
Jermain
Defoe alifunga goli la kwanza kwa Spurs kunako dakika ya 58 kabla ya Bale
kufunga magoli mengine matatu yaliyowapa uhakika wa ushindi katika mchezo huo.
Vijana hao
wanaotoka London ya Kaskazini waliingia katika mchezo huo wakiwa na kumbukumbu
ya sare ya bila kufungana dhidi ya Stoke, ambapo walikuwa wakijua wazi kwamba
muhimu kwao ulikuwa ni ushindi ili kuendelea kuleta ushindani katika nafasi ya
juu katika msimamo wa ligi.
Akinukuliwa kupitia
ukurasa wa mtandao wa kijamii wa twitter wa klabu yake, Bale amesema,
"vizuri kufunga magoli na kupata ‘hat
trick’ yangu ya kwanza katika ‘Premier League’ lakini muhimu ni kupata alama 3".
"wachezaji
wote walifanya kazi nzuri, sasa tunajipanga kwa ajili ya mchezo na Sunderland"
Kwa upande
wake meneja Andre Villas-Boas amepongeza vijana wake walivyokuwa uwanjani tangu
kuanza kwa mchezo mpaka mwisho
No comments:
Post a Comment