Tuesday, January 15, 2013

SIMBA SC KUMSAKA TARATIBU MBADALA WA OKWI BAADA YA JANA KUMUUZA KW AKLABU YA ETOILE DU SAHEL YA TUNISIA


Rage kulia akiwa na rais wa Etoile, kushoto na Okwi katikati jana baada ya kumaliza biashara mjini Tunis, Tunisia 


KLABU ya Simba imesema kwamba haitafanya haraka kuziba nafasi ya mshambuliaji wake wa kimataifa wa Uganda, Emannuel Okwi iliyemuuza Etoile du Sahel ya Tunisia jana.
Hans Poppe
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe alisema jana kwamba kwa kuwa wamekwishakamilisha usajili wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika na muda wa kusajili unaisha leo, hawatafanya haraka ya kusajili mchezaji mwingine.
“Daima sisi huwa tunasajili kwa makini na matunda yake ni kuuza wachezaji kwa bei nzuri, mfano Patrick Ochan, Mganda mwingine tuliyemuuza TP Mazembe (ya DRC), hivyo hatutafanya papara tena katika kusajili, ili tupate mkali kama au zaidi ya Okwi,”alisema Poppe.
Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) alisema kwamba watasubiri kuona kama watafuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika ndipo wasajili mchezaji mwingine, vinginevyo itakuwa hadi msimu ujao.
Simba jana ilimuuza Okwi klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia kwa dau la dola za Kimarekani 300,000, zaidi ya Sh Milioni 450 za Tanzania.
Okwi, aliyezaliwa Desemba 25, mwaka 1992 aliisajiliwa Simba akitoea SC Villa ya Uganda mwaka 2010 akiwa kinda wa miaka 17, akisajiliwa kwa dau la dola za Kimarekani 40,000.
Baada ya kumaliza mkataba wake wa awali, Desemba mwaka jana aliongeza mkataba wa miaka miwili na Simba SC ambao kabla hajaanza kuutumikia, anahamia Sahel.

No comments:

Post a Comment