Wednesday, January 30, 2013

JEMBE LA CHELSEA MOSES LAIOKOA SUPER EAGLES KUCHEZA ROBO FAINALI AFCON CUP

MANCINI HALI TETE ABANWA MBAVU NA QPR BPL HIYO JANAAAAA

LULU ARUDI URAIANI KWA DHAMANA NA AANGUA KILIO CHA FURAHA BAADA YA KUACHIWA


Msanii  Elizabeth "Lulu" Michael tayari amerudi uraiani baada ya kuachiwa kwa dhamana katika mahakama kuu jijini Dar. Licha ya kukamilisha kwa masharti yote aliyopewa jana ikiwa ni pamoja na kutoa milioni 20 kwa wadhamini wawili, kuripoti kila mwanzo wa mwezi na kuacha hati yake ya kusafiria mahakamani hapo, Lulu hakufanikiwa kutoka kwa kile kilichoripotiwa kutokuwepo kwa msajili , hivyo kumlazimu kurudi gerezani

Lulu (katikati) akiwa mwenye majonzi na furaha hapa akitokwa na machozi wakati msemaji wa familia Msanii Dr Cheni akizungumza . Lulu amewaomba watanzania wote wamuombee maana hii ni dhamana tu na kesi yake bado inaendela.


LULU na Mama yake mzazi ndani ya gari tayari kwa safari ya kurudi nyumbani
Wakili wake Ndugu Flugence Massawe amesema kwamba hii ni hatua ya kwanza kwasababu case bado inaendelea. Kwa sasa wanasubiri mahakama itoe tarehe ya Lulu kurudi mahakamani.

KIGWA ALL STARZ FC WAFANYA UCHAGUZI WAO JANA JAN.29,2013 KULE WILAYANI UYUI.


Timu ya kigwa all starz jana january 29,2013 ilifanya uchaguzi w aviongozi ndani ya klabu hiyo wilayani uyui  tayari kwa kushiriki ligi daraja la nne mkoani tabora ambayo inatarajia kuanza kutimua vumbi kuanzia mwezi wa pili mpaka mwezi wa tatu.

Uchaguzi huo jana ulihudhuriwa na wajumbe 20 wakiongozwa na katibu wa chama cha FAU wilayani humo na mjumbe wa kamati tendaji mkoani tabora TAREFA BW.James erick kabepele ,viongozi waliochaguliwa hiyo jana katika nafasi ya mwenyekiti alichaguliwa masinde jonas,na nafasi ya makamu mwenyekiti alichaguliwa mrisho sinundo,kalangu magayu alichaguliwa kuwa katibu mkuu wa klabu hiyo na katika nafasi ya katibu msaidizi alichaguliwa swalehe bilali.

Viongozi wengine waliochaguliwa ni pamoja na hamis mpuma mtunza pesa za klabu na anania lameck alichaguliwa kuwa mjumbe wa mkutano mkuu,na katika nafasi ya kamati ya utendaji walichaguliwa abeid hassan,salum kaswiza,pamoja na minazi rashid.na katika nafasi ya mwakilishi wa klabu kwa upande wa kinamama alichaguliwa ndugu farida ismail.

Katika uchaguzi huo wanachama wa klabu waliadhimia kuwachagua wazee wa timu ili iweze kuwa na taswira ya kisoka nao ni pamoja na sheikh sadala,donard nhwale,,zyagi mmanywa,karenga,msemo,mussa mrisho na wilbert kayanda.

Na makocha wa timu hiyo walichaguliwa akina mnazi rashidy,na kocha na msaidizi ni hussein kitala na makapteni w atimu hiyo ni kulwa jarufu na rashidy majaliwa.

OBI MIKEL ATAMBA NIGERIA KUCHUKUA AFCON.


KIUNGO nyota wa kimataifa wa Nigeria, John Obi Mikel amedai kuwa timu yake ya taifa itaibuka kidedea katika michuano ya Mataifa ya Afrika inayoendelea nchini Afrika Kusini baada ya kutinga hatua ya robo fainali. Nigeria ilifanikiwa kutinga hatua hiyo jana baada ya kuibugiza Ethiopia kwa mabao 2-0 na sasa wanakabiliwa na mchezo dhidi ya Ivory Coast ambao wanapewa nafasi kubwa ya kutwaa taji la michuano hiyo kutokana nyota wake waliosheheni kwenye kikosi chake. Obi Mikel amesema kutokana na kiwango cha hali walichocheza katika mchezo dhidi ya Ethiopia ana imani kuwa wanaweza kuvuka kikwazo kilichopo mbele yao kama wakiendeleza juhudi zilezile. Nigeria imemaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi C ambalo linaongozwa na Burkina Faso.

SHENHUA KUMSHITAKI DROGBA FIFA.


KLABU ya Shanghai Shenhua ya China imedai kuwa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Ivory Coast Didier Drogba hana haki ya kusaini mkataba katika klabu ya Galatasaray ya Uturuki kwakuwa bado hajamaliza mkataba wake. Galatasaray walithibitisha Jumatau kuwa Drogba mwenye umri wa miaka 34 ameshakubali kusaini mkataba wa miezi 18 na klabu hiyo unaokadiriwa kufikia kiasi cha euro milioni sita huku kiasi euro milioni nne akikabidhiwa nyota huyo. Hatahivyo Shenhua ambao walimsajili Drogba baada ya kuondoka Chelsea katika kipindi cha majira ya kiangazi msimu uliopita walionyesha kushangazwa na taarifa hizo na wameamua kulipeleka Shirikisho la Soka la Dunia-FIFA ili lipate ufumbuzi. Kwasasa Drogba yuko ya timu yake ya taifa katika michuano ya Mataifa ya Afrika inayoendelea nchini Afrika Kusini huku timu yake ikiwa tayari imesonga mbele katika hatua ya robo fainali baada ya kushinda michezo yake miwili ya kwanza.

TOTO TUNDU’ BALOTELLI NJIANI KURUDI KWAO ITALY!!



>>INADAIWA MAN CITY IMEKUBALI KUMUUZA AC MILAN!!
BALOTELLI-WHY_ALWAYS_MEMABINGWA wa England, Manchester City, wameripotiwa kuwa wamekubali kumuuza Mchezaji wao makeke Mario Balotelli kwa AC Milan kwa Dau la Pauni Milioni 17.1.MANCINI_n_BALOTELLI-MSHIKEMSHIKE
Imeripotiwa kuwa Klabu hizo mbili zimefikia makubaliano ambayo malipo ya Dau la Uhamisho yatakuwa kwa awamu kwa Kipindi cha Miaka mitano.
Kabla ya kutua Man City, Balotelli alikuwa akiichezea Timu Mahasimu wa AC Milan, Inter Milan, ingawa yeye mwenyewe amekuwa akikiri tangu utoto wake ni Shabiki wa AC Milan.
Pia, inadaiwa Balotelli atakuwa akilipwa na AC Milan chini ya Mshahara aliokuwa akipata Man City wa Pauni 110,000 kwa Wiki na pia atasaini Mkataba wa Miaka minne.
Makubaliano ya Klabu hizo mbili yanagoja kuhitimishwa kwa Mchezaji huyo kupimwa afya yake huko Milan.
Msimu huu, Balotelli, mwenye Miaka 22, amekuwa hana namba ya kudumu na Man City na tangu Novemba amecheza Mechi 5 tu na Msimu huu ameifungia City Bao 1 tu kwenye Ligi.
Hivi karibuni, Balotelli na Meneja wa Man City Roberto Mancini walinaswa wakivutana Mashati wakati wa Mazoezi ya Timu hiyo na hilo likamfanya atimuliwe toka Timu ya Kwanza lakini baadae akarudishwa tena.
Ripoti za ndani ya Klabu ya Man City zimedai leo Balotelli alitinga Mazoezini mwa Man City na kuwaaga Wachezaji wenzake.

COPA CLASICO: VIKOSI REAL v BARCA VINAJULIKANA LAKINI MAKIPA NANI??


>>NI ADAN v PINTO au LOPEZ v VALDES??
EL_CLASICO-KIPA_NANISIO SIRI, ndani ya Mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya COPA del REY itakayochezwa Santiago Bernabeu Jumatano Usiku kati ya Mahasimu wakubwa Real Madrid na Barcelona, Mechi iliyobatizwa, COPA CLASICO, ni lazima Masupastaa Cristiano Ronaldo wa Real na Lionel Messi wa Barca, panga pangua, wamo Kikosini, lakini hadi sasa kitendawili kikubwa ni NANI WATAKUWA WAKILINDA NYAVU ZA TIMU HIZO MBILI?
Ni wazi Real Madrid watatinga kwenye hii EL CLASICO bila ya Wachezaji wao watano Pepe, Sergio Ramos, Casillas, Coentrao na Di Maria, ambao ni majeruhi na wengine Kifungoni, huku Barca ikiwakosa wawili tu, Eric Abidal na Jonathan Dos Santos.
++++++++++++++++++++++++++++++++
COPA del REY
NUSU FAINALI
Jumatano Januari 30
[SAA 5 Usiku]
Real Madrid v Barcelona
Alhamisi Januari 31
[SAA 6 Usiku]
Atletico Madrid v Sevilla
MARUDIANO
Jumatano Februari 27
Sevilla v Atletico Madrid
Barcelona v Real Madrid
++++++++++++++++++++++++++++++++
Lakini kuumia kwa Nahodha na Kipa wao Nambari wani, Iker Casillas, kuliwalazimu Real Madrid Siku mbili tatu nyuma kumnunua Kipa mpya Diego Lopez kutoka Sevilla ingawa kabla ya kuumia Casillas, Meneja wa Real, Jose Mourinho, alianza kumtema Casillas na kumpa Namba Kipa Nambari mbili, Adan.
Lakini, hadi sasa, Kambi ya Real haijadokeza ni nani atapewa Namba kati ya Nambari mbili Adan na Kipa mpya Lopez.
Huko Barcelona pia upo utata wa nani atakuwa Kipa kwani chini ya Pep Guardiola walikuwa na utamaduni wa kuweka Kipa wao Nambari Wani, Valdes, kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI na Jose Manuel Pinto kwenye Mechi zote za COPA del REY.
Wakiwa na Pinto golini, Barca walitinga Fainali 3 kati ya 4 na kutwaa COPA del REY mara mbili kati ya hizo.
Lakini tangu Kocha Tito Vilanova achukue mikoba ya Pep Guardiola, utamaduni huo wa kubadilisha Makipa kati ya Valdes na Pinto umekuwa haupo na hauna uhakika.
Wakati kukosekana kwa Mastaa watano wa Real, Pepe, Sergio Ramos, Casillas, Coentrao na Di Maria, kunaleta kitendawili kwa Kikosi cha Mabingwa hao wa Spain, huko Barca ni rahisi kuotea nini kitakuwa Kikosi chao ukiondoa nafasi ya Kipa.
Wakati Tito Vilanova bado ni mgonjwa, Barca watakuwa chini ya Kocha Msaidizi Jordi Roura, na pengine ugumu pekee kwake ni yupi aanze Fulbeki ya kulia kati ya Alves na Adriano, na ni rahisi kusema Masentahafu ni Pique na Puyol, Fulbeki kushoto ni Alba.
Katikati kwenye Kiungo ni Iniesta, Xavi, Fabregas na Busquets huku Mastraika ni Messi na Pedro.
NI EL CLASICO……COPA CLASICO!!!!

SIR ALEX KUMVAA PILATO FA!!


>>NI KUHUSU KAULI YAKE KWA REFA MSAIDIZI BAADA SARE NA SPURS!!
>>HADI IJUMAA ATAKIWA KUJIBU MASHITAKA!!
>>MACHI 2011 ALIFUNGIWA MECHI 5 AKIMTUHUMU REFA ATKINSON  KUIPENDELEA CHELSEA!!
FERGIE_na_MAJESHISIR ALEX FERGUSON amefunguliwa Mashitaka na FA, Chama cha Soka England, kufuatia kauli yake kuhusu Refa Msaidizi baada ya Timu yake Manchester United kutoka sare 1-1 na Tottenham kwenye Mechi ya Ligi Kuu England iliyochezwa Januari 20 Uwanjani White Hart Lane.
Ferguson alimyooshea kidole Refa Msaidizi Simon Beck kwa kushindwa kuashiria Penati baada ya Straika wake Wayne Rooney kuangushwa ndani ya Boksi.
Mara baada ya kauli ya Ferguson, FA ilimtaka Meneja huyo kujieleza na sasa imeamua kufungua Mashitaka rasmi na amepewa hadi Ijumaa Saa 1 Usiku, Bongo Taimu, kuyajibu.
Kauli ambazo zimemtia matatani Ferguson ni pale alipotamka: “Kulikuwa hamna njia Mshika Kibendera angeweza kutoa ile [Penati!]-aliwapa kila kitu! Kilikuwa kitu cha wazi na alikuwa Yadi 10 au 12 na hakutoa! Wao walipewa kila kitu!”
Pia alikumbushia tukio ambalo Refa Msaidizi Simon Beck alipowakatili Man United Aprili 2010 walipofungwa 2-1 na Chelsea kwa Mshika Kibendera huyo kutokutoa Ofsaidi ya wazi dhidi ya Didier Drogba aliefunga Bao la ushindi.
Kihistoria, Ferguson na FA wana misuguano ya muda mrefu na Machi 2011 alifungiwa Mechi 5 na kupigwa Faini Pauni 30,000 kwa kumtuhumu Refa Martin Atkinson kwa kuipendelea Chelsea.

BPL: MABINGWA MAN CITY WANASA KWA YA MKIANI QPR!

>>NEWCASTLE PEKEE YASHINDA, ZOTE DROO!!
>>LEO ARSENAL v LIVERPOOL, MAN UNITED v SOUTHAMPTON, READING v CHELSEA!
BPL_LOGOJANA USIKU, Mabingwa wa England, Manchester City, wakicheza ugenini na Timu ya mkiani mwa Ligi Kuu England, Queens Park Rangers, walitoka sare ya 0-0 na kubaki nafasi ya Pili wakiwa Pointi 4 nyuma ya Vinara Manchester United ambao leo wana nafasi ya kulipanua pengo hilo kuwa Pointi 7 ikiwa wataifunga Southampton Uwanjani  Old Trafford.
Kati Mechi 4 za Ligi Kuu England, Mechi pekee iliyotoa Mshindi ni ile ya Aston Villa na Newcastle na zote zilizobaki zilimazika kwa sare.
MATOKEO:
Jumanne Januari 29
Aston Villa 1 Newcastle 2
QPR 0 Man City 0
Stoke 2 Wigan 2
Sunderland 0 Swansea 0
++++++++++++++++++++
ASTON VILLA 1 NEWCASTLE 2
Newcastle United wameshinda hii vita ya Timu zinazosuasua na balaa kwa Aston Villa limezidi kuendelea kwa Meneja wao Paul Lambert ambae Wiki iliyopita ilitolewa kwenye Makombe mawili, Capital One Cup na FA Cup, na Timu za Madaraja ya chini.
+++++++++++++++++++++
MAGOLI:
Aston Villa 1
-Benteke Dakika ya 49 (Penati)
Newcastle 2
-Cisse Dakika ya 19
-Cabaye 31
+++++++++++++++++++++
Papiss Cisse na Yohan Cabaye waliwapa Newcastle uongozi wa Bao 2 kabla Haftaimu lakini Penati ya Kipindi cha Pili ya Villa iliyofungwa na Christian Benteke haikutosha kuwakomboa na Newcastle wakapata ushindi wao wa kwanza tangu katikati ya Desemba Mwaka jana.
VIKOSI:
Aston Villa: Guzan, Clark, Vlaar, Baker, Lowton, Westwood, Bannan, N'Zogbia, Bennett, Benteke, Bent
Akiba: Given, Ireland, Agbonlahor, Holman, Bowery, Weimann, Lichaj.
Newcastle: Krul, Debuchy, Steven Taylor, Coloccini, Santon, Perch, Cabaye, Gouffran, Sissoko, Gutierrez, Cisse
Akiba: Harper, Williamson, Anita, Yanga-Mbiwa, Bigirimana, Shola Ameobi, Sammy Ameobi.
Refa: Mike Dean
SUNDERLAND 0 SWANSEA 0
Sunderland na Swansea zilitoka sare katika gemu iliyopooza.
VIKOSI:
Sunderland: Mignolet, Gardner, Bramble, O'Shea, Colback, Johnson, N'Diaye, Vaughan, Larsson, Sessegnon, Fletcher
Akiba: Westwood, Bardsley, Wickham, Kilgallon, Mangane, McClean, Elmohamady.
Swansea: Tremmel, Tiendalli, Williams, Chico, Davies, Dyer, de Guzman, Britton, Hernandez, Shechter, Michu
Akiba: Cornell, Bartley, Graham, Lamah, Routledge, Rangel, Ki.
Refa: Andre Marriner
STOKE 2 WIGAN 2
Wigan walipigana kutoka Bao 2 nyuma kabla ya Haftaimu na kupata sare ya 2-2 walipocheza ugenini na Stoke City.
+++++++++++++++++++++
MAGOLI:
Stoke 2
-Shawcross Dakika ya 23
-Crouch 48
Wigan 2
-McArthur Dakika ya 50
-Di Santo 61
+++++++++++++++++++++
Sare hiyo imewafanya Wigan wapande hadi nafasi ya 17 na hivyo kujinasua mkiani mwa zile Timu 3 za mwisho na kuziacha huko Aston Villa, Reading na QPR.
VIKOSI:
Stoke: Begovic, Cameron, Shawcross, Huth, Whitehead, Whelan, Nzonzi, Adam, Etherington, Walters, Crouch
Akiba: Sorensen, Jones, Owen, Upson, Wilkinson, Shotton, Jerome.
Wigan: Al Habsi, Golobart, Caldwell, Figueroa, Boyce, McArthur, McCarthy, Espinoza, Beausejour, Maloney, Di Santo
Akiba: Robles, Jones, Henriquez, Gomez, McManaman, Stam, Mustoe.
Refa: Mike Jones
QPR 0 MAN CITY 0
Timu ya mkiani mwa Ligi Kuu England Queens Park Rangers imewasimamsha Mabingwa Manchester City kwa kutoka nao sare ya 0-0 na Shujaa wao ni Kipa wao Julio Cesar alieokoa mipira mingi.
Man City walitawala Kipingi cha Kwanza huku Pablo Zabaleta akipiga posti na shuti la Gareth Barry likiokolewa.
VIKOSI:
Queens Park Rangers: Cesar, Onuoha, Nelsen, Hill, Traore, Mbia, Derry, Fabio, Granero, Taarabt, Remy
Akiba: Green, Park, Ben Haim, Zamora, Murphy, Faurlin, Bothroyd.
Manchester City: Hart, Zabaleta, Garcia, Lescott, Clichy, Milner, Barry, Nasri, Aguero, Silva, Tevez
Akiba: Pantilimon, Dzeko, Sinclair, Kolarov, Rodwell, Nastasic, Rekik.
Refa: Phil Dowd
RATIBA:
Jumatano Januari 30
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Arsenal v Liverpool
Everton v West Brom
Norwich v Tottenham
[SAA 5 Usiku]
Fulham v West Ham
Man United v Southampton
Reading v Chelsea
RATIBA MECHI ZA WIKIENDI:
Jumamosi Februari 2
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
QPR v Norwich
[SAA 12 Jioni]
Arsenal v Stoke
Everton v Aston Villa
Newcastle v Chelsea
Reading v Sunderland
West Ham v Swansea
Wigan v Southampton
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Fulham v Man United
Jumapili Februari 3
[SAA 10 na Nusu Jioni]
West Brom v Tottenham
[SAA 1 Usiku]
Man City v Liverpool

NIGERIA YASONGA ROBO, ZAMBIA WATEMESHWA TAJI MAPEMAAA



Striker Victor Moses converted two late penalties to lead Nigeria to a 2-0 win over Ethiopia on Tuesday and a spot in the quarter-finals of the Africa Cup of Nations. 
Moses scored in the 80th and 90th minutes, sparing his team an early exit with a goalless draw at Royal Bafokeng Stadium. 
Ethiopia, appearing in their first tournament for more than 30 years, finished bottom of Group C. 
Defending champions Zambia were also eliminated after a 0-0 draw with Burkina Faso, who won the group with five points. Nigeria also ended with five points, but trailed on goal difference. 
Saviour: Victor Moses scored two penalties to keep Nigeria's tournament alive
Saviour: Victor Moses scored two penalties to keep Nigeria's tournament alive
Elaborate: Nigeria's Efe Ambrose does a back flip in celebration
Elaborate: Nigeria's Efe Ambrose does a back flip in celebration

MATCH FACTS

Ethiopia: Bancha, Gebreyes, Bune, Alula Girma, Elias, Estifanos (Teshome 46), Saleh (Bogale 68), Hintsa, Oukri (Ibrahim 46), Kebede, Said.
Subs Not Used: Tadelle, Zinabu, Hailu, Bekele, Assefa, Tassew.
Sent Off: Bancha (85).
Booked: Elias, Gebreyes, Alula Girma, Bancha.
Nigeria: Enyeama, Ambrose, Omeruo, Oboabona, Echiejile, Mikel (Yobo 90), Ogude, Moses, Mba, Uche (Musa 65), Emenike (Ideye 75).
Subs Not Used: Agbim, Obiorah, Egwueke, Gabriel, Onazi, Uzoenyi, Igiebor, Oshaniwa, Ejide.
Booked: Mba, Ogude.
Goals: Moses (pen) 80, (pen) 90.
Att: 15,000.
Ref: Bouchaib El Ahrach (Morocco).
Moses was twice fouled inside the area to win the penalties, and then kept his cool to find the net both times for the two-time African champions. The Chelsea striker was brought down by defender Alula Girma for the first penalty and then stopped by goalkeeper Sisay Bancha in another breakaway. 
Bancha was sent off for the challenge and midfielder Addis Hintsa had to replace him in goal because all three substitutions had already been made. 
Just after the first Nigeria goal, Ethiopia nearly equalized with a close-range header by Saladin Seid. However, Nigeria goalkeeper Vincent Enyeama made a brilliant save, diving to his right and deflecting the ball with his outstretched arms. 
Seeking its first title since 1994, Nigeria were coming off two 1-1 draws in the first matches, both times after having taken the lead. The Super Eagles didn't qualify for last year's tournament. 
Nigeria's best chance before the penalties came in the 66th, when a header from Chelsea midfielder John Obi Mikel was cleared off the line. 
Without the penalties, Mikel and his teammates would have been eliminated because of their disciplinary record. 
One: Moses scores his first penalty as he sends Sisay Bancha the wrong way
One: Moses scores his first penalty as he sends Sisay Bancha the wrong way
Two: The Chelsea winger added another from the spot in a 2-0 win
Two: The Chelsea winger added another from the spot in a 2-0 win
Nigeria and Zambia were level on points, goal difference and goals scored, so the decision would have gone down to a Fair Play system based on the number of yellow and red cards. Nigeria had more than Zambia until then. 
Ethiopia needed to beat Nigeria and hope that Zambia lost to Burkina Faso. 
It was also without top players Asrat Megerssa and Adane Girma, who were injured in the first half against Burkina Faso, while goalkeeper Jemal Tassew was suspended for two matches after a reckless tackle in the opener against Zambia. 
Ethiopia won the Cup of Nations in 1962 but last qualified for the final tournament in 1982.
Booked: Chelsea's Nigerian midfielder John Obi Mikel gets a yellow card
Booked: Chelsea's Nigerian midfielder John Obi Mikel gets a yellow card
Out: Ethiopian fans enjoyed their first Africa Cup of Nations since 1982 but their journey ended at the group stage
Out: Ethiopian fans enjoyed their first Africa Cup of Nations since 1982 but their journey ended at the group stage
Defending champions Zambia crashed out of the Africa Cup of Nations on Tuesday after being held to a 0-0 draw by Burkina Faso, who advanced to the quarter-finals. 
With Nigeria beating Ethiopia 2-0 in Rustenburg to advance, a third successive draw was not enough for Zambia to progress. 
Burkina Faso sailed through at Zambia's expense, reaching the second round for the first time since they hosted the tournament in 1998 and finishing top of Group C on goal difference. 
Going home: Zambia's Nathan Sinkala shows his disappointment after his team were eliminated
Going home: Zambia's Nathan Sinkala shows his disappointment after his team were eliminated
Going through: Burkina Faso players celebrate finishing top of group C
Going through: Burkina Faso players celebrate finishing top of group C

MATCH FACTS

Burkina Faso: Diakite, Bakary Kone, Panandetiguiri,Keba Paul Koulibaly, Djakaridja Kone, Koffi, Rouamba,Alain Traore (Bance 11), Pitroipa (Abdou Razak Traore 90), Balima (Dah 46), Kabore.
Subs Not Used: Germain Sanou, Henri Traore, Dagano, Ouattara, Rabo, Pan-Pierre Koulibaly, Wilfried Sanou, Nakoulma.
Zambia: Mweene, Sinkala, Mbola, Himoonda, Nkausa (Musonda 17), Sunzu, Kalaba, Chansa (Mukuka Mulenga 56), Mayuka, Lungu (Sakuwaha 81),Mbesuma.
Subs Not Used: Titima, Kasonde, Jacob Mulenga, Felix Katongo, Christopher Katongo, Chamanga, Chivuta, Njovu, Munyao.
Booked: Musonda, Mayuka.
Att: 8,000.
Ref: Neant Alioum (Cameroon).
In a game that was low on quality, Zambia striker Collins Mbesuma missed clear-cut chances either side of the break. 
Burkina Faso knew that a draw was all they needed and was content to flood the midfield and slow down a game that was already held up by a sandy pitch. 
Burkina Faso's initial ambition shrunk even further when they lost leading goalscorer Alain Traore to injury in the opening 10 minutes, but Zambia failed to produce the quality required to break their opponents down. 
Mbesuma had a gilt-edged opportunity in the 17th minute, but hit Chisamba Lungu's cross straight at Burkina Faso goalkeeper Daouda Diakite. 
Rainford Kalaba also forced a save from Diakite in first-half stoppage time as a cross drifted to the back post, but his weak header was easily dealt with. 
Zambia flooded forward as the second half wore on, yet the only genuine opportunity came when Mbesuma headed a corner over the crossbar.
Close: Djakaridja Kone and Zambian forward Collins Mbesuma battle for the ball
Close: Djakaridja Kone and Zambian forward Collins Mbesuma battle for the ball
Winless: Zambia manager Herve Renard saw his side draw all three of their games
Winless: Zambia manager Herve Renard saw his side draw all three of their games
Failure: Zambia came into the tournament with high expectations after winning the title last year, but they slipped to a disappointing early exit
Failure: Zambia came into the tournament with high expectations after winning the title last year, but they slipped to a disappointing early exit

TAIFA STARS KUIKABILI CAMEROON ‘FIFA DATE’



TANZANIA (Taifa Stars) itacheza na Cameroon katika moja ya mechi za kirafiki za Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA)- FIFA Date zitakazofanyika duniani kote Februari 6 mwaka huu.
Mechi hiyo itafanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni. Kikosi cha Cameroon kinachoundwa na wachezaji wengi wa kulipwa wanaocheza katika nchi mbalimbali duniani kitaanza kuwasili nchini Februari 3 mwaka huu.
Nchi kadhaa ziliomba kucheza na Taifa Stars katika tarehe hiyo ya FIFA, lakini Kocha wa Stars, Kim Poulsen ameamua kucheza mechi hiyo dhidi ya Cameroon ambayo nahodha wake ni mchezaji nyota wa kimataifa, Samuel Etoo Fils.
Congo Brazzaville, Equatorial Guinea, Rwanda na Swaziland nazo zilikuwa zimeomba kucheza dhidi ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager. Ukiondoa Swaziland iliyotaka mechi hiyo ichezwe Dar es Salaam, nyingine zilitaka kucheza nyumbani kwao.
Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen atakutana na Waandishi wa Habari kuzungumzia maandalizi ya mechi hiyo ikiwemo kutaja kikosi ambacho atakitumia. Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).