Sunday, February 3, 2013

ROONEY AIPAISHA MAN UNITED POINTI 10 JUU

!


BPL_LOGONDANI ya CRAVEN COTTAGE, iliyozimika Umeme Dakika chache kabla Haftaimu na kusababisha Mechi isimame, Wayne Rooney alipiga Bao moja na la ushindi kwa Manchester United katika Dakika ya 79 walipoitungua Fulham Bao 1-0, na kuwapaisha kileleni wakiwa Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Man City ambao kesho wanaivaa Liverpool Uwanjani Etihad.
++++++++++++++++++++++
BPL:
MSIMAMO-Timu zaJuu:
1 Man United Mechi 25 Pointi 62
2 Man City  Mechi 24 Pointi 52
3 Chelsea  Mechi 25 Pointi 46
4 Tottenham  Mechi 24 Pointi 42
5 Everton  Mechi 25 Pointi 42
6 Arsenal  Mechi 25 Pointi 41
7 Liverpool Mechi 24 Pointi 35
++++++++++++++++++++++
Mechi hii ilikuwa mshikemshike huku kila upande ukikosa Mabao na Rooney kupiga posti lakini ushindi huu, bila shaka, utamfurahisha Sir Alex Ferguson kwa sasa na kuwaachia kibarua kikubwa wapinzani wao kuifukuza.
VIKOSI:
Fulham: Schwarzer, Riether, Hangeland, Senderos, Riise, Duff, Karagounis, Baird, Dejagah, Ruiz, Rodallega
Akiba: Etheridge, Petric, Frimpong, Hughes, Emanuelson, Davies, Kacaniklic.
Man United: De Gea, Da Silva, Ferdinand, Evans, Evra, Valencia, Cleverley, Carrick, Nani, Rooney, van Persie
Akiba: Amos, Anderson, Giggs, Smalling, Hernandez, Welbeck, Kagawa.
Refa: Kevin Friend
++++++++++++++++++++++
RATIBA/MATOKEO:
Jumamosi Februari 2
QPR 0 Norwich 0
Arsenal 1 Stoke 0
Everton 3 Aston Villa 3
Newcastle 3 Chelsea 2
Reading 2 Sunderland 1
West Ham 1 Swansea 0
Wigan 2 Southampton 2
Fulham 0 Man United 1
Jumapili Februari 3
[SAA 10 na Nusu Jioni]
West Brom v Tottenham
[SAA 1 Usiku]
Man City v Liverpool

No comments:

Post a Comment