Thursday, October 18, 2012

TERRY ASALIMU AMRI, akubali Kifungo Mechi 4, aomba Radhi!!


FREDINAND-TERRY_MKNO_HAMNAHatimae Nahodha wa Chelsea John Terry ameamua kutokata Rufaa kupinga Adhabu yake ya kufungiwa Mechi 4 na Faini ya Pauni 220,000 baada ya kupatikana na hatia na FA, Chama cha Soka England, ya kumkashifu kibaguzi Beki wa QPR Anton Ferdinand. 

>>KUZIKOSA Spurs, Man United mara mbili na Swansea!
Uamuzi huu wa Terry, ambao umekuja katika Siku ya mwisho ya yeye kutakiwa akubali au apinge adhabu yake, unamaanisha atazikosa Mechi za Klabu yake Chelsea za Ligi Kuu England dhidi ya Tottenham, Manchester United na Swansea City na pia Mechi ya CAPITAL ONE CUP dhidi ya Man United.
Tukio lililomsulubu Terry lilitokea Oktoba 23 Mwaka jana huko Uwanja wa Loftus Road kwenye Mechi ya Ligi ambayo QPR iliifunga Chelsea bao 1-0.
Baada ya hapo Kesi hiyo ilitinga Mahakamani baada ya Shabiki mmoja kupeleka malalamiko Polisi lakini Mwezi Julai Mahakama ya Westminster ilimwachia huru na hapo ndipo FA ikaamuru Jopo lake Huru la Nidhamu lisikilize Kesi hiyo na ndipo ikamtia hatiani baada ya kutoukubali utetezi wake.
Akikubali adhabu yake, Terry Miaka 31, amesema: “Naomba nichukue nafasi hii kuomba radhi kwa kila mtu kwa lugha niliyotumia.”
Pia aliongeza: “Ingawa nimehuzunishwa na hukumu ya FA, ninakubali kuwa lugha niliyotumia, ukiachilia mbali mazingira yake, haikubaliki kwenye Uwanja wa mpira au popote pale maishani. Kama nilivyosema Mahakamani, ningekuwa najua nini kitatokea, lugha niliyotumia ni wazi haikufaa kwa Mtu wa nafasi kama yangu. Uamuzi uko chini ya kile Klabu ya Chelsea inataka na kwangu pia na hili halitarudiwa tena.’’
Hadi sasa Klabu ya Chelsea haijatoa tamko itamchukulia hatua gani Terry mbali ya kusema inasubiri uamuzi wa Terry kama atakata Rufaa au la.
 

BPL WKIENDI-DABI ya LONDON: Jumamosi AVB kulipa kisasi kwa Chelsea!


RATIBA
Jumamosi Oktoba 20
[SA 8 DAK 45 Mchana]
Tottenham v Chelsea
[SAA 11 JIONI]
Fulham v Aston Villa
Liverpool v Reading
Man Utd v Stoke
Swansea v Wigan
West Brom v Man City
West Ham v Southampton

[SAA 1 na Nusu Usiku]
Norwich v Arsenal
Jumapili Oktoba 21
[SAA 9 na Nusu Mchana]
Sunderland v Newcastle
[SAA 12 Jioni]
QPR v Everton
=============================
BPL_LOGOAndre Villas-Boas, Meneja alietimuliwa kazi na Chelsea baada ya Miezi 9 tu mwanzoni mwa Mwaka huu, Jumamosi atapata nafasi safi ya kulipa kisasi wakati Timu yake anayoiongoza sasa Tottenham itakapoikaribisha Chelsea Uwanjani White Hart Lane katika Mechi ya Ligi Kuu England ambayo ni Dabi ya Jiji la London.
Msimu uliopita, Chelsea walimaliza Ligi wakiwa nafasi ya 6, nafasi mbili nyuma ya Tottenham lakini Chelsea wakaichukua nafasi ya Tottenham kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa vile Chelsea ndio Mabingwa watetezi wa Mashindano hayo na wao Tottenham kutupwa kucheza EUROPA LIGI.
Baada ya kutimuliwa Andre Villas-Boas, mwenye Miaka 34, nafasi yake huko Chelsea ikachukuliwa na aliekuwa Msaidizi wake, Roberto Di Matteo, ambae ndie aliiongoza Chelsea kutwaa Ubingwa wa Ulaya walipoitoa Bayern Munich kwa matuta Mwezi Mei kwenye Fainali huko Munich, Germany.
Chelsea watatinga White Hart Lane wakiwa ndio vinara wa Ligi wakiwa na Pointi 19 baada ya kushinda Mechi 6 na sare 1 na Tottenham wamepanda hadi nafasi ya 5 baada ya kuchinda Mechi zao 4 za mwisho ukiwemo ule ushindi wao murua huko Old Trafford walipoifunga Manchester United bao 3-2 huo ukiwa ushindi wao wa kwanza Uwanjani hapo katika Miaka 23.
Ikiwa Tottenham watamudu kuisimamisha Chelsea hilo litatoa mwanya kwa Timu zinazoifukuza Chelsea ambazo ni Manchester United, Mabingwa Manchester City na Everton.
Man United, ambao wako nafasi ya pili na wenye Pointi 15, wapo kwao Old Trafford kucheza na Stoke City, Man City, ambao pia wana Pointi 15, wapo ugenini kucheza na WBA ambao wako nafasi ya 6, na Everton, walio nafasi ya 4, wanacheza na Timu ya mkiani Queens Park Rangers.


Wachezaji toka Mechi za Kimataifa
Klabu nyingi za Ligi Kuu England zitakuwa zikisubiri kurudi kwa Wachezaji wao kutoka kuzichezea Nchi zao huku wakiwa na wasiwasi kama wako fiti lakini Chelsea watacheza na Spurs bila ya majeruhi Frank Lampard na Ryan Bertrand.
Manchester United, ambao wana listi ndefu ya majeruhi, wanaweza kupata ahueni baada ya Ashley Young na Chris Smalling kupona na kurejea mazoezini tangu Wiki iliyopita.
Man City wataenda huko Hawthorns kucheza na WBA bila ya David Villa ambae aliumia hivi juzi akiichezea Nchi yake Spain na pia Kiungo Jack Rodwell lakini machachari wao Mario Balotelli amepona na juzi alifunga bao wakati Nchi yake Italy ilipoichapa Denmark bao 3-1.
Arsenal, ambao wameteleza hadi nafasi ya 7 wakiwa na Pointi 12, watasafiri kwenda kucheza na Norwich City ambao Msimu huu hawajashinda hata Mechi moja ya Ligi.
Arsenal watacheza bila ya Theo Walcott  alieumizwa kifua kwenye Mechi ya Nchi yake England ilipocheza na San Marino Ijumaa iliyopita lakini Straika wao Olivier Giroud anaweza kucheza baada ya kuifungia Arsenal bao lake la kwanza kwenye Ligi Arsenal ilipoicharaza West Ham 3-1 katika Mechi iliyopita na pia kufunga bao muhimu kwa Nchi yake France ilipotoka 1-1 na Mabingwa wa Dunia Spain katika Mechi ya Kombe la Dunia juzi Jumanne.


MAREFA wa MECHI za WIKIENDI:
Jumamosi Oktoba 20

Tottenham Hotspur v Chelsea
Refa: M Dean
Wasaidizi: S Ledger, J Brooks
Refa wa Akiba: L Mason

Fulham v Aston Villa
Refa: C Foy
Wasaidizi: M McDonough, D C Richards
Refa wa Akiba: I Williamson

Liverpool v Reading
Refa: R East
Wasaidizi: A Garratt, R West
Refa wa Akiba: K Friend

Manchester United v Stoke City
Refa: A Taylor
Wasaidizi: D Cann, S Long
Refa wa Akiba: M Halsey

Swansea City v Wigan Athletic
Refa: M Jones
Wasaidizi: H Lennard, A Halliday
Refa wa Akiba: K A Woolmer

West Bromwich Albion v Manchester City
Refa: M Clattenburg
Wasaidizi: S Beck, S Child
Refa wa Akiba: C Pawson

West Ham United v Southampton
Refa: N Swarbrick
Wasaidizi: J Collin, L Betts
Refa wa Akiba: J Moss

Norwich City v Arsenal
Refa: L Probert
Wasaidizi: R Ganfield, D Bryan
Refa wa Akiba: A Marriner

Jumapili Oktoba 21
Sunderland v Newcastle United
Refa: M Atkinson
Wasaidizi: M Mullarkey, S Burt
Refa wa Akiba: A Taylor

Queens Park Rangers v Everton
Refa: J Moss
Wasaidizi: J Flynn, C Breakspear
Refa wa Akiba: P. Dowd
 

KWA LEO: Mtigila atimuliwa Denmark, France ni mpya!


MARTEN_OLSEN-DENMARKMTIGILA apashwa: ‘HUTAICHEZEA DENMARK TENA!’
Beki wa Kimataifa wa Denmark, Patrick Mtigila, ameambiwa hataichezea Timu ya Taifa tena baada ya kugoma kucheza Mechi  ya juzi ya Nchi hiyo ambayo Denmark ilichapwa 3-1 na Italy kwenye Mechi ya Kombe la Dunia.
Kocha wa Denmark, Morten Olsen, alisema Beki huyo awali alijulishwa atakuwa Benchi na Simon Poulsen ataanza badala yake lakini, wakati Wachezaji wanapasha moto kabla Mechi kuanza huko Mjini Milan, Poulsen aliumia na Mtigila akajulishwa atacheza Mechi hiyo lakini akagoma.
Olsena amesema: “Nipo kwenye Soka kwa Miaka 40 sasa lakini sijashuhudia kitu kama hiki. Amewaangusha wenzake!”
Olsen aliongeza: “Nilimwambia Patrick Mtigila ajipashe lakini alikuwa amehuzunika baada ya kwanza kuambiwa hachezi Mechi hiyo atakuwa Benchi na akasema hawezi kucheza. Hapo hapo nikamwambia aondoke kwenye Timu kwa kuwa amecheza Mechi yake ya mwisho!”
Huko Denmark, Mtigila ni Mchezaji wa Klabu Bingwa yao FC Nordsjaelland.


FRANCE yajipa matumaini!
Baada ya kuchapwa na Japan bao 1-0 katika Mechi ya Kirafiki iliyochezwa Ijumaa iliyopita huko Paris, Watu walianza kuibeza France na walitegemea itatandikwa bao nyingi na Mabingwa wa Dunia Spain Siku 3 zinazifuata huko Madrid katika Mechi ya Kundi I la Kombe la Dunia Barani Ulaya lakini hiyo Jumanne France iligangamala na kutoka 1-1 na Spain.
Katika Mechi hiyo, Spain walitangulia kupata bao lililofungwa na Sergio Ramos na Wadau wakahisi ni ile ile ya EURO 2012 ambapo Mwezi Juni Spain iliichapa France 2-0 kwenye Robo Fainali lakini safari hii France waliibuka kwa nguvu, wakanyimwa Bao safi, Kipa wao Hugo Lloris akaokoa Penati na mwishowe Olivier Giroud akasawazisha bao.
Wachezaji wa France wamekiri Kocha wao, Didier Deschamps, aliwainua morali wakati wa mapumziko wa Mechi hiyo kwa maneno yake.
Sentahafu Mamadou Sakho aliongea: “Hotuba yake ilituinua tukapigana kiume. Alituambia tusikate tamaa, tunaweza kupata sare na kushinda Mechi hii.”
Kwa sasa katika Kundi I Spain na France zimefungana kila moja ikiwa na Pointi 7 kwa Mechi 3 na zitapambana katika marudiano ndani ya Stade de France Jijini Paris hapo Machi 26, 2013.
Mechi zinazofuata kwa France ni mbili za Kirafiki na Italy na Germany kasha Mechi ya Kundi I la Kombe la Dunia dhidi ya Georgia na kufuatia marudiano yao na Spain.
Kocha Deschamps, ambae wakati akiwa Mchezaji wa France alitwaa Ubingwa wa Dunia Mwaka 1998 na wa Ulaya Mwaka 2000, amekiri: “Hii ni Timu changa lakini tunaweza kufanya vizuri na inabidi tuijenge zaidi. Tunajua sisi sio bora lakini pia sisi si Timu mbaya!”
 

KOMBE la DUNIA-Ulaya: Poland 1 England 1


 
>>WACHEZAJI England kufidia Mashabiki £ 50,000!!!
BRAZIL_2014_BESTBaada ya Mechi ya Kundi H la Bara la Ulaya kuwania kucheza Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Brazil kutochezwa jana kufuatia Mvua kubwa na uzembe wa kutofunika Paa la Uwanja wa Taifa huko Warsaw, leo Mechi hiyo imepigwa huku Paa likiwa limefungwa na matokeo kuwa Poland 1 England 1.
+++++++++++++++++++++++

KUNDI H
1 England Mechi 4 Pointi 8
2 Montenegro Mechi 3 Pointi 7
3 Poland Mechi 3 Pointi 5
4 Moldova Mechi 4 Pointi 4
5 Ukraine Mechi 3 Pointi 2
6 San Marino Mechi 3 Pointi 0
+++++++++++++++++++++++
England ndio waliotangulia kupata bao kufuatia kona ya Steven Gerrard kuunganishwa kwa kichwa na Wayne Rooney katika Dakika ya 31 lakini Poland wakasawazisha katika Dakika ya 70 kwa bao la Kamil Glik kufuatia uzembe wa Kipa Joe Hart kukosa kupangua kona.
+++++++++++++++++++++++


MECHI ZIJAZO za ENGLAND:
KIRAFIKI
-Novemba 11: Sweden v England [Ugenini]
-Februari 6: England v Brazil [Wembley, London]


KOMBE la DUNIA KUNDI H:
-Machi 22, 2013: San Marino v England [Ugenini]
-Machi 26, 2013: Montenegro v England [Ugenini]
+++++++++++++++++++++++
Wakati huo huo, Kikosi cha Wachezaji wa England waliokuwepo huko Poland kimetangaza kuwa kitawafidia Mashabiki 2,500 wa England waliosafiri kwenda Poland kushuhudia pambano la jana lililoahirishwa kwa kuchangia Pauni 50,000 na pia kuwaalika wote hao kuhudhuria bure Mazoezi ya Timu hiyo huko England kabla Msimu huu kumalizika.

VIKOSI:
Poland: Tyton, Piszczek, Wasilewski, Wawrzyniak, Glik, Polanski, Krychowiak, Wszolek, Grosicki, Obraniak, Lewandowski
Akiba: Kuszczak, Wojtkowiak, Komorowski, Borysiuk, Murawski, Milik, Mierzejewski, Sobota, Piech, Perquis, Sobiech, Skorupski.


England: Hart, Glen Johnson, Jagielka, Lescott, Cole, Milner, Carrick, Gerrard, Cleverley, Rooney, Defoe
Akiba: Ruddy, Walker, Baines, Cahill, Shawcross, Oxlade-Chamberlain, Shelvey, Lennon, Adam Johnson, Carroll, Welbeck, Forster.
Refa: Gianluca Rocchi (Italy)
++++++++++++++++++++++++++++++


MSIMAMO:
KUNDI A
[Kila Timu imecheza Mechi 4]
1 Belgium Pointi 10
2 Croatia 10
3 Serbia 4
4 Macedonia 4
5 Wales 3
6 Scotland 2
+++++++++++++++++++++++


KUNDI B
1 Italy Mechi 4 Pointi 10
2 Bulgaria Mechi 4 Pointi 6
4 Czech Mechi 3 Pointi 5
3 Armenia Mechi 3 Pointi 3
5 Denmark Mechi 3 Pointi 2
6 Malta Mechi 3 Pointi 0
+++++++++++++++++++++++


KUNDI C
1 Germany Mechi 4 Pointi 10
2 Sweden Mechi 3 Pointi 7
3 Ireland Mechi 3 Pointi 6
4 Austria Mechi 3 Pointi 4
5 Kazakhstan Mechi 4 Pointi 1
6 Faroe Island Mechi 3 Pointi 0
+++++++++++++++++++++++


KUNDI D
[Kila Timu imecheza Mechi 4]
1 Netherlands Pointi 12
2 Hungary 9
3 Romania 9
4 Turkey 3
5 Estonia 3
6 Andorra 0
+++++++++++++++++++++++


KUNDI E
[Kila Timu imecheza Mechi 4]
1 Switzerland Pointi 10
2 Norway 7
3 Albania 6
4 Iceland 6
5 Slovenia 3
6 Cyprus 3
+++++++++++++++++++++++


KUNDI F
1 Russia Mechi 4 Pointi 12
2 Israel Mechi 4 Pointi 7
3 Portugal Mechi 4 Pointi 7
4 Northern Ireland Mechi 3 Pointi 2
5 Azerbaijan Mechi 3 Pointi 1
6 Luxembourg Mechi 4 Pointi 1
+++++++++++++++++++++++


KUNDI G
[Timu zote zimecheza Mechi 4]
1 Bosnia & Herzagovina Pointi 10
2 Greece 10
3 Slovakia 7
4 Lithuania 4
5 Latvia 3
6 Liechtenstein 0
+++++++++++++++++++++++


KUNDI H
1 England Mechi 4 Pointi 8
2 Montenegro Mechi 3 Pointi 7
3 Poland Mechi 3 Pointi 5
4 Moldova Mechi 4 Pointi 4
5 Ukraine Mechi 3 Pointi 2
6 San Marino Mechi 3 Pointi 0
+++++++++++++++++++++++


KUNDI I
1 Spain Mechi 3 Pointi 7 [Tofauti ya Magoli 5]
2 France Mechi 3 Pointi 7 [Tofauti ya Magoli 5]
3 Georgia Mechi 4 Pointi 4
5 Belarus Mechi 4 Pointi 3
4 Finland Mechi 2 Pointi 1
+++++++++++++++++++++++


RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumatano Novemba 14
Northern Ireland v Azerbaijan
Montenegro v San Marino


Ijumaa Machi 22
Slovenia v Iceland
Israel v Portugal
Cyprus v Switzerland
Norway v Albania
Luxembourg v Azerbaijan
Bosnia And Herzegovina v Greece
Netherlands v Estonia
Austria v Faroe Island
Czech Republic v Denmark
Moldova v Montenegro
Poland v Ukraine
Sweden v Ireland
Hungary v Romania
San Marino v England
Scotland v Wales
Spain v Finland
Northern Ireland v Russia
Macedonia v Belgium
Liechtenstein v Latvia
Slovakia v Lithuania
Bulgaria v Malta
Croatia v Serbia
Andorra v Turkey
Kazakstan v Germany

No comments:

Post a Comment