Tuesday, February 5, 2013

PETR CECH MCHEZAJI BORA WA MWAKA NCHINI KWAO.


GOLIKIPA nyota wa kimataifa wa Jamhuri ya Czech na klabu ya Chelsea, Petr Cech amepigiwa kura ya kuwa mchezaji bora wa mwaka 2012 nchini humo. Cech mwenye umri wa miaka 30 alishinda tuzo hiyo jana katika kura zilizopigwa na wachezaji, makocha, maofisa wa shirikisho la soka nchini humo pamoja na waandishi habari hiyo ikiwa ni mara ya tano mfululizo kushinda. Beki anayekipiga katika klabu ya Werder Bremen Theodor Gebre Selassie alishika nafasi ya pili kwenye tuzo hizo huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Petr Jiracek. Mwaka uliopita, Cech alinyakuwa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na klabu ya Chelsea na baadae aliisaidia timu yake ya taifa kufika hatua ya robo fainali ya michuano ya Ulaya iliyofanyika huko Poland na Ukraine.

No comments:

Post a Comment