Thursday, December 27, 2012

BAADA YA JANA KUFUNGWA BAO 1-O MANCINI ALIA NA MWAMUZI ASEMA HAKUWA FITI - NA FAIR PLAY


MENEJA wa klabu ya Manchester City, Roberto Mancini ameponda kiwango alichochezesha mwamuzi Kevin Friend katika mchezo dhidi ya Sunderland ambao umepelekea kufungwa bao 1-0 jana. Winga wa zamani wa City Adam Johnson ndiye aliyeipatia Sunderland bao la ushindi katika mchezo huo lakini Mancini anaamini kuwa kabla ya bao hilo kufungwa Pablo Zabaleta alitakiwa apewe mpira wa adhabu baada ya kuchezewa vibaya na Graig Gardner. Mancini amedai kuwa labda mwamuzi pamoja na mshika kibendera wake pengine walikula chakula kingi wakati wa sikukuu ya Noel ndio maana hawakuwa katika kiwango bora wakati wakichezesha mchezo huo. Kipindi hicho kimeifanya City kubakia nyuma mbele ya vinara wa ligi hiyo Manchester United kwa alama saba na Mancini anamlaumu mwamuzi kwa kipigo hicho ambacho ni cha kwa klabu hiyo msimu huu.

No comments:

Post a Comment