Friday, January 4, 2013

MOUNTAIN BIKER STANDER KILLED IN CRASH.


MWENDESHA baiskeli za milimani raia wa Afrika Kusini, Burry Stander amefariki dunia kutokana na ajali jana huko KwaZulu-Natal na taarifa hizo kuthibitishwa na Chama cha Waendesha Baiskeli nchini humo-CSA. Kwa mujibu wa CSA Stander alikuwa akirejea kutoka mazoezini katika ufukwe wa Shelly Beach ambapo aligongwa na gari na polisi wanafanyia uchunguzi tukio hilo la kusikitisha. Stander mwenye umri wa miaka 25 alikuwa mshindi wa tano katika mashindano ya Cross Country kwenye michuano ya Olympiki iliyofanyika London mwaka jana. Mbali na kushiriki michuano hiyo ya London Stander pia alishiriki mashindano kama hayo ya Cross Country katika michuano ya Olimpiki iliyofanyika Beijing, China mwaka 2008 na kufanikiwa kushika nafasi ya 15 wakati huo akiwa na miaka 20.

No comments:

Post a Comment