Wednesday, January 16, 2013

MARADONA ASEMA HANA MPANGO WA SOKA TENA I QUIT FOOTBALL - MARADONA.


NGULI wa soka nchini Argentina, Diego Maradona amebainisha kuwa hana mpango wa kushughulika mambo  ya soka tena. Maradona ambaye ni kocha wa zamani wa klabu ya Al Wasl ya Dubai amezungumzia kuishiwa kwake hamu na mchezo huo kufuatia kutimuliwa na kutafutwa mbadala wa haraka wa aliyekuwa kocha wa River Plate Matias Almeyda. Akihojiwa Maradaona amesema baada ya kukasirishwa na jinsi walivyomtimua Almeyda na muda mfupi baadae kumteua Ramon Diaz kuziba nafasi yake hahitaji tena kujishughulisha na masuala ya soka. Maradona ambaye nezi zake aliisaidia nchi yake kunyakuwa Kombe la Dunia mwaka 1986 nchini Mexico, amedai kwamba kitendo hicho cha kubadilisha kocha ndani ya siku tatu ndichio kilichomkera na kuamua kuachana na mambo ya soka.

No comments:

Post a Comment