Sunday, January 20, 2013

BAFANA BAFANA YABANWA MBAVU NA CAPE VERDE JANA KULE SOUTH AFRIKA KWA MADIBA


HALI ya baridi kali, mvua, soka lisilovutia na uhaba wa mabao ndio mambo yaliyoonekana kuchukua nafasi katika ufunguzi wa michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon inayofanyika nchini Afrika Kusini jana. Michuano ya 29 inayoandaliwa na Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF kuanzia mwaka 1957 ilishuhudia michezo miwili kuisha ya kundi A kumalizika huku hakuna timu iliyoona lango la mwenzake. Wenyeji wa michuano hiyo Afrika Kusini maarufu kama Bafana Bafana walishindwa kuwapa raha mashabiki wao wapatao 85,000 waliojitokeza katika Uwanja wa Soccer City jijini Johannesburg pale alipong’ang’aniwa na timu ngeni katika mashindano hayo ya Cape Verde. Baada ya mchezo ulifuatiwa na mchezo mwingine katika huohuo kati ya Morocco na Angola lakini mpaka dakika tisini zinamalizika hakuna timu iliyoona lango la mwenzake. Michuano hiyo inaendelea tena baadae leo kwa michezo miwili ya kundi B ambapo katika mchezo wa kwanza Ghana itacheza na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC ukifuatiwa na mchezo kati ya Mali na Niger katika Uwanja wa Nelson Mandela Bay jijini Port Elizabeth.

No comments:

Post a Comment