Friday, January 18, 2013

MAMBO YA TIMUA TIMUA NDANI YA YANGA YAENDELEA MWINGINE ATUPIWA VIRAGO YANGA BENCHI LA UFUNDI



KLABU ya Yanga imefanya marekebisho tena katika benchi lake la Ufundi, kwa kumuondoa Daktari, Sufiani Juma ambaye nafasi yake inachukuliwa na Dk Nassor Matuzya.
Hayo yanakuwa mabadiliko ya pili katika benchi la Ufundi la Yanga ndani ya miezi miwili, kwani awali alienguliwa kocha wa makipa, Mfaume Athumani Samatta ambaye nafasi yake ilichukuliwa na Mkenya, Razack Ssiwa.
Nassor Matuzya. Amechukua nafasi
Kabla ya hapo, Septemba mwaka jana, Yanga ilimuengua Kocha wake Mkuu, Mbelgiji Tom Saintfiet na nafasi yake kupewa Mholanzi, Ernie Brandts.  
Yanga SC iliyorejea wiki Jumapili kutoka Uturuki kwenye kambi ya wiki mbili mjini Antalya, kesho itashuka Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kucheza na Black Leopard ya Afrika Kusini katika mchezo wa kirafiki.
Black Leopard inayoshika nafasi ya 12 katika Ligi Kuu ya Afrika Kusini yenye timu 16, imewasili leo ikiwa na msafara wa watu 42 na kufikia katika hoteli ya White Sands, Mbezi Beach, Dar es Salaam.
Yanga leo asubuhi imeendelea iliyoanza juzi tangu irejee Uturuki katika Uwanja wa Mabatini, Kijitonyama tayari kwa mechi ya kesho.
Wachezaji wote wamefanya mazoezi leo, kasoro kipa wa tatu, Yussuf Abdul na mshambuliaji Hamisi Kiiza 'Diego' wanaosumbuliwa na Malaria.

No comments:

Post a Comment