Saturday, January 5, 2013

RAIS WA PSG NASSER AL KHELAIFI ASEMA HAWEZI KUONGEA NA RONALDO KWA MLANGO WA NYUMA - AL KHELAIFI.


RAIS wa klabu ya Paris Saint-Germain-PSG, Nasser Al Khelaifi amesisitiza kuwa klabu yake haitaanza mbio za kumfukuzia Cristiano Ronaldo bila kwanza kuzungumza na Real Madrid. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ureno anaonekana kutokuwa na furaha katika klabu hiyo yenye maskani yake katika Uwanja wa Santiago Bernabeu ambapo PSG wameonyesha kwamba wapo tayari kumsajili nyota huyo katika Ligi Kuu nchini Ufaransa maarufu kama Ligue 1. Al Khelaifi amesema anatambua Ronaldo ni mchezaji wa Real Madrid na anaheshimiana sana na rais wa klabu hiyo hivyo hawezi kufanya jambo bila kumtaarifu. Mbali na Ronaldo kuripotiwa kutakiwa na PSG lakini pia kocha wa Madrid Jose Mourinho naye amehusishwa na tetesi za kutimkia katika klabu hiyo tajiri nchini Ufaransa lakini Khelaifi amesisitiza bado wana imani kubwa na kocha wa sasa Carlo Ancelotti.

No comments:

Post a Comment