Saturday, October 6, 2012

CHELSEA YAPIGA MTU MKONO KASORO KIDOLE, YAZIDI KUPAA ENGLAND


Chelsea imejiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu ya England, baada ya kuichapa mabao 4-1 Norwich nyumabni. Grant Holt aliifungia Norwich bao la kuongoza dakika ya 11, lakini Chelsea ilisawazisha kupitia kwa Fernando Torres kabla ya Frank Lapard na Eden Hazard kufunga mabao ya ushindi kipindi hicho hicho cha kwanza na Branislav Ivanovic kuhitimisha karamu ya mabao ya ushindi wa 4-1 zikiwa zimebaki dakika 15. Chelsea imefikisha pointi 19, baada ya kucheza mechi saba na kuendelea kuongoza Ligi Kuu, ikiwazidi pointi nne mabingwa watetezi, Man City .  
Easy does it: Eden Hazard puts Chelsea ahead against Norwich
Eden Hazard akiifungia Chelsea 
Outnumbered: Fernando Torres is watched by Javier Garrido and Leon Barnett
Fernando Torres akiwa chini ya ulinzi wa Javier Garrido na Leon Barnett
Back in the game: Torres scores for Chelsea
Torres baada ya kufunga
No chance: John Ruddy stands as Frank Lampard's shot goes past him
John Ruddy akitunguliwa na Frank Lampard
Mr reliable: Frank Lampard scores for Chelsea
Frank Lampard baada ya kuifungia Chelsea
Back doing the day job: John Terry and Ashley Cole both started for Chelsea
John Terry na Ashley Cole wote walicheza leo
Job done: Branislav Ivanovic celebrates scoring Chelsea's fourth
Branislav Ivanovic akipongezwa na John Obi Mikel kwa kufunga bao la nne
 
 
 

MAN CITY SASA YAIPUMULIA CHELSEA

Mabao ya Aleksandar Kolarov, Sergio Aguero na James Milner yameipa Manchester City ushindi wa 3-0 katika Ligi Kuu ya England joni hii dhidi ya Sunderland. Ushindi huo, umeifanya Man City itimize pointi 15 baada ya kucheza mechi saba na inashika nafasi ya pili, nyuma ya Chelsea inayoongoza kwa pointi zake 16, ambayo hivi sasa inacheza mechi ya saba nayo dhidi ya Norwich.
Centre of attention: Kolarov is mobbed after opening the scoring at the Etihad Stadium
Kolarov akipongezwa kufunga bao la kwanza Uwanja wa Etihad

On target: The Serbia international gave City the lead with his first-half free-kick
Mserbia huyo anafunga bao la kuongoza kwa mpira wa adhabu
Advantage City: Aguero gave the hosts a 2-0 lead in the second half
Aguero anagunga la pili 2-0 kipindi cha pili

Ace: Aguero scored shortly after coming on as a substitute
Lilikuwa shuti la pili la Aguero tangu aingie na anafunga
 
City slickers: The champions closed the gap to Chelsea at the summit of the Premier League
Mabingwa hao watetezi sasa wapo jirani na Chelsea kileleni mwa Ligi Kuu
Game over: Balotelli walked straight down the tunnel after he was substituted
Balotelli akiumaliza Uwanja baada ya kutolewa
 
 

MATOKEO MECHI ZOTE ZA LEO NA WAFUNGAJI LIGI KUU ENGLAND


06 October
 
Chelsea4 - 1Norwich
FJS Torres (13)
F Lampard (21)
E Hazard (30)
B Ivanovic (75)

G Holt (10)
Stamford BridgeAttendance (41784)
Teams
06 October
 
West Brom3 - 2QPR
J Morrison (4)
Z Gera (21)
Y Mulumbu (84)

A Taarabt (34)
EM Granero (90)
The HawthornsAttendance (23987)
Teams

06 October
 
Swansea2 - 2Reading
MPC Michu (70)
W Routledge (77)

P Pogrebnyak (30)
N Hunt (43)
Liberty StadiumAttendance (20336)
Teams
06 October
 
Wigan2 - 2Everton
A Kone (9)
F Di Santo (22)

N Jelavic (10)
L Baines (pen 86)
The DW StadiumAttendance (18759)
Teams

06 October
 
Man City3 - 0Sunderland
A Kolarov (4)
SL Aguero (59)
J Milner (88)

 
Etihad StadiumAttendance (47036)
Teams | Report
01 October
 
QPR1 - 2West Ham
A Taarabt (56)
M Jarvis (2)
R Vaz Te (34)
Loftus Road StadiumAttendance (173
 
 

CAF CHAMPIONZ LIGI: KESHO Samatta kuipeleka Mazembe Fainali??

Jumamosi, 06 Oktoba 2012 14:13
   
Straika mahiri wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta, kesho ataongoza majeshi ya Klabu yake TP Mazembe kucheza na Mabingwa watetezi wa Afrika, Espérance Sportive de Tunis, ya Nchini Tunisia, katika Mechi ya kwanza ya Nusu Fainali ya CAF CHAMPIONZ LIGI itakayochezwa huko Stade TP Mazembe, Mjini Lubumbashi, Congo.


Timu hizo zitarudiana huko Tunisia hapo Oktoba 20.
Nusu Fainali nyingine ya Mashindano haya itachezwa huko Nigeria hivi leo kati ya wenyeji Sunshine Stars na Vigogo wa Misri Al Ahly.


Timu hizi zitarudiana huko Cairo hapo Oktoba 21.
Washindi wa Nusu Fainali hizi watacheza Fainali Mwezi Novemba na Bingwa ndie ataiwakilisha Afrika kwenye Mashindano ya FIFA ya Klabu Bingwa Duniani yatakayochezwa huko Japan Mwezi Desemba.


NUSU FAINALI:
[SAA za BONGO]
Jumamosi Oktoba 6        
17:00 Sunshine Stars – Nigeria v Al Ahly - Egypt
Jumapili Oktoba 7         
17:30 TP Mazembe - Congo, DR v Espérance Sportive de Tunis – Tunisia [Stade TP Mazembe Lubumbashi]
MARUDIANO
Jumamosi Oktoba 20         
22:30 Espérance Sportive de Tunis – Tunisia v TP Mazembe - Congo, The Democratic Republic Of The [Stade El Menzah]
Jumapili Oktoba 21         
20:30 Al Ahly – Egypt v Sunshine Stars – Nigeria [Cairo International Stadium]
 

Del Bosque: ‘Juan Mata hana nafasi Spain!’

Jumamosi, 06 Oktoba 2012 13:05
 
BRAZIL_2014_BESTKocha wa Mabingwa wa Dunia na Spain, Vicente Del Bosque, ametoboa kuwa Staa wa Chelsea Juan Mata ameachwa kwenye Kikosi cha Timu hiyo kwa vile hamna nafasi yake.


Del Bosque alitangaza Kikosi chake kwa ajili ya Mechi za Mchujo za Kundi I kwa Kanda ya Ulaya kuwania kuingia Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Brazil ambazo watacheza na Belarus Oktoba 12 ugenini na kisha kucheza nyumbani na France hapo Oktoba 16.



Kwenye Kundi I, Spain wamecheza Mechi moja na kuifunga Georgia bao 1-0.
+++++++++++++++++++++

MSIMAMO:
KUNDI I:
1 France Mechi 2 Pointi 6
2 Spain Mechi 1 Pointi 3
3 Georgia Mechi 2 Pointi 3
4 Finland Mechi 1 Pointi 0
5 Belarus Mechi 2 Pointi 0


FAHAMU: Washindi 9 wa kila Kundi wataingia Fainali moja kwa moja na Washindi wa Pili 8 bora wenye rekodi nzuri dhidi ya Timu zilizomaliza nafasi za Kwanza, Tatu, Nne na Tano kwenye Kundi lao watapelekwa kwenye Droo kupanga Mechi 4 za Mchujo, zitakazochezwa nyumbani na ugenini, ili kupata Timu nne zitakazoingia Fainali.
+++++++++++++++++++++
Ingawa wengi huko Spain wameshangazwa na kutochukuliwa Juan Mata hasa ukizingatia fomu yake ya sasa na Klabu yake Chelsea lakini Del Bosque amesema: “Hatukuweza kupata nafasi yake. Tunao Wachezaji wa kutosha kwa michezo hii. Tumechagua wale tunaohisi wanafaa kwa Mechi hizi.”


KIKOSI KAMILI:
Makipa: Iker Casillas [Real Madrid], Victor Valdes [Barcelona], Jose Manuel Reina [Liverpool]


Mabeki: Raul Albiol [Real Madrid], Sergio Ramos [Real Madrid[ , Juanfran [Atletico Madrid     ], Alvaro Arbeloa [Real Madrid], Ignacio Monreal [Malaga], Jordi Alba [Barcelona]

Viungo: Sergio Busquets [Barcelona], Xabi Alonso [Real Madrid], Cesc Fabregas [Barcelona], Andres Iniesta [Barcelona], Xavi Hernandez [Barcelona], Benat Etxebarria [Real Betis], Javi Martinez [Bayern Munich], Santi Cazorla [Arsenal], David Silva [Manchester City]
 
 
Washambuliaji: Pedro [Barcelona], Jesus Navas [Sevilla], Roberto Soldado [Valencia], David Villa [Barcelona], Fernando Torres [Chelsea]
 

MANCINI alia na RATIBA!!

Jumamosi, 06 Oktoba 2012 08:03
 
>>LEO kuikwaa Sunderland ikiwa ni Siku 2 tu baada ya Dortmund!!
>>NI SUNDERLAND Msimu uliopita walitoka 3-3 na kufungwa nao 1-0!!
MANCINI_n_WENGERKILE kilio cha Siku nyingi cha Sir Alex Ferguson na Arsen Wenger kuitaka FA pamoja na Wasimamizi wa Ligi Kuu England ‘kuzilinda’ Timu za England zinazoshiriki michuano ya Klabu Barani Ulaya sasa kimeangukia kwa Meneja Roberto Mancini wa Mabingwa Manchester City.


Man City walicheza Mechi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI Jumatano Usiku Uwanja wa Etihad na kutoka sare 1-1 na Mabingwa wa Germany Borussia Dortmund na leo Saa 8 Dak 45 Mchana, Bongo taimu, wanatinga tena Uwanja huo huo kucheza Mechi ya Ligi Kuu na Sunderland.


Mancini amebwata: “Tunahitaji muda wa kupumzika, kupona maumivu na hekaheka za Mechi ya juzi lakini tunacheza Jumamosi mapema! Sielewi hili! Inashangaza unacheza Jumatano Usiku na tena Jumamosi mchana! Tuna Siku 2 na Masaa 12 tu kupumzika!”


Aliongeza: “Hatukucheza vizuri Jumatano lakini tulipoteza nguvu nyingi, tunahitaji kupumzika, tupone. Kwingine kote Timu zinazocheza CHAMPIONZ LIGI hucheza Mechi zao za Ligi ya nyumbani Siku 3 au 4 kabla na baadae hupumzika si chini ya Siku 3 baada ya Mechi ya Ulaya!”


Leo, katika Mechi ya kwanza kabisa ya Ligi Kuu England Wikiendi hii, Man City wanaivaa Sunderland, ambayo Msimu huu haijafungwa, na ambayo Msimu uliopita kwenye Ligi Kuu walitoka nayo 3-3 Uwanjani Etihad na kufungwa nayo bao 1-0 nyumbani kwa Sunderland Stadium of Light.
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumamosi Oktoba 6
[Saa 8 Dak 45 Mchana]
Manchester City v Sunderland
[Saa 11 Jioni]
Chelsea v Norwich City
Swansea City v Reading
West Bromwich Albion v Queens Park Rangers
Wigan Athletic v Everton
[Saa 1 na Nusu Usiku]
West Ham United v Arsenal
Jumapili Oktoba 7
[Saa 9 na Nusu Mchana]
Southampton v Fulham
[Saa 11 Jioni]
Tottenham Hotspur v Aston Villa
Liverpool v Stoke City
[Saa 12 Jioni]
Newcastle United v Manchester United
MSIMAMO:
[Kila Timu imecheza Mechi 6 isipokuwa inapotajwa]
1 Chelsea Pointi 16
2 Everton 13
3 Man United 12
4 Man City 12
5 Tottenham 11
6 WBA 11
7 West Ham 11
8 Arsenal 9
9 Fulham 9
10 Newcastle 9
11 Swansea 7
12 Stoke 7
13 Sunderland Mechi 5 Pointi 7
14 Liverpool 5
15 Aston Villa 5
16 Wigan 4
17 Southampton 3
18 Norwich 3
19 Reading Mechi 5 Pointi 2
20 QPR 2
+++++++++++++++++++++++++++++++++
 

KIFUNGO kwa Kocha wa Juve Conte chapunguzwa kuwa Miezi 4!!

Jumamosi, 06 Oktoba 2012 07:01
 
>>NI ADHABU kwa SKANDALI LA the 'CALCIOSCOMMESSE!!'
ANTONIO_CONTE_of_JUVEKocha wa Mabingwa wa Italy, Juventus, Antonio Conte, amepunguziwa adhabu ya Kifungo cha Miezi 10 hadi Miezi 4 kwa kuhusishwa na Skandali la 'Calcioscommesse'. Kamati ya Olimpiki ya Italy, ambayo ndio yenye jukumu la mwisho kwa Rufaa za michezo Nchini humo, imempunguzia adhabu Conte, mwenye Miaka 43, na sasa anaweza kurudi kwenye Benchi la Juventus kuanzia Desemba 9.
Conte alifungiwa Mwezi Agosti Mwaka huu kuhusu tuhuma za Wachezaji kupanga matokeo Mechi kwenye Mechi mbili na yeye kuhusishwa kwa kujua hujuma hizo lakini akashindwa kuziripoti wakati akiwa Meneja wa Klabu ya Serie B, Siena, katika Msimu wa 2010/11.
Baadae, Conte alisafishwa kwenye Mechi moja na adhabu yake kubaki kwa kuhusishwa na Mechi moja.
Conte alijiunga na Juventus kwenye Msimu wa 2011/12 na kuiongoza Klabu hiyo kongwe kutwaa Ubingwa Msimu huo huo bila kufungwa hata Mechi moja.
Adhabu ya Kifungo cha Miezi 10 ilimaanisha haruhusiwi kukaa kwenye Benchi la Juve wakati wa Mechi na pia haruhusiwi kuingia Vyumba vya Kubadili Jezi wakati wa Mechi lakini aliruhusiwa kuifundisha Timu yake wakati wa mazoezi.
Kifungo cha awali cha Miezi 10 kingemfanya aukose Msimu mzima wa 2012/13 lakini sasa kwa kupunguziwa atazikosa Mechi 15 za Serie A na Mechi zote za Kundi lao za UEFA CHAMPIONZ Ligi, ikiwemo ile ya marudiano na Chelsea.
Pia, Msaidizi wa Conte huko Siena, Angelo Alessio, ambae pia ndie Msaidizi wake hapo Juve, amepunguziwa toka adhabu ya Miezi 8 na kubakishiwa 6.
Skandali hili la 'Calcioscommesse' limehusisha kuchunguzwa kwa Klabu zaidi ya 20 huko Italy.

BAHANUZI AMTEGUA BEGA KAPOMBE, KUWAKOSA OLJORO KESHO, NGASSA MALARIA IMEPANDA

Bahanuzi nyuma ya Kapombe


MABINGWA wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simba SC kesho katika mchezo wao dhidi ya JKT Oljoro ya Arusha watawakosa wachezaji wao wanne, wakiwemo beki Shomary Kapombe aliyeumizwa na mshambuliaji Said Bahanuzi wa Yanga Jumatano na Mrisho Ngassa, ambaye ana Malaria.   
 
 
Ofisa Habari wa Simba SC, Ezekiel Kamwaga amesema leo katika Mkutano na Waandishi wa Habari, makao makuu ya klabu hiyo Mtaa wa Msimbazi kwamba, mbali na nyota hao wawili, wengine watakaokosekana kwenye mechi ya kesho ni mabeki Amir Maftahi anayetumikia adhabu ya kadi na Haruna Shamte, ambaye pia ni majeruhi.
 
 
Kamwaga alisema kwamba Kapombe aliumizwa na mshambuliaji wa Yanga, Said Bahanuzi Jumatano katika mechi baina ya watani hao wa jadi wa soka ya Tanzania, iliyopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya 1-1.
 
 
Kuhusu Ngassa, Kamwaga alisema kwamba baada ya mechi hiyo ya Jumatano, naye amepata Malaria, ambayo itamuweka nje ya Uwanja kesho, wakati Haruna aliumia mazoezini, timu hiyo ilipokuwa kambini Zanzibar ikijiandaa na mechi ya Yanga.
 
 
Lakini Kamwaga alisema pamoja na kuwakosa nyota hao, anaamini wachezaji wengine watakaochukua nafasi zao watafanya vizuri. Kumbuka Emmanuel Okwi amemaliza adhabu na kesho anaweza kuiongoza Simba kwenye mechi hiyo.  

RICK ROSS AAHIDI BONGE LA SHOW SERENGETI FIESTA LEO

Rick Ross tayari yupo Dar
MKALI wa muziki wa Hip hop kutoka Marekani, William Leonard Roberts II anayetambulika kama Rick Ross au The Boss, ameahidi kukonga nyoyo za mashabiki watakaohudhuria tamasha la Serengeti Fiesta 2012 jioni ya leo kwenye viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar es Salaam.
 
 
Rapa huyo, aliyefikia katika hoteli ya Hyatt, zamani Kilimanjaro Kempensky, Dar es Salaam, ambaye alizaliwa JanuarI 28, mwaka 1976 huko Carol City, Florida, Marekani alisema hayo baada ya kutua Dar es Salaam usiku wa jana.
 
 
“Rick Ross ametua na ameahidi kufanya shoo kali sana,”alisema Allan Chonjo, Meneja wa Bia ya Serengeti, wadhamini wakuu wa Fiesta.
 
 
Rapa huyo mwenye miraba minne, ambaye ana bifu kali na Curtis Jackson ’50 Cent’ aliyewahi kuzuru Tanzania pia, aliwasili Dar es Salaam usiku wa jana na anatarajiwa kuwapagawisha wapenzi wa Serengeti Fiesta kwa nyimbo kali kutoka kwenye albamu zake za Port of Miami aliyoitoa mwaka 2006, Trilla ya 2008, Deeper Than Rap ya 2009, Teflon Don ya 2010 na God Forgives, I Don't ya mwaka huu.
 
 
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Masoko wa SBL, wadhamini wakuu wa Serengeti Fiesta 2012, Ephraim Mafuru Balozi alisema kwamba wanajisikia fahari kubwa kwa bia ya Serengeti kuwa mdhamini mkuu wa tamasha hilo kwa muda wa miaka minne sasa.
 
 
 
“Bia ya Serengeti inafahamika kwa umahiri wake katika ubora na ladha yake. Imejinyakulia medali za dhahabu kutoka katika mashirika ya ushindanishaji bia duniani DLG na Monde na pia ni fahari kwa kuwa bia ya kwanza Tanzania kuwa na kimea cha asilimia 100. Bia hii imejiwekea historia ya kuwa bia inayokua kwa haraka katika ujazo na thamani yake,”alisema Mafuru.
 
 
Mkurugenzi huyo aliwaomba wakazi wa Dar es Salaam kujitokeze kwa wingi jioni ya leo katika viwanja vya Leaders Club wakaburudike na muziki wa vijana wa Tanzania na pia kumshuhudia mwanamuziki Rick Ross kutoka Marekani. “Pia tunawahakikishia kwamba watapata bia ya Serengeti yenye muonekano mpya, na ladha yake ni ile ile yenye ubora thabiti. Kwa hiyo watapata bia yenye muonekano tofauti, burudani ile ile,”alisema. Mafuru aliongeza; “Tunazo Bia za aina  nyingi kutoka Kampuni ya Bia ya Serengeti pia zitakuwepo kama vile; Tusker Lager, Pilsner Lager, Tusker Malt Lager, Uhuru Peak Lager, Smirnoff Ice Black na Red, na kwa wanaopendelea vinywaji vikali watapata Johnnie Walker Whisky, Smirnoff Vodka, VAT 69, Captain Morgan, Baileys na Gilbeys Gin.  Pia kutakuwa na vinywaji visivyo na kilevi cha Malta Guinness na Alvaro.  Tumejiandaa vya kutosha kuwapatia vinywaji hivyo kwa bei ya shilingi 1,800 tu,”alisema.

MECHI YA YANGA NA KAGERA YASOGEZWA MBELE WAGENI WAKIWA WAMEKWISHAFIKA BUKOBA

Yanga SC


KAMATI ya Ligi imesogeza mbele kwa siku moja mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Kagera Sugar na Yanga iliyokuwa ichezwe kesho mjini Bukoba kutokana na Uwanja wa Kaitaba kuwa na shughuli nyingine za kijamii.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura Mgoyo amesema kwamba sasa mechi hiyo itachezwa Jumatatu kwenye Uwanja huo huo.
 
 
Wambura alisema kwamba mabadiliko hayo pia yameathiri mechi kati ya Toto Africans na Yanga iliyokuwa ichezwe Oktoba 10 mwaka huu Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza na sasa itachezwa Oktoba 11 mwaka huu. Yanga tayari wapo Bukoba tangu asubuhi, baada ya kuondoka Dar es Salaam kwa ndege.
 
 
Katika hatua nyingine, Wambura amesema kwa vile msimu huu mdhamini mwenyewe ndiye anayegawa vifaa kwa timu, Kamati ya Ligi imeagiza Vodacom iandikiwe barua na nakala kwa klabu zote ili kujua timu ambazo tayari zimekabidhiwa vifaa hivyo zikiwemo logo na siku ambapo timu husika zilipokea.
 
 
Baada ya majibu ya Vodacom ndipo Kanuni za Ligi Kuu zitakapotumika kutoka adhabu kwa timu ambazo zitabainika kuwa zilipokea vifaa lakini hazikuvitumia. Hatua hiyo inafuatia timu za Yanga na African Lyon kutovaa jezi za wadhamini wa ligi hiyo hadi sasa, kwa sababu mbalimbali.
 
 
Wakati Yanga wanakataa nembo nyekundu kwenye jezi za wadhamini, Lyon wao wana mkataba wa kampuni nyingine ya simu, Zantel.
Wakati huo huo: Wambura amesema kwamba, Kamati ya Ligi ya TFF iliyokutana jana imepanga Ligi Daraja la Kwanza (FDL), ianze kutimua vumbi Oktoba 20 mwaka huu.
 
 
Alisema timu zimepangwa katika makundi matatu ya timu nane nane ambapo zitacheza ligi hiyo kwa mtindo wa nyumbani na ugenini. Mshindi wa kila kundi ndiye atakayepata tiketi ya kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao wakati timu ya mwisho kila kundi itashuka daraja kurudi Ligi ya Mkoa.
 
 
Kundi A lina timu za Burkina Moro ya Morogoro, Kurugenzi Mufindi ya Iringa, Majimaji ya Songea, Mbeya City ya Mbeya, Mlale JKT ya Ruvuma, Mkamba Rangers ya Morogoro, Polisi Iringa na Small Kids ya Rukwa.
 
 
Ndanda FC ya Mtwara, Ashanti United, Green Warriors, Moro United, Polisi, Tessema, Transit Camp na Villa Squad zote za Dar es Salaam ndizo zinazounda kundi B wakati kundi C ni Kanembwa JKT ya Kigoma, Morani ya Manyara, Mwadui ya Shinyanga, Pamba ya Mwanza Polisi Dodoma, Polisi Mara, Polisi Tabora na Rhino Rangers ya Tabora.
 
 
Ada ya ushiriki wa ligi ni sh. 200,000 zinazotakiwa kulipwa kabla ya Oktoba 13 mwaka huu. Pia Oktoba 13 mwaka huu kutakuwa na kikao kati ya wenyeviti wa klabu zote zinazoshiriki ligi hiyo na Kamati ya Ligi ambapo pia itafanyika draw (ratiba).

REFA ADUI WA YANGA, SWAHIBA WA SIMBA AENDA NA MAJI LIGI KUU

Mathew Akrama


KAMA ilivyotarajiwa na wengi, refa Mathew Akrama wa Mwanza aliyechezesha ovyo mechi ya watani wa jadi katika soka ya Tanzania, Simba na Yanga, Jumatano wiki hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ‘amekwenda na maji’.  
 
 
Taarifa ya Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura imesema kwamba, Kamati ya Ligi imewaondoa marefa watatu wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kutokana na kuvurunda.
 
 
Mbali na Akrama ambaye ‘Yanga hawana hamu naye’ tangu siku hiyo, wengine ni Paul Soleji wa Mwanza aliyechezesha mechi kati ya Simba na Tanzania Prisons, na mwamuzi msaidizi namba mbili kwenye mechi hiyo Mwarabu Mumbi wa Morogoro, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili wa mechi ya Yanga na Simba, Ephrony Ndissa wa Dar es Salaam amepewa onyo.
 
 
Kamishna wa mechi namba 28 kati ya Yanga na African Lyon, Pius Mashera ameondolewa kwenye orodha ya makamishna wa ligi hiyo kwa kuchelewa kufika kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (Pre match meeting) na uwanjani.
 
 
Vilevile Mashera kwenye ripoti yake aliwasilisha malalamiko dhidi ya msimamizi wa kituo cha Dar es Salaam, na kwa vile suala hilo ni la kinidhamu ametakiwa alipeleke kwenye Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF.
 
 
Nayo Simba imepigwa faini ya jumla ya sh. 600,000 kwa kuchelewa kufika kwenye pre match meeting ya mchezo wao dhidi Tanzania Prisons (sh. 100,000) na kwa washabiki wake kuwatupia chupa za maji waamuzi wa mechi hiyo (500,000).
 

Pia Kamati ya Ligi imeagiza kuwa kwa vile suala la kipa Shaabani Kado wa Mtibwa Sugar kudaiwa kumpiga kiongozi mmoja wa Ruvu Shooting mara baada ya mechi kati ya timu hizo iliyochezwa Uwanja wa Azam Complex ni la kinidhamu lipelekwe kwenye Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya TFF.

AZAM YAIPUMULIA SIMBA NG'ADO KWA NG'ADO



Shujaa wa Azam leo; John Bocco
AZAM FC imeisogelea zaidi Simba kileleni mwa Ligi Kuu ya soka ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuifunga African Lyon bao 1-0 kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
 
 
Azam ambayo ilimaliza mechi hiyo ikiwa pungufu ya mchezaji mmoja, baada ya beki wake Samir hajji Nuhu kutolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 83 kwa kuonyeshwa kadi ya pili ya njano, imefikisha pointi 13 sawa mabingwa watetezi Simba, ambao wapo kileleni sasa kwa wastani wa mabao tu.
 
 
Hadi mapumziko, Azam walikuwa tayari mbele kwa bao hilo, lililotiwa kimiani na mfungaji bora wa Ligi Kuu, John Raphael Bocco ‘Adebayor’ katika dakika ya kwanza ya muda wa nyongeza baada ya kutimu dakika 45 za kipindi cha kwanza.
Hilo linakuwa bao lake la pili Adebayor msimu huu ndani ya mechi tano za Ligi Kuu, hali ambayo inaashiria kasi yake yake si ya kuridhisha msimu huu.
 
 
Kikosi cha Azam kilikuwa; Mwadini Ally, Erasto Nyoni, Samir Hajji Nuhu, Aggrey Morris, Said Mourad, Ibrahim Mwaipopo/Salum Abubakar dk57, Jabir Aziz, Himid Mao/Abdulhalim Humud dk60, John Bocco ‘Adebayor’m, Kipre Tcheche na Abdi Kassim ‘Babbi’.  
 
 
Katika mchezo mwingine, wa leo wenyeji Ruvu Shooting wameifunga Coastal Union ya Tanga mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Mabatini ulioko Mlandizi mkoani Pwani, mabao yaliyotiwa kimiani na Hussein Sued dakika ya sita na Hassan Dilunga dakika ya 12.
 
 
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa mabingwa watetezi na vinara wa ligi hiyo, Simba kuumana na Oljoro JKT kwenye  Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati vibonde wa ligi hiyo, Mgambo Shooting watakuwa wenyeji wa vibonde wengine wa ligi hiyo, Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga, wakati Toto Africans wataikaribisha JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Kirumba mjini Mwanza na Tanzania Prisons watakuwa wenyeji wa Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
 
 
Kagera Sugar wataikaribisha Yanga kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba Jumatatu. Hadi sasa, mwenendo wa ligi unaonyesha ushindani ni kati ya mabingwa watetezi, Simba SC na washindi wa pili wa msimu uliopita, Azam FC ambazo zinakabana kileleni.
 
 
Hali bado si nzuri kwa mabingwa wa kihistoria wa ligi hiyo, Yanga SC ambayo inazidiwa pointi tano na mabingwa watetezi, Simba SC ambao pia ni wapinzani wao wa jadi.
 
 
Timu mbili kati ya tatu zilizopanda Ligi Kuu msimu huu JKT Mgambo na Polisi Morogoro ndizo zipo mkiani, wakati Prisons ndio inaonekana kuwa imara zaidi, kwani ipo nafasi ya tano katika msimamo huo.

P       W       D       L        GF     GA     GD     Pts
Simba SC             5          4          1          0          10       3          7          13
Azam FC             5          4          1          0          7          1          6          13
Yanga SC           5          2          2          1          8          6          2          8
Coastal             6          2          2          1          7          7          0          8
Mtibwa Sugar 4          2          1          1          6          3          3          7
Prisons              4          1          2          1          4          4          0          5
JKT Oljoro        4          1          3          1          4          3          1          6
Ruvu Shooting 6          2          0          4          8          10       -2        6
African Lyon   6          2          0          4          5          10       -5        6
Kagera Sugar4         1          1          2          4          4          0          4
Toto African   4          0          3          1          4          4          0          3
JKT Ruvu            4          1          0          3          3          10       -7        3
Polisi Moro       3          0          2          1          0          1          -1        2
JKT Mgambo     3          0          0          3          1          3          -2        0