivyo kwasasa suala la kumsajili halipo. Henry alirejea katika klabu yake hiyo ya zamani mwaka 2011 baada ya kuondoka mwaka 2007 na kujiunga na Barcelona na kufunga bao pekee katika mchezo wa Kombe la FA dhidi ya Leeds United.

NITAPIGANIA NAMBA YANGU - CASILLAS.


NAHODHA wa klabu ya Real Madrid, Iker Casillas amesisitiza kuwa ameongeza muda wa kujifua mazoezini ili aweze`kupata namba tena katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo. Casillas mwenye umri wa miaka 31 alienguliwa katika kikosi cha kwanza wakati Madrid ilipokubali kipigo cha mabao 3-2 dhidi ya Malaga na kocha wake Jose Mourinho na nafasi yake kuchukuliwa na golikipa namba mbili Antonio Adan. Hatahivyo akiongea na waandishi wa habari baada ya mazoezi ya kwanza ya Madrid baada ya mapumziko ya kipindi cha baridi, golikipa huyo amesema anajitahidi kufanya kila awezalo ili aweze kupigania namba yake katika kikosi cha kwanza. Casillas amesema kocha ndio mwenye maamuzi ya kuamua nani acheze na asicheze katika mchezo unaofuata na wote wanamuunga mkono Mourinho na wana imani naye kwa maamuzi atakayochukua. Madrid kwasasa iko katika nafasi ya tatu katika msimamo wa La Liga kwa tofauti ya alama 16 na mahasimu wao Barcelona ambao wanaongoza msimamo wa ligi hiyo.

FRANK DOMAYO, MWINYI KAZIMOTO WACHONGANISHWA TUZO YA KIUNGO BORA TANZANIA



KAMATI ya maandalizi ya Fainali ya tuzo za Mwanasoka Bora wa mwaka (Wazalendo Footballer of the Year), imekamilisha mchakato wa kupitisha majina ya wanasoka walioingia katika fainali ya tuzo hizo mwaka 2012.
Taarifa ya Mratibu, Ahadi Kakore imesema katika mchakato huo kamati iliweza kuangalia  vigezo vikuu vinne ambavyo ndivyo vitaendelea kuwa dira na mwongozo hadi siku ya fainali Januari 31 mwaka 2013.
“Awe ni mchezaji wa timu ya taifa,  mchango wake katika klabu yake na timu ya taifa, nidhamu kwa ujumla ndani na nje ya uwanja na asiwe na kashfa ya utumiaji wa dawa zilizopigwa marufuku michezoni ikiwemo dawa za kulevya,”imesema taarifa hiyo.
Taarifa ya Kakore imesema wapo wachezaji ambao hawajaweza kuwa na vigezo vyote lakini akawa navyo viwili kati ya hivyo aliweza kupita. Kwa mfano wapo wachezaji ambao uwezo wao ni wa hali ya juu ambapo wanastahili kucheza timu ya taifa lakini wameshindwa kupata nafasi kutokana na sababu mbalimbali lakini uwezo wake hauna shaka hivyo ni ngumu kumtoa kwenye kinyang’anyiro hiki.
Tuzo hizo zimegawanyika katika makundi tofauti tofauti ambapo jumla ya tuzo zote ni 12 kutokana na ukweli kwamba katika tuzo za maendeleo ya soka la wanawake zipo tuzo mbili ya wanaume na wanawake.
Mgawanyo wa tuzo hizo ni kama ifuatavyo; Kipa Bora, Beki Bora, Kiungo Bora, Mshambuliaji Bora, Mchezaji anayechipukia, Mchezaji Bora wa Kike, Mchezaji Bora Kigeni, Mchezaji bora wa zamani, Maendeleo soka la Wanawake, Mwanasiasa wa Afrika aliyesadia maendeleo ya michezo pamoja na tuzo kubwa ya Mwanasoka Bora wa mwaka 2012. Fainali ya hizo zitafanyika Januari 31 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
WALIOPITISHWA KUWANIA TUZO:
Kundi A: Kipa Bora
Mwandini Ally- Azam FC, Juma Kaseja- Simba, Shaaban Kado- Mtibwa Sugar, Ally Mustapha-Yanga, Jackson Chove-Coastal Union, Deogratius Munishi- Azam FC
Kundi B: Beki Bora
Nassor Said – Simba, Nadir Haroub – Yanga, Agrey Morris- Azam FC, Amir Maftah- Simba, Kelvin Yondan-Yanga  na Shomari Kapombe-Simba.
Kundi C: Kiungo Bora
Shaban Nditi –Mtibwa, Frank Domayo- Yanga, Mwinyi Kazimoto-Simba, Amri Kiemba-Simba, Chande Mgoja- Mgambo JKT na Abubakar Salum-Azam FC.
Kundi D: Mshambuliaji Bora
John Bocco - Azam FC, Mrisho Ngassa – Simba, Hussein Javu -Mtibwa FC, Amiry Omary-JKT Oljoro, Simon Msuva-Yanga, Nsa Job-Coastal Union.
Kundi E: Mchezaji anayechipukia
Mudasir Yahya-Azam FC, Ramadhan Singano-Simba, Edward Christopher-Simba, Manyika Peter Manyika- Mgambo JKT, Miraji Adam-Simba na Chande Mgoja- Mgambo JKT
Kundi F: Mchezaji Bora wa Kike
Ester Chabruma-Sayari Queens, Mwanahamisi Omar-Mburahati Queens, Mwapewa Mtumwa-Ever Green, Fatuma Mustafa-Sayari Queens, Asha Rashid-Mburahati Queens na Sophia Mwasikili-Luleburgaz Spor Kulubu- Uturuki.
Kundi H: Mchezaji Bora wa mwaka 2012
Mchezaji atakayetwaa tuzo hii atatoka katika makundi yaliyotajwa hapo juu hii ikiwa na maana kwamba kuanzia kundi A-E. hii ni kumaanisha kuwa wanawake hawataingia kwenye kundi hili wala kwa sababu tayari wanayio tuzo yao tayari kama inavyoonekana katika kipengele F.
Kundi I: Mchezaji Bora Kigeni
Haruna Niyonzima-Yanga, Kipre Tchetche-Azam FC, Emmanuel Okwi-Simba,  Felix Sunzu-Simba, Hamis Kiiza-Yanga na Jerry Santo-Coastal Union.
TUZO ZA HESHIMA
Kundi H: Mchezaji bora wa zamani
Madaraka Suleiman – Simba, Edibily Lunyamila-Yanga/Simba/Twiga FC,
Mohamed Mwameja-Simba, Yusuf Macho-Simba/Kagera Sugar, Zamoyoni Mogela-Simba/Yanga na Kenny Mkapa-Yanga.
Kundi I: Maendeleo soka la Wanawake (tuzo mbili Mwanamke na Mwanaume)
Stephania Kubumba-Sayari, Arafa Tamba-Mburahati Queens, Fatma Makambara-Sayari, Pili Kambangwa- Mchangani, Joha Halfan-Vijana Queens, Amin Bakhresa, Frenk Mchaki na  Idd Azan.
Kundi J:Mwanasiasa wa Afrika aliyesadia maendeleo ya michezo
Benjamin Mkapa-Tanzania, Daniel Arap Moi-Kenya na Joachim Chisano-Msumbiji
Katika kipengere hiki ni kwamba kilichoangaliwa ni namna gani mwanasiasa mstaafu alivyweza kusaidia michezo kwa ujumla ikiwemo soka. Hapa inaangaliwa ujewekaji wa miundo mbinu, kama ujezi wa viwanja vya michezo, mafanikio katika klabu na  timu za taifa katika nchi ambayo amekuwa akiiongoza.
Pia kipengere hiki pia kinaangalia katika kipindi kisichozidi miaka 10 ya utawala akiwa kama mkuu wa nchi husika.
Baada ya kufuatilia kwa takriban mwaka mmoja katika nchi zilizopo jirani na Tanzania, imeonekana wazi kuwa viongozi hao wastaafu ndiyo wenye waliofikia viwango ambavyo kamati ilivihitaji.

MFARANSA WA SIMBA AAHIDI KUVUNJA REKODI YA SIANG'A 2003 SIMBA SC


Liewig kushoto akisaini mkataba jana. Kulia Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey Nyange 'Kaburu'

KOCHA mpya wa Simba SC, Mfaransa Patrick Liewig amesema kwamba lengo lake ni kuifikisha klabu hiyo katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka huu na anaamini hilo linawezekana kwa kuwa timu ina wachezaji wazuri.
Akizungumza  jana, Liewig alisema kwamba ana imani Simba ni timu nzuri, kwa sababu katika kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kilichoifunga 1-0 Zambia, kulikuwa kuna wachezaji wengi wa Simba SC.
“Zambia ni timu nzuri, ni mabingwa wa Afrika, kama Tanzania iliifunga Zambia ikiwa na wachezaji wengi wa Simba, sioni kwa nini tusifike Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa,”alisema Liewig.
Liewig alisema leo anakwenda Zanzibar kuungana na kikosi cha timu hiyo ambacho kitakuwa kikishiriki Kombe la Mapinduzi.
“Nitakutana na wenzangu katika benchi la ufundi huko, Julio (Jamhuri Kihwelo) na Moses (Basena), tutashirikiana kufanya kazi, baada ya hapo tutakwenda Oman, tukirudi tutaanza Ligi (Kuu) na Ligi ya Mabingwa.
Nimeambiwa pia kuna Kombe la Kagame (Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati) Rwanda, tutakwenda, pamoja na yote, nitashughulikia pia na program ya vijana, lazima tuibue vipaji kutoka chini,”alisema.  
Simba SC itaanza na Recreativo de Libolo ya Angola, katika Raundi ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Februari 17 hadi 19 na kurudiana nayo kati ya Machi 2 na 4, mwakani.
Mara ya mwisho Simba SC kucheza hatua ya makundi ya michuano hiyo ilikuwa mwaka 2003, wakati huo ikiwa chini ya kocha Mkenya, James Aggrey Siang'a.
Liewig jana alisaini mkataba wa miezi 18 kuifundisha Simba, akimpokea Mserbia Milovan Cirkovick aliyetupiwa virago baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Bara. 
Liewig ni kocha wa zamani wa Akademi ya Paris Saint Germain (PSG) ya Ufaransa, ASEC Mimosas ya Ivory Coast na Club Africain ya Tunisia, ambaye ana Stashahada ya Juu ya ukocha na Shahada ya tatu ya ualimu wa soka ya vijana aliyotunukiwa na Mkurugenzi wa Ufundi wa Ufaransa, Gerard Houiller, anatarajiwa kwenda Zanzibar kesho.
Liewig pia amehudhuria kozi za ufundishaji mazoezi ya viungo Juni mwaka 1999 katika Chuo Kikuu cha Dijon.
Kwa upande wa uzoefu, Liewig alifanya kazi PSG kuanzia mwaka 1989 hadi 1999 kama Kocha Mkuu wa akademi na kuna wakati alikuwa akishirikishwa pia katika programu za timu A, ingawa majukumu yake zaidi yalikuwa ni kwa Under 20, Under 18 aliowawezesha kutwaa Kombe la French Junior Gambardella na Under 16.
Kuanzia mwaka 1989 hadi 1990:  alikuwa Meneja Mkuu wa Tomislav IVIC, 1990 hadi 1991 alikuwa Msaidizi wa Henri Michel, 1991 hadi 1994 alikuwa Msaidizi wa Artur Jorge, 1994 hadi 1996 alikuwa Msaidizi wa Luis Fernandez, 1996 hadi 1998: alikuwa Msaidizi wa Ricardo Gomez, 1998 hadi 1999 alikuwa Msaidizi wa Alain Giresse.
Liewig pia alifundisha Al Wahda FC ya Abu Dhabi kuanzia 1999 hadi 2001, ambayo aliipa ubingwa wa Ligi Kuu ya nchi hiyo na Kombe la Ligi.
Januari mwaka 2003 alikuwa Msimamizi wa Chama cha Soka UAE katika fainali za Afrika za U20 nchini Burkina Faso.
Kuanzia mwaka 2004 hadi 2009 alikuwa Kocha wa ASEC Mimosas ya Ivory Coast aliyoipa mataji matatu ya Ligi Kuu ya nchini humo mfululizo, 2004, 2005 na 2006, Super Cup ya nchini humo 2005, 2007, 2008 na 2009 na akaiwezesha kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa mara tatu, mara moja akiifikisha Nusu Fainali.
Amekuwa Kocha bora wa Ivory Coast miaka mitatu mfululizo, 2004, 2005 na 2006 na tangu Septemba mwaka jana hadi Juni mwaka huu, alikuwa kocha wa Club Africain ya Tunisia

UMONY AWASILI DAR, AENDA NA AZAM ZANZIBAR LEO


Umony
MCHEZAJI bora wa Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Kagame, Brian Umony amewasili jana kujiunga na timu yake mpya, Azam FC na leo mchana atakuwamo kwenye msafara unaokwenda Zanzibar kutetea Kombe la Mapinduzi.
Brian alirejea nyumbani Uganda mwaka jana na kujiunga na KCC baada ya kumaliza mkataba wake katika klabu ya Becamex Binh Duong F.C. ya Vietnam.
Mwaka 2009, ilikuwa aje kuichezea Simba SC ya Dar es Salaam, lakini Wekundu hao wa Msimbazi wakazidiwa kete na SuperSport United ya Afrika Kusini.
Umony aliichezea Supersport United hadi 2010 alipohamia University of Pretoria ya Afrika Kusini pia hadi mwaka 2011 alipohamia Portland Timbers ya Marekani kwa mkopo na mwaka huu akatua Becamex Binh Duong F.C. kabla ya kurejea Uganda na sasa anakuja kuanza maisha mapya Azam FC 2013.
Azam wamepangwa Kundi B, katika Kombe la Mapinduzi pamoja na Mtibwa Sugar ya Morogoro, Coastal Union  ya Tanga na Miembeni ya Unguja, wakati Kundi A lina timu za Simba SC, Tusker FC ya Kenya, Bandari ya Unguja na Jamhuri ya Pemba.
Michuano ya Kombe la Mapinduzi, ambayo ni maalum kwa ajili ya kuherehekea Mapinduzi matukufu ya Zanzaibar, inatarajiwa kuanza kutimua vumbi leo hadi kilele cha miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Januari 12, mwakani, huku ikishirikisha timu kutoka ndani na nje ya Tanzania.

DHAIRA ATUA LEO SIMBA SC, KASEJA AJIENGUA KOMBE LA MAPINDUZI


Abbel Dhaira
KIPA namba moja wa Uganda, Abbel Dhaira anatarajiwa kuwasili leo saa 8:00 mchana kujiunga na klabu yake mpya, Simba SC ya Dar es Salaam, akitokea kwao Uganda.
Dhaira aliyesaini mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya dola za Kimarekani 40,000, na mshahara wa Sh. Mlioni 2 kwa mwezi, baada ya kutua Dar es Salaam atakwenda moja kwa moja Zanzibar, ambako Simba itashiriki Kombe la Mapinduzi.
Kikosi kizima cha Simba, kasoro Nahodha Juma Kaseja, Emmanuel Okwi, Amir Maftah na Amri Kiemba kitaondoka leo mchana kwenda Zanzibar, tayari kwa michuano ya Mapinduzi.
Dhaira aliyeibukia Express ya Uganda mwaka 2006, mwaka 2008 alihamia U.R.A. pia ya Uganda, ambayo aliichezea hadi mwaka 2010 alipohamia Ulaya.
Kwa kumpata Dhaira, Simba SC imepata kipa wa uhakika wa kusaidiana na kipa wake wa kwanza, Juma Kaseja ambaye amekuwa akisoteshwa peke yake bila kupumzika. Na hiyo inafuatia makipa wengine, Wilbert Mweta na Hamadi Waziri kushindwa kuonyesha uwezo wa kumsaidia Kaseja.
Katika mechi za mwishoni za mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara, Kaseja alionekana kuchoka na kudaka chini ya kiwango chake, jambo ambalo lilisababisha mashabiki wenye ‘akili mbovu’ wamfanyie fujo baada ya kufungwa mabao mawili katika mechi dhidi ya Mtibwa Sugar, Simba ikilala 2-0.
Kwa sababu hiyo, Kaseja alikasirika na kujiengua kwenye kikosi cha timu hiyo akisema hataki tena kuchezea Simba.
Lakini pamoja na matatizo hayo, Kaseja ameendelea kuitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ambako ameendelea kufanya vizuri na kuonyesha yeye ni Tanzania One wa ukweli. 

R.I.P JUMA KILOWOKO ....SAJUKI NA MWENYEZI MUNGU AKUPUMZISHE KWA AMANI HUKO UENDAKO


INNA LILLAH WAINNA ILAIH RAAJIUN, hivi ndivyo waislam wanavyopaswa kusema unapotokea msiba. Juma Kilowoko “Sajuki”, hatunae tena, amefariki leo afajiri saa 12.
Sajuki amefariki katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, alipokuwa amelazwa kwa zaidi ya wiki moja.
Sajuki (kulia) akiwa na mkewe, Wastara enzi za uhai wake
Imekuwa ngumu sana kuamini kuwa Sajuki amefariki kutokana na ukweli kuwa mara kadhaa msanii huyo amezushiwa kifo, lakini hatimaye sasa Mungu amempenda zaidi Sajuki.
Marehemu Juma Kilowoko "Sajuki"
Kwa mujibu wa mdogo wa marehemu, Mohameid Said aliyekuwa analala na marehemu hospitalini hapo, hali ya Sajuki ilibadilika ghafla na kufariki alfajiri ya leo.
Mohamed ameimbia Saluti5 kuwa msiba utakuwa Tabata Bima nyumbani kwa marehemu, lakini akaongeza kuwa bado ni mapema mno kueleza Sajuki atazikwa lini na wapi.
“Kwa bahati nzuri Baba na Mama wapo hapa Dar, watatoa uamuzi baadae kama marehemu atazikwa Dar au Songea” alisema Mohamed katika maongezi yake na Saluti5.
Songea ni nyumbani kwa kina Sajuki na ndipo wanapoishi wazazi wake.