Saturday, January 12, 2013

KAMATI TENDAJI YA MPIRA WA MIGUU MKOA WA TABORA TAREFA YAKUTANA KWA MARA YA KWANZA TOKA ICHAGULIWE DEC 22 MWAKA JANA KATIKA UKUMBI WA FRANKMAN



Kamati tendajiya uongozi wa mpira wa miguu mkoa wa tabora TAREFA  leo imekutana kwa mara ya kwanza toka ichaguliwe tarehe 22 dec.2012 mwaka jana kujadili mambo mbali mbali ya soka la mkoa wa tabora kubwa zaidi ajenda zilizojadiliwa  ni pamoja na maandalizi ya timu za daraja la kwanza kuweza kupandisha timu mojawapo ya daraja la kwanza ipande ligi kuu tanzania bara kati ya timu hizo mbili za mkoani tabora Rhino Rangers ama Polisi Tabora.

Ajenda ya pili ni pamoja na kuandaa ligi za wilaya pamoja na mkoa wa tabora ili kupata timu ambazo zitakuwa na makali ya kurudisha taswira ya soka la mkoa wa tabora ni pamoja na kupata timu 2 ambazo zitapatikana wilayani kote za tabora wilaya ya uyui ,skonge,urambo,nzega,igunga na tabora mjini kila wilaya ipate timu 2 na mkoa timu moja.

Ajenda ya tatu ni pamoja na makabidhano ya  nyaraka za TAREFA ikiwemo na vifaa vya ofisi,kwani mpaka sasa ivi katibu wa zamani wa TAREFA bw. Albert Sitta hataki kukabidhisha nyaraka hizo kw auongozi mpya uliochaguliwa tarehe 22 dec.2012 chini ya uenyekiti wa Yussuph Kitumbo.

Ajenda nyingine ni pamoja na kujaza nafasi zilizowazi katika uongozi kama nafasi ya katibu msaidizi  kwani mwenyekiti aliridhia kumjaza katibu mkuu wa TUFA bw.Juma Mapunda kuwa kaimu katibu msaidizi na kamjaza bi Janethi Michael kuwa kaimu  mweka hazina wa TAREFA.

Ajenda nyingine iliyojadiliwa ni pamoja na maendeleo ya soka mawilayani mkoani tabora wamehakikisha kuwa soka la wilayani liwe na taswira ya kisoka siyo kama ilivyopotea kutokana na uongozi uliopita chini ya uenyekiti wa Ismail Aden Ragge pamoja na katibu mkuu wake Albert Sitta kuwa hawana organization nzuri juu ya uongozi wao pamoja na ajenda nyingine mengineyo kama kuandaa vitega uchumi,kuandaa ligi mbalimbali,kuandaa kozi za waamuzi,marefarii pamoja na kozi za makocha..

No comments:

Post a Comment