Friday, January 4, 2013

INNA LILLAHI WA INNA ILAYHI RAJ'UN [MUNGU IWEKE MAHALI PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU JUMA KILOWOKO A.K.A. SAJUKI LEO ALIVYOPUMZISHWA KATIKA MAKABURI YA KISUTU




 Waombolezaji wa Msiba wa Msanii wa Filamu hapa nchini Marehemu  Sadick Juma Kilowoko wakibeba jeneza lenye mwili wake tayari kwa taratibu za kwenda Mazikoni, wakitokea Nyumbani kwa Marehemu Tabata Bima.
Mwili wa Marehemu Sajuki ukipakiwa kwenye gari
Dua ikisomwa kabla ya kuondoka kwa Mwili wa Marehemu kwenda mazikoni.
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania,Saimon Mwakifwamba akimpokea Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh. Zitto Kabwe alipokuwa akiwasili msibani hapo

Pamoja na mvua kubwa kunyesha haikuzuia watu kufika kwa aajili ya kuomboleza kifo cha Marehemu sajuki
Waombolezaji wakiwa wanajifunika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar
Mwili wa marehemu Sajuki ukiondoka nyumbani kuelekea makaburi ya Kisutu
 Sehemu ya waliohudhuria msiba wa Sajuki katika makaburi ya Kisutu 
Wadau mabali mbali wakisubiria mwili wa Marehemu Sajuki, huku Profesa Jay akionekana kwa mbali miongoni mwa wanaousubiri mwili.
Umati wa watu ukiwa makaburini Kisutu Dar
 Mwili wa marehemu Sajuki ukiwasili katika makaburi ya Kisutu tayari kwa mazishi
 Rais Kikwete pia alihudhuria mazishi ya marehemu Sajuki
 Jeneza liliobeba mwili wa marehemu Sajuki
Hili ndilo kaburi alilo zikiwa Maehemu Sajuki
 Jeneza lililobeba Mwili wa Marehemu Sadick Juma Kilowoko (SAJUKI) likiwasili kwenye Makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam mchana huu tayari kwa Mazishi yaliyoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh. Jakaya Mrisho Kikwete.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka udongo kwenye Kaburi la Marehemu Sadick Juma Kilowoko (SAJUKI) yaliyofanyika mchana huu kwenye Makaburi ya Kisutu,Jijini Dar es Salaam.
Msanii Z Anto akiswali juu ya kaburi la Marehemu Sajuki.
This is it! Hapa ndipo sajuki amelala! May his soul R.I.P

Inna Lillahi Wa Inna Ilayhi Raj'un

No comments:

Post a Comment