Saturday, January 5, 2013

KATIBU MKUU WA TAREFA FATTY REMTULA AKABIDHI VYETI KWA MAKOCHA 30 MKOANI TABORA LEO



Chama cha soka mkoa wa tabora TAREFA chini ya uenyekiti wa Yusuph Kitumbo  na katibu mkuu FATTY DEWJ REMTULA leo  kimetoa  vyeti vya wahitimu ngazi ya preliminary ya ukocha ambao bado hawajapatiwa vyeti vyao,ambao walimaliza mafunzo miaka ya nyuma na a mbao wamemaliza mafunzo hivi majuzi chini ya ukufuzi wa SLIVESTER MARSH kocha msaidizi w atimu ya Taifa ya Tanzania.

Akikabidhi vyeti hivyo katibu mkuu wa TAREFA mkoa wa tabora FATTY REMTULA ametoa vyeti hivyo kwa  Makocha 30 ambao walihitimu ngazi hiyo  wa awali ni hawa wafuatao,Stephen Paulo Luziga,Hassan Omary Morrocco,Balunda K. Njeno,Emmanuel M,Kahuka,Gidion P.K Masunga,Kopa Rashid,Kopa,Bastidi G Protas,Seif Salim Omary,Joseph R Kitwenya,Maganga J Brighton ,Selemani Ally Malenge,na Fredrick D Jairos.

Wengine wanaotarajia kukabidhiwa vyeti hivyo ni Mashaka S Kalunga,Mohamedy J Mkoko,Emmanuely P Kinandikwa,Gift E Mwinuka,Milambo Camil Yusuph,Eliah John Lusinde,Hamady Hamis Simba,Osborn Mathew Msaka,Reuben Maige Lishim ,Donard S Mlawa,Fedinand S Machunde,Goerge Marriot Kazi,Revocatus M Fundi,Peter Seif Sizya,Joel Mathayo Rukutsa,Charles K Kidifu,Bora Frank Nduguru na Yahaya Masimba Mntangi.

WAKATI HUO HUO Chama cha makocha mkoa wa Tabora TAFCA  kimeamua kuufuta uchaguzi ambao ulikuwa unatarajia kufanyika mkoa Tabora tarehe 10/1/2013 hapa mkoani tabora umefutwa kutokana na wanachama wa TAFCA kuridhia kuwa ni bora kwanza chama kikafufuliwa ili kiwe hai kwani kuna baadhi ya wanachama wanalipa pesa zao za uanachama lakini hawatambuliwi kuwa ni wanachama kutokana na ubazilifu wa pesa kwa baadhi ya viongozi wa TAFCA kuziminya pesa za wajumbe hao.

No comments:

Post a Comment