Thursday, December 27, 2012

NEW CASTLE KUKUMBANA NA RUNGU LA FIFA


  Newcastle na Millwall huenda wakakumbana na adhabu ya shirikisho la soka duniani FIFA kufuatia vilabu hivyo kugomea kuwaachia wachezaji wa kimataifa wa Nigeria  Shola Ameobi na Danny Shittu kwa ajili ya kulitumikia taifa lao katika michuano ya fainali za mataifa ya Afrika nchini Afrika Kusini mwezi Januari

Bosi wa Newcastle Alan Pardew anasema mshambuliaji wake Shola Ameobi hatasafiri kuelekea Afrika katika fainali hizo.

Ameobi na Shittu wote wanatarajiwa kujitoa rasmi katika uteuzi wao katika timu ya taifa ya Nigeria (Super Eagles), jambo ambalo limeonekana kulikasirisha shirikisho la soka la nchi hiyo (NFF).

Meneja wa Newcastle Alan Pardew amesema Ameobi hatatokezea katika michuano hiyo ambayo inatarajiwa kuanza January 19, wakati ambapo mlinzi wa Millwall er Shittu naye anatarajiwa kutolea nje uteuzi wake kama ilivyo kwa Ameobi.

Sheria za FIFA zinasema mchezaji yoyote ambaye atashindwa kuripoti katika timu yake ya taifa baada ya kutajwa na nchi yake kwa ajili ya majukumu ya kimataifa , basi mchezaji huyo atakuwa si halali kutumika katika kipindi chote kilichopendekezwa wakati wa jukumu hilo pamoja na kuongezewa siku tano zaidi kama itawezekana vinginevyo kuwepo na makubaliano mengine kati ya klabu yake na nchi husika.

Mjumbe wa bodi ya shirikisho la soka la Nigeria Chris Green amesema watahakikisha klabu za wachezaji hao zinaadhibiwa kama watagomea kuwaachia wachezaji hao.

No comments:

Post a Comment