Sunday, January 20, 2013

PETERHANSEL, DESPRES WATAMBA MBIO ZA DAKAR RALLY.


DEREVA nyota wa mashindano ya Dakar Rally, Stephane Peterhansel amefanikiwa kushinda taji la tano la mashindano hayo na kuweka rekodi kuwa dereva wa kwanza kufanya hivyo, wakati Mfaransa mwenzake Cyril Despres naye alishinda taji la tano kwa upande wa mbio za pikipiki. Peterhensel ambaye ameshinda mbio za magari za Dakar mwaka 2004, 2005, 2007, 2012 na mwaka huu, na pia kuwa bingwa katika mbio za pikipiki mara sita na kuvunja rekodi ya Ari Vatanen aliyewahi kushinda mbio hizo mara nne. 
Akihojiwa mara baada ya ushindi huo Peterhensel alidai kuwa hiyo ni siku muhimu kwake kwa kuweka rekodi hiyo na kushukuru kwakuwa ni mara ya kwanza anamaliza mbio za zilizochukua siku 15 bila kupata matatizo yoyote katika gari lake. Wapinzani wakubwa wa Peterhensel kwenye mbio hizo Carlos Sainz na Nasser al-Attiyah walijitoa mapema baada ya magari kupata matatizo ya kiufundi.

No comments:

Post a Comment