Wednesday, January 16, 2013

MAMBO YAMEKWIVA UCHAGUZI MKUU WA TFF MALINZI,NYAMLANI WAUTAKA URAIS WA TFF KUMRITHI TENGA NAYE BOSSI WA YANGA YUMO NDANI YUSUPH MANJI NI BALAAAAAAAAAA



Manji anazungumza na Waandishi wa Habari baada ya kuchukua fomu
Mmiliki wa klabu ya African Lyon, Rahim Kangenzi ‘Zamunda’ akimchukulia fomu ya kugombea Uenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu kwa niaba ya klabu za Ligi Kuu zilizompendekeza, Mwenyekiti wa Yanga SC, Yusuf Mehbub Manji (kulia) ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ilala, Dar es Salaam mida hii, kuelekea uchaguzi utakaofanyika Februari 24, mwaka huu mjini Dar es Salaam. Anayetoa fomu hiyo kushoto ni Ofisa wa TFF, Jonathan Aloyce Kakwaya.   
Zamunda anamkabidhi fomu yake Manji
Mhasibu wa TFF anamuandikia Manji risiti

Mwenyekiti wa Chama cha Soka Kagera (KRFA), Jamal Emil Malinzi akirejesha fomu ya kugombea urais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ofisi za shirikisho hilo, Ilala, Dar es Salaam mida hii, kuelekea uchaguzi utakaofanyika Februari 24, mwaka huu mjini Dar es Salaam. Anayepokea fomu hiyo ambayo Malinzi alichukua kwenye tovuti ya TFF na kujaza kisha kuilipia katika benki ya CRDB kushoto ni Ofisa wa TFF, Jonathan Aloyce Kakwaya.   
Anashuka kwenye gari

Anaanza kuekelea ofisi za TFF
Anajiorodhesha
Risiti yake ya benki
  

Anazungumza na Waandishi wa Habari


Makamu wa kwanza wa rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Athumani Jumanne Nyamlani akichukua fomu ya kugombea urais wa shirikisho hilo, kwenye ofisi za TFF, Ilala, Dar es Salaam mida hii kwa ajili ya uchaguzi utakaofanyika Februari 24, mwaka huu mjini Dar es Salaam. Anayekabidhi fomu kushoto ni Ofisa wa TFF, Jonathan Aloyce Kakwaya.
Akiwa na rafiki zake waliomsindikiza kuchukua fomu
Anahesabu fedha

Makamu wa kwanza wa rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Athumani Jumanne Nyamlani akikabidhi fedha za malipo ya fomu ya kugombea urais wa shirikisho hilo, katika uchaguzi utakaofanyika Februari 24, mwaka huu mjini Dar es Salaam. Anayepokea kushoto ni Ofisa wa TFF, Jonathan Aloyce Kakwaya.

No comments:

Post a Comment