Thursday, December 27, 2012

GARETH BALE AFURAHIA HAT TRICK YAKE YA KWANZA BPL

Winga wa Tottenham Gareth Bale amefurahia kufanikiwa kufunga mabao matatu ya kwanza katika mchezo mmoja ‘Hat trick’ katika ligi kuu ya soka ya England ‘Premier League’ lakini anasema kikubwa ulikuwa ni ushindi ambao uliipatia alama tatu muhimu Spurs baada ya kuichapa Aston Villa mabao 4-0 hapo jana.

Jermain Defoe alifunga goli la kwanza kwa Spurs kunako dakika ya 58 kabla ya Bale kufunga magoli mengine matatu yaliyowapa uhakika wa ushindi katika mchezo huo.

Vijana hao wanaotoka London ya Kaskazini waliingia katika mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya sare ya bila kufungana dhidi ya Stoke, ambapo walikuwa wakijua wazi kwamba muhimu kwao ulikuwa ni ushindi ili kuendelea kuleta ushindani katika nafasi ya juu katika msimamo wa ligi.

Akinukuliwa kupitia ukurasa wa mtandao wa kijamii wa twitter  wa klabu yake, Bale amesema,

 "vizuri kufunga magoli na kupata ‘hat trick’ yangu ya kwanza katika ‘Premier League’ lakini muhimu ni kupata alama 3".

"wachezaji wote walifanya kazi nzuri, sasa tunajipanga kwa ajili ya mchezo na Sunderland"

Kwa upande wake meneja Andre Villas-Boas amepongeza vijana wake walivyokuwa uwanjani tangu kuanza kwa mchezo mpaka mwisho

No comments:

Post a Comment