Sunday, January 20, 2013

LIVERPOOL INAHITAJI KUONGEZA WACHEZAJI WAWILI AU WATATU ILI IWE MOTO - GERRARD.


KIUNGO nyota wa klabu ya Liverpool Steven Gerrard anaamini kuwa timu hiyo inaweza kucheza na timu yoyote chini ya meneja mpya Brandan Rogders lakini inahitaji kuongeza wachezaji wawili au watatu ili kusaidia kuongeza nguvu. Liverpool jana wakicheza kwa kiwango bora iliifunga Norwich mabao 5-0 katika Uwanja wa Anfield huku Daniel Sturridge aliyesajiliwa kwa paundi milioni 12 kutoka Chelsea akifunga bao lake la tatu katika michezo mitatu toka atue hapo. Lakini pamoja na ushindi huo mnono Gerrard anaamini kuwa bado wanahitaji wachezaji wawili au watatu wakubwa ili waweze kufukuzia mataji. Liverpool inakabiliwa na mchezo mgumu wa ligi dhidi ya Arsenal katika Uwanja wa Emirates mwishoni mwa wiki ijayo baada ya kucheza mchezo wao wa mzunguko wa nne wa Kombe la FA huko Oldham.

No comments:

Post a Comment