Saturday, December 29, 2012

GUADIOLA KUREJEA KUFUNDISHA SOKA MWAKANI 2013


 Pep Guardiola atarejea kufundisha soka mwakani 2013 baada ya muda mrefu nje ya soka kwa mujibu wa Rais wa zamani wa Barcelona Joan Laporta.

Guardiola aliondoka kuifundisha Barcelona baada ya kumalizika msimu uliopita akitaka kupumzika kwa muda baada ya misimu minne ya kuifundisha kwa mafanikio vijana wa Catalunya.

Kocha huyo raia wa Hispania alikuwa akihusishwa na kujiunga na moja ya vilabu vukubwa barani Ulaya tangu wakati ho alipoa achana na Barcelona, ikiwa ni pamoja na Paris Saint-Germain, ingawa Laporta anaamini kuwa klabu hiyo ya nchini Ufaransa haimfai Guardiola.

Akikaririwa amesema"nadhani Pep atarejea kufundisha mwakani. Ana mvuto mkubwa wa kufundisha, ana mawazo safi na ana akili"  Najisikia mwenye heshima kuwa karibu na Pep, kwangu mimi ndiye kocha bora dunia

No comments:

Post a Comment