CHELSEA YAPIGA MTU MKONO KASORO KIDOLE, YAZIDI KUPAA ENGLAND
Chelsea
imejiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu ya England, baada ya kuichapa mabao
4-1 Norwich nyumabni. Grant Holt aliifungia Norwich bao la kuongoza
dakika ya 11, lakini Chelsea ilisawazisha kupitia kwa Fernando Torres
kabla ya Frank Lapard na Eden Hazard kufunga mabao ya ushindi kipindi
hicho hicho cha kwanza na Branislav Ivanovic kuhitimisha karamu ya mabao
ya ushindi wa 4-1 zikiwa zimebaki dakika 15. Chelsea imefikisha pointi
19, baada ya kucheza mechi saba na kuendelea kuongoza Ligi Kuu,
ikiwazidi pointi nne mabingwa watetezi, Man City .

Eden Hazard akiifungia Chelsea

Fernando Torres akiwa chini ya ulinzi wa Javier Garrido na Leon Barnett

Torres baada ya kufunga

John Ruddy akitunguliwa na Frank Lampard

Frank Lampard baada ya kuifungia Chelsea

John Terry na Ashley Cole wote walicheza leo

Branislav Ivanovic akipongezwa na John Obi Mikel kwa kufunga bao la nne
MAN CITY SASA YAIPUMULIA CHELSEA

Kolarov akipongezwa kufunga bao la kwanza Uwanja wa Etihad

Mserbia huyo anafunga bao la kuongoza kwa mpira wa adhabu

Aguero anagunga la pili 2-0 kipindi cha pili

Lilikuwa shuti la pili la Aguero tangu aingie na anafunga

Mabingwa hao watetezi sasa wapo jirani na Chelsea kileleni mwa Ligi Kuu

Balotelli akiumaliza Uwanja baada ya kutolewa
MATOKEO MECHI ZOTE ZA LEO NA WAFUNGAJI LIGI KUU ENGLAND
|
| ||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
| ||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
| ||||||||||||||||||||||||||||||||||||
Kocha
wa Mabingwa wa Dunia na Spain, Vicente Del Bosque, ametoboa kuwa Staa
wa Chelsea Juan Mata ameachwa kwenye Kikosi cha Timu hiyo kwa vile hamna
nafasi yake.
KILE
kilio cha Siku nyingi cha Sir Alex Ferguson na Arsen Wenger kuitaka FA
pamoja na Wasimamizi wa Ligi Kuu England ‘kuzilinda’ Timu za England
zinazoshiriki michuano ya Klabu Barani Ulaya sasa kimeangukia kwa Meneja
Roberto Mancini wa Mabingwa Manchester City.
Kocha
wa Mabingwa wa Italy, Juventus, Antonio Conte, amepunguziwa adhabu ya
Kifungo cha Miezi 10 hadi Miezi 4 kwa kuhusishwa na Skandali la
'Calcioscommesse'. Kamati ya Olimpiki ya Italy, ambayo ndio yenye jukumu
la mwisho kwa Rufaa za michezo Nchini humo, imempunguzia adhabu Conte,
mwenye Miaka 43, na sasa anaweza kurudi kwenye Benchi la Juventus
kuanzia Desemba 9.



