Sunday, February 3, 2013

AFCON 2013: WENYEJI AFRIKA KUSINI NJE KWA MATUTA!

  

>>LEO NI ROBO FAINALI: IVORY COAST v NIGERIA & BURKINA FASO v TOGO.
AFCON_2013-NA_KABUMBU_LIANZEWenyeji wa AFCON 2013, Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, Afrika Kusini, wametupwa nje ya Mashindano hayo kwa kushindwa Mikwaju ya Penati tano tano walipopigwa kwa Penati 3-1 na Mali baada ya kwenda sare ya Bao 1-1 katika Dakika 120 za Mchezo.
+++++++++++++++++
PENATI:
Afrika Kusini 1
-Tshabala= Alifunga
-Furman= Iliokolewa
-Mahlagu= Iliokolewa
-Majoro= Alikosa
Mali 3
-Diabate= Alifunga
-Tamboura= Alifunga
-M Traore= Alifunga
+++++++++++++++++
Katika Dakika 90, Afrika Kusini walitangulia kufunga kwa Bao la Tokelo Rantie katika Dakika ya 32 na Mali kurudisha Dakika ya 58 kwa Bao la Seydou Keita.
Mabao hayo yalidumu hadi Dakika 90 za Mchezo na Nyongeza ya Dakika 30 haikubadilisha matokeo hayo ndipo zikaja Penati na Afrika Kusini kufunga moja tu kupitia Siphiwe Tshabalala.
Leo zipo Robo Fainali mbili za mwisho kati ya Ivory Coast v Nigeria na Burkina Faso v Togo.
Mali watacheza na Mshindi kati ya Ivory Coast v Nigeria kwenye Nusu Fainali.
Mapema jana, Ghana waliichapa Cape Verde 2-0 na kutinga Nusu Fainali ambako watacheza na Mshindi kati ya Burkina Faso v Togo.
VIKOSI:
Afrika Kusini: Khune, Gaxa, Masilela, Khumalo, Sangweni, Furman, Mahlangu, Phala (Serero 89’), Letsholonyane, Parker (Tshabalala 105’), Rantie (Majoro 41’)
Mali: So Diakite, Diawara, Tamboura, A.Coulibaly, Wague, Keita, Sissoko (M Traore 55’), Sow, Sa Diakite (Diarra 24’), Maiga, Samassa (Diabate 88’)

No comments:

Post a Comment