Saturday, December 29, 2012

ANZHI MAKHACHKALA WAPUUZA MADAI YA KWAMBA WANAMWITAJI LIONELL MESSI KWA EUO ML 250


 Anzhi Makhachkala imekanusha taarifa zilizowahusisha kuwa wametenga euro milioni 250 kwa ajili ya kumsajili nyota wa Barcelona Lionel Messi.

Taarifa zilizo ripotiwa na jarida la Mundo Deportivo ziliarifu kuwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentina amekataa ofa ya euro milioni 30 kutoka katika klabu hiyo ya Russia.


Hata hivyo mshauri wao wa mambo ya masoko, German Tkachenko ameponda taarifa hiyo na kusema ilikuwa ni uongo mtupu na kusisitiza kwamba klabu yake haifanyi shughuli za uhamisho kwa namna hiyo.

Akiongea na gazeti la Russia la Sports-Express amesema

"hakuna hata chembe ya ukweli katika hilo"

Gazeti hilo la nchini Russia pia limearifu kuwa Messi si tu amekataa ofa hiyo, lakini pia kama mpango huyo ungefanikiwa basi mkataba wake ungemuweka katika klabu hiyo mpaka 2018.

Mshambuliaji mwenzake wa zamani wa Camp Nou Samuel Eto’o, ambaye alicheza pamoja na Messi  Barca, aliondoka Russia na kuelekea katika klabu hiyo kwa mshahara mnono akiwa ndiye mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa duniani na alihama kwa uhamisho wa euro milioni 20 kwa mwaka.

No comments:

Post a Comment