Tuesday, February 5, 2013

MABINGWA W AULAYA CHELSEA WAKUMBWA NA MAJERUHI SASA KUZIKOSA MECHI ZA KESHO ZA NCHI ZAO ZA FIFA DATE ,,,BA AVUNJIKA PUA,CECH AVUNJIKA KIDOLE CHA MKONO NA DAVID LUIZ MISULI

>>NAE LUIZ YUPO KIKOSI CHA BRAZIL, HATIHATI KUCHEZA!!
CHELSEA_ULAYA_2012MABINGWA wa ULAYA, Chelsea, wamekumbwa na balaa ya Wachezaji wao Nyota na wa Kimataifa kuzikosa Mechi za Nchi zao za Jumatano Februari 6 na pia wataikosa Mechi ya Klabu yao ya Ligi Kuu England hapo Jumamosi dhidi ya Wigan Uwanjani Stamford Bridge na hao ni Kipa Petrc Cech, alievunjika Kidole mkononi, Demba Ba, alievunjika Pua na David Luiz, ambae ana matatizo ya Musuli za Mguu.
Demba Ba amelazimika kujitoa kwenye Kikosi cha Nchi yake Senegal baada ya kuvunjwa Pua na Buti ya Beki wa Newcastle Fabricio Coloccini Jumamosi iliyopita Chelsea ilipotwangwa 3-2 kwenye Mechi ya Ligi na Kipa Petr Cech alilazimika kujitoa kwenye Kikosi cha Czech Republic ambao wanacheza na Uturuki baada ya kuwa na maumivu ya Kidole kidogo cha Mkononi na uchunguzi kuthibitisha kimevunjika.
Lakini, huko Kambi ya Brazil, Kocha Luiz Felipe Scolari, amesema hatamchezesha Beki David Luiz ikiwa hataonekana fiti kutokana na maumivu ya Musuli za Mguu wake.
Luiz aliumia kwenye Dakika za mwisho za Mechi ya CAPITAL ONE CUP walipocheza na Swansea City Januari 23.
Kwenye Mechi hiyo na Wigan, Chelsea watamkaribisha tena Winga wao Eden Hazard ambae alikuwa Kifungoni kwa Mechi 3 alichopata baada ya kuchapwa Kadi Nyekundu kwa kumpiga teke Kijana muokota Mipira wakati wa Mechi ya Nusu Fainali ya CAPITAL ONE CUP kati ya Swansea City na Chelsea iliyochezwa Uwanja wa Liberty.
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA:
Jumamosi Februari 9
[Saa 9 Dak 45 Mchana]
Tottenham Hotspur v Newcastle United
[Saa 12 Jioni]
Chelsea v Wigan Athletic
Norwich City v Fulham
Stoke City v Reading
Sunderland v Arsenal
Swansea City v Queens Park Rangers
[Saa 2 na Nusu Usiku]
Southampton          v Manchester City
Jumapili Februari 10
[Saa 10 na Nusu Jioni]
Aston Villa v West Ham United
[Saa 1 Usiku]
Manchester United v Everton
Jumatatu Februari 11
[Saa 5 Usiku]
Liverpool v West Bromwich Albion
++++++++++++++++++++++
BPL:
MSIMAMO:
[Kila Timu imecheza Mechi 25]
1 Man United  Pointi 62
2 Man City   53
3 Chelsea   46
4 Tottenham   45
5 Everton   42
6 Arsenal   41
7 Liverpool  36
8 Swansea  34
9 WBA  34
10 Stoke  30
11 West Ham  30
12 Sunderland  29
13 Fulham  28
14 Norwich  28
15 Newcastle  27
16 Southampton  24
17 Reading  23
18 Wigan  21
19 Aston Villa  21
20 QPR  17

No comments:

Post a Comment