Thursday, January 10, 2013

BPL WIKIENDI: BIGI MECHI MAN UNITED v LIVERPOOL, ARSENAL v MAN CITY!


BARCLAYS PREMIER LEAGUE, BPL, inarejea kilingeni Wikiendi hii baada ya kuzipisha Mechi za Raundi ya 3 ya FA CUP Wikiendi iliyopita na Mechi zenye mvuto ni zile BIGI MECHI mbili zitakazochezwa Jumapili, Man United v Liverpool, na Arsenal v Man City.

RATIBA:
Jumamosi 12 Januari 2013
[SAA 12 Jioni]
Aston Villa v Southampton
Everton v Swansea
Fulham v Wigan
Norwich v Newcastle
Reading v West Brom
Stoke v Chelsea
Sunderland v West Ham
Jumapili 13 Januari 2013
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Man United v Liverpool
[SAA 1 Usiku]
Arsenal v Man City
Jumatatu 14 Januari 2013
[SAA 5 Usiku]
QPR v Tottenham

EVRA_N_SUAREZAkiongelea Mechi yao na Liverpool, Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amesema maombi yake kuhusu Mechi hiyo ni kuwa iweke Vichwa vya Habari kwenye Vyombo vya Habari vinavyohusu mpira tu.
Mara ya mwisho kwa Man United kukutana na Liverpool Uwanjani Old Trafford, Gemu hiyo iligubikwa na kituko cha Straika wa Liverpool, Luis Suarez, kukataa kumpa mkono Patrice Evra lakini katika Mechi yao ya mwisho iliyochezwa huko Anfield Mwezi Septemba, Wachezaji hao walipeana mikono.
Suarez aligoma kumpa mkono Evra baada ya kuadhibiwa kwa kumkashifu Kibaguzi Evra kwenye Mechi ya nyuma Liverpool walipokutana na Man United.

MSIMAMO:
1 Man Utd Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 26] Pointi 52
2 Man City Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 22] Pointi 45
3 Tottenham Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 12] Pointi 39
4 Chelsea Mechi 19 [Tofauti ya Magoli 21] Pointi 38
5 Arsenal Mechi 20 [Tofauti ya Magoli 18] Pointi 34
6 Everton Mechi 20 [Tofauti ya Magoli 8] Pointi 33
7 West Brom Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 2] Pointi 33
8 Swansea Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 5] Pointi 29
9 Stoke Mechi 21 [Tofauti ya Magoli 1] Pointi 29
10 Liverpool Mechi 20 [Tofauti ya Magoli 5] Pointi 28
11 West Ham Mechi 20 [Tofauti ya Magoli 0] Pointi 26
12 Norwich Mechi 21 [Tofauti ya Magoli -10] Pointi 25
13 Fulham Mechi 21 [Tofauti ya Magoli -5] Pointi 24
14 Sunderland Mechi 20 [Tofauti ya Magoli -5] Pointi 22
15 Newcastle Mechi 20 [Tofauti ya Magoli -11] Pointi 20
16 Aston Villa Mechi 21 [Tofauti ya Magoli -24] Pointi 19
17 Southampton Mechi 20 [Tofauti ya Magoli -11]  Pointi 18
18 Wigan Mechi 21 [Tofauti ya Magoli -17] Pointi 18
19 Reading Mechi 20 [Tofauti ya Magoli -17] Pointi 13
20 QPR Mechi 20 [Tofauti ya Magoli -20] Pointi 10

Ferguson ametamka: “Siku zote kutakuwa na kukuzwa kwa Mechi kati ya Manchester United na Liverpool kwa sababu tu ya Historia ya Timu hizi, ambazo ndizo zenye mafanikio makubwa kupita zozote nyingine Nchini humu!”
Ferguson ameongeza kuwa Watu wengi huleta Ajenda zao kuhusu Mechi hii na kuzikuza kupita kiasi na akatamka: “Bahati mbaya Mwaka jana kulikuwa na matukio ya Suarez. Natumai sasa hilo limepitwa na kila Klabu itilie mkazo Gemu tu!”

No comments:

Post a Comment