Thursday, January 3, 2013

PONGEZI KWA KOCHA WA BARCA VILANOVA AANZA KAZI RASMI.


MENEJA wa klabu ya Barcelona, Tito Vilanova amerejea mapema kuliko ilivyotegemewa na kuonekana mazoezini jana kwa mara ya kwanza toka alipofanyiwa upasuaji wa koo wiki mbili zilizopita. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 44 alihitaji upasuaji mwingine kufuatia upasuaji aliofanyiwa mara ya kwanza kuondoa uvimbe wa kansa katika koo lake Novemba 2011 na msaidizi wake Jordi Roura kuchukua nafasi yake wakati akijiuguza. Vilanova alitegemewa kurejea tena uwanjani katikati ya Januari lakini aliwatembelea wachezaji jana asubuhi na baadae kuwasimamia wachezaji mazoezini katika kipindi cha mchana. Wachezaji wengi katika kikosi hicho walikuwa hawapo kwasababu ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Nigeria huku nyota wengine wakiwa ndege zao zikiwa zimechelewa kufika wakati wakitoka katika mapumziko ya sikukuu za Noel na mwaka mpya.

No comments:

Post a Comment