Thursday, January 3, 2013

KIPA NAMBA MOJA WA ZAMANI WA URUGUAY AFARIKI DUNIA.


GOLIKIPA wa zamani wa kimataifa wa Uruguay, Ladislao Mazurkiewicz amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 67 baada ya kuugua kwa muda mfupi. Golikipa huyo alikimbizwa hospitalini wiki iliyopita kutokana na matatizo ya kushindwa kupumua vizuri lakini hali yake ilishindwa kutengemaa na kuaga dunia. Mazurkiewicz anachukuliwa kama mmoja wa makipa bora kuwahi kutokea duniani huku akikumbukwa zaidi kwa kiwango cha hali ya juu alichokionyesha katika michuano ya Kombe la Dunia iliyofanyika nchini Mexico mwaka 1970. Nyota huyo enzi zake alijikusanyia mataji mengi akiwa ameshinda mataji matatu ya ya Ligi Kuu nchini Brazil, Kombe la Klabu Bingwa ya Amerika Kusini na Kombe la Intercontinental mwaka 1966 pamoja na Kombe la Ligi akiwa na klabu ya Atletico Mineiro ambayo kwasasa nyota wa Brazil Ronaldinho ndipo anapocheza.

No comments:

Post a Comment