Thursday, January 3, 2013

DEMBA BAAA AMEKAMILISHA USAJILI WAKE CHELSEA NA SASA NI MCHEZAJI HALALI WA THE BLUES,,AMENUNULIWA KWA PAUNDI MIL.7.5 TOKA NEWCASTLE


ALIYEKUWA mshambuliaji nyota wa klabu ya Newcastle United, Demba Ba amekamilisha usajili wake kwenda Chelsea huku kocha Alan Pardew akisisitiza kuwa nyota huyo ameondoka kwa Baraka zote za klabu. Ba mwenye umri wa miaka 27, mapema leo alikuwa kwenye mazungumzo na Chelsea kuhusiana na maslahi yake binafsi baada ya klabu hiyo kukubali kulipa kiasi cha paundi milioni 7.5 kwa Newcastle. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Senegal aliachwa katika kikosi kilichopambana na Everton jana usiku na Pardew alifunguka kwa kusema mshambuliaji huyo wa zamani wa West Ham United ameshakubaliana maslahi binafsi na Chelsea. Ba alijiunga na Newcastle mwaka 2011 akitokea West Ham na amefunga mabao 29 katika michezo 54 ya ligi aliyocheza. Newcastle kwasasa inamfukuzia mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Ufaransa na klabu ya Olympique Marseille, Loic Remy ili kuziba pengo la Ba

No comments:

Post a Comment