Monday, January 21, 2013

HAMISI KIIZA DIEGO APONA, AANZA MAZOEZI YANGA KUELEKEA DURU LA PILI LA VPL



Kiiza
KIPA wa tatu wa Yanga SC, Yussuf Abdul na mshambuliaji Mganda, Hamisi Kiiza ‘Diego’ waliokuwa wanasumbuliwa na Malaria, wamepona na leo wamefanya mazoezi na wenzao kwenye Uwanja wa Mabatini, Kijitonyama, Dar es Salaam.
Wawili hao walikosa mchezo wa kujipima nguvu dhidi ya Black Leopard ya Afrika Kusini juzi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ambao timu yao ilishinda mabao 3-2.
Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizguto amesema  leo kwamba, timu imeendelea na mazoezi leo na wachezaji wote wameshiriki wakiwemo Abdul na Kiiza.
Alisema kwa sasa Yanga haina majeruhi hata mmoja na inaendelea vema na mazoezi yake kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu hya Vodacom Tanzania Bara unaoanza mwishoni mwa wiki.
Mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati, katika kujiandaa na mzunguko huo wa pili wa Ligi Kuu, waliweka kambi ya wiki mbili Jijini Antalya, Uturuki kuanzia Desemba 30 mwaka jana hadi Januari 12 mwaka huu.
Katika kambi hiyo, pamoja na kufanya mazoezi ya nguvu ya ufukweni, uwanjani na gym, Yanga ilipata mechi tatu za kujipima nguvu dhidi ya Ariminia Bielefed ya Daraja la Nne Ujerumani waliyotoka nayo sare ya 1-1, kabla ya kufungwa 2-1 na Denizlispor FC ya Daraja la Kwanza Uturuki na 2-0 na Emmen FC ya Daraja la Kwanza Uholanzi.
Yanga ilimaliza mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu, ikiwa inaongoza ligi hiyo kwa pointi zake 29, baada ya kucheza mechi 13, ikifuatiwa na Azam iliyomaliza na pointi zake 24 na mabingwa watetezi, Simba SC waliomaliza na pointi 23.  
MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM 2012/2103:
                              P    W  D   L    GF GA GD Pts
1    Yanga               13 9    2    2    25 10 15 29
2    Azam                13 7    3    3    17 11 6    24
3    Simba SC         13 6    5    2    20 11 9    23
4    Mtibwa Sugar    13 6    4    3    18 12 6    22
5    Coastal Union   13 6    4    3    16 14 2    22
6    Kagera Sugar    13 5    6    2    15 10 5    21
7    Ruvu Shooting  13 6    2    5    19 17 2    20
8    Mgambo JKT    13 5    2    6    10 13 -3  17
9    JKT Ruvu          13 4    3    6    13 20 -7  15
10 JKT Oljoro          13 3    5    5    13 16 -3  14
11 TZ Prisons          13 3    5    5    8    12 -4  14
12 Toto African        13 2    6    5    10 15 -5  12
13 African Lyon       13 2    3    8    9    20 -11 9
14 Polisi Moro         13 0    4    9    4    16 -12 4

No comments:

Post a Comment