Tuesday, January 8, 2013

MAKOMBE ULAYA: LEO COPA del REY & ITALIAN CUP!

>>NI KIMBEMBE KWA REAL MADRID KWENYE COPA del REY!!
>>ITALIAN CUP: NI JUVE v AC MILAN!!
BARCA_v_REALVIGOGO, Real Madrid, wakiwa wamepoteza matumaini ya kutetea Ubingwa wao wa La Liga wakiwa Pointi 16 nyuma ya vinara FC Barcelona, Jumatano watacheza Mechi ya marudiano ya COPA del REY na Celta Vigo Uwanjani Santiago Bernabeu huku wakitakiwa kupindua kipigo cha 2-1 walichokipata katika Mechi ya kwanza la sivyo Msimu wao wote utabaki kuomba waifunge Manchester United kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI ili wawe na matumaini ya kuambua Taji.
Barcelona, ambao ndio Mabingwa watetezi, wana kazi nyepesi kidogo kwani wapo nyumbani Nou Camp kucheza na Cordoba Timu ambayo waliichapa 2-0 katika Mechi ya kwanza.
Huko Italy, Italian Cup inaingia hatua ya Robo Fainali na Mechi ya mvuto kabisa ni ile ya Juventus v AC Milan.
COPA del REY
RAUNDI ya 4
MECHI za MARUDIANO
Jumanne Januari 8
[Matokeo Mechi ya kwanza katika Mabano]
Valencia v Osasuna [2-0]
Jumatano Januari 9
Sevilla v Real Mallorca [5-0]
Real Madrid v Celta Vigo [1-2]
Real Zaragoza v Levante [1-0]
Alhamisi Januari 10
Getafe v Atletico Madrid [0-3]
Barcelona v Cordoba [2-0]
Real Betis v Las Palmas [1-1]
ITALIAN CUP
ROBO FAINALI
Jumanne Januari 8
SS Lazio v Catania
Jumatano Januari 9
Juventus v AC Milan
Jumanne Januari 15
Inter Milan v Bologna
Jumatano Januari 16
Fiorentina v AS Roma

No comments:

Post a Comment