Meneja wa Liverpool
Brendan Rodgers amesisitiza kuwa hawakuwa na la kujivunia katika mchezo ambao
walipoteza kwa kuchapwa mabao 3-1 na Stoke City iliyocheza vema hapo jana kule
katika dimba la Britannia jioni ya jana.
Wekundu hao
walipata bao la mapema kupitia kwa nahodha Steven Gerrard kwa njia ya penati
baada ya Luis Suarez kuangushwa katika eneo la hatari na Ryan Shawcross.
Hata hivyo
Stoke wakafanikiwa kusawazisha na baadaye kuandika bao la pili la uongozi
kupitia kwa Jonathan Walters na kisha bao la kichwa la Kenwyne Jones.
Brendan Rodgers
amekiri kikosi chake kuvurunda katika mchezo huo lakini pia akionekana kuhuzunishwa
na aina ya magoli yaliyokuwa yakifungwa na kusema timu yake inapaswa kujifunza
namna ya kulinda kama inataka kupata alama katika michezo ya ugenini.
“ulikuwa ni
mwanzo mzuri kwetu kwa kupata goli la mapema kupitia njia ya penati, lakini tulishindwa
kujilinda nadhani magoli yote matatu na makosa ya ulinzi, kiukweli
hatukustahili chochote katika mchezo huu”
No comments:
Post a Comment