Blackburn
Rovers imemfukuza kazi meneja wake Henning Berg na maafisa wengine watatu
katika safu ya makocha ikiwa ni hatua ambayo imefuatia klabu hiyo kutereza
katika vibaya katika msimamo wa ligi ndogo ya nchini England, Championship.
Meneja huyo
raia wa Norway, ambaye aliajiriwa mwezi October, katika jumla ya michezo 10
amefanikiwa kushinda mchezo mmoja tu katika kipindi chake cha utumishi wake wa
siku 57.
Berg, ambaye
alikuwa mchezaji wa Rovers mwaka 1995 wakati huo Rovers ilishinda taji la ligi
kuu ya England “Premier League” na
baadaye akishinda taji la “League Cup” akiwa nahodha wa kikosi mwaka 2002, alirejeshwa
katika klabu hiyo kama meneja mwezi Oktoba.
Baada ya Blackburn
kuanza kwa kusuasua chini ya meneja wake wa zamani Lyn Oslo na Lillestrom klabu
hiyo ikaamua kumpa Berg jukumu la kukinoa kikosi hicho katika kipindi hiki cha
mwisho wa mwaka.
Kichapo cha
bao 1-0 kutoka kwa Middlesbrough jana Boxing Day kilipelekea Rovers kujikuta
katika nafasi ya 17 ikifanikiwa kukusanya alama 7 ndani ya uwezo wake wa
kukusanya alama 30 kama wangeshinda michezo yote chini ya meneja Henning Berg.
Meneja msaidizi,
Eric Black, kocha wa namba moja Iain Brunskill kocha wa makipa Bobby Mimms nap
wamekumbwa na dhahma hiyo ya kufukuzwa kazi pamoja na Berg kutoka katika viunga
vya Ewood Park.
No comments:
Post a Comment