Mwaka 2012 ulikuwa na
mafanikio makubwa kwa Messi baada ya kufunga mabao mengi na kuipita
rekodi iliyowekwa miaka 40 iliyopita na Gerd Muller ambaye alifunga
mabao 85 huku yeye akimaliza mwaka jana akiwa amefunga mabao 91. Akishukuru
mara baada ya kupokea tuzo hiyo Messi aliwashukuru waandaji na wale
wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika kupiga kura ya
kumchagua kubeba tuzo hiyo kwa mara ya nne.
Nyota huyo pia
aliwashukuru wachezaji wenzake wa Barcelona akiwemo Iniesta ambaye
walikuwa wakigombea wote tuzo makocha na viongozi bila kusahau wachezaji
wenzake wa timu ya taifa ya Argentina na mashabiki wake wote wa ujumla.
KIKOSI bora cha
mwaka 2012 maarufu kama FIFPro waliosimama mbele kulia na timu zao
katika mabano Xabi Alonso (Real Madrid, Hispania), Xavi Hernandez
(Barcelona, Hispania), Andres Iniesta (Barcelona, Hispania), Lionel
Messi (Barcelona, Argentina), Radamel Falcao (Atletico Madrid,
Colombia), Cristiano Ronaldo (Real Madrid, Ureno), Marcelo (Real Madrid,
Brazil), Sergio Ramos (Real Madrid, Hispania), Gerard Pique (Barcelona,
Hispania), Dani Alves (Barcelona, Brazil) na Iker Casillas (Real
Madrid, Hispania).
No comments:
Post a Comment