Wednesday, June 26, 2013

MOURINHO AANZA 'MATUSI' CHELSEA, ADONDOSHA KIFAA CHA KWANZA DARAJANI KUTOKA UJERUMANI, KINAPIGA MASHUTI BALAA!


KLABU ya Chelsea imekamilisha usajili wa winga wa kimataifa wa Ujerumani, Andre Schurrle kutoka Bayer Leverkusen kwa dau la Pauni Milioni 18, huu ukiwa ni usajili wa kwanza chini ya kocha mpya, Jose Mourinho.
Kinda wa miaka 22 amesaini Mkataba wa miaka mitano na atakuwa anavaa jezi namba 14 Stamford Bridge.
"Nina furaha mno sasa nimesaini na ni heshima kwangu kuchezea klabu hii, kwa timu hii na mashabiki hawa wakubwa," alisema Schurrle. 
Signed on the dotted line: Andre Schurrle has penned a five-year-deal and will wear the No 14 shirt
Andre Schurrle amesaini miaka mitano na kupewa jezi namba 14
Schurrle 
Schurrle signs
Schurrle, ambaye anaweza kucheza kama mshambuliaji, anafahamika kwa uwezo wake wa kufunga kutokea mbali. Amefunga mabao saba katika mechi 24 za timu yake ya taifa na alikuwemo kwenye kikosi cha Euro 2012.
Ready for a fight: Schurrle said he is not scared of failing like Marko Marin
Tayari kwa mapambano: Schurrle hahofii chochote
Big boss: Schurrle can't wait to work with Jose Mourinho
Bosi kubwa: Schurrle hawezi kusubiri kufanya kazi na Jose Mourinho

No comments:

Post a Comment